Mazungumzo katika Pepo na Jahannam (sehemu ya 1 kati ya 3): Kuzungumza na Malaika

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Wenzetu wa daima watakachotuambia tunapoingia katika makao yetu ya milele.

  • Na Aisha Stacey (© 2012 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 11 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 25 Jul 2022
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,324 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

conversationinParadise.jpgTunaanza na mfululizo mpya wa makala kuhusu mazungumzo yanayotokea Peponi na Jahannamu. Tunatazamia kuwa, kwa kukumbushana tuliyo ambiwa kuhusu Pepo na Jahannamu, tutaweza kuona na kufikiria matukio yatakayofanyika tutakapo kutana na makao yetu ya milele katika Akhera. Kwa nini Mungu anatuambia kuhusu mazungumzo haya?

Kwa nini Mungu anatuambia kuhusu mazungumzo haya? Qur'ani imejaa sio tu maelezo ya Bustani za Mbinguni na Jahannamu, lakini pia mazungumzo, majadiliano na malumbano ya kimantiki. Matukio kama hayo yanaporudiwa tena na tena ni dalili kwamba Mungu anasema, “kuweni makini!” Kwa hivyo inatupasa kufanya hivyo tu, tutafakari vizuri kwa matumaini ya kuingia makao ya neema yanayojulikana kama Pepo, au tujilinde na Moto wa Jahannamu. Habari hurudiwa tena na tena ili kutufanya tufikirie vizuri kwa muda mrefu.

Katika makala zifuatazo tutaangalia aina kadhaa za mazungumzo. Mazungumzo baina ya Malaika na watu wa Peponi, na watu wa Jahannamu, na mazungumzo baina ya watu wa Peponi na wa Jahannamu na familia zao, na mazungumzo ya Mwenyezi Mungu na watu wa Pepo na wa Jahannamu. Mbali na hayo tutaangalia pia yale wanayo sema watu wa peponi na wa Jahannamu baina yao, kati yao wenyewe na majadiliano yao ya ndani. Tuanze na mazungumzo baina ya Malaika na watu wa Akhera.

Mazungumzo na Malaika

Malaika hukaa nasi tangu mwanzo wa maisha yetu hadi mwisho. Wana wajibu wa kupumua roho kwa mtoto mchanga akiwa tumboni, wanaandika matendo yetu mema na mabaya na hutoa roho kutoka miili yetu wakati wa kufa. Tunapoingia makao yetu ya milele, maisha yetu ya baadaye, wako pamoja nasi na tutaweza kuzungumza nao.

Watu wa Mabustani Za Mbinguni

Makao ya milele ya wale ambao wameishi maisha yao kwa subira katika nyakati za dhiki, na wakajitahidi kuwa wema kwa nyakati za shida na wema, ni Bustani za Mbinguni za milele zinazojulikana kama Jannah. Na watakapo ingia na kuishi milele kwenye nyumba zao mpya katika Bustani za Mbinguni, Malaika watawasalimu. Hao ndio mabawabu wa Peponi, na watasema: 'Ingieni kwa amani kwa sababu ya kusubiri kwenu!' Bustani za Mbinguni ni pahali pa utulivu wa milele na radhi za kudumu.

Na walio mcha Mola wao Mlezi wataongozwa kuendea Peponi kwa makundi, mpaka watakapo fikilia, nayo milango yake imekwisha funguliwa. Walinzi wake watawaambia: Salaam Alaikum, Amani iwe juu yenu! Mmet'ahirika. Basi ingieni humu mkae milele.” (Kurani 39:73)

Hisia zote za maumivu zitaondolewa kwenye nyoyo zao. Watawaitikia malaika kwa kumsifu Mwenyezi Mungu, na mazungumzo yanaendelea.

“… Alhamdulillah! Kuhimidiwa ni kwa Mwenyezi Mungu, ambaye aliye tuhidi kufikia haya. Wala hatukuwa wenye kuhidika wenyewe ingeli kuwa Mwenyezi Mungu hakutuhidi. Hakika Mitume wa Mola wetu Mlezi walileta Haki. Na watanadiwa kwamba: Hiyo ndiyo Pepo mliyo rithishwa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyafanya.” (Kurani 7:43)

Watu wa Motoni

Mazungumzo yatakayofanyika baina ya watu wa Jahannamu na Malaika yatakuwa tofauti kabisa. Wakaazi wa Jahannamu watakuwa na hali tofauti kabisa. Badala ya kusubiri kwa shauku kuingia katika makaazi yao ya milele, watu wa Jahannam watalazimishwa na kuvutwa na Malaika wasimamizi wa Moto. Na watakapotupwa motoni, Malaika watasema: Je! Hakukujieni mwonyaji?

Inakaribia kupasuka kwa hasira. Kila mara likitupwa kundi humo walinzi wake huwauliza: Kwani hakukujieni mwonyaji? Watasema: Kwani! Ametujia mwonyaji, lakini tulimkadhibisha, na tukasema: Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote. Nyinyi hamumo ila katika upotovu mkubwa! Na watasema: Lau kuwa tungeli sikia, au tungeli kuwa na akili, tusingeli kuwa katika watu wa Motoni!” (Kurani 67:8-10)

Hata hivyo hii si mara ya kwanza wakazi hawa wa moto walifanya mazungumzo na malaika. Malaika wa mauti na wasaidizi wake wanapo kusanyika ili waondoe nafsi za watu hawa, watawauliza wako wapi mlio waabudu badala ya Mwenyezi Mungu? Kwa sababu katika hatua hii ya maisha ya mtu sanamu zake hazitakuwepo.

…mpaka watakapo wafikia wajumbe wetu kuwafisha, watawaambia: Wako wapi mlio kuwa mkiwaomba badala ya Mwenyezi Mungu? Watasema: Wametupotea! Na watajishuhudia wenyewe kwamba walikuwa makafiri. (Kurani 7:37)

Baada ya muda fulani wakazi wa Jahannamu wanaanza kupoteza matumaini yote. Wamekuwa wakimwomba Mwenyezi Mungu, lakini hawapokei jibu. Hivyo wataanza kuwaomba Malaika ambao ndio mabawabu. Mwombeni Mola wenu Mlezi atupunguzie adhabu yetu. Malaika hujibu kwa maneno ambayo huwakatisha tamaa kabisa.

Na walio Motoni watawaambia walinzi wa Jahannamu: Mwombeni Mola wenu Mlezi atupunguzie walau siku moja ya adhabu. Nao watasema: Je! Hawakuwa wakikufikieni Mitume wenu kwa hoja zilio wazi? Watasema: Kwani? Watasema: Basi ombeni! Na maombi ya makafiri hayawi ila ni kupotea bure.… (Kurani 40:49-50)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.