Hadithi ya Adamu (sehemu ya 1 kati ya 5): Mwanadamu wa Kwanza

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Hadithi ya kusisimua ya Adamu iliyoelezewa kwenye marejeleo kutoka kwa Vitabu Vitakatifu.

  • Na Aisha Stacey (© 2008 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 09 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 6
  • Imetazamwa: 9,453 (wastani wa kila siku: 11)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Story_of_Adam_(part_1_of_5)_001.jpgUislamu unatupatia maelezo ya kustaajabisha ya uumbwaji wa Adam[1]. Tamaduni za Kikristo na Kiyahudi hazina maelezo mengi lakini zinafanana sana na Kurani. Kitabu cha Mwanzo kinamuelezea kuwa Adam aliumbwa kutokana na “vumbi” na katika Talmud, Adam anaelezewa kuwa alifinyangwa kutoka kwa matope.

Na Mungu aliwaambia malaika:

“‘Na pale Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Mimi nitamweka katika ardhi Khalifa (mfwatizi), wakasema: Utaweka humo atakaye fanya uharibifu humo na kumwaga damu, hali sisi tunakutakasa kwa sifa zako na tunakutaja kwa utakatifu wako? Akasema: Hakika Mimi nayajua msiyo yajua.’” (Kurani 2:30)

Kwa kuanzia hadithi ya Adam, mtu wa kwanza, mwanadamu wa kwanza. Mwenyezi Mungu alimuumba Adam kutokana na kidonge cha udongo ulio na aina mbali mbali za udongo ardhini. Malaika walitumwa duniani kukusanya udongo ambao ulitumika kumuumba Adam. Ulikuwa mwekundu, mweupe, hudhurungi, na mweusi; ulikuwa laini na nyumbufu, vile vile mgumu na wenye changarawe; ulitoka kwenye milima na mabonde; kutoka kwenye majangwa yasiyo na rutuba na vile vile kutoka kwenye tambarare zenye rutuba ya asili pamoja na kila aina katikati. Kizazi cha Adamkilikusudiwa kuwa tofauti kama uchache wa udongo ambao uliumba wahenga wao; wote wana umbo, sifa na ubora tofauti.

Mchanga au Udongo?

Katika Kurani nzima, udongo uliotumika kumuumba Adam unajulikana kwa majina mengi, na kutokana na hili tunaweza kuelewa baadhi ya mbinu za uumbaji wake. Kila jina la udongo lilitumika katika hatua tofauti ya uumbaji wa Adam. Mchanga, uliochukuliwa kutoka ardhini, hujulikana kamamchanga; Mwenyezi Mungu pia anautaja kama udongo. Unapochanganywa na maji huwa matope, Unapoachwa kwa muda, kiwango cha maji ndani yake hupungua na kuwa udongo wa kunata (au tope). Unapoachwa kwa muda fulani huanza kunuka, na kuanza kuwa rangi nzito - mweusi, udongo laini. Mwenyezi Mungu alifinyanga umbo la Adam Kutokana na dutu hili. Kiwiliwili chake kilichokuwa hakina roho kiliachwa ili kukauka, na kuwa kama kile kinachofahamika kwenye Kurani kama udongo wenye sauti. Adam alifinyangwa kutokana na kitu kinachofanana na udongo wa mfinyanzi. Unapofungwa hutoa sauti ya mlio.[2]

Mwanadamu wa Kwanza Anathaminiwa

Na Mwenyezi Mungu akawaambia Malaika:

“Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo. Na nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa kumt'ii.” (Kurani 38:71-72)

Mungu alimthamini mwanadamu wa kwanza, Adamu, kwa njia nyingi sana. Mwenyezi Mungu akampulizia nafsi yake, akamtengeneza kwa mikono yake, na akawaamrisha Malaika wamsujudie. Na Mungu akawaambia Malaika:

“....Msujudieni Adamu. Basi wakasujudu isipo kuwa Iblisi, hakuwa miongoni mwa walio sujudu....(Kurani 7:11)

Ingawa ibada imekusidiwa kwa ajili ya Mungu Peke Yake, kusujudiwa kwa Adam na Malaika kunaashiria heshima na utukufu. Inasemekana kwamba, pindi kiwiliwili cha Adam kilipopuliziwa uhai kilitaharuki, alipiga chafya na hapo hapo akasema ‘Sifa zote na shukrani ni kwa sababu ya Mungu;’ hivyo basi, Mungu akaitikia kwa kumpa Adam rehema Zake. Ingawa simulizi hii haikutajwa ndani ya Kurani au riwaya sahihi za Mtume Muhammad, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, imetajwa katika baadhi ya tafsiri za Kurani. Hivyo, katika sekunde zake za kwanza za uhai, mwanadamu wa kwanza ametambuliwa kuwa kiumbe wa kuheshimiwa, aliyefunikwa na Rehema isiyo na kifani ya Mwenyezi Mungu.[3]

Kadhalika, Mtume Muhammad alisema kwamba Mwenyezi Mungu alimuumba Adam kwa uumbaji wake.[4] Hii haimaanishi kwamba Adam aliumbwa ili aonekane rika la Mwenyezi Mungu, kwani Mungu ni wa pekee katika nyanja Zake zote, hatuwezi kuitambua au kuumba sura Yake. Hata hivyo, inamaanisha kwamba Adam alipewa sifa fulani ambazo pia Mwenyezi Mungu anazo, ingawa haziwezi kulinganishwa. Alipewa sifa za rehema, upendo, uhuru wa kuchagua, na nyinginezo.

Salamu ya Kwanza

Adam aliagizwa aende mbele ya kikundi cha Malaika waliokaa karibu naye na awasalimie kwa maneno Assalamu alaikum (rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yenu), walijibu ‘amani, rehema na baraka za ya Mwenyezi Mungu ziwe juu yako pia’. Kuanzia siku hiyo na kuendelea maneno haya yakawa ni salamu za wale waliojisalimisha kwa Mwenyezi Mungu. Kuanzia wakati wa uumbaji wa Adam, kizazi chake tukaagizwa kueneza amani.

Adam, aliye Mlinzi

Mwenyezi Mungu aliwaambia wanadamu kwamba hakuwaumba isipokuwa wanapaswa kumuabudu Yeye. Kila kitu katika ulimwengu huu kiliumbwa kwa ajili ya Adam na kizazi chake, ili kutusaidia katika uwezo wetu wa kumwabudu na kumjua Mwenyezi Mungu. Kwa sababu ya Hekima ya Mungu isiyo na kifani, Adam na kizazi chake walipaswa kuwa walezi duniani, kwa hiyo, ili kutekeleza jukumu hili Mwenyezi Mungu alimfundisha Adam kile alichohitajika kujua. Mungu anataja:

Na akamfundisha Adamu majina ya vitu vyote.” (Kurani 2:31)

Mungu alimpa Adam uwezo wa kutambua na kutaja majina ya kila kitu; Alimfundisha lugha, hotuba na uwezo wa kuwasiliana. Mwenyezi Mungu alimjaza tele Adam sababu ya upendo na elimu. Baada ya Adam kujifunza majina na matumizi ya vitu vyote Mungu aliwaambia Malaika...

“‘kisha akaviweka mbele ya Malaika, na akasema: Niambieni majina ya hivi ikiwa mnasema kweli. Wakasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hatuna ujuzi isipokuwa kwa uliyo tufunza Wewe. Hakika Wewe ndiye Mjuzi Mwenye hikima.’” (Kurani 2:31-32)

Mungu akamgeukia Adam na kusema:

“‘Akasema: Ewe Adamu! Waambie majina yake. Basi alipo waambia majina yake alisema: Sikukwambieni kwamba Mimi ninajua siri za mbinguni na za duniani, na ninayajua mnayo yadhihirisha na mliyo kuwa mnayaficha?” (Kurani 2:33)

Adam alijaribu kuongea na Malaika, lakini walikuwa wamejishughulisha na kumwabudu Mwenyezi Mungu. Malaika hawakupewa elimu maalum au uhuru wa mapenzi, lengo lao pekee lilikuwa kumwabudu na kumsifu Mwenyezi Mungu. Kwa upande mwingine, Adam alipewa uwezo wa kufikiri, kuchagua na kutambua vitu na malengo yake. Hii ilimsaidia kumtayarisha Adam kwa jukumu lake la kuja duniani. Kwa hivyo, Adam alijua majina ya kila kitu, hata hivyo alikuwa peke yake Mbinguni. Asubuhi moja Adam aliamka na kumkuta mwanamke akimtazama.[5]



Rejeleo la maelezo:

[1] Kutokana na kazi ya Al Imam ibn Katheer, Hadithi za Mitume.

[2] Saheeh Al-Bukhari

[3] Al Imam ibn Katheer. Hadithi za Mitume

[4] Saheeh Muslim

[5] Ibn Katheer.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.