Kristin, Mkatoliki wa zamani, Marekani (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mkristo wa zamani anajadili mambo ya Kikristo ambayo aliyaona hayapatani na akili na alivyozingatia Uyahudi.

  • Na Kristin
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,795
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Utafiti wangu wa dini ulianza nikiwa katika shule ya sekondari nilipokuwa na umri wa miaka 15 au 16. Nilikuwa nikishirikiana na kundi la watu wabaya ambao nilidhani walikuwa marafiki zangu, lakini baada ya muda nilitambua watu hawa walikuwa hawana maana yoyote. Niliona mwelekeo gani maisha yao yalikuwa yakielekea, na haukuwa mzuri. Sikutaka watu hawa wawe na athari yoyote juu ya mafanikio yangu kwa siku zijazo, kwa hivyo niliwachana nao kabisa. Ilikuwa vigumu mwanzoni kwa sababu nilikuwa peke yangu bila marafiki. Nilianza kutafuta kitu cha kujiunga nacho na kitu ambacho ningeweza kukitegemea na kuhusisha maisha yangu nacho... kitu ambacho hakuna mtu angeweza kukitumia kuharibu mustakabali wangu nacho. Kwa kawaida, niligeuka kumtafuta Mungu. Hata hivyo, kujua Mungu alikuwa nani na ukweli ulikuwa nini halikuwa jambo rahisi. Kwani, hivi ukweli ni nini?! Hili lilikuwa swali langu la msingi nilipoanza kutafuta dini.

Katika familia yangu, kumekuwa na mabadiliko mengi ya kidini. Familia yangu ina Wayahudi na aina chache za Ukristo ndani yake, na sasa, Alhumdulilah (wa kutukuzwa ni Mwenyezi Mungu) ina Uislamu.

Mama yangu na baba yangu walipoana, walihisi kulikuwa na haja ya kuamua watawalea watoto wao kwa dini gani. Kwa kuwa Kanisa Katoliki lilikuwa ndilo chaguo pekee kwao (mji wetu una watu 600 tu) wote wawili wakawa wakatoliki na kutulea mimi na dada yangu kama Wakatoliki. Nikirudi kupitia hadithi za ubadilishaji wa dini katika familia yangu, inaonekana kwamba yote ni mabadiliko ya kutafuta masilahi ya kibinafsi. Sidhani walikuwa wanamtafuta Mungu kikweli, bali walitumia dini kama njia tu ya kufikia lengo fulani. Hata baada ya mabadiliko haya yote ya mbeleni, dini haikuwa na umuhimu mkubwa kwa mama, baba na dada yangu, na kwangu mimi pia. Yetu ilikuwa kama zile familia unaowaona kanisani wakati wa Krismasi na Pasaka. Siku zote nilihisi kuwa dini ilikuwa kitu tofauti na maisha yangu, siku 6 kwa wiki kwa maisha yangu na siku moja kwa wiki kwa ajili ya kanisa, katika siku chache nilipokwenda. Kwa maneno mengine, sikuwa na ufahamu wa Mungu wala jinsi ya kuishi kulingana na mafundisho yake kila siku.

Sikukubaliana na baadhi ya sera za Kikatoliki kama:

1) Kukiri dhambi kwa kuhani: Nilifikiria kwa nini sikuweza kukiri tu kwa Mungu bila ya kwenda kupitia mwanadamu ili kumfikia?

2) Papa “Mkamilifu ”- Itakuwaje mwanadamu, ambaye hata si mtume, awe mkamilifu?!

3) Kuabudu watakatifu- je, hii haikuwa ukiukaji wa moja kwa moja wa amri ya kwanza? Hata baada ya miaka 14 ya kulazimishwa kuhudhuria shule ya Jumapili, majibu niliyopokea kwa maswali haya na mengine yalikuwa, “Unahitaji tu kuwa na imani!!” Je, nafaa kuwa na imani kwa sababu mtu ALINIAMBIA hivyo?! Nilidhani imani inapaswa kutokana na ukweli na majibu ambayo yaliafikiana na mantiki. Nilikuwa na nia ya kupata baadhi ya majibu haya.

Sikutaka ukweli wa wazazi wangu, au marafiki, au mtu mwingine yeyote. Nilitaka ukweli wa Mungu. Nilitaka kila fikira niliyoshikilia iwe kweli kwangu kwa sababu niliiamini kabisa, kwa moyo na roho. Niliamua kwamba iwapo ningepata majibu ya maswali yangu, ningetafuta kwa akili wazi, na nilianza kusoma...

Niliamua kwamba Ukristo haungekuwa dini yangu. Sikuwa na uadui wowote binafsi na Wakristo, lakini nimeona kuwa dini yenyewe ilikuwa inatofautiana kwa wingi, hasa niliposoma Biblia. Katika Biblia, tofauti nilizokutana nazo na mambo ambayo hayakunikaa akilini kabisa yalikuwa mengi kiasi kwamba nilihisi aibu kwamba sijawahi kujiuliza kuhusu hayo mbeleni au hata kuyaona!

Kwa kuwa baadhi ya watu katika familia yangu ni Wayahudi, nilianza kuchunguza Uyahudi. Nilidhani jibu linaweza kuwa pale. Kwa hivyo kwa mwaka mmoja nilifanya utafiti juu ya kitu chochote kuhusu Uyahudi, namaanisha utafiti WA KINA!! Kila siku nilijaribu kusoma na kujifunza kitu (bado najua kuhusu sheria za Kiorthodoksi za Kiyahudi za kosha!). Nilikwenda maktabani na kuangalia kila kitabu kuhusu Uyahudi ndani ya muda wa miezi miwili. Kwenye mtandao, nilikwenda kwenye sinagogi, nikazungumza na Wayahudi wengine katika miji ya jirani na kusoma Torati na Talmud. Hadi nilimuita mmoja wa marafiki zangu wa Kiyahudi kuja kunitembelea kutoka Israeli! Nilidhani labda nimepata kile nilichokuwa nikitafuta. Hata hivyo, ile siku nilitakiwa kwenda sinagogi na kukutana na rabi kuhusu uwezekano wa kuingia rasmi kwenye Uyahudi, nilijiondoa. Kusema kweli sijui nini ilinizuia kuondoka nyumbani siku hiyo, lakini nilisimama tu nilipokuwa karibu kwenda nje ya mlango na kurudi ndani na kukaa chini. Nilihisi kana kwamba nilikuwa katika mojawapo ya ndoto hizo ambapo unajaribu kukimbia lakini kila kitu kinakwenda polepole. Nilijua rabi alikuwa pale akinisubiri, lakini sikumpigia hata kumwambia kuwa naja. Rabbi hakunipigia pia. Kuna kitu kilikuwa hakiko...

Baada ya kujifunza kwamba Uyahudi pia haukuwa jibu, nilifikiri (pia baada ya shinikizo kubwa kutoka kwa wazazi wangu) kujaribu Ukristo mara nyingine. Nilikuwa na, kama nilivyosema, historia nzuri katika misingi kutokana na miaka yangu ya shule za Jumapili, lakini nilikuwa nataka kujua zaidi na kupata ukweli nyuma ya misingi hii. Uzuri wake ulikuwa wapi, usalama wake ulikuwa wapi na ningeweza vipi kuikubali kimantiki? Nilijua kwamba iwapo ningezingatia Ukristo, Ukatoliki haukuwa hiari kwangu. Nilikwenda kwa kila kanisa lingine la Kikristo katika mji wangu, Kilutheri, Pentekoste, Watakatifu wa Siku za Mwisho (Mormoni), na makanisa yasiyo ya madhehebu. Sikupata kile nilichokuwa nikitafuta - majibu!! Haikuwa mazingira ya watu ndio niliyokataa; ilikuwa ni utofauti kati ya madhehebu ndio ulinisumbua. Niliamini kulikuwa na njia moja sahihi, kwa hivyo ningewezaje kuchagua dhehebu “sahihi”? Katika makadirio yangu ilikuwa haiwezekani kwa Mungu mwenye huruma kuwaacha wanadamu na chaguo kama hilo. Nilikuwa nimepotea...

Mbaya Nzuri zaidi

Kristin, Mkatoliki wa Zamani, Marekani (sehemu ya 2 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Baada ya kujua kuhusu Uislamu katika chumba cha mazungumzo mtandaoni, Kristin anajikuta akilia huku akisoma Qurani katika maktaba huku akitafiti dini.

  • Na Kristin
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,571
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Katika hatua hii nilikuwa nimechanganyikiwa kama nilivyokuwa hapo awali nilipoanza utafiti wangu. Nilihisi kutupa mikono yangu kwa Mungu na kupiga kelele, “Nifanye nini sasa?” Sikuwa Myahudi, sikuwa Mkristo; nilikuwa tu mtu aliyemwamini Mungu mmoja. Nilifikiria kuacha kabisa dini zilizopangika. Nilitaka tu ukweli, sikujali umetoka kwa kitabu kipi kitakatifu; Niliutaka ukweli tu.

Siku moja nilikuwa nikisoma kwenye mtandao na nikaamua kuchukua mapumziko na kuingia katika chumba cha mazungumzo kwenye mtandao. Niliona chumba cha “mazungumzo ya dini”, ambayo bila shaka nilikuwa nakitaka, kwa hivyo nilikifungua. Niliona chumba kinachoitwa “Mazungumzo ya Kiislamu”. Niingie? Nilikuwa natumai hakukuwa na magaidi ambao wangeweza kupata barua pepe yangu na kunituma virusi vya kompyuta - au mbaya zaidi. Picha za majitu waliokuwa wamevaa nguo nyeusi na wenye ndevu kubwa wakija mlangoni na kuniteka nyara zilinijia akilini. (Unaweza kusema nilikuwa na taarifa ya kiasi gani kuhusu Uislamu - sufuri!) Lakini nikajiambia, huu ni uchunguzi tu usio na hatia. Niliamua kuingia na kugundua kwamba watu katika chumba hiki hawakuwa wa kutisha kama nilivyofikiri wangekuwa. Kwa kweli, wengi wao waliitana “ndugu” au “dada” hata kama walikuwa wamekutana hapo tu! Niliwasalimia wote na kuwaambia wanieleze kuhusu misingi ya Uislamu - ambayo sikujua chochote kuihusu. Walichokuwa wakisema kilikuwa cha kuvutia na kiliafikiana na kile nilichoamini tayari. Baadhi ya watu walijitolea wanitumie vitabu na kwa hivyo nikasema sawa. (Aidha, sijawahi kupata virusi vyovyote na hakuna wanaume waliokuja mlangoni mwangu kunichukua, isipokuwa mume wangu lakini nilikwenda kwa hiari!)

Nilipotoka kwenye gumzo, Nilikwenda moja kwa moja kwa maktaba na kuangalia kila kitabu kilichohusu Uislamu, kama nilivyofanya na Uyahudi. Sasa nilikuwa na nia ya kusoma na kujifunza zaidi. Kabla ya hata kuweza kupeleka mzigo mkubwa wa vitabu nyumbani, nilitaka kuangalia ndani ya baadhi ya vitabu hivyo. Hii ilikuwa ni hatua muhimu sana kwangu... Vichache vya kwanza nilivyovioangalia vilielezea misingi kwa undani zaidi, vingine vilikuwa vya wasomi na baadhi vilikuwa na picha za misikiti nzuri sana na wanawake wenye mitandio. Kwa bahati nzuri nilipitia pia Qur'ani... niliifungua tu kokote na kuanza kusoma. Lugha ndio ilinivutia mwanzo, nilihisi kana kwamba ninaongeleshwa na mwenye mamlaka juu yangu, si mwanadamu anayezungumza kama nilivyopata katika maandiko mengine “matakatifu”. Kifungu nilichokisoma (na kwa bahati mbaya sijui ni kipi) kilizungumzia kile ambacho Mungu anatarajia tukifanye katika maisha haya na jinsi ya kuishi kulingana na amri zake. Kilisema kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kurehemu, Mwenye rehema, Mwenye kusamehe. Muhimu zaidi, kwake Yeye ndio kurudi kwetu. Kabla ya kujua, ningeweza kuhisi machozi yakianguka kwa kurasa ambazo nilikuwa nikisoma. Nilikuwa nikilia katikati ya maktaba, kwa sababu hatimaye, baada ya kutafuta kwangu na kuchanganyikiwa kwangu, nimepata nilichokuwa nikitafuta- Uislamu. Nilijua Qurani ilikuwa ni kitu cha kipekee kwa sababu nilikuwa nimesoma maandiko mengi ya kidini, na HAKUNA hata moja ilikuwa wazi hivi au kunipa hisia kama hiyo. Sasa ninaweza kuona hekima ya Mungu... kwa kuniruhusu nichunguze Uyahudi na Ukristo vizuri kabla sijapata Uislamu, hivyo ningeweza kulinganisha zote na kutambua kuwa HAKUNA kitu kinachofanana na Uislamu.

Kuanzia wakati huo niliendelea kutafiti Uislamu. Niliianza kwa kutafuta hitilafu kama nilivyofanya na Uyahudi na Ukristo, lakini hapakuwa na zozote. Nilipitia kwa kina Qur'ani nzima nikitafuta hitilafu yoyote; na hata leo sijaweza kupata hitilafu au utofauti hata MMOJA ndani yake! Kitu kingine kikubwa ninachokipenda kuhusu Qurani ni kuwa inatoa wito kwa msomaji kujiuliza maswali kuihusu. Inasema kujihusu kwamba kama haingetoka kwa Mungu hakika ungepata hitilafu nyingi ndani yake! Sio tu kwamba Uislamu haukuwa na hitilafu, bali pia ulikuwa na jibu kwa swali lolote ambalo ningeweza kufikiria - jibu ambalo lina maana.

Baada ya miezi mitatu, niliamua kuwa Uislamu ndio jibu na kuingia rasmi katika Uislamu kwa kusema Shahadah. Hata hivyo, ilibidi niseme Shahadah yangu kwa simu nikizungumza na imam mmoja kutoka Pennsylvania kwa sababu hapakuwa na Waislamu au misikiti karibu nami (Msikiti wa KARIBU kabisa ulikuwa na umbali wa saa 6). Sijawahi kujuta kuhusu uamuzi wangu wa kuingia katika uislamu. Kwa kuwa hapakuwa na Waislamu wanaoishi karibu nami, nilipaswa kuchukua hatua na kujifunza mengi peke yangu, lakini sijawahi kuchoka nayo kwa sababu nilikuwa nikijifunza ukweli. Kukubali Uislamu kulikuwa kama kuamka kwa roho yangu, akili yangu na hata jinsi nilivyouangalia ulimwengu.

Ninaweza kuilinganisha na mtu ambaye haoni vizuri; anajitahidi kuona na kuelewa kila kitu darasani, hawezi kuwa makini na daima anapitia changamoto kwa sababu ya ulemavu wake. Ukimpa miwani, kila kitu kinakuwa wazi . Hivi ndivyo uzoefu wangu wa Uislamu ulivyo: kama kupokea miwani, ambayo imeniwezesha, kwa mara ya kwanza, kuona ukweli.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.