Eric Schrody, MKatoliki wa Zamani, Marekani (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mazungumzo na mwimbaji wa zamani wa rapu, nyota EverLast na safari yake kuelekea Uislamu. Sehemu ya 1.

  • Na Adisa Banjoko (interviewer)
  • Iliyochapishwa mnamo 14 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,012
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Muziki wa Rapu umepata hadhi mkubwa kwa kiasi fulani kutokana na dini ya Uislamu. Makundi kama vile Public Enemy yalitoa muziki kuhusu heshima yao kwa kundi la Taifa la Islam, huku watu kama vile Q-Tip wa kundi linaloitwa Quest wakiingia katika Uislamu, dini hii inaonekana kuwa maudhui ya kurejea rejea katika muziki wa Rapu, ikiathiri mistari na maisha pia. Msanii mmoja ambaye hivi karibuni aliathirika na Uislamu ni Eric Schrody, anayefahamika zaidi katika dunia ya muziki kama Everlast.

Ingawa Everlast alianza kazi yake ya muziki kama msanii wa rapu, hivi karibuni amejionyesha kuwa na kina zaidi na utofauti. Albamu yake ya sasa, Whitey Ford Sings the Blues (kwa sasa imeshika nafasi ya #49 kwenye chati za Billboard baada ya kushika nafasi ya #9) inaonyesha hili kwa sauti yake ya kutafakari na kwa kiasi fulani ya kifalsafa, ikionyesha athari Uislamu umekuwa nayo katika maisha yake.

Kinachofuata ni mahojiano ambapo Everlast anaeleza safari yake kwa Uislamu na changamoto anazozikabili kama Mwislamu.

AB: Niambie mara ya kwanza ulipojifunza kuhusu Uislamu?

E: Ilikuwa labda karibu na mwishoni mwa miaka ya 1980. Nilikuwa naketi na Divine Styler (msanii maarufu wa rapu wa Los Angeles). Alikuwa mwishoni mwa kipindi chake cha 5% (akimaanisha dhehebu la bandia la “Taifa la Miungu na Dunia” kundi). Alikuwa akianza kuingia katika Uislamu. Aliishi na familia ya Bashir. Abdullah Bashir alikuwa kwa kiwango fulani mwalimu wake; na baadaye akawa wangu pia. Alipokuwa akifanya mpito kutoka 5% kuingia Uislamu, ningekuwa karibu naye na hivyo kujua mambo mengi.

Ninajaribu kufikiria mara ya kwanza nilipoitambua kama Uislamu. Nadhani ilikuwa wakati mmoja wa marafiki wa Divine alipochukua Shahadah (ushuhuda wa Kiislamu wa imani) na nilikuwa huko. Nikamsikia akisema: “Nashuhudia ya kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu, na Muhammad ni mtumwa na Mtume.“ Na ninakumbuka nikiwaza, “Hii ni nini? Mimi ni mzungu. Naruhusiwa kuwa hapa kweli?” Ilikuwa ni kutokana na ujahili, kwa sababu hapa Marekani, Uislamu unachukuliwa kuwa “kitu cha watu weusi.” Na hapo ndipo mtu aliniambia, “Huwezi amini kuna Waislamu wangapi weupe duniani.” Nilisema , “Kwa uhakika?” na mtu akanieleza. Nikasema, “Hilo ni jambo kubwa. Sikujua.“

AB: Je, unahisi shinikizo lolote la ziada kwa kuwa Muislamu mweupe nchini Marekani?

E: Siifikirii kwa kiwango kikubwa. Kwangu mimi, Uislamu ni wangu. Mwenyezi Mungu ni Mungu wa walimwengu wote, na wanadamu wote, na Aalameen (walimwengu wote). Uislamu ni uhusiano wangu binafsi na Mungu. Kwa hivyo hakuna yeyote anayeweza kunishinikiza zaidi kuliko ninavyoweza kujishinikiza. Lakini kulingana na msikiti ambapo ninaswali, sijawahi kuhisi nipo nyumbani kwingine kama ninavyohisi nikiwa huko. Na siyo wangu tu. Misikiti michache ambayo nimeenda kote nchini, sijawahi kufanywa kusikia wasiwasi. Kama huko New York, msikiti ni mkubwa na kuna watu wengi sana hadi kwamba hakuna mtu anayekutazama au kukutambua. Kulikuwa na Wachina, Wakorea, Wahisapania- kila mtu, na hilo ni jambo zuri kwangu kwa sababu katika msikiti wangu mimi ndiye kiume pekee mweupe, [ingawa] kuna wanawake wazungu.

Nadhani kwa mara ya kwanza, nilifikiria kuhusu hilo zaidi ya kila mtu mwingine nilipokwenda Jumma (sala ya mkutano wa Ijumaa). Mara yangu ya kwanza kwenda Jumma, nilichukuliwa na rafiki yangu huko New York. Ilikuwa katika Brooklyn katika Bed-Stuy (Bedford Stuyvestant). Nilikuwa na wasiwasi kuhusu mtaa niliokuwa, si msikiti. Lakini niliishiwa na wasiwasi wote pindi nilipofika huko. Niliwaza, “Haya ni mazuri.” Sikuhisi utofauti wowote kuliko mtu mwingine yeyote katika msikiti.

AB: Familia yako ilichukulia aje Uislamu wako? Kwa sababu ulilelewa kikatoliki, sivyo?

E: Kusema kweli, unajua mama yangu ni mtu mwenye nia safi sana, mwenye ujuzi mwingi. Mama yangu anaishi nami. Na nimelelewa maishani mwangu wote bila kuamini kwa Mungu, bali elimu tu ya kwamba yupo. Nilifundishwa kwamba kama [ningejua] chochote ulimwenguni, ningejua ya kuwa Mungu yupo. Na mama yangu, ingawa alikuwa Mkatoliki, alikuwa mtu wa kwanza kuelezea unafiki katika kanisa. Mama yangu kwa kweli hajahudhuria kanisa kwa muda mrefu. Lakini kuhusiana na mimi, mama yangu anafurahi kwamba nina Mungu katika maisha yangu.

Ananiona nikiswali. Na Kasisi ni mmoja wa watu anaowapenda sana duniani. Anajua jinsi tulivyobadilika sana kwa sababu alitujua tangu utotoni. Mimi na Kasisi tulipopatana mara ya kwanza, tulikuwa vichaa. Tulikuwa tukipoteza wakati kwa masherehe, vita, na kufanya chochote tulichohitaji kufanya. Tuliwaza, “Naam, hivi ndivyo mwanaume anafaa kuwa. Tutakwenda nje tuwe wahuni.”

[Lakini] ameona ni kiasi gani uislamu umetubadilisha mimi na yeye; na ni kiasi gani umeleta amani kwa maisha yangu tangu nianze kuyatumia vizuri. Hivi karibuni nilikuwa na majadiliano marefu na mama yangu na tulikuwa tukiongelea mada ya dini. Kwa kweli tulikuwa tunazungumzia kuhusu maisha na kifo, na wakati ujao na wakati anapoweza kwenda (kufa, kufariki). Hayo hayatakuwa karibuni, inshallah (Mwenyezi Mungu akipenda). Lakini nikamwomba anifanyie jambo moja. Nikasema, “Mama, unapokufa huenda kuna malaika watakaokuuliza swali, na nataka ujibu; na sijui hasa jinsi itakavyokwenda, kwa sababu sijafa bado. Kumbuka kwamba kuna Mungu mmoja tu, na hajawahi kuwa mwanadamu.“

Akasema, “Najua unachojaribu kuniambia.” [Na] nikasema, “Yesu hakuwa Mungu, Ma.”

Baadhi ya ninayoyajua kwa hakika yamedhihirika katika maisha ya mama yangu. Yeye si Muislamu, lakini anajua kuna Mungu mmoja tu. Na hilo hunifurahisha sana. Najua vijana wengi ambao wameingia Uislamu, na jamaa zao zimewageukia (wamewakataa).

Mbaya Nzuri zaidi

Eric Schrody, Mkatoliki wa Zamani, Marekani (sehemu ya 2 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mazungumzo na mwimabji wa zamani wa rapu, nyota EverLast na safari yake ya kuelekea Uislamu. Sehemu ya 2.

  • Na Adisa Banjoko (interviewer)
  • Iliyochapishwa mnamo 14 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,713
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

AB: Familia yangu ilijaribu hivyo. Kusema kweli, siwezi kuelewa hilo. Lakini unajua nini? Hilo ni mtihani. Ingawa nimebadilisha jina langu kwa miaka kama nane sasa, bado wananiita kwa jina langu la kuzaliwa. Kisha ni, “Oh Nimesahau wewe ni Muislamu.” Kisha ni utani wa nyama ya nguruwe. Haiishi kamwe.

E: Ni mojawapo ya mambo ambapo watu huchekelea kile ambacho hawakielewi. Au wanaogopa wasichoweza kukifahamu. Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kujifanya kuwa haelewi. Kwa sababu sijawahi kukutana na kitu chochote rahisi zaidi kuliko uislamu katika maisha yangu.

Kwa mfano ninakumbuka kwamba nilipokuwa nikiketi na kuuliza, “Sasa, Muislamu anaamini nini,” na nikapewa orodha ya vitu kadhaa. Nikasema, “Hamuweki ukuta kati ya Ukristo na Uyahudi.” Wakasema, “La, ni mambo yale yale.”

Ikiwa utaketi chini na kusoma Qurani, Biblia na Torati, ambayo ni Agano la Kale tu, utaona kwamba Qur'ani ni uthibitisho wa yaliyo sahihi na yasiyo sahihi ndani ya vitabu hivyo (Biblia na Torati). Na kisha unajiambia, “Jinsi gani jambo hilo lilitokea ilhali vitabu hivi vilishuka katika sehemu tofauti tofauti ardhini?” Lakini vyote vinathibitisha mafundisho ya kila moja.

Sahii ninasoma kitabu kinachoitwa Muhammad: Maisha ya Mtume, cha Karen Armstrong. Iliandikwa na mtu ambaye si Mwislamu. Kwa sasa, niko karibu kufika robo ya kitabu hicho; lakini inaanza kukueleza jinsi walivyojaribu kumfanya Muhammad aonekane kama mtu mbaya zaidi duniani; kwamba alianzisha Uislamu kwa kutumia upanga. Lakini unajifunza baadaye kuwa Muhammad alipigana tu ilipobidi apigane. Muhammad alipigana tu ili kulinda Uislamu. Ni kitabu kizuri sana kuhusu mtume. Inakuwezesha kujua kwamba alikuwa binadamu tu. Hatujaribu kukuambia kwamba alikuwa kitu kingine chochote isipokuwa mwanadamu. Tunakuambia kama Waislamu kwamba alikuwa mfano kamili kabisa wa mwanadmu bora aliyewahi kutembea ardhini mpaka sasa. Na kutokana na kile nilichokisoma yeye ndiye wa mwisho kuja wa aina yake.

Unapojiondolea woga wa Farrakhan na anachosema -- na hapa ninaongea kama mtu mweupe -- unapopita kiwango cha ujahili wa kuamini kuwa Uislamu unahusiana tu na watu wanaolipua vitu, unakuja kuelewa kuwa hao hawana uhusiano wowote na Uislamu. Wanaweza kufanya mambo yao kwa jina la Uislamu. Lakini hawahusiani na Uislamu. Huwezi kubishana na hilo.

Ninapoeleza kuhusu Yesu kwa Mkristo, hawezi kubishana na mimi. Wala simaanishi abishane kwa kusema, “Yesu si Mungu!” Namaanisha, ni mantiki ya kiasi gani iko katika kusema kuwa yeye ni mwanadamu? Kama ningekuwa Mkristo, ambayo kwangu ina maana ya kuwa kama Kristo, na Mungu aniulize, “Kwa nini hukuwa kama Yesu?” Nitasema, Sikuwa kama Yesu kwa sababu umemfanya awe nusu Mungu [na] mimi ni mwanadamu tu?” Hiyo haileti maana yoyote.

Mungu hataki mambo yawe magumu kwetu. Mwenyezi Mungu anataka mambo yawe mepesi iwezekanavyo. Mungu atayafanya yawe rahisi iwezekanavyo. Ukiuliza, ilhali wewe ni mkweli, Mwenyezi Mungu atakupa. Anaweza kuweka baadhi ya mawe kwa njia yako, ili uteleze na ujikwae. Lakini utaipata hatimaye.

AB: Niambie kuhusu mara ya kwanza na ya pili ulipochukua Shahadah yako (ushuhuda wa imani).

E: Kwa mara ya kwanza ilikuwa ni baada ya kusikia kanda kutoka kwa Warith Deen Muhammad (mwana wa mwanzilishi wa Taifa la Islam Elijah Muhammad, ambaye alipeleka sehemu kubwa ya Taifa la Uislamu kwa Uislamu wa kawaida). Alieleza vizuri mambo yote kuhusiana na Yesu. Alifafanua kwamba sisi (Waislamu) tunawafanyia Wakristo hisani kubwa kwa kumleta Yesu chini kwa kiwango cha mwanadamu. Kwa nini Mungu amuumbe mtu ambaye ni nusu Mungu na kutulinganisha naye? Na hilo lililipua bomu katika kichwa changu. Hivyo nikachukua Shahadah. Na kisha hisia za awali zikaisha.

Ni kama Mkristo anayesema kwamba anamkubali Yesu. Kisha anasema, “Haijalishi ninachofanya sasa, nimeokoka.” Kwa sababu nililelewa na mawazo ya aina hayo. Yaani, “ Nakubali ukweli sasa, hivyo basi wacha tu niende zangu na nifanye madhambi ninayoyataka kwa sababu nimeokoka.”

Kwa kweli sikujidai kuwa Muislamu wakati huo. Nilichukua na kuchagua nilichotaka kuamini. Mungu alinipa nafasi kwa muda. Lakini hatimaye wakati uliwadia. Nilifika kiwango ambapo sikuridhika kihisia na kiroho. Nilikuwa na pesa kwenye benki na gari la dola 100,000, wanawake kushoto na kulia -- kila kitu unachofikiri unakitaka. Na kisha nimekaa tu hapo nikiwaza, “Mbona sina furaha?” Hatimaye sauti hiyo inayozungumza nawe -- sio minong'ono (ya Shetani) -- sauti ikasema, “Naam, kimsingi huna furaha kwa sababu unaishi maisha machafu na hutaki kujaribu kufanya chochote kuhusu hilo.”

Ukaidi wangu wakati huo haungeweza kuniruhusu kuzungumza juu ya hilo wakati huo. Unaingia katika hali hiyo ya akili ambapo unajiambia, “Ninaweza kutatua haya yote peke yangu.”

Hatimaye nilipata unyenyekevu wa kutosha kuzungumza na Divine na Abdullah kuhusu hilo. Wakaniuliza, “Unasikiaje? Unafikiri ni nini?” Kwa hivyo hatimaye nimeketi hapo nikichukua Shahadah tena. Kutoka wakati huo nimejiahidi kuwa nitajaribu kwa kadri ya uwezo wangu. Nitajitahidi sana kuswali sala zangu, hebu tuanze huko. Tusijilaumu vibaya kwa sababu tulitoka jana usiku na kulewa. Hebu tuswali sala zetu na kuomba tupate nguvu ya kuacha kufanya jambo moja kwa wakati. Hiyo ndio bado nashughulika nayo.

Unajua, mara baada ya kujiondolea mambo makubwa, mengine yatafuata kichini chini tu. Unaweza kumwona mtu, na hata usimzungumzie vibaya, lakini unamsengenya akilini. Yale yaliyo rahisi kuyashinda -- sipaswi kusema rahisi -- yale makubwa ni rahisi kuyaona. Ni mabadiliko madogo madogo ya kisaikolojia yasiyoonekana ambayo hukusaidia kubadilika vizuri. Lazima uwe na uwezo wa kukubali ukweli wa hali yako. Kama huwezi kukubali ukweli wako na kujua wewe ni nani, utabomoka kwa urahisi.

Watu wananiuliza , “Wewe ni Muislamu?” Nasema, “Naam, mimi ni Muislamu, lakini mimi pia ni mfanya dhambi mtaalamu.” Najaribu kuziacha, najaribu kustaafu. Siwezi simama mbele na kusema mimi ni bora kuliko wewe. Ninaamini tu kwamba nimeonyeshwa ukweli na ninatumai ukweli huo utaniokoa.”

Adisa Banjoko ni mwandishi huru katika eneo la Bay la San Francisco.

mada

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.