Hadithi ya Ibrahimu (sehemu ya 7 kati ya 7): Ujenzi wa Mahali Patakatifu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Ibrahimu anamtembelea tena mwanawe Ishmaeli, lakini wakati huu ili kutimiza kazi adhimu, ujenzi wa Nyumba ya Ibada, pahala patakatifu kwa wanadamu wote.

  • Na IslamReligion.com
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 2
  • Imetazamwa: 5,719 (wastani wa kila siku: 7)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Ibrahimu and Ishmaeli Wajenga Kaaba

Baada ya utengano wa miaka kadhaa, baba na mwana walikutana tena. Ilikuwa katika safari hii ambapo hao wawili walijenga Kaaba kwa amri ya Mungu kama pahala patakatifu pa kudumu; pahala palipojengwa kwa ajili ya ibada ya Mungu. Ilikuwa ni hapa, katika jangwa hili ambako Ibrahimu alikuwa amewaacha Hagari na Ishmaeli hapo awali, ndipo alipomwomba Mungu apafanye mahali ambapo wangeweza kushikilia sala, na kuepukana na ibada ya sanamu.

"Na Ibrahim alipo sema: Ewe Mola wangu Mlezi! Ujaalie mji huu uwe wa amani, na uniepushe mimi na wanangu na kuabudu masanamu. Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika hayo yamewapoteza watu wengi. Basi aliye nifuata mimi huyo ni wangu, na aliye niasi, hakika Wewe ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu. Mola wetu Mlezi! Hakika mimi nimewaweka baadhi ya dhuriya zangu katika bonde lisilo kuwa na mimea, kwenye Nyumba yako Takatifu, ewe Mola wetu Mlezi, ili washike Sala. Basi zijaalie nyoyo za watu zielekee kwao, na waruzuku matunda, ili wapata kushukuru. Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika Wewe unajua tunayo yaficha na tunayo yatangaza. Na hapana kitu kinacho fichikana kwa Mwenyezi Mungu katika ardhi wala katika mbingu. Alhamdulillahi! Himdi zote ni za Mwenyezi Mungu aliye nipa juu ya uzee wangu Ismail na Is-haq. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kusikia maombi. Mola wangu Mlezi! Nijaalie niwe mwenye kushika Sala, na katika dhuriya zangu pia. Ewe Mola wetu Mlezi, na ipokee dua yangu. Mola wetu! Unighufirie mimi na wazazi wangu wote wawili, na Waumini, siku ya kusimama hisabu." (Kurani 14:35-41)

Miaka mingi baadaye, Ibrahimu anaungana tena na mwanawe Ishmaeli, ili waanzishe Nyumba ya Mungu iliyoheshimiwa, iwe kituo cha ibada, ambapo watu wangeelekeza nyuso zao wakisali, na kuifanya kuwa mahali pa Hija. Kuna aya nyingi nzuri katika Qurani zinazoelezea utakatifu wa Kaaba na kusudi la ujenzi wake.

"Na pale tulipomweka Ibrahim pahala penye ile Nyumba tukamwambia: Usinishirikishe na chochote; na isafishe Nyumba yangu kwa ajili ya wanao izunguka kwa kut'ufu, na wanao kaa hapo kwa ibada, na wanao rukuu, na wanao sujudu. Na watangazie watu Hija; watakujia kwa miguu na juu ya kila ngamia aliye konda, wakija kutoka katika kila njia ya mbali." (Kurani 22:26-27)

"Na kumbukeni tulipo ifanya ile Nyumba (ya Alkaaba) iwe pahala pa kukusanyikia watu na pahala pa amani. Na alipo kuwa akisimama Ibrahim pafanyeni pawe pa kusalia. Na tuliagana na Ibrahim na Ismail: Itakaseni Nyumba yangu kwa ajili ya wanao izunguka kwa kut'ufu na wanao jitenga huko kwa ibada, na wanao inama na kusujudu." (Kurani 2:125)

Kaaba ni mahali ya kwanza ya ibada iliyoteuliwa kwa ajili ya wanadamu wote kwa lengo la mwongozo na baraka:

"Hakika Nyumba ya kwanza walio wekewa watu kwa ibada ni ile iliyoko Bakka, iliyo barikiwa na yenye uwongofu kwa walimwengu wote. Ndani yake zipo Ishara zilizo wazi - masimamio ya Ibrahim, na mwenye kuingia humo anakuwa katika amani. Na kwa ajili ya Mwenyezi Mungu imewajibikia watu wahiji kwenye Nyumba hiyo, kwa yule awezae njia ya kwendea. " (Kurani 3:96-97)

Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema:

"Hakika Mwenyezi Mungu amepafanya patakatifu pahala hapa siku alipo ziumba mbingu na ardhi, na patakuwa hivyo mpaka Siku ya Kiyama." (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)

Dua za Ibrahimu

Kwa hakika, ujenzi wa pahala patakatifu patakapoheshimiwa na vizazi vyote vijavyo ulikuwa ni mojawapo ya njia bora za ibada ambazo watu wa Mungu wangeweza kufanya. Walimwomba Mwenyezi Mungu wakati wa tendo lao:

"Ewe Mola Mlezi wetu! Tutakabalie! Hakika Wewe ndiye Msikizi Mjuzi. Ewe Mola Mlezi wetu! Tujaalie tuwe ni wenye kusilimu kwako, na pia miongoni mwa vizazi vyetu wawe umma ulio silimu kwako. Na utuonyeshe njia za ibada yetu na utusamehe. Bila shaka Wewe ndiye Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu!" (Kurani 2:127-128)

" Na alipo sema Ibrahim: Ee Mola wangu Mlezi! Ufanye huu uwe mji wa amani, na uwaruzuku watu wake matunda, wale wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho...." (Kurani 2:126)

Ibrahimu pia aliomba kwamba nabii afufuliwe kutoka katika uzao wa Ishmaeli, ambao wangekuwa wenyeji wa nchi hii, kama vile wazao wa Isaka wangekuwa wenyeji wa nchi za Kanaani.

"Ewe Mola Mlezi wetu! Waletee Mtume anaye tokana na wao, awasomee Aya zako, na awafundishe Kitabu na hikima na awatakase. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima." (Kurani 2:127-129)

The_Story_of_Abraham_(part_7_of_7)_001.jpg

Kaabah iliyojengwa na Ibrahimu na Ishmaeli na Kituo cha Ibrahimu, ambacho kinahifadhi nyayo za Mtume Ibrahimu.

Maombi ya Ibrahimu ya kuletwa kwa Mtume yalijibiwa baada ya maelfu kadhaa ya miaka wakati Mungu alipomtoa Mtume Muhammad kutoka kwa Waarabu, na kama Makka ilivyochaguliwa kuwa patakatifu na Nyumba ya Ibada kwa wanadamu wote, hivyo pia Mtume wa Makka alitumwa kwa wanadamu wote.

Ilikuwa ni kilele hiki cha maisha ya Ibrahimu kilichokuwa kukamilika kwa lengo lake: kujenga pahala pa ibada kwa wanadamu wote, si kwa ajili ya kabila lolote au rangi, bali kwa ajili ya ibada ya Mungu Mmoja wa Kweli. Ni kupitia kuanzishwa kwa nyumba hii ndipo palikuwa dhamana ya kwamba Mungu, Mungu ambaye alimwomba na ambaye alimtolea dhabihu zisizo na mwisho, Ataabudiwa milele, bila ya kumshirikisha na miungu mingine. Hakika hii ilikuwa katika fadhila kubwa alizopewa mwanaadamu yeyote.

Ibrahimu na Hija

Kila mwaka, Waislamu kutoka duniani kote hukusanyika kutoka kwa matabaka yote ya maisha, na hilo ni jibu la maombi ya Ibrahimu na wito wa Hija. Ibada hii inaitwa Hajj, na inaadhimisha matukio mengi ya mtumishi mpendwa wa Mungu Ibrahimu na familia yake. Baada ya kuzunguka Kaaba, Mwislamu anasali nyuma ya Kituo cha Ibrahimu, jiwe ambalo Ibrahimu alisimamia kujenga Kaaba. Baada ya sala, Waislamu hunywa kutoka kwa kisima kiitwacho Zamzam, kilichotokea kama jibu la ombi la Ibrahimu na Hagar, ili kuwapa riziki Ishmaeli na Hajari, na ndiyo sababu ya watu kukaa katika nchi hiyo. Ibada ya kutembea kati ya Safaa na Marwah inaadhimisha kutafuta maji kwa Hagar wakati yeye na mtoto wake walikuwa peke yao huko Makka. Kuchinjwa kwa mnyama huko Mina wakati wa Hija, na Waislamu duniani kote katika nchi zao wenyewe wanavyofanya, ni katika kufuata mfano wa nia ya Ibrahimu ya kumtoa mwanawe kama dhabihu kwa ajili ya Mungu. Mwishowe, kupiga mawe kwa nguzo za mawe huko Mina kunaonyesha jinsi Ibrahimu alivyokataa ushawishi wa kishetani wa kumzuia kumtoa Ishmaeli kama dhabihu.

“Mtumishi mpendwa wa Mungu” ambaye Mungu alisema juu yake,"Hakika Mimi nitakufanya uwe mwongozi wa watu,,"[1]akarudi Palestina na kufa huko.



Rejeleo la maelezo:

[1] Quran 2:125

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.