Huruma Yangu Inashinda Ghadhabu Yangu (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi Rehema inavyodhihirika kwa Mwenyezi Mungu, na mifano ya rehema ya Mtume na Maswahaba wake.

  • Na Hala Salah (Reading Islam)
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,994 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

My_Mercy_Prevails_Over_My_Wrath_(part_1_of_2)_001.jpg“Utayari wa kusamehe na kutokuadhibu” ni tafsiri inayotumika mara kwa mara kwa neno rehema, lakini rehema ni nini katika Uislamu?

Kwa Uislamu, rehema ilipewa maana ya ndani zaidi ambayo ilijenga kipengele muhimu katika maisha ya kila Muislamu, ambacho anazawadiwa na Mungu kwa ajili ya kuonyesha.

Rehema ya Mungu, ambayo vimepewa viumbe Vyake vyote, inaonekana katika kila kitu tunachokitazama: katika jua ambalo hutoa mwanga na joto, na katika hewa na maji ambayo ni muhimu kwa wote walio hai.

Sura nzima katika Quran imepewa jina la sifa ya Mwenyezi Mungu Ar-Rahman au "Mwingi wa Rehema." Pia sifa mbili za Mungu zinatokana na neno la rehema. Nazo ni Ar-Rahman na Ar-Rahim, ambayo ina maana ya “Mwingi wa Fadhila” na “Mwingi wa Rehema.” Sifa hizi mbili zimetajwa katika maneno yaliyosomwa mwanzoni mwa sura 113 za Quran: “Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.” Maneno haya ni ukumbusho endelevu kwa msomaji wa rehema zisizo na mwisho za Mungu na fadhila kuu.

Mwenyezi Mungu anatuhakikishia kwamba anayefanya dhambi atasamehewa ikiwa atatubu na kuacha kitendo hiki, ambapo anasema:

“Mola wenu Mlezi amejilazimisha rehema, ya kwamba atakaye fanya uovu miongoni mwenu kwa ujinga, kisha akatubu baada yake na akatengenea, basi hakika Yeye ni Mwenye maghfira na Mwenye kurehemu.” (Quran 6:54)

Aya hii inathibitishwa na riwaya ya Mtume Muhammad ambapo amesema kuwa Mwenyezi Mungu alisema:

“Rehema yangu inashinda ghadhabu yangu.”

Malipo ya wema na huruma pia yalihakikishwa na Mtume Muhammad:

“Wenye kurehemu wanahurumiwa na Mwingi wa Rehema. Warehemuni waliomo ardhini, na Yeye aliye mbinguni atakurehemuni” (As-Suyuti).

Rehema ya Mtume

Kuhusu rehema ya Mtume Muhammad ni vyema kutaja kwanza yale ambayo Mwenyezi Mungu amesema juu yake:

“Nasi hatukukutuma ila uwe ni Rehema kwa walimwengu wote.” (Quran 21:107)

…ambayo inahakikisha kwamba Uislamu umejengwa juu ya rehema, na kwamba Mwenyezi Mungu alimtuma Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kama rehema kwa viumbe vyote bila ubaguzi.

Katika Quran Mwenyezi Mungu pia anasema:

“Hakika amekwisha kujieni Mtume kutokana na nyinyi wenyewe; yanamhuzunisha yanayo kutaabisheni; anakuhangaikieni sana. Kwa Waumini ni mpole na mwenye huruma.” (Quran 9:128)

Aya hizi zilidhihirika kwa uwazi kabisa katika tabia na matendo ya Mtume, kwani alivumilia matatizo mengi kwa ajili ya kufikisha ujumbe wa Mungu. Mtume pia alikuwa mpole sana katika kuwaongoza watu wake, na kila walipokuwa wakimfanyia ubaya alimwomba Mwenyezi Mungu awasamehe kwa ujinga na ukatili wao.

Maswahaba wa Mtume

Anapowaelezea Maswahaba katika Quran Mungu anasema:

“Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na walio pamoja naye wana nguvu mbele ya makafiri, na wanahurumiana wao kwa wao.” (Quran 48:29).

Baadhi ya watu wanaweza kufikiri ni dhahiri kwa Muhammad kuwa na maadili, kwa sababu yeye ni Mtume, lakini Maswahaba walikuwa ni watu wa kawaida ambao walijitolea maisha yao kwa ajili ya kumtii Mungu na Mtume Wake. Kwa mfano Abu Bakr As-Siddiq alijitolea mali yake yote kwa ajili ya kununua watumwa kutoka kwa mabwana wao wakatili na kisha akawaacha huru kwa ajili ya Mungu.

Wakati mmoja alipokuwa akifafanua dhana sahihi ya rehema kwa Maswahaba zake, Mtume alisema kwamba si kwa wema wa mtu kwa familia na marafiki, bali ni kwa kuonyesha rehema na huruma kwa umma kwa ujumla, iwe unawajua au huwajui.

Rehema "Ndogo"

Baadhi ya mila zisizo na huruma za kabla ya Uislamu zilikuwa zinatoa mtoto kama kafara kwa ajili ya miungu na kuzika wasichana wakiwa hai. Vitendo hivi dhidi ya watoto vilikatazwa vikali na Quran na Sunnah za Kinabii mara nyingi.

Kwa rehema za Mtume kwa watoto, siku moja alikuwa akiongoza swala na wajukuu zake, Al-Hasan na Al-Husein, bado walikuwa ni wavulana wadogo wakicheza na kupanda juu ya mgongo wake, hivyo kwa khofu ya kuwadhuru akiwa anasimama, Mtume akarefusha sajda yake. Wakati mwingine, Mtume aliswali huku akiwa amembeba Umamah, mjukuu wake wa kike.

Wema huu wa Mtume haukutawazwa kwa watoto wake tu bali pia ulienezwa kwa watoto wanaocheza mitaani. Mara tu walipomwona Mtume, walimkimbilia, na alikuwa akiwapokea wote kwa tabasamu mchangamfu na kwa mikono wazi.

Hata wakati wa kuswali wema wa asili wa Mtume ulikuwa wazi, kama alivyowahi kusema:

“(Inatokea kwamba) naanza swala nikikusudia kurefusha, lakini nikisikia kilio cha mtoto, nafupisha Swalah kwa sababu najua kwamba kilio cha mtoto kitachochea matamanio ya mama yake” (Saheeh Al-Bukhari).

Katika hali nyingi Mtume alitufundisha jinsi watoto wanapaswa kulelewa katika hali nzuri na ya upendo, na kwamba wasipigwe, au kupigwa usoni, ili kuepuka unyonge wao. Wakati mtu mmoja alipomwona Mtume akimbusu mjukuu wake, alistaajabishwa na upole wa Mtume na akasema, “Nina watoto kumi lakini sijawahi kumbusu hata mmoja wao.” Mtume akajibu,

“Asiye rehemu hatarehemewa” (Saheeh Al-Bukhari).

Kipande cha Nywele tu

Mungu alipowataja mayatima ndani ya Quran alisema nini maana yake:

“Basi yatima usimwonee!” (Quran 93:9)

Kwa mujibu wa Aya hii zilikuja adabu za Mtume kwa mayatima, kwani alisema:

“Mimi na yule anayemlea yatima na kumruzuku, tutakuwa Peponi namna hii,” akiweka pamoja vidole vyake vya shahada na vya kati. (Abu Dawud)

Ili kumfanya yatima ajisikie kuthaminiwa na kwamba ikiwa amepoteza penzi la wazazi wake bado kuna watu ambao wako tayari kumpenda na kumtunza, Mtume alihimiza wema kwa kusema kwamba mtu hulipwa kwa matendo mema kwa kila nywele anayopiga katika kichwa cha yatima.

Ulinzi wa mali ya yatima ulithibitishwa wazi na Mungu na Mtume Wake. Kwa mfano, Mungu anasema maana yake:

“Hakika wanao kula mali ya mayatima kwa dhulma, hapana shaka yoyote wanakula matumboni mwao moto, na wataingia Motoni.” (Quran 4:10)

Kauli ya Mtume pia inatufahamisha kwamba moja ya madhambi saba makubwa ni kula mali ya yatima.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.