Jeffrey Lang, Profesa wa Hisabati na Mwandishi, Marekani

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Hadithi ya profesa mshirika na baadaye mwandishi wa vitabu vitatu safari ya kuelekea Uislamu.

  • Na Ammar Bakkar
  • Iliyochapishwa mnamo 18 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,315 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Jeffrey_Lang__Professor_of_Mathematics_and_Writer__USA_001.jpgDkt. Jeffrey Lang ni Profesa Mshirika wa Hisabati katika Chuo Kikuu cha Kansas, mojawapo ya vyuo vikuu vikubwa zaidi nchini Marekani. Alianza safari yake ya kidini mnamo Januari 30, 1954, alipozaliwa katika familia ya Kikatoliki huko Bridgeport, Connecticut. Miaka 18 ya kwanza ya maisha yake aliitumia katika shule za Kikatoliki, jambo ambalo lilimwacha na maswali mengi yasiyo na majibu kuhusu Mungu na dini ya Kikristo, Lang alisema, alipokuwa akisimulia hadithi yake ya Uislamu. "Kama watoto wengi huko nyuma mwishoni mwa miaka ya 60 na mwanzoni mwa miaka ya 70, nilianza kutilia shaka maadili yote tuliyokuwa nayo wakati huo, kisiasa, kijamii na kidini," Lang alisema. "Niliasi taasisi zote ambazo jamii iliziona kuwa takatifu, ikiwemo Kanisa Katoliki," alisema.

Kufikia umri wa miaka 18, Lang alikuwa haamini kabisa kwamba kuna Mungu. “Ikiwa kuna Mungu, na Yeye ni mwenye rehema na upendo wote, basi kwa nini kuna kuteseka duniani? Kwa nini hatupeleki tu mbinguni? Kwa nini aliwaumba watu hawa wote wateseke?” Hayo ndiyo maswali yaliyokuwa yakimjia kichwani siku hizo.

Akiwa mhadhiri mchanga wa hisabati katika Chuo Kikuu cha San Francisco, Lang aliipata dini yake ambapo hatimaye Mungu ni kiumbe halisi . Hilo alionyeshwa na marafiki wachache wa Kiislamu aliokutana nao chuoni hapo. “Tulizungumza kuhusu dini. Niliwauliza maswali yangu, na nilishangazwa sana na jinsi walivyofikiria majibu yao kwa uangalifu,” Lang alisema.

Dkt. Lang alikutana na Mahmoud Qandeel, mwanafunzi wa Kisaudi ambaye alilivutia darasa zima alipoingia ndani. Lang alipouliza swali kuhusu utafiti wa kimatibabu, Qandeel alijibu swali hilo kwa Kiingereza kikamilifu na kwa kujiamini sana. Kila mtu alimjua Qandeel - meya, mkuu wa polisi, na watu wa kawaida. Profesa pamoja na mwanafunzi huyo walienda sehemu zote zenye kumeta-meta ambako “hakukuwa na shangwe wala furaha, bali vicheko tu.” Lakini mwisho, Qandeel kwa mshangao alimpa nakala ya Quran na baadhi ya vitabu kuhusu Uislamu. Lang alisoma Quran peke yake, akapata njia ya kuelekea kwenye ukumbi wa maombi unaoendeshwa na wanafunzi katika chuo kikuu, na kimsingi akajisalimisha bila kuhangaika sana. Alitekwa na Quran. Sura mbili za kwanza ni simulizi ya kukutana huko na ni ya kuvutia.

“Wachoraji wanaweza kufanya macho ya picha yaonekane yanakufuata kutoka sehemu moja hadi nyingine, lakini ni mwandishi gani anayeweza kuandika andiko ambalo linatarajia mabadiliko yako ya kila siku?... Kila usiku ningetunga maswali na pingamizi na kwa namna fulani kugundua jibu kesho yake. Ilionekana kuwa mwandishi alikuwa akisoma mawazo yangu na kuandika katika mistari mahususi katika kipindi cha usomaji wangu unaofuata. Nimekutana na mimi kwenye kurasa zake…”

Lang huswali mara tano kila siku na hupata radhi nyingi za kiroho. Anaiona swala ya Alfajiri (kabla ya alfajiri) kama mojawapo ya ibada nzuri na zenye kusisimua katika Uislamu.

Kwa swali la jinsi gani anavutiwa na usomaji wa Kurani wakati ipo kwa Kiarabu, jambo ambalo ni geni kabisa kwake, anajibu; "Kwa nini mtoto hufarijiwa na sauti ya mama yake?" Alisema kusoma Quran kulimpa faraja na nguvu kubwa katika nyakati ngumu. Kuanzia hapo na kuendelea, imani ilikuwa suala la mazoezi kwa ukuaji wa kiroho wa Lang.

Kwa upande mwingine, Lang aliifuatilia kazi ya hisabati. Alipata digrii zake za uzamili na udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Purdue. Lang alisema kwamba sikuzote amekuwa akivutiwa na hisabati. “Hesabu ina mantiki. Inajumuisha kutumia ukweli na takwimu kupata majibu halisi," Lang alisema. "Hivyo ndivyo akili yangu inavyofanya kazi, na inafadhaisha ninaposhughulika na mambo ambayo hayana wajibu kamili." Kuwa na akili inayokubali mawazo juu ya uhalali wao hufanya kuamini dini kuwa ngumu kwa sababu dini nyingi zinahitaji kukubalika kwa imani, alisema. Uislamu unavutia fikra za mwanadamu, alisema.

Kama mshauri wa kitivo cha Jumuiya ya Wanafunzi wa Kiislamu, Lang alisema alijiona kama kiunganishi kati ya wanafunzi na vyuo vyao vikuu. Anapata kibali kutoka kwenye mamlaka ya chuo kikuu kufanya mihadhara ya Kiislamu. "Lengo la kuwa mshauri wa kitivo chao ni kuwasaidia kupata mahitaji yao hadi kuzoea utamaduni wa Marekani na taratibu za chuo kikuu. Wanathamini fursa ya marekebisho ya imani potofu,” alisema.

Lang alioa mwanamke Mwislamu wa Saudia, Raika, miaka 12 iliyopita. Lang ameandika vitabu kadhaa vya Kiislamu ambavyo vinauzwa zaidi miongoni mwa jamii ya Kiislamu nchini Marekani. Moja ya vitabu vyake muhimu ni “Even Angels ask; A Journey to Islam in America”. Katika kitabu hiki, Dkt. Lang anawashirikisha wasomaji wake maarifa mengi ambayo yamejitokeza kwa ajili yake kupitia ugunduzi wake binafsi na maendeleo ndani ya dini ya Uislamu.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.