Wasomi wa Kikristo Wanaujua Utofauti katika Biblia (sehemu ya 1 kati ya 7): Utangulizi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Angalia kile baadhi ya Wasomi Wakubwa wa Kikristo wamesema kuhusu usahihi wa Biblia.

  • Na Misha’al ibn Abdullah (taken from the Book: What did Jesus really Say?)
  • Iliyochapishwa mnamo 19 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 2
  • Imetazamwa: 8,585 (wastani wa kila siku: 10)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

“Basi ole wao wanao andika kitabu kwa mikono yao, kisha wakasema: Hiki kimetoka kwa Mwenyezi Mungu, ili wachumie kwacho pato dogo. Basi ole wao kwa yale iliyo andika mikono yao, na ole wao kwa yale wanayo yachuma.” (Kurani 2:79)

“Na alipo wajia Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu, mwenye kuthibitisha yale waliyo nayo, kundi moja miongoni mwa wale walio pewa Kitabu lilitupa Kitabu cha Mwenyezi Mungu hicho nyuma ya migongo yao kama kwamba hawajui.” (Kurani 2:101)

“Msiliongeze neno niwaamurulo wala msilipunguze, mpate kuzishika amri za Bwana, Mungu wenu, niwaamuruzo.” (Kumbukumbu la Torati 4:2)

Christian_Scholars_Recognize_Contradictions_in_the_Bible_(part_1_of_5)_001.jpgNgoja tuanze kuanzia mwanzo. Hakuna msomi wa kibiblia hapa duniani atakayedai kuwa Biblia iliandikwa na Yesu mwenyewe. Wote wanakubali kuwa Biblia iliandikwa baada ya kuondoka kwa Yesu amani iwe juu yake na wafuasi wake. Dkt W Graham Scroggie wa Taasisi ya Moody Bible, Chicago, katika ujumbe mashuhuri wa Kiinjili wa Kikristo, anasema:

“..Ndio, Biblia ni ya kibinadamu, japokuwa kuna wengine wana bidii ambayo hailingani na maarifa, wamekataa hili. Vitabu hivyo vimepita kwenye akili za wanadamu, vimeandikwa kwa lugha ya wanadamu, viliandikwa na mikono ya wanadamu na kwa mtindo wake una tabia za kibinadamu .... Ni ya Binadamu, ila ni ya Kimungu.”[1]

Msomi mwingine wa Kikristo, Kenneth Cragg, Askofu wa Anglikana Yerusalemu, anasema:

“...Sio Agano Jipya ... Kuna kubadilishwa na kuhariri; kuna uzazi bora na ushuhuda. Injili zimekuja kupitia akili ya kanisa nyuma ya waandishi. Wanawakilisha uzoefu na historia...”[2]

"Inajulikana sana kuwa Injili ya kale ya Kikristo ilipitishwa kwa neno la mdomo na kuwa desturi hii ya mdomo ilisababisha nakala mbalimbali za maneno na matendo. Ni kweli kwamba nakala ya Kikristo ilipotaka kuandikwa iliendelea kuwa na maudhui tofauti ya maneno. Kwa kujitolea na kukusudia, mikononi mwa waandishi na wahariri.”[3]

“Ila, kwa hakika, kila kitabu cha Agano Jipya isipokuwa nyaraka nne kuu za Mtakatifu Paulo ambazo sasa ni mada zenye utata, na usahihi wake wenyewe unapimwapia.”[4]

Dkt.Lobegott Friedrich Konstantin Von Tischendorf, mmoja wa watetezi wa Kikristo wenye msimamo mkali wa Utatu yeye mwenyewe alivutwa kukubali kwamba:

“[Agano Jipya lilikuwa] katika vifungu vingi vilibadilishwa maana kiasi cha kutuacha tukiwa na maumivu ya kutokuwa na uhakika juu ya kile Mitume walikuwa wamekiandika kweli”[5]

Baada ya kuorodhesha mifano mingi ya taarifa zinazopingana katika Biblia, Dkt Frederic Kenyon anasema:

“Mbali na tofauti kubwa, kama hizi, hakuna aya ambayo haina utofauti wa kifungu katika nakala zingine [za maandiko ya zamani ambazo Biblia imekusanywa]. Hakuna mtu anayeweza kusema kuwa nyongeza au upungufu au mabadiliko ni mambo madogo tu”[6]

Katika kitabu hiki chote, utapata nukuu zingine nyingi kama hizo kutoka kwa wasomi wakuu wa Jumuiya za Wakristo. Acha tutosheke na hizi kwa sasa.

Wakristo, kwa ujumla, ni watu wazuri na wenye adabu, na imani zao zinaimarika ndivyo wao wanavyokuwa. Hii inathibitishwa katika Kurani Tukufu.

“...na utawakuta walio karibu mno kwa mapenzi ni wale wanao sema: Sisi ni Manasara. Hayo ni kwa sababu wapo miongoni mwao makasisi na wamonaki, na kwa sababu wao hawafanyi kiburi. Na wanaposikia yaliyo teremshwa kwa Mtume utaona macho yao yanachururika machozi kwa sababu ya Haki waliyo itambua. Wanasema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini. Basi tuandike pamoja na wanao shuhudia.’” (Kurani 5:82-83)

"Matoleo" yote ya Biblia kabla ya toleo lililorekebishwa la 1881 zilitegemea "Nakala za Kale" (zile zilizo kati ya miaka mia tano hadi sita baada ya Yesu). Waangalizi wa Matoleo yaliyorekebishwa (RSV) 1952 walikuwa wasomi wa kwanza wa kibiblia kupata "nakala za kale ZAIDI" ambazo zimetoka miaka mia tatu hadi nne baada ya Kristo. Ni jambo la busara kwetu kukubali kwamba nakala ya karibu zaidi katika chanzo ndivyo ilivyo halisi zaidi. Ngoja tuone maoni ya Jumuiya ya Wakristo ni yapi kuhusu toleo la Biblia lililorekebishwa zaidi (lilirekebishwa mnamo 1952 na tena mnamo 1971):

“Toleo bora kabisa ambalo limetolewa katika karne ya sasa ”- (Gazeti la Kanisa la England)

“Tafsiri mpya kabisa ya wasomi wa hali ya juu kabisa ”- (Times literary supplement)

“Tabia zinazopendwa zaidi za toleo lililoidhinishwa pamoja na usahihi mpya wa tafsiri ”- (Life and Work)

“Tafsiri sahihi zaidi na ya karibu zaidi ya ile asili” - (The Times)

Wachapishaji wenyewe (Collins) wanataja kwenye ukurasa wa 10 wa maelezo yao:

"Biblia hii (RSV) ni zao la wasomi thelathini na wawili wakisaidiwa na kamati ya ushauri inayowakilisha madhehebu hamsini yanayoshirikiana"

Ngoja tuone wasomi hawa wa Kikristo thelathini na wawili wa hali ya juu wanaoungwa mkono na madhehebu ya Kikristo yanayoshirikiana wanasema nini juu ya Toleo lililothibitishwa (AV), au kama inavyojulikana zaidi, King James Version (KJV). Katika dibaji ya RSV 1971 tunapata yafuatayo:

“...Hata hivyo Toleo la King James lina kasoro za KABURI..”

Wanaendelea kututahadhalisha kuwa:

"Kwamba kasoro hizi ni NYINGI SANA NA KUBWA SANA zinazohitaji marekebisho“

Mashahidi wa Yehova katika Jarida lao la "AWAKE" la tarehe 8 Septemba 1957 walichapisha kichwa kifuatacho: "Makosa 50,000 katika Biblia" ambapo wanasema".. pengine kuna makosa 50,000 katika Biblia ... makosa ambayo yameingia kwenye maandishi ya Biblia ... 50,000 ni makosa makubwa kama haya ...”Baada ya haya yote, hata hivyo, wanaendelea kusema:" ... kwa ujumla Biblia yote ipo sahihi." Ngoja tuangalie machache tu ya makosa haya.



Rejeleo la maelezo:

[1] W Graham Scroggie, uk. 17

[2] Wito wa Minaret, Kenneth Cragg, uk 277

[3] Maoni ya Peake juu ya Biblia, uk. 633

[4] Encyclopaedia Brittanica, 12th Ed. Vol. 3, uk. 643

[5] Siri za Mlima Sinai, James Bentley, uk. 117

[6] Biblia Yetu na Hati za Kale, Dr. Frederic Kenyon, Eyre and Spottiswoode, uk. 3

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.