Yesu, mwana wa Maryamu (sehemu ya 5 kati ya 5): Watu wa Kitabu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Muhtasari wa baadhi ya istilahi zilizotumiwa na Kurani kwa ajili ya Isa na wafuasi wake kabla ya ujio wa Muhammad: "Bani Israeel”, “Eissa” na "Watu wa Kitabu".

  • Na Aisha Stacey (© 2008 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 09 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,177 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Baada ya kusoma na kuelewa kile Waislamu wanachoamini kuhusu Yesu, mwana wa Maryamu, kunaweza kuwa na maswali ambayo yanakuja akilini, au masuala ambayo yanahitaji ufafanuzi. Huenda umesoma neno “Watu wa Kitabu” na maana yake haikuwa wazi kabisa. Vivyo hivyo, unapochunguza vitabu vilivyopo kuhusu Yesu unaweza kukutana na jina Eissa na kujiuliza ikiwa Yesu na Eissa ni mtu mmoja. Ikiwa unafikiria kuchunguza zaidi kidogo au pengine kusoma Kurani, mambo yafuatayo yanaweza kukuvutia.

Isa ni nani?

Eissani Yesu. Labda kwa sababu ya tofauti ya matamshi, watu wengi wanaweza kuwa hawajui kwamba wanapomsikia Mwislamu akizungumza kuhusu Eissa, anazungumza juu ya Mtume Eissa. Tahajia ya Eissa inaweza kuwa ya aina nyingi – Isa, Esa, Essa, na Eissa. Lugha ya Kiarabu imeandikwa kwa herufi za Kiarabu, kwa hivyo mfumo wowote wa unukuzi hujaribu kutoa sauti ya kifonetiki. Haijalishi ni tahajia gani, zote zinaashiria Yesu, Mjumbe wa Mungu.

Yesu na watu wake walizungumza Kiaramu, lugha ya familia ya Wasemiti. Lugha za Kisemiti zinazozungumzwa na zaidi ya watu milioni 300 kote Mashariki ya Kati, Afrika Kaskazini na Pembe ya Afrika, ni pamoja na Kiarabu na Kiebrania. Matumizi ya neno Eissa ni tafsiri ya karibu zaidi ya neno la Kiaramu la Yesu – Eeshu. Kwa Kiebrania hii inatafsiriwa kwa Yeshua.

Kutafsiri jina Jesus (Yesu) katika lugha zisizo za Kisemiti kulizua utata. Hakukuwa na "J" katika lugha yoyote hadi karne ya kumi na nne[1], hivyo basi, jina Jesus lilipotafsiriwa katika Kigiriki, likawa Iesous, na katika Kilatini, Iesus[2]. Baadaye, herufi “I” na “J” zilitumiwa kwa kubadilishana, na hatimaye jina hilo likabadilishwa kuwa Kiingereza na kuwa Jesus. "S" ya mwisho kwenye mwisho ni kiashiria cha lugha ya Kigiriki ambapo majina yote ya kiume huishia kwa "S".

Kiaramu

Kiarabu

Kiebrania

Kigiriki

Kilatini

Kiingereza

Eeshu

Eisa

Yeshua

Iesous

Iesus

Jesus

Ni nani wenye vitabu vitukufu?

Mwenyezi Mungu anapowataja Watu wa Kitabu, anazungumzia zaidi kuhusu Mayahudi na Wakristo. Katika Kurani, watu wa Kiyahudi wanaitwa Bani Israeel, hasa Wana wa Israeli, au kwa kawaida Waisraeli. Makundi haya mahususi yanafuata, au yalifuata wahyi wa Mwenyezi Mungu kama ulivyoteremshwa katika Taurati na Injili. Unaweza pia kusikia Mayahudi na Wakristo wakiitwa "Watu wa Maandiko".

Waislamu wanaamini kwamba vitabu vilivyofunuliwa na Mwenyezi Mungu kabla ya Kurani vilipotea zamani, au vimebadilishwa na kupotoshwa, lakini pia wanatambua kwamba wafuasi wa kweli wa Musa na Yesu walikuwa Waislamu waliomwabudu Mungu Mmoja kwa utiifu wa kweli. Alikuja Yesu mwana wa Maryamu ili kusadikisha ujumbe wa Musa na kuwaongoza Wana wa Israili kwenye njia iliyonyooka. Waislamu wanaamini Mayahudi (Wana wa Israeli) walikataa utume na ujumbe wa Yesu, na Wakristo walimnyanyua kimakosa hadi hadhi ya mungu.

“Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Msipite kiasi katika dini yenu bila ya haki. Wala msifuate matamanio ya watu waliokwisha potea tangu zamani, na wakawapoteza wengi, na wenyewe wakapotea njia iliyo sawa.” (Kurani 5:77)

Tumeshajadili katika sehemu zilizopita jinsi Kurani inavyohusika kwa mapana na Mtume Yesu na mama yake Maryamu. Hata hivyo, Kurani pia inajumuisha aya nyingi ambapo Mungu anazungumza moja kwa moja na Watu wa Kitabu, hasa wale wanaojiita Wakristo.

Wakristo na Mayahudi wanaambiwa wasiwachambue Waislamu bila sababu yoyote isipokuwa kuamini Mungu Mmoja, lakini Mungu pia anaelekeza kwa makini kwenye ukweli kwamba Wakristo (wale wanaofuata mafundisho ya Kristo) na Waislamu wana mambo mengi yanayofanana, pamoja na mapenzi yao na heshima kwa Yesu na Manabii wote.

“...Na utawakuta walio karibu mno kwa mapenzi ni wale wanaosema: ‘Sisi ni Manasara.’ Hayo ni kwa sababu wapo miongoni mwao makasisi na wamonaki, na kwa sababu wao hawafanyi kiburi. Na wanaposikia yaliyoteremshwa kwa Mtume, utaona macho yao yanachururika machozi kwa sababu ya Haki waliyoitambua. Wanasema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini. Basi tuandike pamoja na wanaoshuhudia.” (Kurani 5:82-83)

Sawa na Yesu mwana wa Maryamu, Mtume Muhammad alikuja kuthibitisha ujumbe wa Mitume wote waliomtangulia; aliwaita watu kumwabudu Mungu Mmoja. Utume wake, hata hivyo, ulikuwa tofauti na Mitume waliotangulia, (Nuhu, Ibrahimu, Musa, Yesu na wengineo) kwa namna moja. Mtume Muhammad alikuja kwa ajili ya wanadamu wote na Mitume kabla yake walikuja mahususi kwa ajili ya wakati wao na watu wao. Kuja kwa Mtume Muhammad na kuteremshwa Kurani kulikamilisha dini iliyoteremshwa kwa Watu wa Kitabu.

Na Mwenyezi Mungu alizungumza na Mtume Muhammad katika Kurani na kumsihi kuwaita Watu wa Kitabu kwa kusema:

“Sema: ‘Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lililo sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi Mungu...’” (Kurani 3:64)

Mtume Muhammad aliwaambia masahaba zake, na hivyo kwa wanadamu wote:

“Mimi ni mtu wa karibu zaidi na mwana wa Maryamu, na Mitume wote ni ndugu na hakuna mtume mwingine baina yangu na yeye.”

Isitoshe:

“Mtu akimwamini Isa na kisha kuniamini atapata thawabu maradufu.” (Saheeh Al-Bukhari)

Uislamu ni dini ya amani, heshima na uvumilivu, na inatekeleza uadilifu na huruma kwa dini nyingine, hasa kwa Watu wa Kitabu.


Rejeleo la maelezo:

[1] The Encyclopaedia Americana.

[2] The Oxford English dictionary.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.