Safari ya Kuelekea Akhera (sehemu ya 8 kati ya 8): Hitimisho

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Baadhi ya sababu za kuwepo Pepo na Moto.

  • Na Imam Mufti (co-author Abdurrahman Mahdi)
  • Iliyochapishwa mnamo 14 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 1
  • Imetazamwa: 3,097 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Journey_into_the_Hereafter_(part_8_of_8)_001.jpgMuhammad, Mtume wa Uislamu, aliyefariki mwaka 632, alisimulia:

"Dunia hii ni gereza kwa Muumini, lakini kwa kafiri ni Pepo. Na kwa kafiri, Akhera itakuwa gereza, lakini kwa Muumini itakuwa ni Pepo yake."

Wakati mmoja, katika kipindi cha mwanzo cha Uislamu, Mkristo maskini alitokea kwa mmoja wa wanazuoni wakubwa wa Uislamu, ambaye wakati huo alikuwa amepanda farasi mzuri na aliyevaa nguo nzuri. Mkristo huyo alimsomea Muislamu mwenye mali Hadithi iliyonukuliwa hapo juu, kabla ya kutoa maoni: "Lakini mimi nasimama mbele yako nikiwa sio Muislamu, maskini na fukara katika dunia hii, ilhali wewe ni Muislamu, tajiri na aliyefanikiwa.” Mwanachuoni wa Uislamu akamjibu: “Hakika ndivyo hivyo. Lakini lau ungejua hakika ya yale yanayoweza kukungojea (ya adhabu ya milele) huko Akhera, ungejiona kuwa wewe sasa uko Peponi kwa kulinganisha. Na lau ungejua hakika ya yale yanayoweza kuningojea (ya raha ya milele) huko Akhera, ungeniona kuwa mimi sasa niko gerezani kwa kulinganisha."

Kwa hivyo, ni kutokana na rehema kubwa na uadilifu wa Mwenyezi Mungu kwamba aliumba Mbingu na Jehanamu. Ujuzi wa Moto wa Jehanamu unatumika kumzuilia mwanadamu asitende maovu na wakati huo huo kuchungulia kwenye hazina za Peponi kunamchochea kutenda matendo mema na kuwa mwadilifu. Wale waliomkadhibisha Mola wao Mlezi na wakatenda maovu na hawakutubia, wataingia Jehanamu, mahali pa maumivu ya hakika na mateso. Wakati malipo ya uadilifu ni pahali pasipofikirika uzuri na ukamilifu wake, nayo ni Pepo ya Mungu.

Mara kwa mara, watu hushuhudia wema wa nafsi zao wenyewe kwa kudai kwamba wema wowote wanaoufanya ni kwa njia safi na pekee ya upendo wa kweli wa Mungu au kuishi kulingana na kanuni za maadili na wema wa ulimwengu wote, na kwa ajili hiyo, hawahitaji fimbo au karoti yoyote (ya kuwalazimisha au kuwashawishi kuyatenda mema). Lakini Mungu anapozungumza na mwanadamu ndani ya Kurani, hufanya hivyo akijua ugeugeu wa nafsi ya mwanadamu. Furaha za Peponi ni furaha halisi, za kimwili na zinazoonekana. Mwanadamu anaweza kuanza kufahamu jinsi ambavyo uchu wa kutaka vyakula, mavazi na makazi ya Peponi vilivyo kamilifu, vingi na visivyoisha, kuwa ni halisi kwa sababu anafahamu jinsi vitu hivyo vinaweza kuridhisha na kuwa vitamu katika ulimwengu halisia wa sasa.

"Watu wamepambiwa kupenda matamanio ya wanawake, na wana, na mirundo ya dhahabu na fedha, na farasi asili, na mifugo, na mashamba. Hayo ni starehe ya maisha ya duniani; na kwa Mwenyezi Mungu ndio kwenye marejeo mema." (Kurani 3:14)

Vivyo hivyo, mwanadamu anaweza kuanza kufahamu jinsi Moto wa mateso na wa kuogofya unavyoweza kuwa hasa kwa sababu anajua jinsi uchomaji wa moto unavyoweza kuwa mbaya sana katika ulimwengu huu. Kwa hivyo, safari ya roho baada ya kifo, kama ilivyoelezwa kwetu kwa kina na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu zimshukie, inapaswa, kwa vyovyote vile, kutuchochea sisi wanadamu wote kutambua lengo tukufu: nalo ni kumwabudu na kumtumikia Muumba wetu kwa upendo wa dhati usio na ubinafsi, na kunyenyekea na kushukuru. Baada ya yote,

"...nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu..." (Kurani 98:5)

Lakini, kuhusu yale makundi mengi miongoni mwa wanadamu ambayo, katika zama zote, yalipuuza wajibu wao wa kimaadili kwa Mola wao Mlezi na wanadamu wenzao, basi yasisahau kwamba:

"Kila nafsi itaonja mauti. Na bila ya shaka mtapewa ujira wenu kamili Siku ya Kiyama. Na atakayeepushwa na Moto na akatiwa Peponi basi huyo amefuzu. Na maisha ya dunia si kitu ila ni starehe ya udanganyifu." (Kurani 3:185)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.