Utangulizi mfupi wa Uislamu (sehemu ya 2 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jukumu la Kurani na Mtume Muhammad katika kufikisha ujumbe wa Mungu ulio safi, ambao haujabadilishwa kwa wanadamu, na maelezo ya jinsi ya kuishi njia ya Uislamu inayoelekea kwenye maisha bora.

  • Na Daniel Masters, AbdurRahman Squires, and I. Kaka
  • Iliyochapishwa mnamo 06 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,862 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kurani

Neno la Kiarabu "Al-Quran" lina maana "kusoma". Wakati linatumiwa kuhusu Uislamu, neno Kurani linamaanisha ujumbe wa mwisho wa Mungu kwa wanadamu, ambao uliofunuliwa kwa Mtume Muhammad. Kurani, wakati mwingine inaandikwa Koran, ni neno halisi la Mungu - kama inavyojieleza bayana mara kwa mara. Tofauti na maandiko mengine matakatifu, Kurani imehifadhiwa kikamilifu kwa maneno na maana yake katika lugha iliyo hai. Kurani ni muujiza unaoishi katika lugha ya Kiarabu; na inajulikana kuwa ya kifani kwa mtindo wake, mtindo na athari za kiroho. Ufunuo wa mwisho wa Mungu kwa wanadamu, Kurani, ulifunuliwa kwa Mtume Muhammad kwa kipindi cha miaka 23.

Kurani, tofauti na vitabu vingine vingi vya kidini, kila wakati ilifikiriwa kuwa ni Neno la Mungu na wale ambao waliiamini, yaani haikuwa kitu kilichopangwa na viongozi wa kidini miaka mingi baada ya kuandikwa. Pia, Kurani ilisomwa hadharani mbele ya jamii zote za Waislamu na zisizo za Waislamu wakati wa uhai wa Mtume Muhammad. Kurani yote pia iliandikwa wakati wa uhai wa Mtume, na masahaba wengi wa Mtume walihifadhi Kurani nzima neno kwa neno kama ilivyofunuliwa. Kwa hivyo, tofauti na maandiko mengine, Kurani kila wakati ilikuwa mikononi mwa waumini wa kawaida; ilifikiriwa kila wakati kuwa ni neno la Mungu na, kwa sababu wengi walikariri, ilihifadhiwa kikamilifu.

Kulingana na mafundisho ya Kurani - ni maandiko ya ulimwengu yaliyoelekezwa kwa wanadamu wote, na sio kuelekezwa kwa kabila fulani tu au "watu waliochaguliwa". Ujumbe ambao unaletwa siyo mpya, lakini ujumbe ule ule wa manabii wote - Kujisalimisha kwa Mungu Mtukufu na kumuabudu Yeye peke yake. Kwa hivyo, ufunuo wa Mungu katika Kurani unazingatia kufundisha wanadamu umuhimu wa kuamini Umoja wa Mungu na kuunda maisha yao karibu na mwongozo ambao ametuma. Cha kuongezea, Kurani ina hadithi za manabii waliopita, kama vile Ibrahim, Nuhu, Musa na Yesu; vile vile amri nyingi na makatazo kutoka kwa Mungu. Katika nyakati za kisasa ambapo watu wengi wameshikwa na mashaka, kukata tamaa kwa kiroho na "usahihi wa kisiasa", mafundisho ya Kurani yanatoa suluhisho kwa uwazi wa maisha yetu na machafuko ambayo yanaikumba dunia leo. Kwa kifupi, Kurani ni kitabu cha mwongozo kwa ubora.

Mtume Muhammad

Tofauti na waanzilishi wa dini nyingi, mtume wa mwisho wa Uislamu ni mtu halisi aliyeandikwa na wa kihistoria. Aliishi katika nuru kamili ya historia, na maelezo ya dakika ya mwisho yanajulikana. Sio tu Waislamu wana maandishi kamili ya maneno ya Mungu ambayo yalifunuliwa kwa Muhammad, lakini pia wamehifadhi maneno na mafundisho yake katika kile kinachoitwa fasihi ya "hadeeth". Hii imesemwa, inapaswa kueleweka kwamba Waislamu wanaamini kwamba Mtume Muhammad alikuwa mtu aliyechaguliwa na Mungu, na kwamba yeye sio mungu kwa njia yoyote. Ili kuzuia upotofu wa kumfanya mungu, Mtume Muhammad aliwafundisha Waislamu kumtaja kama "Mjumbe wa Mungu na Mtumwa Wake". Ujumbe wa mtume wa mwisho wa mwisho wa Mungu ilikuwa kufundisha tu "hakuna chenye uumungu au kinachostahili kuabudiwa isipokuwa Mungu Mtukufu", na vile vile kuwa mfano unaoishi wa ufunuo wa Mungu. Kwa maneno rahisi, Mungu alituma ufunuo huo kwa Muhammad, ambaye naye aliufundisha, akauhubiri, akauishi na akaufanyia kazi.

Kwa njia hii, Muhammad alikuwa zaidi ya "mtume" kwa maana ya manabii wengi wa Bibilia, kwa kuwa pia alikuwa kiongozi na mtawala. Alikuwa mtu aliyeishi maisha ya unyenyekevu katika kumtumikia Mungu, na akaanzisha dini inayojumuisha yote na njia ya maisha kwa kuonyesha maana ya kuwa rafiki bora, mume, mwalimu, mtawala, shujaa na jaji. Kwa sababu hii, Waislamu hawamfuati yeye kwa ajili yake mwenyewe, bali kwa kumtii Mungu, kwa sababu Muhammad hakutuonyesha tu jinsi ya kushughulika na wanadamu wenzetu, lakini muhimu zaidi, alituonyesha jinsi ya kuhusishwa na kumwabudu Mungu; mwabuduni Yeye kwa njia pekee inayompendeza.

Kama manabii wengine, Muhammad alikabiliwa na upinzani mkubwa na mateso wakati wa kazi yake. Ila, kila wakati alikuwa mvumilivu na mwenye haki, na aliwatendea maadui wake vizuri. Matokeo ya kazi yake yalifanikiwa sana, na ingawa kazi yake ilianza katika moja ya maeneo ya nyuma sana na ya mbali duniani, ndani ya miaka mia moja tangu kifo cha Muhammad, Uislamu ulikuwa umeenea kutoka Uhispania hadi Uchina. Mtume Muhammad alikuwa Mtume mkuu kuliko Mitume wote wa Mungu, sio kwa sababu alikuwa na mafundisho mapya au miujiza mikubwa, lakini kwa sababu ni yeye aliyechaguliwa kubeba ufunuo wa mwisho ambao ungekuja kwa wanadamu kutoka kwa Mungu, unaofaa katika sehemu zote, muda, na watu, wa milele na usio badilika hadi Siku ya Mwisho.

Njia ya Maisha ya Uislamu

Katika Kurani Tukufu, Mungu uwafundisha wanadamu kuwa waliumbwa ili wamwabudu Yeye, na kwamba msingi wa ibada yote ya kweli ni kumjua Mungu. Kwa kuwa mafundisho ya Uislamuyanajumuisha nyanja zote za maisha na maadili, ufahamu wa Mungu unahamasisha katika mambo yote ya mwanadamu. Uislamu unaweka wazi kuwa matendo yote ya mwanadamu ni matendo ya ibada ikiwa yatafanywa kwa mujibu ya Mungu peke yake na kwa mujibu wa Sheria Yake ya Kimungu. Hivyo, ibada katika Uislamu haina mipaka ya mila ya kidini.

Mafundisho ya Uislamu huwa kama rehema na uponyaji kwa roho ya mwanadamu, na sifa kama vile unyenyekevu, uaminifu, uvumilivu na sadaka huhimizwa sana. Kwa kuongezea, Uislamu unalaani kiburi na kujiona, kwani Mwenyezi Mungu ndiye hakimu pekee wa haki ya mwanadamu.

Mtazamo wa Kiislamu juu ya asali ya mwanadamu pia ni ya kweli na yenye usawa. Binadamu hawaaminiwi kuwa wenye asili ya dhambi, lakini wanaonekana kama wenye uwezo sawa wa kufanya mema na mabaya.

Uisilamu pia unafundisha kuwa imani na vitendo vinaenda mkono kwa mkono. Mungu amewapa watu hiari, na kipimo cha imani yake ni matendo na vitendo vya mtu. Ila, wanadamu pia wameumbwa dhaifu na huangukia kwenye dhambi mara kwa mara. Hii ndio hali ya mwanadamu aliyeumbwa na Mungu katika Hekima Yake, na hajalithi "udhalimu" au aihitaji marekebisho. Hii ndio sababu njia ya toba iko wazi kwa wanadamu wote, na Mungu Mtukufu anampenda mwenye dhambi anayetubu kuliko yule asiyefanya dhambi kabisa.

Usawa wa kweli wa maisha ya Uislamu uanzishwa kwa kuwa na hofu yenye afya ya Mungu na pia imani ya kweli juu ya Rehema Yake isiyo na kikomo. Maisha bila hofu ya Mungu husababisha dhambi na kutotii, wakati kuamini kuwa tukiwa tumetenda dhambi sana kuwa Mungu hatatusamehe hii husababisha kukata tamaa. Kutilia maanani, Uislamu unafundisha kuwa kukata tamaa kunaleta upotovu wa Rehema za Mola wao.

Cha kuongezea, Kurani Tukufu, ambayo ilifunuliwa kwa Mtume Muhammad, ina mafundisho mengi juu ya maisha ya baadae na Siku ya Kiyama. Kwa sababu hii, Waislamu wanaamini kwamba wanadamu wote mwisho watahukumiwa na Mungu kwa imani na matendo yao katika maisha yao ya kidunia. Katika kuwahukumu wanadamu, Mungu Mtukufu atakuwa Mwenye Rehema na Haki, na watu watahukumiwa tu kwa kile walichokuwa na uwezo nacho.

Inatosha kusema kuwa Uislamu unafundisha kwamba maisha ni mtihani, na kuwa wanadamu wote watawajibika mbele za Mungu. Imani ya dhati katika maisha ya baadae ni ufunguo wa kuongoza maisha yenye usawa na maadili. Vinginevyo, maisha yanaonekana kama mwisho wake wenyewe, ambayo husababisha wanadamu kuwa wabinafsi zaidi, wapenda mali na wasio na maadili.

Uislamu kwa Maisha Bora

Uislamu unafundisha kwamba furaha ya kweli inaweza kupatikana tu kwa kuishi maisha yaliyojaa ufahamu wa Mungu na kuridhika na kile Mungu ametupatia. Cha kuongezea, "uhuru" wa kweli ni uhuru kutoka kwa kudhibitiwa na tamaa zetu za kibinadamu na kutawaliwa na itikadi za wanadamu. Hii ni tofauti kabisa na maoni ya watu wengi katika ulimwengu wa kisasa, ambao wanachukulia "uhuru" kuwa uwezo wa kukidhi matakwa yao yote bila kizuizi. Mwongozo wa wazi na wa kina wa Uislamu huwapa wanadamu kusudi na mwelekeo ulioeleweka maishani. Mbali na kuwa washirika wa undugu wa kibinadamu wa Uislamu, mafundisho yake yenye usawa na vitendo ni chanzo cha faraja ya kiroho, mwongozo na maadili. Uhusiano wa moja kwa moja na yenye uwazi na Mungu Mtukufu, pamoja na hali ya kusudi na wokovu ambao kwa mwenye kujihisi kuwa Muislamu , humwokoa mtu kutokana na hofu nyingi za maisha ya kila siku.

Kwa kifupi, njia ya maisha ya Uislamu ni safi na nzuri. Hujenga nidhamu ya kibinafsi na kujidhibiti kwa njia ya sala ya kawaida na kufunga, na huwaokoa wanadamu kutokana na ushirikina na kila aina ya ubaguzi wa asili, kabila na kitaifa. Kwa kukubali kuishi maisha ya kumtambua Mungu, na kutambua kwamba kitu pekee kinachowatofautisha watu machoni mwa Mungu ni ufahamu wao kwake, hadhi ya kweli ya mwanadamu ujulikana.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.