Kisa cha Isa na Maryamu katika Kurani Tukufu (sehemu ya 3 kati ya 3): Isa II

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Sehemu hii inaangazia aya za Kurani Tukufu zinazozungumzia ulinzi wa Mwenyezi Mungu kwa Isa, wafuasi wake, ujio wake wa pili katika ulimwengu huu na yale atakayokumbana nayo Siku ya Kiyama.

  • Na IslamReligion.com
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 3
  • Imetazamwa: 3,059 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Shauku ya Kristo

“Isa alipohisi kuwa kati yao pana ukafiri alisema: ‘Ni nani wasaidizi wangu kwa Mwenyezi Mungu?’ Wanafunzi wake wakasema: ‘Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu. Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na shuhudia kwamba sisi hakika ni Waislamu.’[1] Mola wetu Mlezi! Tumeyaamini uliyoyateremsha, na tumemfuata huyu mtume, basi tuandike pamoja na wanaoshuhudia.’ Na makafiri walipanga mipango, na Mwenyezi Mungu akapanga mipango, na Mwenyezi Mungu ndiye mbora wa wenye kupanga.[2] Pale Mwenyezi Mungu aliposema: ‘Ewe Isa! Mimi nitakufisha, na nitakunyanyua kwangu, na nitakutakasa na wale waliokufuru, na nitawaweka wale waliokufuata juu ya wale waliokufuru, mpaka Siku ya Kiyama. Kisha marejeo yenu yatakuwa kwangu, nikuhukumuni katika yale mliyokuwa mkikhitalifiana.’” (Kurani 3:52-55)

“Na kwa kusema kwao: ‘Sisi tumemuuwa Masihi Isa, mwana wa Maryamu, mtume wa Mwenyezi Mungu - nao hawakumuuwa wala hawakumsulubu, bali walifananishiwa tu.[3] Na hakika waliokhitalifiana katika haya wamo katika shaka nayo. Wao hawana ujuzi wowote nayo, ila ni kufuata dhana tu. Wala hawakumuuwa kwa yakini. Bali Mwenyezi Mungu alimtukuza kwake.[4] na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hekima.” (Kurani 4:157-158)

Wafuasi wa Yesu

“Watakaokuhoji katika haya baada ya kukufikilia elimu hii waambie: ‘Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wake zetu na wake zenu, na sisi wenyewe na nyinyi wenyewe, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.’ Hakika haya ndiyo maelezo ya kweli. Na hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu tu, na hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye nguvu na Mwenye hekima. Na kama wakigeuka, basi Mwenyezi Mungu anawajua waharibifu. Sema: ‘Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lililo sawa baina yetu na nyinyi[5] Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi Mungu[6].’ Na, wakigeuka basi semeni: ‘Shuhudieni ya kwamba sisi ni Waislamu.’” (Kurani 3:61-64)

“Hakika wamekufuru waliosema: ‘Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu.’ Sema: ‘Ni nani mwenye kumiliki chochote mbele ya Mwenyezi Mungu ikiwa Yeye angetaka kumuangamiza Masihi mwana wa Maryamu, na mama yake, na wote waliomo katika ardhi?’ Na mamlaka ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ni vya Mwenyezi Mungu. Huumba apendavyo. Na Mwenyezi Mungu anao uweza juu ya kila kitu. Na Mayahudi na Wakristo wanasema: ‘Sisi ni wana wa Mwenyezi Mungu na vipenzi vyake.’ Sema: ‘Basi kwa nini anakuadhibuni kwa ajili ya madhambi yenu?’ Bali nyinyi ni watu tu kama wale wengine aliowaumba. Humsamehe amtakaye na humuadhibu amtakaye. Na ni wa Mwenyezi Mungu tu ufalme wa mbingu na ardhi. Na marejeo ni kwake Yeye.” (Kurani 5:17-18)

“Hakika wamekufuru waliosema: ‘Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu!’ Na hali Masihi mwenyewe alisema: ‘Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Kwani anayemshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na waliodhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru.’ Kwa hakika wamekufuru waliosema: ‘Mwenyezi Mungu ni wa tatu wa Utatu.’[7] Hali hakuna mungu ila Mungu Mmoja. Na ikiwa hawaachi hayo wanayoyasema, kwa yakini itawakamata adhabu chungu wale wanaokufuru. Je, hawatubu kwa Mwenyezi Mungu na wakamwomba msamaha? Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira na Mwenye kurehemu.” (Kurani 5:72-74)

“Na Mayahudi wanasema: ‘Uzeir ni mwana wa Mungu,’[8] Na Wakristo wanasema: ‘Masihi ni mwana wa Mungu.’ Hiyo ndiyo kauli yao kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya waliokufuru kabla yao. Mwenyezi Mungu awaangamize! Wanageuzwa namna gani hawa! Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Mwenyezi Mungu, na pia Masihi mwana wa Maryamu. Na wala hawakuamrishwa isipokuwa wamuabudu Mungu Mmoja, hapana mungu ila Yeye. Subhanahu, Ametakasika na hayo wanayomshirikisha nayo.”[9] (Kurani 9:30-31)

“Enyi mlioamini! Hakika wengi katika makuhani na wamonaki wanakula mali za watu kwa batili na wanazuilia njia ya Mwenyezi Mungu. Na wanaokusanya dhahabu na fedha, wala hawazitumii katika njia ya Mwenyezi Mungu, wabashirie khabari ya adhabu iliyo chungu.” (Kurani 9:34)

Ujio wa Pili

“Na hawi katika watu wa Kitabu ila hakika atamuamini yeye kabla ya kufa kwake.[10] Naye Siku ya Kiyama atakuwa shahidi juu yao.”[11] (Kurani 4:159)

“Na kwa hakika yeye (Isa) ni alama ya Saa ya Kiyama. Basi usiitilie shaka,[12] na nifuateni. Hii ndiyo njia Iliyonyooka.” (Kurani 43:61)

Yesu Siku ya Kiyama

“Na pale Mwenyezi Mungu atakaposema: ‘Ewe Isa mwana wa Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipokutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyokufunza kuandika na hekima na Taurati na Injili. Na ulipotengeneza udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipowaponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na ulipowafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipokukinga na Wana wa Israili ulipowajia na hoja zilizo wazi,’ na wakasema waliokufuru miongoni mwao: ‘Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!’” (Kurani 5:110)

“Na pale Mwenyezi Mungu atakaposema: ‘Ewe Isa mwana wa Maryamu! Ati wewe uliwaambia watu: ‘Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu?’[13]’ (Na Isa) atasema: ‘Subhanaka, Wewe umetakasika! Hainifalii mimi kusema ambayo si haki yangu. Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwisha yajua. Wewe unayajua yaliyo ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo katika nafsi yako. Hakika Wewe ndiye Mjuzi mkubwa wa yaliyofichikana.’[14] ‘Sikuwaambia lolote ila uliyoniamrisha, nayo ni: ‘Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi.’ Na mimi nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa nao. Na uliponifisha ukawa Wewe ndiye Muangalizi juu yao. Na Wewe ni shahidi juu ya kila kitu. Ukiwaadhibu basi hao ni waja wako. Na ukiwasamehe basi Wewe ndiye Mwenye nguvu na Mwenye hikima.’[15] Mwenyezi Mungu atasema: ‘Hii ndiyo Siku ambayo wasemao kweli utawafaa ukweli wao. Wao watapata bustani zipitazo mito kati yake. Humo watadumu milele. Mwenyezi Mungu amewawia radhi, nao wawe radhi naye. Huku ndiko kufuzu kukubwa.’ Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi na vilivyomo. Naye ni Muweza wa kila kitu.” (Kurani 5:116-120)



Rejeleo la maelezo:

[1] Jina lililotolewa la wanafunzi katika Kurani ni al-Hawariyyun, ambalo linamaanisha waliotakaswa, kama rangi nyeupe. Pia inaripotiwa kuwa walikuwa wakivaa nguo nyeupe.

[2] Isa alipaishwa katika hali ya usingizi. Neno linalotumika hapa ni wafah, ambalo linaweza kumaanisha usingizi au kifo. Kwa Kiarabu, usingizi huitwa kifo kidogo. Tazama pia aya 6:60 na 39:42, ambapo neno wafah hurejelea usingizi na sio kifo. Kwa kuwa aya ya 4:157 inakanusha kuuawa na kusulubishwa kwa Isa, na kwa kuwa kila mwanadamu hufa mara moja lakini Isa anatakiwa kurudi duniani, tafsiri pekee iliyobaki ya aya hiyo ni kulala.

[3] Wajihi wa mfanano wa Isa uliwekwa kwa mwingine, na ni mtu huyo ndiye, sio Isa, aliyesulubiwa. Kwa mujibu wa maelezo kadhaa ya Kurani, aliyesulubiwa alikuwa mmoja wa wanafunzi, aliyekubali afananishwe na Isa, na kujifia shahidi ili kumwokoa Isa kwa malipo ya peponi.

[4] Isa alipaishwa akiwa mzima wa mwili na roho, na hakufa. Bado anaishi huko juu, na atarudi kuelekea wakati wa mwisho wa dunia. Baada ya kutimiza daraka lake duniani, hatimaye atakufa.

[5] Hivi ndivyo mitume wote wa Mungu walilingania na kukubaliana. Na kwa hivyo, kauli hii sio ya kundi moja pekee, bali ni misingi ya kawaida kwa wale wanaotaka kumwabudu Mungu.

[6] Mtu anapomtii mwanadamu mwingine kwa kumuasi Mungu, anakuwa amemfanya kuwa bwana badala ya Mungu.

[7] Kwa kurejelea Utatu.

[8] Ingawa sio Mayahudi wote waliiamini, walishindwa kuishutumu (tazama aya 5:78-79). Dhambi linaporuhusiwa kuendelea na kuenea bila kupingwa, jamii nzima inapatilizwa kwa kutowajibika.

[9] Wanachuoni wa dini ndio wenye elimu, na watawa ndio waliozama katika ada na ibada. Wote wawili wanachukuliwa kuwa viongozi wa kidini na viigizo, na kupitia ushawishi wao wanaweza kuwapotosha watu.

[10] Kiwakilishi katika "kifo chake" kinaweza kurejelea Isa au mtu kutoka kwa watu wa Maandiko. Ikiwa inamrejelea Isa, inamaanisha kwamba watu wote wa Maandiko Matakatifu watakuja kumwamini Isa atakaporudi mara ya pili duniani na kabla ya kifo chake. Kisha Isa atathibitisha kwamba yeye ni mtume kutoka kwa Mungu, sio Mungu wala mwana wa Mungu, na atawataka watu wote kumwabudu Mungu peke yake na kujisalimisha Kwake katika Uislamu. Ikiwa kiwakilishi kinamrejelea mtu mmoja mmoja kutoka kwa watu wa Kitabu, basi aya hiyo ina maana kwamba kila mmoja wao ataona kabla tu ya kufa kwake ni nini kitakachomshawishi kwamba Isa alikuwa mtume wa kweli kutoka kwa Mungu, na sio Mungu. Lakini imani hiyo wakati huo haitamnufaisha, kwa kuwa haitokani na uchaguzi huru, bali anapowaona malaika wa adhabu.

[11] Tazama aya 5:116-118.

[12] Ujio wa pili wa Yesu kutakuwa ishara kwamba Siku ya Hukumu imekaribia.

[13] Kuabudu wengine pamoja na Mungu ni sawa na kuwaabudu wao badala ya Mungu. Yote mawili yanamaanisha kuwa ibada inaelekezwa na kufanyiwa mtu mwingine asiyekuwa Mungu, lakini Mungu ndiye Pekee anayefaa kuabudiwa.

[14] Mungu, kama Isa alivyosema, anajua kwamba Isa hakulingania ibada ifanywe kwa ajili yake mwenyewe au ya mama yake. Lengo la swali ni kuwaelekeza wale wanaomwabudu Isa au Mariamu kwamba kama wangekuwa wafuasi wa kweli wa Isa, wangeacha mazoea hayo, kwa sababu Isa hakuwaita kwayo kamwe. Lakini ikiwa wataendelea, basi wajue kwamba Isa atawakana Siku ya Mwisho, na kwamba wamekuwa hawamfuati, bali wanafuata tu matakwa yao binafsi.

[15]Kwa maneno mengine, Wewe unamjua ni nani anayestahiki adhabu, basi utamuadhibu. Na unamjua ni nani anayestahiki kusamehewa, basi utamsamehe. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu na Mwenye kuadhibu, na Wewe ni Mwenye hekima katika kuendesha kila jambo, basi unawasamehe wanaostahiki msamaha.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.