Safari ya Kuelekea Akhera (sehemu ya 7 kati ya 8): Kafiri na Moto

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi Moto wa Jehanamu utawapokea makafiri.

  • Na Imam Mufti (co-author Abdurrahman Mahdi)
  • Iliyochapishwa mnamo 14 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,370 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Jehanamu itawapokea makafiri kwa ghadhabu yake na kishindo chake.

"…na Sisi tumemuandalia Moto mkali kabisa huyo mwenye kuikanusha Saa. Ule Moto ukiwaona tangu mahali mbali wao watasikia hasira yake na mngurumo wake." (Kurani 25:11-12)

Watakapoikaribia, watatazamia kufungwa pingu na hatima yao ni kufanywa kuni.

"Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali." (Kurani 76:4)

"Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unaowaka kwa ukali kabisa!" (Kurani 73:12)

Malaika watakimbia kutii amri ya Mwenyezi Mungu ya kumkamata na kumfunga pingu:

"(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!" (Kurani 69:30)

"…na Tutaweka makongwa shingoni mwao waliokufuru..." (Kurani 34:33)

Atafungwa kwa minyororo...

"…mnyororo wenye [kipimo cha] urefu wa dhiraa sabini!" (Kurani 69:32)

...ataburutwa:

"Zitakapokuwa pingu shingoni mwao na minyororo, huku wanabururwa." (Kurani 40:71)

Wakiwa wamefungwa chini, kwa minyororo, na kuburutwa ili watumbukizwe Motoni, watasikia hasira ya Moto.

"Na kwa waliomkufuru Mola wao Mlezi ipo adhabu ya Jehanamu. Na ni marejeo maovu yalioje hayo! Watakapotupwa humo watausikia mngurumo wake na huku inafoka..." (Kurani 67:6-8)

Kwa kuwa watakokotwa kwenye uwanja mkubwa wa kukusanywa, wakiwa uchi na wenye njaa, watawaomba watu wa Peponi maji:

"Na watu wa Motoni watawaita watu wa Peponi: ‘Tumimieni maji, au chochote alichokuruzukuni Mwenyezi Mungu.’ Nao watasema: ‘Hakika Mwenyezi Mungu ameviharimisha hivyo kwa makafiri.’" (Kurani 7:50)

Wakati huo huo waumini ndani ya Pepo wakipokelewa kwa heshima, kustareheshwa, na kuhudumiwa kwa karamu za ladha, naye kafiri atakula akiwa ndani ya Moto.

"Kisha nyinyi, mliopotea, mnaokanusha, kwa yakini mtakula mti wa Zakumu. Na kwa mti huo mtajaza matumbo." (Kurani 56:51-53)

Zakumu: mti ambao mizizi yake iko chini ya Jahannamu na ambayo inatawanya matawi yake sehemu nyingine; matunda yake yanafanana na vichwa vya mashetani:

"Je, kukaribishwa hivi [Peponi] si ndio bora, au mti wa Zakumu? Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa waliodhulumu. Hakika huo ni mti unaotoka katikati ya Jehanamu. Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashetani. Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo." (Kurani 37:62-66)

Waovu watakuwa na mlo mwingine wa kula, mwingine ambao hukaba koo,[1] na mwingine kama vichaka vikavu, vyenye miiba.[2]

"Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni. Chakula hicho hawakili ila wakosefu." (Kurani 69:36-37)

Na kufuatanisha vyakula vyao vya kusikitisha, ni vinywaji vya mchanganyiko baridi sana wa usaha wao wenyewe, damu, jasho na usaha wa jeraha[3] pamoja na maji yanayochemka, yanayotokota na kuteketeza, ambayo huyeyusha matumbo yao;

"…na wakinyweshwa maji yanayochemka ya kuwakata matumbo yao?" (Kurani 47:15)

Mavazi ya wakaazi wa Motoni yametengenezwa kwa moto na lami.

"...Basi waliokufuru watakatiwa nguo za moto, na yatamiminwa juu ya vichwa vyao maji yanayochemka." (Kurani 22:19)

"Nguo zao zitakuwa za lami, na Moto utazigubika nyuso zao." (Kurani 14:50)

Viatu vyao,[4] kitanda, na dari vivyo hivyo vitatengenezwa kwa moto;[5] adhabu inayozunguka mwili mzima, kutoka kichwa kisichojali hadi kidole cha mguu kinachovuka mipaka:

"Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayochemka." (Kurani 44:48)

"Siku itakapowafunika adhabu hiyo kutoka juu yao na chini ya miguu yao, na itasemwa: ‘Onjeni hayo mliyokuwa mkiyatenda!’" (Kurani 29:55)

Adhabu yao katika Jehanamu itatofautiana kulingana na ukafiri wao na madhambi mengineo.

"Hasha! Atavurumishwa katika Hutwama. Na nani atakujuvya ni nini Hutwama? Moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa. Ambao unapanda nyoyoni. Hakika huo utafungiwa nao, kwenye nguzo zilizonyooshwa." (Kurani 104:4-9)

Kila wakati ngozi ikiungua, itabadilishwa na ngozi mpya:

"Hakika wale waliozikataa ishara Zetu tutawaingiza Motoni. Kila zitakapowiva ngozi zao tutawabadilishia ngozi nyengine ili waionje hiyo adhabu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hekima." (Kurani 4:56)

Mbaya zaidi ni kuwa, adhabu itaendelea kuongezeka:

"Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!" (Kurani 78:30)

Athari ya kisaikolojia ya kuadhibiwa huku itakuwa kubwa sana. Itakuwa adhabu kali sana hata watakaoteseka kwa maumivu yake watapiga kelele ili iongezewe waliosababisha wao kupotea:

"Waseme: ‘Mola wetu Mlezi! Aliyetusabibisha haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni.’" (Kurani 38:61)

Wenye kuthubutu watafanya jaribio lao la kwanza kutoroka, lakini:

"Na kwa ajili yao yatakuwapo marungu ya chuma. Kila wakitaka kutoka humo kwa sababu ya uchungu watarudishwa humo humo, na wataambiwa: ‘Onjeni adhabu ya kuungua!’" (Kurani 22:21-22)

Baada ya kushindwa mara kadhaa, watatafuta msaada kutoka kwa Ibilisi, Shetani Mkuu mwenyewe.

"Na Shetani atasema itakapokatwa hukumu: ‘Hakika Mwenyezi Mungu alikuahidini ahadi ya kweli. Nami nalikuahidini; lakini sikukutimizieni. Na sikuwa na mamlaka juu yenu, isipokuwa nilikuiteni, nanyi mkaniitikia. Basi msinilaumu mimi, bali jilaumuni wenyewe. Mimi siwezi kuwa mtetezi wenu, wala nyinyi hamwezi kuwa watetezi wangu. Hakika mimi nilikataa tangu zamani kunishirikisha na Mwenyezi Mungu. Hakika madhalimu watakuwa na adhabu chungu.’" (Kurani 14:22)

Wakiwa wamevunjika moyo na Shetani, watawaelekea malaika walindao Jehanamu ili wawapunguzie adhabu, hata kama kwa siku moja tu:

"Na walio Motoni watawaambia walinzi wa Jehanamu: ‘Mwombeni Mola wenu Mlezi atupunguzie walau siku moja ya adhabu.’" (Kurani 40:49)

Wakingoja majibu kwa muda ambao Mungu apendavyo, walinzi watarudi na kuuliza:

"Nao watasema: ‘Je, hawakuwa wakikufikieni mitume wenu kwa hoja zilizo wazi?’ Watasema: ‘Kwani?’ Watasema: ‘Basi ombeni! Na maombi ya makafiri hayawi ila ni kupotea bure.’" (Kurani 40:50)

Wakiwa wamepoteza matumaini ya kupunguziwa adhabu, watatafuta njia ya kuuawa. Wakati huu watamgeukia Mlinzi Mkuu wa Jehanamu, malaika aitwaye Malik, wakimsihi kwa muda wa miaka arobaini:

"Nao watapiga kelele waseme: ‘Ewe Malik! Na atufishe Mola wako Mlezi!...’" (Kurani 43:77)

Jibu la mkato la kupinga kwake baada ya miaka elfu litakuwa:

"…Naye aseme: ‘Hakika nyinyi mtakaa humo humo!" (Kurani 43:77)

Hatimaye watarejea kwa Yule Ambaye walikataa kurejea kwake wakiwa duniani, wakiomba fursa ya mwisho:

"(Watasema) ‘Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu [upotofu] wetu na tukawa watu tuliopotea. Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena [maovu], basi kweli sisi ni wenye kudhulumu.’" (Kurani 23:106-107)

Jibu la Mungu litakuwa hivi:

"...‘Tokomeeni humo, wala msinisemeze." (Kurani 23:108)

Maumivu kutoka kwa majibu haya yatakuwa mabaya zaidi kuliko mateso yao ya moto. Kwani kafiri atajua kukaa kwake Motoni ni milele, na kutokuwepo kwake Peponi ni hakika na ni uamuzi wa mwisho:

"Hakika wale waliokufuru na wakadhulumu hawi Mwenyezi Mungu kuwasamehe wala kuwaongoa njia. Isipokuwa njia ya Jehanamu. Humo watadumu milele. Na hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi." (Kurani 4:168-169)

Kunyimwa na huzuni kubwa zaidi kwa asiyeamini itakuwa ya kiroho: atazibwa na kunyimwa kumuona Mungu:

"Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi." (Kurani 83:15)

Kama vile walivyokataa “kumwona” katika maisha haya, watatengwa na Mungu katika maisha yajayo. Waumini watawadhihaki.

"Basi leo walioamini ndio watawacheka makafiri, nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia. Je, makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyokuwa wakiyatenda?" (Kurani 83:34-36)

Kukata tamaa na huzuni yao kamili itafikia kilele wakati kifo kitakapoletwa kama umbo la kondoo dume na kuchinjwa mbele yao, kuashiria kwamba hakuna kimbilio litakalopatikana baada ya uamuzi wa mwisho wa maangamizo.

"Na waonye, (Ewe Muhammad), siku ya majuto itakapokatwa amri; nao wamo katika ghafla, wala hawaamini!" (Kurani19:39)



Rejeleo la maelezo:

[1]Kurani 72:13.

[2]Kurani 88:6-7.

[3] Kurani 78:24-25.

[4] Saheeh Muslim.

[5] Kurani 7:41.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.