Uhifadhi wa Kurani (Sehemu 1 kati ya 2): Kuhifadhi Akilini

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Uhifadhi wa Kurani akilini kwenye zama za Muhammad, rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, na uhifadhi wake leo na mamilioni ya Waislamu.

  • Na iiie.net (edited by IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 27 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 07 Feb 2022
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,226
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Preservation_of_the_Quran_(part_1_of_2)_001.jpgKurani tukufu, ambayo ni maandiko ya kidini ya Waislamu, ilifunuliwa kwa Kiarabu kwa Mtume Muhammad, Mungu ambariki, kupitia kwa malaika Gabrieli. Ufunuo huo ulitokea kwa vipande vipande, kwa kipindi cha miaka ishirini na mitatu, wakati mwingine kwa aya fupi fupi na wakati mwingine katika sura ndefu ndefu.[1]

Kurani (maana: “kusoma” au “kisomo”) ni tofauti na maneno na matendo yaliyorekodiwa (Sunnah) ya Mtume Muhammad, ambayo badala yake huhifadhiwa katika kundi tofauti la fasihi linaloitwa “Ahadeeth” (maana: “habari”; “ripoti”; au “simulizi”).

Baada ya kupokea ufunuo, Nabii alijihusisha na wajibu wa kuwasilisha ujumbe kwa Masahaba wakekwa kusoma maneno halisi aliyoyasikia kwa utaratibu wao halisi. Hii ni dhahiri katika kuweka kwake hata maneno ya Mungu ambayo yalielekezwa hasa kwake, kwa mfano: “Kul” (“Sema [kwa watu, Ewe Muhammad]”). Mtindo wa kimahadhi wa Kurani na usemi wake wa fasaha huifanya iwe rahisi kukaririka. Hakika, Mungu anaelezea hili kama mojawapo ya sifa zake muhimu kwa ajili ya kuhifadhika na kukumbukwa (Kurani 44:58; 54:17, 22, 32, 40), hasa katika jamii ya Kiarabu ambayo ilijigamba kwa ulumbi na mashairi marefu. Michael Zwettler anabainisha kwamba:

“katika nyakati za kale, wakati kuandika kulitumika kwa uchache, kumbukumbu na uwasilishaji wa mdomo ulikuwa ukitekelezwa na kuimarishwa kwa kiwango ambacho kwa sasa takriban haijulikani.”[2]

Sehemu kubwa za ufunuo huo zilihifadhiwa akilini kwa urahisi na idadi kubwa ya watu katika jamii ya Mtume.

Nabii aliwahimiza Masahaba wake kujifunza kila aya iliyofunuliwa na kuiwasilisha kwa wengine.[3] Kurani ilitakiwa pia kusomwa kila mara kama kitendo cha ibada, hasa wakati wa sala za wajibu za kila siku. Kwa njia hizi, wengi walisikia mara kwa mara vifungu kutoka kwa ufunuo uliosomwa, wakavihifadhi akilini na kuvitumia katika sala. Kurani nzima ilihifadhiwa akilini, neno kwa neno, na baadhi ya masahaba wa Mtume. Kati yao walikuwa Zaid ibn Thabit, Ubayy ibn Ka'b, Muadh ibn Jabal, na Abu Zaid.[4]

Siyo tu maneno ya Kurani yaliyohifadhiwa, bali pia matamshi yao, ambayo baadaye yalikuja kuwa sayansi kivyao inayoitwa Tajweed. Sayansi hii inaelezea kwa undani jinsi kila herufi inapaswa kutamkwa, pamoja na neno kwa ujumla, yote kwa kuzingatia herufi zingine na maneno. Leo hii tunaweza kuwapata watu wa lugha mbalimbali wenye uwezo wa kusoma Kurani kana kwamba wao ni Waarabu, wanaoishi wakati wa Mtume.

Zaidi ya hayo, ufuatilizi au utaratibu wa Kurani ulipangwa na Mtume mwenyewe na pia ulijulikana na Maswahaba.[5] Kila Ramadhani, Mtume angerudia baada ya Malaika Gabrieli (kwa kusoma) kurani nzima kwa utaratibu wake kama ilivyokuwa imefunuliwa, na mbele ya idadi kubwa ya Masahaba.[6] Katika mwaka wa kifo chake, aliisoma mara mbili.[7] Kwa hiyo, utaratibu wa aya katika kila sura na utaratibu wa sura zenyewe uliimarishwa katika kumbukumbu za kila mmoja wa Masahaba waliopo.

Wakati Masahaba walienea katika majimbo mbalimbali yenye wakazi tofauti, walipeleka masomo yao huko ili kuwafundisha wengine.[8] Kwa njia hii Kurani ile ile ilihifadhiwa kwa upana katika kumbukumbu za watu wengi katika maeneo makubwa na tofauti ya ardhi.

Hakika, uhifadhi wa Kurani ulijitokeza kuwa mila inayoendelea katika karne nyingi, huku vitengo/shule za kukariri zikianzishwa kote ulimwenguni na Waislamu. [9] Katika shule hizi, wanafunzi hujifunza na kukariri kurani pamoja na Tajweed yake, kutoka kwa mwalimu ambaye kwa upande wake alipata ujuzi Kutoka kwa mwalimu wake, 'mnyororo kamilifu' kutoka enzi za Mtume wa Mungu. Mchakato wenyewe huchukua takriban kati ya miaka 3 na 6. Baada ya kupata ujuzi na kisomo kimechunguzwa ili kukosoa makosa, mtu anapewa leseni rasmi (ijaza) kuthibitisha kuwa amejifunza sheria za kisomo na sasa anaweza kuisoma Kurani jinsi ilivyosomwa na Muhammad, Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Preservation_of_the_Quran_(part_1_of_2)_002.jpg

Picha hii ni leseni ya kawaida (ijaza) iliyotolewa mwishoni mwa kukamilisha kisomo cha Kurani na kuthibitisha mlolongo wa walimu usiovunjika hadi kufikia kwa Mtume wa Uislamu. Picha hiyo hapo juu ni cheti cha ijaza cha Qari Mishari ibn Rashid al-Afasy, Qari anayejulikana sana kutoka Kuwait, iliyotolewa na Sheikh Ahmad al-Ziyyat. Picha kwa hisani ya (http://www.alafasy.com.)

A.T. Welch, Mtaalamu wa mambo ya Mashariki ambaye si Muislamu, anaandika:

“Kwa Waislamu Kurani ni zaidi ya maandiko au fasihi takatifu kwa maana ya kawaida ya Kimagharibi. Umuhimu wake wa kimsingi kwa idadi kubwa ya watu kwa karne nyingi umekuwa katika mfumo wake wa mdomo, mfumo ambao ulionekana kwanza kama “kisomo” kilichosomwa na Muhammad kwa wafuasi wake kwa kipindi cha miaka ishirini... Aya hizo zilihifadhiwa akilini na baadhi ya wafuasi wa Muhammad wakati wa maisha yake, na Mfumo wa mdomo ulioanzishwa hivyo umekuwa na historia inayoendelea tangu wakati huo, kwa namna fulani huru, na bora, kuliko Kurani iliyoandikwa... Kupitia karne zote mfumo wa mdomo wa Kurani nzima umedumishwa na wasomaji wataalamu (kurraa). Hadi hivi karibuni, umuhimu wa Usomaji wa Kurani haujawahi kueleweka kikamilifu katika nchi za Magharibi.”[10]

Kurani ni labda kitabu pekee, kidini au kidunia, ambacho kimehifadhiwa akilini kikamilifu na mamilioni ya watu.[11] Mtaalamu Mkubwa wa masuala ya Mashariki Kenneth Cragg anaonyesha kwamba:

“…jambo hili la usomaji wa Kurani lina maana kwamba maandishi yamepitia karne tofauti huku mlolongo ukidumishwa kama ibada. Haiwezi, kwa hivyo, kushughulikiwa kama kitu cha kale, wala kama maandishi ya kihistoria ya zamani za kale. Jambo la hifdh (kukariri Kurani) limeifanya Kurani kuwa milki ya kisasa katika muda wote wa Kiislamu na kuipa sarafu ya kibinadamu katika kila kizazi, na kutoruhusu kamwe kuachwa kama mamlaka tupu kwa ajili ya kumbukumbu peke yake.”[12]



Vielezi-chini:

[1] Muhammad Hamidullah, Introduction to Islam, London: MWH Publishers, 1979, uk.17.

[2] Michael Zwettler, The Oral Tradition of Classical Arabic Poetry, Ohio State Press, 1978, uk.14.

[3] Saheeh Al-Bukhari Vol.6, Hadith No.546.

[4]Saheeh Al-Bukhari Vol.6, Hadith No.525.

[5] Ahmad von Denffer, Ulum al-Quran, The Islamic Foundation, UK, 1983, uk.41-42; Arthur Jeffery, Materials for the History of the Text of the Quran, Leiden: Brill, 1937, uk.31.

[6] Saheeh Al-Bukhari Vol.6, Hadith No.519.

[7]Saheeh Al-Bukhari Vol.6, Hadith Nos.518 & 520.

[8] Ibn Hisham, Seerah al-Nabi, Cairo, n.d., Vol.1, p.199.

[9] Labib as-Said, The Recited Koran, imetafsiriwa na Morroe Berger, A. Rauf, and Bernard Weiss, Princeton: The Darwin Press, 1975, p.59.

[10]The Encyclopedia of Islam, ‘The Quran in Muslim Life and Thought.’

[11]William Graham, Beyond the Written Word, UK: Cambridge University Press, 1993, uk.80.

[12]Kenneth Cragg, The Mind of the Quran, London: George Allen & Unwin, 1973, uk.26.

Mbaya Nzuri zaidi

Utunzaji wa Kurani (Sehemu ya 2 kati ya 2): Kurani Iliyoandikwa

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Uandishi wa Kurani wakati wa Muhammad na utunzaji wake hadi leo hii.

  • Na iiie.net (edited by IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 24 Nov 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,974
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kurani nzima hata hivyo ilirekodiwa kwa maandishi wakati wa ufunuo kutoka kwa imla ya Mtume, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake. Ilirekodiwa na baadhi ya masahaba zake, anayejulikana zaidi kati yao akiwa ni Zaid ibn Thabit.[1] Wengine miongoni mwa waandishi wake wakuu walikuwa Ubayy ibn Ka'b, Ibn Mas'ud, Mu'awiyah ibn Abi-Sufyan, Khalid ibn Al-Waleed na Az-Zubayr ibn Al-Awwam.[2] Aya ziliandikwa juu ya ngozi, vipande, mifupa ya bega ya wanyama na mabua ya mitende.[3]

Ukusanyaji wa Kurani kwa namna ya kitabu ulifanyika punde tu baada ya vita vya Yamama (11AH/633 BK), baada ya kifo cha Mtume, wakati wa Ukhalifa wa Abu Bakr. Masahaba wengi wakawa mashahidi katika vita hivyo, na waliobaki wakaogopa kwamba iwapo nakala iliyoandikwa ya Kurani nzima haita tayarishwa, sehemu kubwa za Kurani zingeweza kupotea baada ya kifo cha wale waliokuwa wameihifadhi akilini. Kwa hivyo, kwa pendekezo la Umar kukusanya Kurani kwa namna ya kitabu, Zaid ibn Thabit alifanywa na Abu Bakr kuwa mkuu wa kamati ambayo ingekusanya pamoja rekodi zilizotawanyika za Kurani na kutayarisha msahafu- karatasi za kushikana ambazo zimebeba ufunuo wote .[4] Ili kulinda mkusanyiko kutokana na makosa, kamati hiyo ilikubali tu nyenzo ambazo zimeandikwa mbele ya Mtume mwenyewe, na ambazo zinaweza kuthibitishwa na angalau mashahidi wawili wa kuaminika ambao kwa kweli walikuwa wamesikia Mtume akisoma kifungu kinachohusika[5]. Baada ya kukamilika na kupitishwa kwa kauli moja na Masahaba wa Mtume, majarida haya yalitunzwa na Khalifa Abu Bakr (kifo. 13AH/634 BK), kisha kupitishwa kwa Khalifa Umar (13-23AH/634-644 BK), halafu binti wa Umar na mjane wa Mtume, Hafsah[6].

Khalifa wa tatu Uthman (23AH-35AH/644-656 BK) aliitisha kutoka kwa Hafsah mswada wa Kurani uliokuwa katika utunzaji wake, na kuamuru utengenezaji wa nakala kadhaa zilizoshikana (masaahif, kwa umoja: msahafu). Kazi hii ilikabidhiwa Sahaba Zaid ibn Thabit, Abdullah ibn Az-Zubair, Sa'eed ibn Al-'As, na Abdur-Rahman ibn Al-Harith ibn Hisham[7] .Baada ya kukamilishwa (mnamo 25AH/646 BK), Uthman alirudisha mswada wa awali kwa Hafsah na kupeleka nakala zingine katika majimbo makubwa ya Kiislamu.

Wasomi kadhaa wasio Waislamu ambao wamechunguza kwa kina suala la ukusanyaji na ulinzi wa Kurani pia wameshuhudia ukweli wake. John Burton, mwishoni mwa kazi yake kubwa katika mkusanyiko wa Kurani, anasema kwamba Kurani kama tulivyo nayo leo ni:

“…Nakala ambayo imefika kwetu imo katika namna ambayo iliandaliwa na kupitishwa na Mtume... Tuliyo nayo leo mikononi mwetu ni msahafu wa Muhammad.[8]

Kenneth Cragg anaeleza kuwa uwasilishaji wa Kurani kutoka kwa wakati wa ufunuo hadi leo umetokea katika “mlolongo hai usiovunjika wa ujitoaji.[9] Schwally anakubali kuwa:

“Kuhusiana na vipande mbalimbali vya ufunuo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba maandiko yao yamepitishwa kwa ujumla kama ilivyopatikana katika urithi wa Mtume.”[10]

Uaminifu wa kihistoria wa Kurani unabainika zaidi tukijua kuwa moja kati ya nakala zilizotumwa na Khalifa Uthman bado ipo leo. Iko katika Makavazi ya Jiji la Tashkent huko Uzbekistan, Asia ya Kati.[11] Kwa mujibu wa Mpango wa Kumbukumbu ya Dunia, UNESCO, tawi la Umoja wa Mataifa, 'ni toleo lauhakika, linalojulikana kama Msahafu wa Uthman.’[12]

Preservation_of_the_Quran_(part_2_of_2)_001.jpg

Mswada huu, unaoshikiliwa na Bodi ya Kiislamu ya Uzbekistan, ni toleo la kwanza kabisa lililoandikwa la Kurani. Ni toleo la hakika, linalojulikana kama Mushaf wa Othman. Picha kwa hisani ya Rekodi ya Kumbukumbu ya Dunia, UNESCO.

Nakala pacha ya msahafu ulioko Tashkent inapatikana katika Maktaba ya Chuo Kikuu cha Columbia nchini Marekani.[13] Nakala hii ni ushahidi kwamba maandiko ya Kurani tuliyo nayo leo yanafanana na yale ya wakati wa Mtume na masahaba. Nakala ya msahafu iliyotumwa Syria (iliyonakiliwa kabla ya moto kuharibu Masjid ya Jaami ambapo ilikuwa mnamo mwaka wa 1310AH/1892 BK ) pia ipo katika Makavazi ya Topkapi mjini Istanbul [14], na mswada wa kale ulioandikwa juu ya ngozi ya swara upo kwenye Dar al-Kutub as-Sultaniyyah nchini Misri. Maandishi ya kale zaidi kutoka vipindi vyote vya historia ya Kiislamu yaliyopatikana katika Maktaba ya Kongres huko Washington, Makumbusho ya Chester Beatty huko Dublin (Ireland) na Makumbusho ya London yamefananishwa na yale ya Tashkent, Uturuki na Misri, huku matokeo yakihakikisha kuwa hakuna mabadiliko yoyote katika maandishi kutoka wakati wake wa awali wa uandishi.[15]

Taasisi ya Koranforschung, kwa mfano, katika Chuo Kikuu cha Munich (Ujerumani), ilikusanya zaidi ya nakala 42,000 kamili au isiyo kamili ya kale ya Kurani. Baada ya miaka hamsini ya utafiti, waliripoti kwamba hakukuwa na tofauti kati ya nakala mbalimbali, isipokuwa makosa ya mara kwa mara ya mnakili ambayo ingeweza kuhakikishwa kwa urahisi. Taasisi hii kwa bahati mbaya iliharibiwa na mabomu wakati wa vita vya pili vya Dunia.[16]

Hivyo, kutokana na juhudi za masahaba wa mwanzo, kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, Kurani kama tulivyo nayo leo inasomwa kwa namna ile ile ilivyofunuliwa.. Hili linafanya Kurani kuwa maandiko pekee ya kidini ambayo bado yanahifadhiwa kabisa na kueleweka katika lugha yake ya asili. Hakika, kama Sir William Muir anasema, “Pengine hakuna kitabu kingine duniani ambacho kimesalia kwa karne kumi na mbili (sasa kumi na nne) ikiwa na maandishi safi sana hivyo.”[17]

Ushahidi huo hapo juu unathibitisha ahadi ya Mungu katika Kurani:

“Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.” (Kurani 15:9)

Kurani imehifadhiwa kwa namna ya kimdomo na ya kimaandishi kwa jinsi ambayo hakuna kitabu kingine kimehifadhiwa, huku kila namna ikiwa kidhibiti kwa usahihi wa kingine.



Vielezi-chini:

[1]Jalal al-Din Suyuti, Al-Itqan fee ‘Uloom al-Quran, Beirut: Maktab al-Thiqaafiyya, 1973, Vol.1, p.41 & 99.

[2]Ibn Hajar al-’Asqalani, Al-Isabah fee Taymeez as-Sahabah, Beirut: Dar al-Fikr, 1978; Bayard Dodge, The Fihrist of al-Nadeem: A Tenth Century Survey of Muslim Culture, NY: Columbia University Press, 1970, p.53-63. Muhammad M. Azami, katika Kuttab al-Nabi, Beirut: Al-Maktab al-Islami, 1974, anataja watu 48 waliokuwa wakimwandikia Mtume.

[3]Al-Harith al-Muhasabi, Kitab Fahm al-Sunan, cited in Suyuti, Al-Itqan fi ‘Uloom al-Quran, Vol.1, p.58.

[4]Saheeh Al-Bukhari Vol.6, Hadith Nos.201 & 509; Vol.9, Hadith No.301.

[5]Ibn Hajar al-’Asqalani, Fath al-Bari, Vol.9, p.10-11.

[6]Saheeh Al-Bukhari, Vol.6, Hadith No.201.

[7] Saheeh Al-Bukhari Vol.4, Hadith No.709; Vol.6, Hadith No.507

[8] John Burton, The Collection of the Quran, Cambridge: Cambridge University Press, 1977, p.239-40.

[9]Kenneth Cragg, The Mind of the Quran, London: George Allen & Unwin, 1973, p.26.

[10] Schwally, Geschichte des Qorans, Leipzig: Dieterich’sche Verlagsbuchhandlung,1909-38, Vol.2, p.120.

[11] Yusuf Ibrahim al-Nur, Ma’ al-Masaahif, Dubai: Dar al-Manar, 1st ed., 1993, p.117; Isma’il Makhdum, Tarikh al-Mushaf al-Uthmani fi Tashqand, Tashkent: Al-Idara al-Diniya, 1971, p.22ff.

[12] (http://www.unesco.org.)

I. Mendelsohn, “The Columbia University Copy Of The Samarqand Kufic Quran”, The Moslem World, 1940, p. 357-358.

A. Jeffery & I. Mendelsohn, “The Orthography Of The Samarqand Quran Codex”, Journal Of The American Oriental Society, 1942, Volume 62, pp. 175-195.

[13]The Muslim World, 1940, Vol.30, p.357-358

[14] Yusuf Ibrahim al-Nur, Ma’ al-Masaahif, Dubai: Dar al-Manar, 1st ed., 1993, p.113

[15] Bilal Philips, Usool at-Tafseer, Sharjah: Dar al-Fatah, 1997, p.157

[16] Mohammed Hamidullah, Muhammad Rasullullah, Lahore: Idara-e-Islamiat, n.d., p.179.

[17] Sir William Muir, Life of Mohamet, London, 1894, Vol.1, Introduction.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.