Michael Wolfe, Mwandishi wa Habari, Marekani

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mshindi wa Tuzo ya Wilbur ya 2003 ya kitabu bora cha mwaka kwenye mada ya dini, mwandishi na mshairi na kuonekana kwenye "Nightline" ya Ted Koppel inayoandika Hija, Michael Wolfe anaelezea motisha zake za kuukubali Uislamu.

  • Na Michael Wolfe
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,420 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Michael_Wolfe__Journalist__USA_001.jpgBaada ya miaka ishirini na tano kama mwandishi Marekani, nilitaka kitu cha kupunguza wasiwasi wangu. Nilikuwa nikitafuta maneno mapya ya kuona. Jinsi mtu anavyokuzwa huanzisha mahitaji fulani katika eneo hili. Kutokana na historia nyingi, kwa kawaida niliweka mkazo mkubwa juu ya masuala ya ubaguzi wa rangi na uhuru. Kisha, katika miaka yangu ya mwanzo ya ishirini, nilikuwa nimeenda kuishi Afrika kwa miaka mitatu. Wakati huo, ambao ulikuwa wa mafunzo kwangu, nilikutana na watu weusi wa makabila mengi tofauti, na Waarabu, Wabeberu, na hata Wazungu, ambao walikuwa Waislamu. Kwa wingi watu hawa hawakukubaliana na mtazamo wa Magharibi wa asili kuwa kama aina ya kijamii. Katika makutano yetu, kuwa na rangi isiyo ya kawaida sio swala la muhimu sana. Nilikaribishwa kwanza na kuhukumiwa kwa sifa baadaye. Kinyume chake, Waulaya na Wamarekani , ikiwa ni pamoja na wengi ambao hawana mawazo ya ubaguzi wa rangi, moja kwa moja huwapanga watu kwa minajili ya rangi. Waislamu waliainisha watu kwa imani na matendo yao. Niliiona hii ya kushangaza na kuburudisha. Malcolm X aliona wokovu wa taifa lake ndani yake. "marekani inahitaji kuuelewa Uislamu," aliandika, "kwa sababu hii ndiyo dini moja ambayo inafuta katika jamii yake tatizo la rangi."

Nilikuwa nikitafuta njia ya kutoroka, pia, kutoka kwenye kujitenga na utamaduni wa kupenda vitu. Nilitaka kufikia hali ya kiroho, lakini njia za kawaida nilizozijua nikiwa kijana zilifungwa. Baba yangu alikuwa Myahudi; mama yangu alikuwa Mkristo. Kwa sababu ya malezi yangu, niliweza kutembea katika kambi mbili za kidini. Imani zote mbili bila shaka zilikuwa ni kubwa . Bado ile inayosisitiza watu waliochaguliwa nikaona haiungwi mkono; wakati mwingine, kwa msingi wa siri, alinikataa. Karne moja kabla, jina la bibi yang lilikuwa limewekwa kwenye kioo cha rangi kwenye Kanisa la Church of Christ barabara kuu huko Hamilton, Ohio. Nilipokuwa na umri wa miaka ishirini, hii haikuwa na maana yoyote kwangu.

Haya ndiyo masharti ambayo maisha yangu ya utotoni yalitoa. Kadiri nilivyofikiria sasa, ndivyo nilivyorudi kwenye uzoefu wangu katika Uislamu wa Afrika. Baada ya safari mbili za kurudi Moroko, katika mwaka wa 1981 na 1985, nilikuja kuhisi kuwa Afrika, bara hilo, halikuhusika sana na maisha yenye usawa nilioupata huko. Halikuwa, bara nililolifuata, wala taasisi. Nilikuwa nikitafuta mfumo ambao ningeweza kuishi nao, mfumo wa dhana za kiroho zinazotumika katika maisha niliyokuwa nikiishi sasa. Sikutaka "kuufanyia biashara" utamaduni wangu. Nilitaka kupata maana mpya.

Baada ya chakula cha jioni cha katikati ya Atlantiki, nilienda kunawa bafuni. Wakati wa kutokuwepo kwangu, akidi ya Hasidim ilijipanga kusali nje ya mlango. Muda nilipomaliza, walikuwa wamezama sana wasiweze kuniona. nikitoka bafuni, sikuweza kufungua kitasa kwa urahisi. Kuingia njiani.

Niliweza tu kusimama kichwa changu kikiwa barabara ya ukumbi, nikitazama migongo ya washiriki. Wakiwa wameshika vitabu vya maombi vyenye ukubwa wa viganja, walikaa katika mkao wa kuvutia, wakigusa maandiko kwenye vifua vyao walipokuwa wakisali. Hatua kwa hatua mienendo ilikua isiyokuwa ya kawaida, kama aina ndogo ya rock na roll. Nilitazama kutoka kwenye mlango wa bafuni hadi walipomaliza, kisha nikarudi nyuma kwenye njia ya kiti changu.

Tulitua pamoja baadaye usiku huo huko Brussels. Nikiwa nimepanda tena, nilipata gazeti la Kiyidi lililotupwa kwenye trei ya chakula. Ndege ilipopaa kuelekea Moroko, walikuwa wamekwenda.

Simaanishi kuwa maisha yangu katika kipindi hiki yalilingana na muundo wowote mzuri. Mwanzoni, mnamo miaka ya 1981, nilichochewa na udadisi na hamu ya kusafiri. Mahali nilipenda sana kwenda, nilipokuwa na pesa, ilikuwa Moroko. Pindi nisipoweza kusafiri, kulikuwa na vitabu. Hali hii ilinikutanisha na waandishi wachache waliosukumwa na watu wa kigeni, waandishi wenye uwezo wa kutunga sentensi kama hii, na Freya Stark:

“Uzuri wa kudumu wa Uarabuni ni kwamba msafiri hupata kiwango chake kama mwanadamu; mwelekeo wa watu, ni mbaya kwa hisia au ukosoaji, kama fadhila zisizo ngumu; na uzuri wa kupendwa kwa nafsi pekee, nafikiri, kuongezwe kwenye sababu tano za kusafiri nilizopewa na Sayyid Abdulla, mtazamaji; "kuziacha shida za mtu nyuma; kupata riziki; kupata kujifunza; kutenda tabia njema, na kukutana na watu wenye heshima”.

Sikuweza kuandaa orodha ya mahitaji, lakini nilikuwa na wazo la haki juu ya kile nilichofuata. Dini niliyotaka iwe metafizikia kama metafizikia ilivyo kwa sayansi. isingeweza kuthibitishwa kwa mawazo madogo au lundo la usiri ili kuwafurahisha makuhani wake. Kusingekuwa na makuhani, bila utengano kati ya asili na vitu vitakatifu. Hakungekuwa na vita vya mwili, kama ningeweza kuusaidia. tendo la ndoa lingekuwa la asili, si kiti cha laana kwa viumbe. Hatimaye, nilitaka vitu vya ibada, utaratibu wa kila siku ili kuimarisha hisia na nidhamu ya akili yangu. Zaidi ya yote, nilitaka uwazi na uhuru. Sikutaka kuachana na sababu ili tu kubaki na itikadi fulani.

Kadiri nilivyojifunza zaidi kuhusu Uislamu, ndivyo ulivyoonekana kuendana na nilivyokuwa nilitafuta.

Watu wengi wa Magharibi waliosoma niliowajua kipindi hicho walitilia shaka hali yoyote ya kidini yenye nguvu. Waliainisha dini kuwa ulaghai wa kisiasa, au waliipuuza kuwa dhana ya enzi za kati, wakilenga mawazo ya zamanikutoka kwenye Ulaya yao ya zamani.

Haikuwa ngumu kupata chanzo cha maoni yao. Miaka elfu moja ya historia ya Magharibi ilikuwa imetuachia sababu nyingi za kujutia njia iliyoongoza kwenye ujinga mwingi na mauaji. Kuanzia Vita vya Watoto wa Msalaba na Baraza la Kuhukumu hadi imani zilizobadilishwa za unazi na ukomunisti katika karne yetu, nchi zote zimechoshwa na imani. Hofu ya Nietzsche, kuwa taifa la kisasa lingekuwa dini , imethibitika kuwa sahihi kwa njia ya kuhuzunisha. Karne yetu, ilionekana kwangu, ilikuwa ikiishia katika enzi za zaidi ya imani, ambayo walioamini waliishi zaidi ya watu wasioamini.

Bila kujali ushirika wa kanisa, ubinadamu wa kilimwengu ni hewa ya wamagharibi wanayopumulia, lenzi tunayopitia kutazama. Kama mtazamo wowote wa ulimwengu, mtazamo huu unaenea na upo wazi. unaunda msingi wa utambulisho wetu mpana na demokrasia na kutafuta uhuru katika mifumo yake yote isiyohesabika na ya kudanganya. Kwa kuzama katika shughuli zetu za pamoja, mtu anaweza kusahau kirahisi kuwa njia zingine za maisha zipo kwenye sayari moja.

Wakati wa safari yangu, kwa mfano, Waislamu milioni 650 wenye wawakilishi wengi katika nchi arobaini na nne walifuata mafundisho rasmi ya Uislamu. Isitoshe, watu zaidi ya milioni 400 walikuwa wawakilishi ndani ya Ulaya, Asia, na Marekani. Kwa kusaidiwa na uchumi wa baada ya ukoloni, Uislamu umekuwa katika kipindi cha miaka thelathini cha imani ndani ya Ulaya Magharibi. Kati ya dini kuu za ulimwengu, Uislamu pekee ndio ulikuwa unaongezeka katika kundi lake.

Marafiki zangu wa kisiasa walisikitishwa na matamanio yangu mapya. Hao wote na ulimwengu waliuchanganya Uislamu na hila za nusu dazeni ya madhalimu wa mashariki ya kati. Vitabu walivyosoma, matangazo mapya waliyotazama yalionyesha imani kama seti ya kazi za kisiasa. Karibu vyote hakuna kilichosewa kuhusu matendo yake ya kiroho. Nilipenda kumnukuu Mae West kwao: “Wakati wowote unapoichukulia dini kuwa mzaha, kicheko huwa juu yako.”

Kihistoria, Muislamu huona Uislamu kama ni mwisho, mkomao wa dini ya asili inayorudi nyuma hadi kwa Adamu. Ni imani ya Mungu mmoja kwa uthabiti kama Uyahudi, ambao Mitume wao wakuu Uislamu wanaheshimu kama viungo katika mlolongo unaoendelea, unaoishia kwa Yesu na Muhammad, amani iwe juu yao. Kimsingi ujumbe wa kufanywa upya, Uislamu umefanya sehemu yake katika jukwaa la dunia kurudisha ladha iliyosahaulika ya utamu uliopotea wa maisha kwa mamilioni ya watu. Kitabu chake, Quran, kilimfanya Goethe kutamka, “Unaona, mafundisho haya hayashindwi kamwe; kwa mifumo yetu yote, hatuwezi kwenda, na kwa ujumla hakuna mtu anayeweza kwenda zaidi.

Uislamu wa Jadi unadhihirika kupitia matendo ya nguzo tano. Kukubali kuamini, kuswali, kutoa sadaka, na kufunga ni shughuli zinazofuatiliwa mara kwa mara katika maisha yake yote. Masharti yanayoruhusu, kila Muislamu kuhiji Makka mara moja katika maisha. Neno la Kiarabu kwa ibada hii ya tano ni Hijja. Wanachuoni wanahusisha neno hili na dhana ya ‘qasd’, “matamanio,” na dhana ya wanaume na wanawake kuwa wasafiri duniani. Katika dini za Kimagharibi, kuhiji ni tamaduni ya kupuuza, dhana ya kawaida, ambayo kwa kawaida hupunguzwa kuwa msamiati. Miongoni mwa Waislamu, kwa upande mwingine, Hija inajumuisha uzoefu muhimu kwa mamilioni ya mahujaji wapya kila mwaka. Licha ya maudhui ya kisasa ya maisha yao, inabakia kuwa kitendo cha utii, taaluma ya imani, na mwonekano wa jumuiya ya kiroho. Kwa Waislamu walio wengi, Hajj ni lengo kuu, safari ya maisha.

Kama niyeukubali Uislam, nilijiona kuwa na wajibu wa kwenda Makka. Kama mpenzi wa kusafiri sikuweza kufikiria lengo la kulazimisha zaidi.

Mfungo wa kila mwaka, wa mwezi mzima wa Ramadhani hutanguliwa na Hajj kwa takriban siku mia moja. Ibada hizi mbili zinaunda kipindi cha ufahamu ulioimarishwa katika jamii ya Kiislamu. Nilitaka kukitumia kipindi hiki. liliusoma Uislamu; [Nilihudhuria] Msikiti wa karibu na nyumbani kwangu huko California; Nilikuwa nimeanza mazoezi. Sasa nilitarajia kuimarisha kile nilichokuwa nikijifunza kwa kujizamisha katika dini ambayo Uislamu unaingiza kila kipengele cha kuwepo.

Nilipanga kuanzia Moroko, kwa sababu niliijua nchi hiyo vizuri na kwa sababu iliufuata Uislamu wa jadi na ilikuwa na utulivu. Mahali pa mwisho nilipotaka kuanza lilikuwa eneo la maji lililojaa wafuasi wa madhehebu wenye ghasia. Nilitaka kupiga kasia kwenye mkondo wa maji, mkubwa, maji tulivu.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.