Kisa cha Uumbaji (sehemu ya 2 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Makala hii inazungumzia kuhusu Kibao takatifu, uumbaji wa mbingu, ardhi, bahari, mito, mvua, jua, mwezi, malaika, majini, na wanadamu.

  • Na Imam Mufti (© 2016 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,822 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kibao Kilichohifadhiwa (Al-Lawh Al-Mahfuz)

Story_of_Creation_(Part_2_of_2)._001.jpgKalamu, ambayo iliundwa miaka 50,000 kabla ya mbingu na ardhi, iliandika katika kile kinachojulikana kama Al-lawh al-Mahfuz, Runulishi iliyohifadhiwa. Mungu anakiita al-Lawh Al-Mahfuz kwa sababu imehifadhiwa kutokana na mabadiliko yoyote na pia imehifadhiwa kutokana na upatikanaji. Kila kitu kiko ndani ya Kitabu hicho, na kama anavyotuambia Mwenyezi Mungu, hata jani linaloanguka kutoka kwa mti limetajwa. Kila kitu ambacho kingetokea, kilichotokea, na kitakachotokea kimeandikwa huko.

Kinachofanya ni kuthibitisha imani ya muumini kwa Mungu kwamba yale aliyoyaandika yaliandikwa kwa wema wetu, na kwamba kila kitu kinatokea kwa hekima. Wakati mwingine tunaweza kuielewa, lakini wakati mwingine tunafarijiwa na kuridhika tukijua kwamba Mungu anajua anachofanya.

Mbingu na Ardhi

Ikizungumzia kile wanasayansi hukiita Mlipuko Mkubwa leo, Qur'ani inasema, "Je! Hao walio kufuru hawakuona kwamba mbingu na ardhi zilikuwa zimeambatana, kisha Sisi tukazibabandua? Na tukajaalia kwa maji kila kilicho hai? Basi je, hawaamini?" (Kurani 21:30)

Kulingana na aya inayofuata, baadhi ya wasomi wanasema kuwa Mungu aliumba mbingu kabla hajaumba ardhi, "Je, Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu na yeye Ndiye aliyeijenga. Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri. Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake. Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi." (Kurani 79:27-30)

Mungu anasema katika Qurani,

"Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi katika siku sita." (Kurani 7:54)

Hakika Mungu hahitaji siku sita, Mungu angeweza kusema tu, “Kuwa,” na ingekuwa imekuwepo. Kwa nini Mungu ameziumba katika siku sita kinyume na sekunde moja tu au chini yake? Pengine, Mungu alitaka kutufundisha mojawapo ya sifa zinazopendwa Kwake, ambazo ni kuchukua vitu polepole na kuzipanga vizuri.

Bahari, Mito na Mvua

Mwenyezi Mungu anatuambia kwamba Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi, na akateremsha mvua kutoka mbinguni, inayoleta matunda na riziki kwa ajili ya kuishi kwetu. Mungu alitupatia bahari na merikebu ili tupite juu ya bahari hizi. Mungu aliiweka mito kwa huduma yetu na kuweka jua na mwezi katika mizunguko yao. Mungu aliweka usiku na mchana kwa ajili ya maslahi yetu. Mungu anasema kwamba alitupa kila kitu tunachohitaji ili tuweze kuishi. Kama tungejaribu kuhesabu baraka za Mungu, hatungeweza kufanya hivyo. (tazama Qurani 14:32-34).

"Yeye ndiye aliye ifanya bahari ikutumikieni, ili kutokana na humo mpate kula nyama laini, na mtoe humo mapambo mnayo yavaa. Na unaona marikebu zikikata maji humo, ili mtafute fadhila yake, na mpate kushukuru.Na kaweka katika ardhi milima ili ardhi isiyumbe yumbe nanyi.Na mito, na njia ili mpate kuongoka.Na alama nyengine. Na kwa nyota wao wanajiongoza.Ati anaye umba ni kama asiye umba? Basi hebu, hamkumbuki?Na mkizihisabu neema za Mwenyezi Mungu, hamwezi kuzidhibiti.Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira, Mwenye kurehemu." (Kurani 16:14-18)

Ardhi inatufaidisha kwa njia zisizohesabika. Ukiangalia uso wa ardhi, Mungu anasema kwamba alitufanyia kuwa rahisi kwa ajili yetu, yaani ni rahisi kutembea juu yake. Sasa fikiria kama uso wa ardhi ungekuwa kama milima na sisi sote tulipaswa kuishi katika mikoa ambayo ni mbaya na vigumu kutembea. Alifanya uso laini ili tuweze kuchimba ndani yake na kupanda mbegu. Lakini wakati huo huo, alifanya dunia imara ili kuruhusu ujenzi na matumizi ya vifaa vyake kwa ujenzi huo. Pia aliunda nguvu za uvutano au graviti ili tusiruke ruke kila mahali.

Jua na Mwezi

Jua ni uumbaji mkubwa wa Mungu na utaona kwamba Mungu anaapa kwa jua katika Sura ya Ash-Shams ili tutoe shukrani zaidi kwa zawadi hii aliyotupa. Dini nyingi zamani zilipea jua sifa za kipekee; watu wengi waliabudu jua. Mungu anasema,

"Na katika Ishara zake ni usiku na mchana, na jua na mwezi. Basi msilisujudie jua wala mwezi, bali msujudieni Mwenyezi Mungu aliye viumba, ikiwa nyinyi mnamuabudu Yeye tu." (Kurani 41:37)

Kwa jua, mwezi, na nyota kuna ushirikina mwingi na hata wanadamu wenye busara watakuwa na ushirikina huu wa ajabu sana. Watu mara nyingi huweka mantiki kando linapokuja kwa suala la ushirikina. Kuna unajimu, na mambo mengine yanayofanana nayo ambayo hayana maana kabisa, lakini huwapa watu matumaini ambayo sio kweli au huwapa watu sababu ya woga wao. Uislamu unakataza kabisa kwenda kwa wanajimu au kuwaamini.

Uumbaji wa Malaika

Kisha Mwenyezi Mungu akawaumba Malaika kutokana na nuru. Hawana uwezo wa kumuasi Yeye, na hufanya kama walivyo amrishwa. Wana wajibu wa kufanya kazi nyingi tofauti. Kwa mfano, Gabrieli alikuwa na jukumu la kufikisha ufunuo kutoka kwa Mungu kwa mitume. Mungu kwa kutufundisha kuhusu malaika, anatufafanulia uadilifu wa ujumbe kama ulivyokuja kwa mitume, kati ya mambo mengine mengi.

Kitu cha pekee kuhusiana na imani ya Kiislamu kuhusu malaika ni kwamba hatuamini kwamba kuna malaika yeyote aliyeasi, na hatuamini kwamba Ibilisi alikuwa malaika.

Zaidi ya hayo, malaika sio roboti. Wana tabia nyingi; hupenda na huchukia, huomba, na huegemea mambo fulani, lakini yote ni ndani ya upeo wa utiifu kwa Mungu.

Uumbaji wa Majinni

Waliumbwa kutoka kwa moto, lakini sio tu kutoka kwa aina yoyote ya moto, lakini kutoka kwa moto usio na moshi.[1] Mungu aliwaumba mbele yetu. Lengo la uumbaji wao ni sawa na la wanadamu: kumwabudu na kumtumikia Mungu peke yake.

Uumbaji wa Wanadamu

Binadamu wa kwanza kuumbwa alikuwa Adamu. Hadithi ya uumbaji wake na matukio yaliyofuata yameongelewa kwa undani katika mfululizo mwingine wa makala kwenye tovuti yetu [2].



Vielezi-chini:

[1] Ili kujifunza mengi zaidi kuwahusu, tafadhali tazma: https://www.islamreligion.com/articles/669/viewall/world-of-jinn/

[2] Ili kutazama mfululizo wa makala hii, tafadhali bonyeza hapa: https://www.islamreligion.com/articles/1190/viewall/story-of-adam/

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa