Safari ya Kuelekea Akhera (sehemu ya 5 kati ya 8): Kafiri ndani ya Kaburi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Ufafanuzi wa maisha ndani ya kaburi kuanzia kifo hadi Siku ya Hukumu kwa kafiri aliyekanusha.

  • Na Imam Mufti (co-author Abdurrahman Mahdi)
  • Iliyochapishwa mnamo 14 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 1
  • Imetazamwa: 3,903 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Journey_into_the_Hereafter_(part_5_of_8)_001.jpgMauti yanapomkaribia kafiri muovu, anafanywa kuhisi kitu cha joto la Moto wa Jehanamu. Mwonjo huu wa kile kitakachokuja humfanya aombe kupewa nafasi ya pili duniani kufanya yale mema ambayo alijua angepaswa kuyafanya. Ole wake! Ombi lake litakuwa bure.

"Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: ‘Mola wangu Mlezi! Nirudishe (duniani). Ili nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha.’ Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi (maisha ya Barzakhi) mpaka siku watakapofufuliwa." (Kurani 23:99-100)

Ghadhabu za Mungu na adhabu huwasilishwa kwa roho mbaya na malaika wabaya sana, weusi ambao hukaa mbali nayo:

"Pokea habari za kusikitisha za maji yanayochemka, usaha kutoka kwa jeraha, na mateso mengi kama hayo." (Ibn Majah, Ibn Katheer)

Roho iliyokufuru haitarajii kukutana na Mola wake Mlezi, kama Mtume alivyoeleza:

"Inapokaribia wakati wa kifo cha kafiri, hupokea habari mbaya za adhabu ya Mwenyezi Mungu na malipo yake, ambapo hakuna kinachochukiza zaidi kwake kuliko yale yaliyo kabla yake. Kwa hiyo, anachukia kukutana na Mungu, na Mungu pia anachukia kukutana naye." (Saheeh Al-Bukhari)

Mtume pia alisema:

"Yeyote anayependa kukutana na Mungu, Mungu hupenda kukutana naye, na yeyote anayechukia kukutana na Mungu, Mungu huchukia kukutana naye." (Saheeh Al-Bukhari)

Malaika wa mauti anakaa kichwani mwa kafiri katika kaburi lake na kusema: "Nafsi mbaya, toka mwilini kwa hasira ya Mwenyezi Mungu" huku akiinyakua roho nje ya mwili.

"...Na lau ungeliwaona madhalimu wanavyokuwa katika mahangaiko ya mauti, na malaika wamewanyooshea mikono wakiwambia: ‘Zitoeni roho zenu! Leo mtalipwa adhabu ya fedheha kwa sababu ya mliyokuwa mkiyasema juu ya Mwenyezi Mungu yasiyo ya haki, na mlivyokuwa mkizifanyia kiburi ishara zake.’" (Kurani 6:93)

"Na laiti ungeliona malaika wanapowafisha wale waliokufuru wakiwapiga nyuso zao na migongo yao, na kuwaambia: ‘Ionjeni adhabu ya Moto!’" (Kurani 8:50)

Nafsi mbaya huacha mwili kwa shida sana, inayotolewa na malaika kama vibaniko huvutwa kupitia pamba yenye unyevu.[1] Kisha Malaika wa Mauti huikamata roho na kuiweka kwenye gunia lililofumwa kwa nywele ambalo linatoa uvundo uliooza, kama uchafu wa kukirihisha wa mfu uliooza wenye harufu mbaya zaidi inayopatikana duniani. Kisha malaika huichukua roho juu akipita kundi jingine la malaika wanaomuuliza: "Nani huyu roho mbaya?" na atawajibu: "Fulani wa fulani, mwana wa fulani na fulani." - akitumia majina mabaya sana ambayo aliwahi kuitwa wakati alipokuwa duniani. Kisha, anapoletwa kwenye mbingu ya chini kabisa, ombi linatumwa kwamba lango lake lifunguliwe, lakini ombi hilo linakataliwa. Mtume alipokuwa akielezea matukio haya, na alipofikia hapa, alisoma:

"...hawafunguliwi milango ya mbingu, wala hawataingia Peponi mpaka apite ngamia katika tundu la sindano..." (Kurani 7:40)

Mungu atasema: "Rekodi kitabu chake katika Sijjin katika ardhi ya chini kabisa."

…na roho yake itatupwa chini. Katika hatua hii, Mtume, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu zimshukie, alisoma:

"...Na anayemshirikisha Mwenyezi Mungu ni kama kwamba ameporomoka kutoka mbinguni, kisha ndege wakamnyakua au upepo ukamtupa pahala mbali." (Kurani 22:31)

Kisha nafsi ovu itarejeshwa kwenye mwili wake na wale malaika wawili wa kutisha, Munkar na Nakir, watakuja humo kwa ajili ya kumhoji. Baada ya kumfanya aketi, watauliza:

Munkar na Nakir: "Nani Mola wako?"

Roho ya Asiyeamini: "Aah, aah, sijui."

Munkar na Nakir: "Nini dini yako?"

Roho ya Asiyeamini: "Aah, aah, sijui."

Munkar na Nakir: "Unasemaje kuhusu huyu mwanamume (Muhammad) aliyetumwa kwenu?"

Roho ya Asiyeamini: "Aah, aah, sijui."

Akiwa ameshindwa mtihani wake, kichwa cha kafiri kitapigwa kwa nyundo ya chuma kwa nguvu nyingi ya kishindo hivi kwamba ingebomoa mlima. Kilio kitasikika kutoka mbinguni: "Amesema uongo, basi mkunjulieni mazulia ya Jehanamu, na mfungulie mlango wa kuingia Motoni."[2] Sakafu ya kaburi lake litawashwa moto kidogo mkali wa Jehanamu, na kaburi lake litafanywa kuwa jembamba na kubanwa, kiasi cha mbavu zake kuunganika mwili wake unapopondwa.[3] Kisha kiumbe chenye sura mbaya, kilichovaa nguo mbaya na kutoa harufu mbaya ya kukirihisha kitaijia nafsi iliyokufuru na kusema: "Uwe na huzuni kwa yale yanayokuchukiza, kwani hii ndiyo siku yako uliyoahidiwa." Kafiri atauliza: "Wewe ni nani, mwenye uso mbaya na kuleta maovu?"Kile kiumbe kibaya kitajibu:"Mimi ni matendo yako maovu!"Kisha kafiri ataonjeshwa majuto ya uchungu huku akionyeshwa yale yangekuwa makazi yake Peponi - lau angeishi maisha mema ya uadilifu - hayo yatatendeka kabla ya kufunguliwa mlango kwa ajili yake kila asubuhi na jioni ukimuonyesha makazi yake halisi ya Motoni.[4]Mwenyezi Mungu anataja katika Kitabu Chake jinsi watu waovu wa Firauni wanavyoteseka wakati huu kwa kufichuliwa Jehanamu kutoka ndani ya makaburi yao:

"Wanaonyeshwa Moto asubuhi na jioni. Na itakapofika Saa ya Kiyama patasemwa: ‘Waingizeni watu wa Firauni katika adhabu kali kabisa!’" (Kurani 40:46)

Akiwa ameingiwa na hofu na chuki, wasiwasi na kukata tamaa, kafiri ndani ya kaburi lake ataendelea kuuliza: "Mola wangu Mlezi, usilete saa ya mwisho. Usilete saa ya mwisho."

Sahaba, Zaid b. Thabit, alisimulia jinsi, wakati Mtume Muhammad na Maswahaba zake walipokuwa wakipita kando ya baadhi ya makaburi ya washirikina, farasi wa Mtume alikurupuka na karibu kumwangusha. Kisha Mtume, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu zimshukie, akasema:

"Watu hawa wanateswa makaburini mwao, na lau si kwamba nyinyi mngeacha kuwazika wafu wenu, ningemuomba Mwenyezi Mungu awape masikizi ya kusikia adhabu ya kaburini ambayo mimi (na farasi huyu) huisikia." (Saheeh Muslim)



Rejeleo la maelezo:

[1] Al-Hakim, Abu Dawood, na wengine.

[2] Musnad Ahmad.

[3] Musnad Ahmad.

[4] Ibn Hibban.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.