Vitu 5 Vinaleta Amani ya ndani na utulivu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kupata amani na utulivu ni mbinu ambao unahitaji hatua fulani. Nakala hii inazungumzia hatua kadhaa muhimu katika suala hili.

  • Na Raiiq Ridwan (aboutislam.net) [edited by IslamReligion.com]
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 23
  • Imetazamwa: 2,504 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

5-Things-Bring-Inner-Peace-and-Tranquility.jpgMoja ya hamu kubwa katika maisha ya mwanadamu ni kutafuta amani.

Wanasaikolojia wengi wanasema kuwa harakati kubwa zaidi ya wanadamu ni kutafuta amani, kwamba chochote wanadamu wanachofanya, hufanya ili wapate amani na utulivu.

Vivyo hivyo, moja ya majina ya Pepo katika Kurani ni Dar As-Salam (Nyumba ya Amani). Moja ya majina ya Mungu ni As-Salam, Mkamilifu, chanzo cha amani yote. Neno Uislamu lenyewe linahusiana na neno "salam" ambalo linamaanisha amani.

Imam Ibn Taymiyyah alisema kuwa kuna Peponi au paradiso ya hapa duniani ambayo mtu anahitaji kuingia ili kuingia Peponi ya Akhera. Paradiso hii, anasema, ni utulivu na utoshelevu wa mtima.

Kuridhika kwa moyo ni tabia ngumu sana kuwa nayo. Ulimwengu unaotuzunguka na vitu vinavyotutendekea hutufanya tuwe watu wenye shida sana

Barabara ya utulivu

Isitoshe, kama kitu chochote kile katika Uislamu utulivu sio tu hali ya kuwa. Ni njia ambayo inabidi ufuatwe na matendo ambayo yanahitajika kufanywa ili tufikie kiwango hicho ambapo tuna amani na sisi wenyewe.

Sehemu ya hamu ya kufikia utulivu imeumbwa ndani yetu. Mungu aliweka ndani yetu pengo ambao unaweza kujazwa na Mungu tu. Imam Ibn al-Qayyim aliandika ubeti maarufu juu ya hili.

"Ndani ya moyo, kuna hali isiyo safi ambayo inaweza kusafishwa tu kwa kumgeukia Mungu.

Na ndani ya moyo kuna hali ya upweke ambayo inaweza kuondolewa tu kwa kukaribia Mungu.

Na moyoni kuna hofu na wasiwasi, ambayo huondoka tu kwa kumkimbilia Mungu.

Na moyoni kuna hali ya majuto, ambayo inaweza kuondolewa tu kwa kuridhika na Mungu. "

Utulivu vinaweza kupatikana tu tunapofikia mahali ambapo tunajua ukweli wa maisha yetu, na Ukuu wa Mungu. Ni kuelewa aya ya Surah Ar-Rahman (Sura ya 55) ambapo Mungu anasema:

"Kila kitu ulimwenguni kitaangamia ila uso wa Mola wako uliojaa Utukufu na Heshima unabaki." (Kurani 55: 26-27)

Chochote kilicho duniani kitapotea au kufa. Chochote kinachotufanya tuwe na wasiwasi, kitaangamia. Chochote kinachotusikitisha kitaondoka. Chochote kinachotufanya tukereke na tukasirike ni cha muda mfupi.

Kila kinachotendwa bila kutafuta radhi ya Mungu kitaenda tu lakini kile kinachofanyika kutafuta radhi Yake na Neema Yake kitadumu na kuishi. Hii inabadilisha mtazamo wetu juu ya maisha kabisa.

Kifo, kupoteza, kuvunjika kwa moyo na kutafarukiana sio chungu tena kama ilivyokuwa zamani, kwa sababu mwishowe matarajio hufikia sifuri.

Wakati mtu hatarajii chochote, kila kitu wanachopata ni chanzo cha raha, na kila kitu wasichopata haiwatatanishi kamwe.

Mtazamo maishani unakuwa Mungu, Mwalimu wa Ulimwengu sio ni kadri gani ya mapenzi mtu hupokea kwenye Facebook, ni nani anapenda picha zao au ni alitoa pongezi na mengineyo mengi.

Maisha yanaonekana zaidi ya haya mambo madogo. Mtu hujifunza kuwasamehe wale wanaowaumiza, kuwathamini wale wanaowapenda na kutiisha ubinafsi kwa sababu haya hayana faida kwa mtu mwenye atazikwa mita sita chini ya ardhi siku mbili baadaye?

Mwandishi Jose Addison alisema kwamba wanadamu wanahitaji vitu vitatu ili kuwa na furaha— ni kitu cha kufanya, kitu cha kupenda, na kitu cha kutumaini. Yote haya yanaweza kupatikana katika aya hii ya Kurani:

"Na ukimbilieni msamaha wa mola wenu na pepo ambayo upana wake ni mbingu na ardhi iliyowekewa tayari kwa wachamungu." (Kurani 3: 133)

Kitu cha kufanya—haraka kusamehe.

Kitu cha kupenda—msamaha kutoka kwa Mola wako.

Kitu cha kutumaini—Paradiso/peponi pana kama mbingu na dunia.

Inakuwaje kwamba tunapata utulivu?

Tulisema mbeleni kuwa ni mchakato na unahitaji hatua. Kuna mengi kwa hivyo nakala hii inatarajia kumsaidia mtu kuelewa mwanzo.

1. Elewa Ukuu wa Mungu

Kuelewa Mungu ni nani, na jinsi alivyo mkuu.

Mtu anayeelewa ukuu na utukufu wa Mungu atapata amani akijua kuwa kila kitu kingine ni kidogo na hakina maana.

2. Elewa Ukweli wa Maisha haya

Tunapojua kuwa maisha ni zaidi ya madoido ya maisha ambayo tunaona na kuithamini, tunaelewa kuwa wakati wote mwelekeo wetu unapaswa kuwa wa kufikiria mbele. Kuelewa kuwa maisha ya ahera ni ya milele hutusaidia kuweka umakini wetu na sio kupoteza akili zetu juu ya mambo ya ulimwengu huu.

3. Kumkumbuka Mungu kila wakati kunatusaidia kuweka umakini wetu.

Binadamu huwa na tabia ya kusahau na kumkumbuka Mungu kila wakati hutukumbusha kuhusu Mungu wakati wote na mahali popote. Moja ya ushauri wa Mtume Muhammad rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake ilikuwa:

Dumu kumtaja Mola wako wakati wote [1]

Mungu anasema:

"Katika kumkumbuka Mungu mioyo hupata utulivu." (Kurani 13:28)

4. Shukuru

"Na mkishukuru nitawaongeza." (Kurani 14: 7)

Ikiwa tunashukuru, Mungu atatupa zaidi na zaidi ya kila kitu tulicho nacho. Atazidi kutuongeza, na pia itakuwa katika hali ya utulivu wetu.

5. Ridhika na Agizo la Mungu

Njia moja bora ya utulivu ni kutosheka na Mungu.

Ni kwa kuelewa kwamba chochote kinachtupata ni kwa mpango wa Mungu na mipapgo yake ndiyo bora. Tunaporidhika na agizo la Mungu, tutafanya bidii lakini tutosheke na matokeo yoyote yatakayotokea.

Amri ya Mungu ni ya Kimungu, na sio inayoeleweka kila wakati kwetu. Tunapotazama nyuma tu ndio tunaelewa jinsi mpango wa Mungu ulikuwa kamili. Mpango wa Mungu kwetu ndiyo bora, na kujua kwamba hufanya maisha kuwa ya amani sana.

Mungu atufanye watu wenye utulivu katika maisha na pia kwa kifo.

Mungu atufanye kati ya wale wanaosikia wito huu:

"Ewe nafsi tulivu, rejea kwa Mola wako, umeridhika na umeridhisha. Ingia miongoni mwa waja wangu, Ingia katika Pepo yangu." (Kurani 89: 27-30)



Rejeleo la maelezo:

[1] At-Tirmidhi

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.