Safari ya Kuelekea Akhera (sehemu ya 4 kati ya 8): Muumini na Pepo

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi wanavyopokelewa humo wenye kufaulu kufika Peponi kwa ajili ya imani.

  • Na Imam Mufti (co-author Abdurrahman Mahdi)
  • Iliyochapishwa mnamo 14 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,486 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Peponi

Waumini wataongozwa kuelekea kwenye milango minane mikuu ya Peponi. Huko, watapata mapokezi ya furaha ya kimalaika na kupongezwa kwa sababu ya kuwasili kwao salama na kuokoka na Jahannamu.

"Na waliomcha Mola wao Mlezi wataongozwa kuendea Peponi kwa makundi, mpaka watakapofikilia, nayo milango yake imekwishafunguliwa. Walinzi wake watawaambia: ‘Salaam Alaikum, [Amani iwe juu yenu]! Mmetwahirika. Basi ingieni humu mkae milele.’" (Kurani 39:73)

(Watu wema wataambiwa): "Ewe nafsi iliyotua! Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha. Basi ingia miongoni mwa waja wangu. Na ingia katika Pepo yangu." (Kurani 89:27-30)

Waliobora miongoni mwa Waislamu wataingia Peponi kwanza. Waliowema zaidi nao watapandishwa daraja za juu.[1]

"Na atakayemjia [Mwenyezi Mungu] naye ni muumini aliyetenda mema, basi hao ndio wenye vyeo vya juu." (Kurani 20:75)

"Na wa mbele [katika imani] watakuwa mbele [Akhera]. Hao ndio watakaokaribishwa [mbele kwa Mungu], katika Bustani zenye neema..." (Kurani 56:10-12)

Maelezo ya Kurani ya Pepo yanatupatia maono ya jinsi palivyo pahali pazuri sana. Nyumba ya milele ambayo itatimiza matamanio yetu yote mazuri, ishawishi hisia zetu zote, itupe kila kitu tunachoweza kutaka na mengine mengi zaidi. Mungu anaielezea Pepo Yake kuwa kama ardhi iliotengenezwa kwapoda au unga laini wa miski,[2] udongo wa zafarani,[3] matofali ya dhahabu na fedha, na changarawe za lulu na yakuti/ rubi/ marijani. Chini ya bustani za Peponi inapita mito ya maji inayong'aa, ya maziwa matamu, ya asali safi, na ya mvinyo usio na kilevi. Hema zilizo kwenye kingo zao ni mfano wa makuba ya lulu yaliyo wazi.[4] Nafasi nzima imejazwa mwangaza unaometameta, mimea yenye kutoa harufu nzuri na manukato ambayo yanaweza kunusika kutoka mbali.[5] Kuna makasri ya kifahari, majumba makubwa, mizabibu, mitende, mikomamanga,[6] myungiyungi na mikangazi ambayo mashina yake yametengenezwa kwa dhahabu.[7] Matunda yaliyoiva, mengi ya kila aina: jamii ya beri au vitole, jamii ya machungwa, aprikoti, zabibu, tikiti, mbwembwe; kila aina ya matunda, ya kitropiki na ya kigeni; chochote ambacho waumini wangeweza kutamani!

"…na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia..." (Kurani 43:71)

Kila Muumini atakuwa na mke mrembo sana, mchaji Mungu na msafi, aliyevaa mavazi maridadi; nakutakuwa na mengi zaidi katika ulimwengu mpya wa furaha ya milele, ng'aavu.

"Nafsi yoyote haijui waliyofichiwa katika hayo yanayofurahisha macho - ni malipo ya yale waliyokuwa wakiyatenda." (Kurani 32:17)

Pamoja na furaha za kimwili, Pepo pia itawapa wakazi wake hali ya furaha ya kihisia na kisaikolojia, kama Mtume alivyosema:

"Mwenye kuingia Peponi amebarikiwa maisha ya furaha; hatahisi huzuni kamwe, nguo zake hazitachakaa, na ujana wake hautafifia. Watu watasikia mwito wa kimungu: ‘Ninawapa hiba ya kwamba mtakuwa na afya njema na kamwe hamtaugua, mtaishi na kamwe hamtakufa, mtakuwa vijana na kamwe hamzeeka, mtakuwa na furaha na kamwe hamtahisi huzuni.’" (Saheeh Muslim)

Hatimaye, jambo litakalopendeza zaidi macho litakuwa kuona Uso wa Mwenyezi Mungu Mwenyewe. Kwa muumini wa kweli, kuuona utukufu wa Mungu ni kuwa ameshinda tuzo kuu.

"Zipo nyuso siku hiyo zitakazong'ara, zinamwangallia Mola wao Mlezi." (Kurani 75:22-23)

Hii ndiyo Pepo, makazi ya milele na mwisho wa safari ya muumini mwema. Tunamuomba Mwenyezi Mungu, Aliye Juu Zaidi, atufanye tustahiki kupata Pepo.



Rejeleo la maelezo:

[1]Sahih al-Jami.

[2]Saheeh Muslim

[3]Mishkat

[4]Saheeh Al-Bukhari

[5]Sahih al-Jami

[6]Kurani 56:27-32

[7]Sahih al-Jami

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.