Kusudi la Uumbaji (sehemu ya 1 ya 3): Utangulizi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Utangulizi wa swali la kutatanisha zaidi katika historia ya binadamu, na mjadala kuhusu vyanzo ambavyo vinaweza kutumika kupata jibu. Sehemu ya 1: Chanzo cha jibu.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 16 Jul 2023
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,772
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Utangulizi

The_Purpose_of_Creation_(part_1_of_3)_001.jpgMadhumuni ya uumbaji ni mada ambayo hutatanisha kila mwanadamu wakati fulani katika maisha yake. Kila mtu kwa wakati fulani au mwingine anajiuliza swali la “Kwa nini ninaishi?” au “Kwa nini niko hapa duniani?”

Utofauti na utata wa mifumo yanayowazunguka wanadamu na ulimwengu huonyesha kwamba lazima kuna Mkuu aliyewaumba. Kilichobuniwa kinaonyesha mbuni. Wanadamu wanapoona nyayo kwenye ufuo, wanaelewa kwamba kuna mtu alikuwa ametembea huko wakati fulani hapo awali. Hakuna mtu anayefikiria kwamba mawimbi kutoka baharini yalifunika mchanga na kwa bahati kuweka nyayo zinazoonekana hasa kufanana na nyayo za kibinadamu. Wanadamu pia huelewa kiasili kwamba waliletwa duniani ili kutimiza lengo fulani. Kwa kuwa tendo la kimakusudi ni zao la kiasili ya akili ya kibinadamu, binadamu huelewa kwamba aliyewaumba, mwenye hekima kuu, lazima amefanya hivyo kwa lengo maalum. Kwa hivyo, binadamu wanahitaji kujua kusudi la kuwepo kwao ili kuyaelewa maisha haya na kufanya kinacholeta manufaa kwao.

Hata hivyo, katika miaka yoye ya historia ya binadamu, kumekuwa na wachache miongoni mwa wanadamu ambao wamekanusha kuwepo kwa Mungu. Vipengele, kwa maoni yao, ni vya milele na wanadamu ni matokeo ya kibahati ya mchanganyiko wa ajali wa vipengele vyake. Kwa sababu hiyo, kulingana nao, swali la “Kwa nini Mungu alimuumba mwanadamu?” bado halina jibu. Kulingana na wao, hakuna madhumuni ya kuwepo kwa mwanadamu duniani. Hata hivyo, idadi kubwa ya wanadamu katika miaka yote ya historia ya wanadamu wameamini na kuendelea kuamini kuwepo kwa Muumba mkuu ambaye aliumba ulimwengu huu kwa lengo. Kwao ilikuwa ni muhimu kujua kuhusu Muumba na lengo ambalo aliwaumbia wanadamu.

Jibu

Ili kujibu swali la “Kwa nini Mungu aliumba mwanadamu?” ni lazima kwanza tujue ni kutoka kwa mtazamo upi swali linaulizwa. Kutokana na mtazamo wa Mungu ungemaanisha, “Ni nini kilichosababisha Mungu kuumba binadamu?” huku mtazamo wa kibinadamu ungemaanisha “Kwa nini Mungu aliumba binadamu?” Mitazamo yote mbili inawakilisha vipengele vya swali muhimu la “Kwa nini naishi?” ... vipengele vyote vya swali vitachunguzwa kulingana na taswira ya ufunuo wa Mungu. Hii sio mada inayoweza kukisiwa na wanadamu, kwa sababu kukisia kwa binadamu hakuwezi eleza ukweli wowote katika suala hili. Je, wanadamu wanaweza kueleza vipi ukweli wa kuwepo kwao wakati hawawezi kuelewa jinsi ubongo wao wenyewe au akili zao hufanya kazi? Kwa sababu hiyo, wanafalsafa wengi ambao wamekisia juu ya swali hili kwa miaka wamekuja na majibu yasiyohesabika, yote ambayo yanategemea mawazo ambayo hayawezi kuthibitishwa. Maswali juu ya mada hii yamesababisha hata wanafalsafa kadhaa kudai kwamba hatupo kikweli na kwamba ulimwengu wote ni fikra tu na sio halisi. Kwa mfano, mwanafalsafa wa Kigiriki Plato (428-348 KK) alisema kuwa ulimwengu wa kila siku wa kubadilika badilika, ambao mtu huja kujua kwa kutumia akili zake, sio ukweli wa msingi, lakini ni ulimwengu wa kivuli na sio halisi. Wengine wengi, kama ilivyoelezwa hapo awali, walidai na kuendelea kudai kwamba hakuna kusudi la kuumbwa kwa binadamu hata kidogo. Kulingana na wao, kuwepo kwa binadamu ni jambo la kibahati tu. Hatuwezi kuwa na lengo kama maisha yamebadilika kutokana na kipengele kisicho na uhai kilichokuja kuwa hai tu kwa bahati. Wanaodhaniwa kuwa 'binamu wa binadamu 'tumbili na nyani, hawasumbuliwi na maswali ya kuwepo kwao, basi kwa nini wanadamu wanapaswa kuwa na wasiwasi nao?

Ingawa watu wengi huweka swali la kwa nini tumeumbwa kando baada ya kutafakari kwa muda mfupi, ni muhimu sana kwa wanadamu kujua jibu. Bila ujuzi wa jibu sahihi, wanadamu hawawezi kutofautishwa na wanyama wengine waliowazunguka. Mahitaji ya wanyama na tamaa za kula, kunywa na kuzaa huanza kuwa lengo la kuwepo kwa binadamu, na juhudi za kibinadamu zinalenga uwanja huu mdogo. Utimizaji wa mahitaji ya kimwili unapokuwa lengo muhimu zaidi katika maisha, kuwepo kwa binadamu kunakosa maana na mwanadamu huwa na kiwango kama cha wanyama wa chini kabisa. Wanadamu watatumia vibaya akili zao walizopewa na Mungu wanapokosa kuelewa lengo lao la kuishi. Akili ya binadamu itatumia uwezo wake kuunda madawa ya kulevya na mabomu na itajihusisha na uasherati, ngono, ushoga, urogi, kujiua, nk. Kwa kutoelewa madhumuni ya maisha, kuwepo kwa binadamu kunapoteza maana yake yote na hivyo hupotea, na malipo ya uzima wa milele wa Furaha katika Akhera hupotea kabisa. Kwa hivyo, ni muhimu sana kwa mwanadamu kujibu kwa usahihi swali la “Kwa nini tuko hapa?”

Binadamu mara nyingi hugeuka kwa wanadamu wenzao ili kupata majibu. Hata hivyo, mahali pekee ambapo majibu ya wazi na sahihi ya maswali haya yanaweza kupatikana ni katika vitabu vya ufunuo wa Mungu. Ilikuwa ni dharura Mungu aeleze lengo la maisha kwa binadamu kupitia manabii Wake, kwa sababu binadamu hawawezi kupata majibu sahihi kivyao. Manabii wote wa Mungu waliwafundisha wafuasi wao majibu ya swali la “Kwa nini Mungu aliumba mwanadamu?”

Mbaya Nzuri zaidi

Kusudi la Uumbaji (sehemu ya 2 ya 3): Jibu la Kiyahudi-Kikristo

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Utangulizi kwa swali la kutatiza zaidi katika historia ya binadamu, na mjadala kuhusu vyanzo ambavyo vinaweza kutumika kupata jibu. Sehemu ya 2: Mtazamo katika Biblia na imani ya Kikristo kuhusu mada hii.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,934
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Maandishi ya Kiyahudi na ya Kikristo

Utafiti katika Biblia humwacha mtafutaji wa ukweli mwaminifu akiwa amechanganyikiwa. Agano la Kale linaonekana kujihusisha zaidi na sheria na historia ya mwanadamu wa kwanza na Wayahudi kuliko kujibu swali muhimu kuhusu uumbaji wa binadamu. Katika kitabu cha Mwanzo, Mungu anaumba ulimwengu na Adamu na Hawa kwa siku sita na 'anapumzika' kutoka kazi yake siku ya saba. Adamu na Hawa wanavunja amri za Mungu na wanaadhibiwa, na mwana wao Kaini anamwua mtoto wao mwingine Abeli na kuenda kuishi katika nchi ya Nodi. Naye Mungu 'akasikitika' kwamba alikuwa amemuumba mwanadamu! Kwa nini majibu hayapo hapo kwa maneno wazi na yasiyo na shaka? Kwa nini lugha yote ni ya kimajazi tu, na huacha msomaji akikisia maana yake? Kwa mfano, katika Mwanzo 6:6 inasemwa:

“Binadamu walipozidi kuongezeka duniani na kuzaa wasichana, watoto wa kiume wa Mungu waliwaona hao wasichana wa watu kuwa ni wazuri, wakawachukua wale waliowapenda kuwa wake zao.”

Hawa “wana wa Mungu” ni kina nani? Kila madhehebu ya Kiyahudi na kila moja kati ya madhehebu mengi ya Ukristo yaliyowafuata yana maelezo yao wenyewe. Ni nini tafsiri sahihi? Ukweli ni kwamba kusudi la uumbaji wa mwanadamu lilifundishwa na manabii wa zamani, hata hivyo, baadhi ya wafuasi wao - kwa kushirikiana na mashetani - baadaye walibadilisha maandiko. Majibu yakawa yasiyoeleweka na mengi ya ufunuo yalifichwa kwa lugha ya kimajazi. Mungu alipomtuma Yesu Kristo kwa Wayahudi, alipindua meza za wafanyabiashara hao walioanzisha biashara ndani ya hekalu, naye alihubiri kinyume cha tafsiri ya ibada ya sheria iliyofanywa na marabbi wa Kiyahudi. Akaithibitisha Sheria ya Nabii Musa na akaifufua. Alifundisha kusudi la maisha kwa wanafunzi wake na kuonyesha jinsi ya kuitimiza mpaka wakati wake wa mwisho katika ulimwengu huu. Hata hivyo, baada ya kuondoka kwake kutoka dunia hii, ujumbe wake pia ulipotoshwa na wengine waliodai kuwa miongoni mwa wafuasi wake. Ukweli ulio wazi alioleta ukawa usio dhahiri , kama ujumbe wa manabii mbele yake. Ufananishi ulianzishwa, hasa kupitia “Ufunuo” wa Yohana, na Injili iliyofunuliwa kwa Yesu ikapotea. Injili zingine nne zilizotungwa na wanadamu zilichaguliwa na Athanasius, askofu wa karne ya nne, kuchukua nafasi ya Injili iliyopotea ya Yesu Kristo. Na vitabu 23 vya maandishi ya Paulo na vingine vilivyojumuishwa katika Agano Jipya vilikuwa vimezidi hata matoleo manne ya Injili. Matokeo yake ni kuwa wasomaji wa Agano Jipya hawawezi kupata majibu sahihi ya swali la “Kwa nini Mungu alimuumba mwanadamu?” Na mtu hulazimika kufuata kwa upofu mafundisho yaliyoundwa na madhehebu yake. Injili hutafsiriwa kulingana na imani za kila kundi, na mtafutaji wa ukweli anaachwa tena akishangaa, ni ipi iliyo sahihi?

Umwilisho wa Mungu

Pengine dhana pekee inayowaleta pamoja madhehebu mengi ya Ukristo kuhusu kusudi la uumbaji wa wanadamu ni kwamba Mungu akawa mwanadamu ili aweze kufa mikononi mwa watu ili kuwatakasa dhambi iliyorithiwa kutoka kwa Adamu na wazao wake. Kulingana nao, dhambi hii ilikuwa kubwa kiasi kwamba hakuna tendo la kibinadamu la upatanisho au toba lingeweza kuifuta. Mungu ni mwema kiasi kwamba mtu mwenye dhambi hawezi kusimama mbele yake. Kwa hivyo, kafara ya Mungu peke yake inaweza kuokoa wanadamu kutokana na dhambi.

Imani katika kisasili hiki kilichobuniwa na mwanadamu kikawa chanzo pekee cha wokovu, kulingana na Kanisa. Kwa hivyo, kusudi la Kikristo la uumbaji likawa kutambua 'kafara ya Kimungu' na kumkubali Yesu Kristo kama Bwana Mungu. Hii inaweza kueleweka kutoka kwa maneno yafuatayo yanayohusishwa na Yesu katika Injili kulingana na Yohana:

“Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kiasi cha kumtoa Mwanae pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”

Hata hivyo, kama hii ndiyo kusudi la uumbaji na sharti la uzima wa milele, kwa nini haikufundishwa na manabii wote? Kwa nini Mungu hakuwa mwanadamu wakati wa Adamu na wazao wake ili watu wote wawe na nafasi sawa ya kutimiza kusudi lao la kuwepo na kufikia uzima wa milele. Au je, wale waliokuja kabla ya wakati wa Yesu walikuwa na lengo lingine la kuishi? Watu wote leo ambao Mungu hakutaka kamwe wasikie habari za Yesu pia hawana nafasi ya kutimiza lengo waliloumbiwa. Madhumuni hayo, ni dhahiri kwamba ni madogo zaidi na hayawezi kutimiza haja ya wanadamu.

Mbaya Nzuri zaidi

Kusudi la Uumbaji (sehemu ya 3 kati ya 3): Tamaduni za Kihindu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Utangulizi kwa swali la kushangaza zaidi katika historia ya binadamu, na mjadala kuhusu vyanzo ambavyo vinaweza kutumika kupata jibu. sehemu ya 3: Uchunguzi wa Maandiko ya Kihindu, na hitimisho kwa jambo hilo.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,377
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kila kitu ni Mungu

Maandiko ya Kihindu yanafundisha kwamba kuna miungu mingi, umwilisho wa miungu, watu ambao ni Mungu na kwamba kila kitu ni Mungu, Brahman. Licha ya imani kwamba nafsi (atman) za viumbe vyote vilivyo hai ni Brahman, mfumo wa matabaka wenye ukandamizaji uliibuka ambapo Brahmans wenye matabaka ya kuhani, waadhama wa kiroho tangu kuzaliwa kwao. Wao ni walimu wa Vedas na wanawakilisha ubora wa usafi wa ibada na ufahari wa kijamii. Kwa upande mwingine, tabaka la Sudra linatengwa kutoka kwa hadhi ya kidini na wajibu wao wa pekee katika maisha ni “kutumikia kwa unyenyekevu” matabaka mengine matatu na maelfu ya matabaka ndogo ndogo yanayokuja chini yao.

Kulingana na wanafalsafa wa Kihindu, lengo la wanadamu ni kutambua utukufu wao na kufuata njia (marga) ya kuelekea ukombozi (moksha) kutoka gurudumu la kuzaliwa upya -kufufuka kwa nafsi ya binadamu (atman) katika ukweli wa mwisho ambao ni Brahman. Kwa wale wanaofuata njia ya bhakti, lengo ni kumpenda Mungu kwa sababu Mungu aliumba binadamu “kufurahia uhusiano - kama baba anavyofurahia watoto wake” (Srimad Bhagwatam). Kwa Hindu wa kawaida, lengo kuu la maisha ya kidunia liko katika kuendana na majukumu ya kijamii na ibada, kwa sheria za jadi za maadili kwa ajili ya tabaka la mtu - njia ya karma.

Ingawa sehemu kubwa ya dini ya maandiko ya Vedic, ambayo yanahusu mila ya sadaka kwa moto, imefichwa na mafundisho ya Kihindu yanayopatikana katika maandiko mengine, mamlaka kamili na utakatifu wa Veda bado ni nguzo kuu kwa takriban madhehebu na mila zote za Kihindu. Veda inajumuisha makusanyo manne, ya zamani zaidi ikiwa ni Rigveda (“Hekima ya Mistari”). Katika maandiko haya, Mungu anaelezwa kwa maneno yanayochanganya sana. Dini inayojitokeza katika Rigveda ni ushirikina hasa unaohusisha miungu yenye kupendeza inayohusishwa na anga na hewa , na ya muhimu zaidi ikiwa Indra (mungu wa mbingu na mvua), Baruna (mlezi wa utaratibu wa anga), Agni (moto wa dhabihu au kafara), na Surya (jua). Katika maandiko ya baadaye ya Vedic, dhima ya miungu ya mapema ya Rigvedic inapungua, na ushirikina huanza kubadilishwa na kafara kwa ulimwengu (pantheism) na mungu wa viumbe vyote (Prajapati). Katika Upanishad (mafundisho ya siri kuhusu utaratibu wa ulimwengu), Prajapati inaungana na dhana ya Brahman, ukweli mkuu na kiini cha ulimwengu, na kuchukua nafasi ya utambulisho wowote maalum, hivyo kubadilisha kisasili kiwe falsafa halisi. Ikiwa yaliyomo katika maandiko haya yangekuwa yote ambayo binadamu alipaswa kuchagua ili kupata uongozi, binadamu angepaswa kudhani kuwa Mungu alijificha Yeye mwenyewe pamoja na lengo la uumbaji kutoka kwa wanadamu.

Mwenyezi Mungu si mwenye kuchanganya wala hataki ugumu kwa watu. Kwa hivyo alipofunua mawasiliano yake ya mwisho kwa wanadamu miaka elfu moja mia nne iliyopita, Alihakikisha kwamba ilihifadhiwa kikamilifu kwa vizazi vyote vya binadamu vijavyo. Katika maandiko hayo ya mwisho, Qurani (Kurani), Mungu alifunua kusudi lake la kuumba wanadamu, na kupitia kwa njia ya nabii wake wa mwisho, alifafanua maelezo yote ambayo mwanadamu angeweza kuelewa. Ni kwa misingi ya ufunuo huu na maelezo ya kinabii ndipo [lazima] tuchambue majibu sahihi ya swali “Kwa nini Mungu aliumba mwanadamu?”...

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.