Craig Robertson, Mkatoliki wa Zamani, Canada (sehemu ya 1 kati ya 2): Kutoka hali mbaya hadi mbaya zaidi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Baada ya kulelewa katika nyumba ya Kikatoliki na kutumia sehemu kubwa ya utotoni mwake kuhudhuria kanisa, Craig anakataa imani na kujiingiza maisha ya anasa.

  • Na Craig Robertson
  • Iliyochapishwa mnamo 14 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,274
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Craig_Robertson__Ex-Catholic__Canada_(part_1_of_2)_-_From_Bad_to_Worse_001.jpgJina langu ni Abdullah Al-Kanadi. Nilizaliwa huko Vancouver, Canada. Familia yangu, ambao walikuwa Wakatoliki wa Kirumi, walinilea kama Mkatoliki wa Roma hadi nilipokuwa na umri wa miaka 12. Nimekuwa Muislamu kwa takriban miaka sita, na ningependa kushiriki nanyi hadithi ya safari yangu kuingia Uislamu.

Nadhani katika hadithi yoyote ni bora kuanzia kutoka mwanzo. Utotoni mwangu nilihudhuria shule ya kidini ya Kikatoliki na nilifundishwa kuhusu imani ya Kikatoliki, pamoja na masomo mengine. Soma la kidini lilikuwa daima somo langu bora; Nilifaulu kitaaluma katika mafundisho ya Kanisa. Nililazimishwa kuwa 'mtumishi wa madhabahu' na wazazi wangu tangu nikiwa mdogo sana, jambo ambalo liliwapendeza babu na nyanya kwa kiasi kikubwa. Lakini kadiri nilipojifunza kuhusu dini yangu, ndivyo nilivyojiuliza maswali! Nina kumbukumbu hili kutoka utotoni mwangu; nilimwuliza mama yangu katika Misa: “Je, dini yetu ni ya ukweli?” Jibu la mama yangu bado ninalikumbuka hadi leo: “Craig, zote ni sawa, zote ni nzuri!” Lakini kwangu hili halikuonekana kuwa sawa. Ni faida gani kujifunza dini yangu ikiwa zote zilikuwa sawa?

Nilipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, nyanya yangu alipata saratani ya koloni na akafa miezi michache baadaye , baada ya kupigana vita vikali na ugonjwa huo. Sijawahi kutambua jinsi kifo chake kilivyoniathiri sana mpaka baadaye katika maishani mwangu. Wakati huo, nikiwa na umri mdogo wa miaka kumi na miwili, niliamua kuwa mkanaji Mungu ili kumwadhibu Mungu (kama unaweza hata kutambua kitu kama hicho!) Nilikuwa kijana mdogo mwenye hasira; Niliukasirikia ulimwengu, nikajikasiria mimi binafsi na mbaya zaidi kuliko yote, nilimkasirikia Mungu. Nilitumia miaka yangu ya ujana nikijaribu kufanya kila kitu nilichoweza ili kuwavutia “marafiki” wangu wapya katika shule ya sekondari ya umma. Nilitambua haraka kwamba nilikuwa na mengi ya kujifunza, kwa kuwa sikufundishwa mengi katika shule ya kidini kama unavyofunzwa katika shule ya umma. Niliwashawishi marafiki zangu wote faraghani wanifundishe kuhusu mambo yote ambayo sijajifunza, punde nilipata tabia ya kuapa na kuwadharau walio dhaifu kuliniliko. Ingawa nilijaribu sana kukubaliwa na wenzangu kwa uwezo wangu wote, sikufaulu. Nilikuwa nikinyanyaswa sana na wanafunzi wenzangu, na wasichana walikua wakinikejeli. Kwa mtoto wa umri wangu, hii ilikuwa mateso. Nilijirudia mwenyewe, katika kile unachokiita 'ganda la hisia'.

Miaka yangu ya ujana yalijaa taabu na upweke. Wazazi wangu walijaribu kuzungumza nami, lakini nilikuwa na ugomvi nao na kuwakosea heshima. Nilihitimu shule ya sekondari katika majira ya joto ya 1996 na nilihisi kuwa mambo yangeweza kubadilika yawe bora, kwani niliamini hayangeweza kuwa mbaya zaidi! Nilikubaliwa katika shule ya kiufundi ya kienyeji na nikaamua kuzidisha elimu yangu na labda nipate pesa nzuri, ili nipate furaha. Nilipata kazi katika mkahawa wa chakula cha haraka iliyokuwa karibu na nyumba yangu ili kujilipia karo.

Wiki kadhaa kabla ya kuanza shule, nilialikwa kuondoka kwetu na marafiki wengine kutoka kazi. Kwangu, hii ilionekana kama jibu la matatizo yangu! Ningeweza kusahau familia yangu na kuwa na marafiki zangu wakati wote. Usiku mmoja, niliwaambia wazazi wangu kuwa ningeondoka hivi karibuni. Waliniambia Siwezi, na kwamba sikuwa tayari na kwamba hawataniruhusu! Nilikuwa na umri wa miaka 17 na nilikuwa mkaidi sana; niliwaapia wazazi wangu na kuwaambia kila aina ya maovu, jambo ambalo bado ninajuta hata leo. Nilihisi kukumbwa na uhuru wangu mpya, nilihisi kana kwamba nimetolewa jela, na ningeweza kufuata tamaa zangu kama nilivyoona sawa. Nilihamia kwa marafiki zangu na sikuzungumza na wazazi wangu kwa muda mrefu baada ya hapo.

Nilikuwa nikifanya kazi na kwenda shule wakati wenzangu nilioishi nao walinifunza kuvuta bangi. Niliipenda baada ya kuivuta maara ya kwanza! Ningeivuta baada ya kurudi nyumbani kutoka kazini ili nipumzike. Hata hivyo, nilianza kuvuta bangi zaidi na zaidi, mpaka wakati mmoja, mwishoni mwa wiki, nilikuwa nikiivuta sana, hadi jumatatu ikafika na kabla sijajua, wakati wa shule ulikuwa umefika. Nikaamua kukosa shule siku moja na kwenda siku inayofuata, kwani hawangenikosa. Sijawahi kurudi shuleni baada ya hapo. Hatimaye niligundua bahati nzuri niliokuwa nao. Chakula chote cha mgahawa nilichoweza kuiba na bangi zote ambazo ningeweza kuvuta, na bado nihitaji shule ya nini?

Nilikuwa nikiishi maisha mazuri, au hivyo ndivyo nilifikiri; nilikuwa kijana mhuni wa kazi na hivyo wasichana walianza kutanabahi, kinyume na walivyokuwa katika shule ya sekondari. Nilijaribu madawa mabaya zaidi ya kulevya, lakini alhamdulillah, niliokolewa kutokana na mambo ya kutisha. Jambo la ajabu lilikuwa, wakati sikuwa nimelewa au kunywa madawa haya nilikuwa na huzuni. Nilihisi kutokuwa na maana na asiyekuwa na thamani kabisa. Nilikuwa nikiiba kazini na kutoka kwa marafiki ili kudumisha 'moshi wa kemikali'. Nilianza kushuku watu waliokuwa karibu nami na kufikiri maafisa wa polisi walikuwa wakinifukuza kwa kila kona. Nilikuwa nimeanza kulemewa na nilihitaji suluhisho, na nikaona kuwa dini ingenisaidia.

Nakumbuka nikiona filamu kuhusu uchawi na nilifikiri kwamba hiyo ingekuwa suluhisho kamili kwangu. Nilinunua vitabu kadhaa kuhusu Wicca na Ibada ya Maumbile, na kugundua kwamba vilihimiza matumizi ya dawa za kiasili na hivyo nikaendelea. Watu wangeniuliza kama namwamini Mungu, na tungekuwa na mazungumzo ya ajabu sana huku nikiwa nimelewa, lakini ninakumbuka wazi nikisema kwamba hapana, kwa kweli simwamini Mungu kabisa, bali naamini miungu mingi isiyo kamili kama mimi.

Kupitia yote haya, kulikuwa na rafiki mmoja ambaye alikwama nami. Alikuwa ni Mkristo 'Aliyezaliwa Upya' na alikuwa akinihubiria kila wakati, ingawa ningedhihaki imani yake kila mara. Alikuwa rafiki pekee niliyekuwa naye wakati huo ambaye hakunihukumu, hivyo aliponialika kwenda kambi ya vijana mwishoni mwa wiki niliamua kwenda naye. Sikuwa na matarajio. Nilidhani ningekuwa na kicheko kikubwa nikiwadhihaki “Wabeba Biblia” wote. Siku ya pili Wakati wa jioni, walikuwa na ibada kubwa katika ukumbi. Walicheza kila aina ya muziki ambayo ilimsifu Mungu. Niliwatazama vijana na wazee, wanaume na wanawake wakipiga kelele na kuomba msamaha na kumwaga machozi. Nilisisimuka kikweli na nikasema dua kimya kama ifuatavyo “Mungu, najua nilikuwa mtu mbaya, tafadhali nisaidie, na unisamehe na uniruhusu kuanza upya.” Nilihisi kulemewa na hisia, na nilihisi machozi yakimwagika chini kwa mashavu yangu. Niliamua wakati huo kumkubali Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wangu binafsi. Niliinua mikono yangu juu na kuanza kucheza na kupiga densi (ndiyo, densi!) Wakristo wote waliokuwa karibu nami walikuwa wananiangalia kwa kimya na kushangaa; yule kijana aliyewadhihaki na kuwaambia jinsi walivyokuwa wajinga kwa kumwamini Mungu, alikuwa akicheza na kumsifu Mungu!

Nilirudi nyumbani na kutupilia mbali madawa yote, ulevi, na wasichana. Niliwaambia marafiki zangu jinsi walivyohitaji kuwa Wakristo ili waweze kuokolewa. Nilishangaa kuwa walinikataa, kwa sababu daima walinisikiliza kabla ya hapo. Hatimaye nilihamia kwa wazazi wangu baada ya kutokuwepo kwa muda mrefu na nilianza kuwaambia walipaswa kuwa wakristo. Kwa kuwa walikuwa Wakatoliki waliona kuwa tayari walikuwa Wakristo, lakini nilihisi hawakuwa, kwa kuwa waliwaabudu Watakatifu. Niliamua kuhama tena lakini wakati huu tuliwachana kwa nia nzuri na nilipewa kazi na babu yangu ambaye alitaka kunisaidia katika “kupona” kwangu.

Nilianza kuenda “nyumba ya vijana” ya Kikristo ambayo ilikuwa nyumba ambapo vijana wangeweza kwenda, ili kuondokana na shinikizo la familia na kujadili Ukristo. Nilikuwa na umri mkubwa kuliko wengi wa wavulana hao, hivyo nikawa mmoja wa wale waliozungumza zaidi na kujaribu kuwafanya wavulana wahisi wapo nyumbani. Licha ya hayo, nilihisi kama mlaghai, kwani nilianza kunywa na kuenda na wasichana tena. Ningewaambia watoto kuhusu upendo wa Yesu kwao, na wakati wa usiku ningelewa. Kupitia yote haya, rafiki wangu mmoja wa Kikristo angejaribu kunipa ushauri na kuniweka kwenye njia sahihi.

Mbaya Nzuri zaidi

Craig Robertson, Mkatoliki wa zamani, Kanada (sehemu ya 2 kati ya 2): Kujifunza Kukubali

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Baada ya kupata njia yake ya kurudi kwa Ukristo, Craig anasalitiwa na marafiki zake na anapotea tena, hadi anapopatana na Muislamu akiwa kazini.

  • Na Craig Robertson
  • Iliyochapishwa mnamo 14 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,483
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Bado ninakumbuka hadi leo mkutano wangu wa kwanza na Muislamu. Mmoja wa wavulana alimleta rafiki yake kwenye nyumba ya vijana. Alikuwa mtoto wa Kiislamu ambaye jina lake nimesahau. Ninachokumbuka ni mvulana huyo akisema “Nimemleta rafiki yangu 'fulani', yeye ni Muislamu na nataka kumsaidia awe Mkristo”. Nilishangaa kabisa na mtoto huyu mwenye umri wa miaka 14, alikuwa na utulivu na urafiki! Amini au usiamini, alijitetea mwenyewe NA Uislamu dhidi ya Wakristo kadhaa ambao walikuwa wanamtukana yeye na Uislamu! Tulipokuwa tukiketi pale tukipitia Biblia zetu na kuzidi kukasirika, aliketi pale tu, akitabasamu na kutuambia kuhusu kuabudu wengine badala ya Mungu na jinsi kuna upendo katika Uislamu. Alikuwa kama swara aliyezungukwa na mafisi kadhaa, lakini wakati wote huo, alikuwa na utulivu na heshima. Nilishangazwa sana!

Mtoto huyo wa Kiislamu aliacha nakala ya Qurani kwenye rafu, huenda aliisahau au aliiacha kwa kusudi, sijui, lakini nilianza kuisoma. Hapo hapo nilipandwa na hasira nilipoona kitabu hiki kilikuwa na mantiki inayoeleweka zaidi kuliko Biblia. Nilikitupa juu ya kitanda na kuenda zangu, nikiungua kwa hasira; lakini baada ya kukisoma, nilikuwa na shaka ya kunung'unika katika moyo wangu. Nilijaribu sana kusahau kuhusu mtoto huyo wa Kiislamu na kufurahia muda wangu na marafiki zangu katika nyumba ya vijana. Kikundi cha vijana kilikuwa kikikwenda Makanisa mbalimbali mwishoni mwa wiki kwa ajili ya sala, na usiku wa Jumamosi ulitumika kukaa katika Kanisa moja kubwa badala ya kukaa kwenye baa. Nakumbuka nikiwa katika tukio moja la namna hiyo liitwalo 'Kisima' na nilijisikia nikiwa karibu sana na Mungu na nilitaka kujinyenyekeza na kumwonyesha Muumba wangu upendo wangu kwake. Nilifanya nilichokiona kuwa asili, nilisujudu. Nimesujudu kama Waislamu wanavyofanya katika sala za kila siku, lakini sikujua niliyokuwa nikifanya, yote ninayoyajua ni kwamba nilihisi vizuri sana... nilihisi nilifanya kitu sawa na nzuri kuliko kitu kingine chochote nilichowahi kufanya. Nilijihisi mwema sana na kuendelea katika njia yangu lakini kama kawaida, nilianza kuona mambo yakiteleza tena.

Mchungaji daima alitufundisha kwamba ni lazima tuwasilishe nia yetu kwa Mungu, na sikutaka chochote zaidi ya kufanya hivyo; lakini sikujua ni kwa jinsi gani! Daima niliomba “Tafadhali Mungu, fanya nia yangu iwe yako, nifanye kufuata nia Yako” na kadhalika, lakini hakuna kitu kilichotokea. Nilijihisi nikiteleza na kwenda polepole mbali na Kanisa huku imani yangu ikiyeyuka. Ilikuwa wakati huo ndipo rafiki yangu , yule Mkristo ambaye alikuwa amenisaidia kuja kwa Yesu, pamoja na rafiki yangu mwingine wa karibu, walimbaka mpenzi wangu ambaye nilikuwa naye kwa miaka miwili. Nilikuwa katika chumba kingine nikiwa nimelewa, sijui nini kinatokea na siwezi kuzuia chochote. Wiki kadhaa baadaye, ilijulikana kwamba aliyekuwa akisimamia nyumba ya vijana alikuwa amemlawiti mmoja wa wavulana ambaye alikuwa rafiki yangu.

Ulimwengu wangu ulikuwa umevunjika! Nilikuwa nimesalitiwa na marafiki zangu wengi, watu ambao walidhaniwa kuwa karibu na Mwenyezi Mungu, na wanafanya kazi ya kuelekeza watu Peponi. Sikuwa na chochote zaidi cha kutoa, Nilikuwa mtupu tena. Nilitembea tu kila mahali kama hapo awali, kwa upofu na bila mwelekeo wowote, nikifanya tu kazi na kulala na kuenda sherehe mbalimbali. Mpenzi wangu aliniacha baada ya muda mfupi. Hisia za hatia, hasira na huzuni zimezunguka uhai wangu wote. Muumba wangu angewezaje kuruhusu kitu kama hicho? Ubinafsi wangu ulikuwa mkubwa aje?

Baada ya muda mfupi, meneja wangu wa kazi aliniambia kuwa “Mwislamu” mmoja angekuja kufanya kazi nasi, alikuwa mtu wa dini na kuwa tunapaswa kujaribu kuwa na heshima tukiwa naye. Mwislamu huyo alipokuja tu alianza Da'wah. Hakupoteza muda wowote katika kutuambia kuhusu Uislamu na kila mtu alimwambia kwamba hakutaka kusikia chochote kuhusu Uislamu, isipokuwa mimi! Roho yangu ilikuwa ikilia na hata ukaidi wangu haukuweza kuzuia kilio. Tulianza kufanya kazi pamoja na kujadili imani zetu. Nilikuwa nimepoteza matumaini na Ukristo kabisa, lakini alipoanza kuniuliza maswali, imani yangu iliongezeka na nilihisi kama mpiganaji wa vita vya 'Krusedi' anayetetea Imani kutoka kwa uovu wa “Mwislamu” huyu.

Ukweli wa jambo hilo ni kwamba Mwislamu huyo hakuwa mbaya kama nilivyoambiwa. Kwa kweli, alikuwa bora kuliko mimi. Hakulaani, hakuwahi kukasirika na daima alikuwa na utulivu, mwenye fadhili na mwenye heshima. Nilivutiwa kweli na kuamua kwamba angekuwa Mkristo mzuri. Tulijadiliana na kuulizana mambo kuhusu dini za kila mmoja wetu, lakini baada ya muda nilihisi nikijihami zaidi na zaidi. Wakati mmoja, nilikasirika sana... hapa nilikuwa nikijaribu kumshawishi akubali ukweli wa Ukristo, na nilihisi ni yeye ndiye alikuwa kwa njia ya ukweli! Nilianza kuchanganyikiwa zaidi na zaidi na sikujua cha kufanya. Kile nilichokijua ni kwamba nilifaa kuongeza imani yangu, hivyo nikaruka katika gari langu na kunguruma mbali kueleka 'Kisima'. Niliamini kwamba kama ningeweza kusali tena, ningeweza kurudisha hisia hizo na imani imara na kisha ningeweza kumshawishi Muislamu huyo vizuri. Hatimaye nilifika huko, baada ya kuharakisha kwa njia nzima, na nikapata kumefungwa! Hakuna mtu mwingine alikuwa hapo, nilitazama kote ili angalau nipate tukio lingine linalofanana na la kwanza ili niweze 'kupata nguvu' lakini hakuna kitu kilitokea. Nilirudi nyumbani huku nikiwa nimekata tamaa.

Nilianza kutambua kwamba nilikuwa nikisukumwa katika mwelekeo fulani, kwa hivyo nikaomba tena na tena kwa Muumba wangu ili aelekeze nia yangu Kwake. Nilihisi kwamba dua yangu ilikuwa ikijibiwa; Nilikwenda nyumbani na kulala kitandani na wakati huo nilitambua kwamba nilihitaji kuomba kwa jinsi ambayo sijawahi omba mbeleni. Niliketi kitandani na kulia, 'Yesu, Mungu, Buddha, yeyote uliye, tafadhali, tafadhali niongoze, nakuhitaji Wewe! Nimefanya maovu mengi sana katika maisha yangu na nahitaji msaada wako. Ikiwa Ukristo ndio njia sahihi basi unipe nguvu, na ikiwa ni Uislamu basi nilete kwake!' Niliacha kuomba na machozi yalikwenda, na ndani kwa kiini cha nafsi yangu nilihisi utulivu, nilijua jibu lilikuwa nini. Nilikwenda kazini siku iliyofuata na kumwambia ndugu wa Kiislamu “naweza kukusalimia aje?” Aliniuliza nilimaanisha nini na nikasema, “Nataka kuwa Muislamu”. Aliniangalia na akasema “Allahu Akbar!”. Tulikumbatiana kwa dakika nzima na nikamshukuru kwa kila kitu na nikaanza safari yangu katika Uislamu.

Nikitazama nyuma kwa matukio yote yaliyotokea katika maisha yangu kwa muda wote huo, natambua kwamba nilikuwa natayarishwa kuwa Muislamu. Mungu alinionyesha huruma nyingi. Kati ya yote yaliyotokea katika maisha yangu, kulikuwa na kitu cha kujifunza. Nilijifunza uzuri wa kwa nini Uislamu ulikataza ulevi, zinaa, na haja ya kuvaa Hijab. Hatimaye niko kwa ardhi iliyonyooka, sielekei tena upande mmoja; ninaishi maisha ya wastani, na ninajitahidi kuwa Muislamu mwema.

Kuna changamoto kila wakati, na nina uhakika wengi wenu mmezipitia, kama nilivyozipitia mimi. Lakini kupitia changamoto hizi, kupitia maumivu haya ya kihisia, tunakuwa na nguvu; tunajifunza na ninatumai tutageuka kwa Mungu. Kwa wale miongoni mwetu ambao wamekubali Uislamu wakati fulani maishani mwao, sisi kweli tumepata kheri na bahati. Tumepewa nafasi, nafasi ya kupata rehema kubwa kabisa! Rehema ambayo hatustahili, lakini Mungu bado atatupea siku ya Kiyama. Nimejenga amani na familia yangu na ninatumai kuanza yangu mwenyewe Mungu akipenda. Uislamu kwa kweli ni njia ya maisha, na hata tunapopitia mateso kwa mikono ya Waislamu wenzetu au wasio Waislamu, lazima tukumbuke daima kuwa tunafaa kuwa na subira na kumgeukia Mungu tu.

Ikiwa nimesema kitu kisicho sahihi ni kutoka kwangu, na ikiwa nimesema kitu kilicho sahihi kimetoka kwa Mwenyezi Mungu, Sifa zote ni za Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu amjalie rehema na baraka Mtume wake Muhammad, Amina.

Mungu aongeze Imani yetu na kuifanya iambatane na yale yanayompendeza Yeye na kutupatia Pepo Yake, Amina!

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.