Utafutaji wa Amani ya ndani (sehemu ya 2 kati ya 4): Kukubali Hatima au takdiri

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Nakala hii ya pili inatoa mifano halisi na hadithi zinazoonyesha umuhimu wa kutambua kwamba kila mtu maishani anakabiliwa na vizuizi ndani ya uwezo wake na vizuizi vilivyo nje ya uwezo wake na kwamba vizuizi vilivyo nje ya uwezo wa mtu vinapaswa kuzingatiwa kama hatima kutoka kwa Mungu Mwenyezi.

  • Na Dr. Bilal Philips (transcribed from an audio lecture by Aboo Uthmaan)
  • Iliyochapishwa mnamo 04 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,200 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Tuna shida nyingi, vikwazo vingi sana kwamba ni kama magonjwa. Tukijaribu kushughulikia moja baada ya nyingine hatutavimaliza vyote. Tunahitaji kuvitambua, kuviweka katika jumla na kukabiliana navyo kama kikundi badala ya kujaribu kushughulikia kikwazo na shida ya kila mtu.

Ili kufanya hivyo lazima kwanza tuondoe vizuizi ambavyo viko zaidi ya uwezo wetu. Tunapaswa kuwa na uwezo wa kutofautisha ni vizuizi vipi ambavyo viko ndani ya udhibiti wetu na ni vipi ambavyo viko nje ya uwezo wetu. Wakati tunatambua zile ambazo ziko nje ya uwezo wetu kama vizuizi ukweli ni kwamba sio. Ndio vitu ambavyo Mungu amekusudia kwa ajili yetu katika maisha yetu, sio vizuizi kweli, lakini tumevitafsiri vibaya kuwa ni vizuizi.

Kwa mfano, katika wakati huu mtu anaweza kujikuta amezaliwa mweusi katika ulimwengu ambao unapendelea watu weupe kuliko watu weusi au kuzaliwa maskini katika ulimwengu unaowapendelea matajiri kuliko masikini, au aliyezaliwa mfupi, vilema au hali nyingine yoyote ya mwili ambayo inachukuliwa kuwa ni ulemavu.

Hivi ni vitu vyote ambavyo vilikuwa na viko nje ya uwezo wetu. Hatukuchagua familia ipi ingetuzaa;ni mwili gani ili roho zetu zipulizwe, hii sio chaguo letu. Kwa hivyo chochote tunachopata ya aina hizi za vizuizi basi lazima tuwe na subira nazo na tujue kwamba sio vizuizi kweli. Mungu alituambia:

“… Lakini huenda mkachukia kitu nacho ni kheri kwenu. Na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu. Na Mwenyezi Mungu anajua na nyinyi hamjui.” (Kurani 2: 216)

Kwa hivyo vizuizi ambavyo viko nje ya uwezo wetu tunaweza kuvichukia na kutaka kuvibadilisha, na watu wengine hutumia pesa nyingi kujaribu kuvibadilisha. Michael Jackson ni mfano bora. Alizaliwa mweusi katika ulimwengu unaopendelea watu weupe, kwa hivyo alitumia pesa nyingi kujaribu kujibadilisha lakini aliishia kuharibu mambo.

Amani ya ndani inaweza kupatikana tu ikiwa vizuizi ambavyo viko nje ya udhibiti wetu vinakubaliwa na sisi kwa uvumilivu kama sehemu ya hatima ya Mungu.

Jua kuwa chochote kinachotokea au hatuna uwezo juu yake, basi Mungu ameweka ndani yake kitu kizuri, ikiwa tunao au hatuna uwezo wa kufahamu yaliyo mema ndani yake basi mema bado yapo. Kwa hivyo tunaikubali!

Kulikuwa na nakala kwenye gazeti ambayo ilikuwa na picha ya mtu wa Misri anayetabasamu. Alikuwa na tabasamu usoni mwake kutoka sikio hadi sikio huku mikono yake ikiwa imenyooshwa na vidole gumba vyote vikiwa vimeinama juu baba yake alikuwa akimbusu kwenye shavu moja na dada yake kwenye shavu lingine.

Chini ya picha hiyo kulikuwa na maelezo mafupi. Alipaswa kuwa kwenye ndege ya Gulf Air ya Uarabuni siku iliyopita kutoka Kairo kwenda Bahrain. Alikuwa amekimbilia uwanja wa ndege kuwahi ndege na alipofika huko alikosa mhuri mmoja kwenye Pasipoti yake (huko Cairo lazima uwe na mihuri mingi kwenye stakbathi zako. Unapata mtu wa kupiga muhuri hii na kusaini hiyo na mtu huyo mwingine kufanya vile) lakini hapo alipo kwenye uwanja wa ndege bila muhuri mmoja. Kwa kuwa alikuwa mwalimu huko Bahrain na ndege hii ilikuwa ya mwisho kurudi Bahrain ambayo ingemwezesha kufika kwa wakati, kukosa ilimaanisha kuwa angepoteza kazi. Kwa hivyo aliwasumbua wamruhusu kwenye ndege. Alijawa na wasiwasi, akaanza kulia na kupiga kelele na kuchanganyikiwa akili, lakini hakuweza kupanda kwenye ndege. Ilienda bila yeye. Alikwenda (nyumbani kwake Kairo) akiwa na wasiwasi akifikiri kwamba alikuwa amefika mwisho na kwamba kazi yake ilikuwa imekwisha. Familia yake ilimfariji na kumwambia asijali. Siku iliyofuata, alisikia habari kwamba ndege aliyokusudiwa kupanda ilianguka na kila mtu ndani ya ndege alikufa. Na hapo alikuwa anafurahi kwamba hakufanya safari, lakini siku moja kabla yake ilikuwa kana kwamba ulikuwa mwisho wa maisha yake, msiba ambao hakuupata wakati wa kuwahi ndege.

Hizi ni ishara na ishara kama hizo zinaweza kupatikana katika hadithi ya Mosa na Khidr (ambayo boratusome kila Jumu’ah, yaani Sura ya al-Kahf ya Kurani Tukufu). Wakati Khidr alipofanya shimo kwenye mashua ya watu ambao walikuwa wema kumchukua yeye na Mosa kuvuka mto, Mosa aliuliza ni kwanini yeye (Khidr) alifanya hivyo.

Wamiliki wa mashua walipoona shimo kwenye mashua walishangaa ni nani aliyeifanya na walidhani kuwa ni jambo baya kufanya. Muda mfupi baadaye mfalme alishuka mtoni na kujinyakulia mashua zote isipokuwa ile iliyo na shimo. Kwa hivyo wamiliki wa mashua walimsifu Mungu kwa sababu ya ukweli kwamba kulikuwa na shimo katika mashua yao.[1]

Kuna vikwazo vingine au tuseme mambo ambayo yanaonekana kama vizuizi katika maisha yetu. Haya ni mambo ambayo hatuwezi kujua ni nini kilicho mbele yao. Jambo hufanyika na hatujui ni kwanini, hatuna ufafanuzi wake. Kwa watu wengine hii inawafanya wakufuru. Ikiwa utamskiliza mkanamungu, hana amani ya ndani na amemkataa Mungu. Kwa nini mtu huyo haamini uwepo wa Mungu? Si kawaida kutomwamini Mungu, wakati ni kawaida kwetu kumwamini Mungu kwa sababu Mungu alituumba tukiwa na mwelekeo wa asili wa kumwamini.

Mungu anasema:

"Basi (ewe Muhammad) uwelekeze uso wako sawa sawa kwenye Dini (msimwabudu mwingine isipokuwa Mungu Peke Yake) Ndilo umbile la Mwenyezi Mungu (yaani Mungu wa Kiislamu wa Mungu Mmoja), alilo waumbia watu. Hapana mabadilko katika uumbaji wa Mwenyezi Mungu (yaani umoja wa Mungu ya Kiislamu). Hiyo ndio Dini ilionyoka sawa, lakini watu wengi hawajui." (Kurani 30:30) [2]

Nabii Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alisema:

"Kila mtoto huzaliwa na asili safi (kama Mwislamu na mwelekeo wa asili wa kumwamini Mungu)…" (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)

Hii ndio hali ya wanadamu, lakini mtu ambaye anakanusha kuwepo kwa Mungu bila kufundishwa tangu utoto kawaida hufanya hivyo kwa sababu ya msiba. Ikiwa msiba unatokea katika maisha yao hawana maelezo kwa nini ilitokea.

Kwa mfano, mtu ambaye alikua haamini Mungu anaweza kusema kwamba alikuwa na shangazi mzuri; alikuwa mtu mzuri sana na kila mtu alimpenda, lakini siku moja wakati alikuwa nje akivuka barabara gari ilitoka ghafla na kumpiga na akafa. Kwa nini hii ilitokea kwake miongoni mwa watu wote? Kwa nini? Hakuna maelezo! Au mtu (ambaye alikua haamini Mungu) anaweza kuwa na mtoto aliyekufa na kusema kwanini hii ilitokea kwa mtoto wangu? Kwa nini? Hakuna maelezo! Kama matokeo ya mikosi kwa hiyo basi wanafikiria kwamba haiwezekani kuwepo kwa Mungu.



Rejeleo la maelezo:

[1] Mfalme alikuwa mkandamizaji na alijulikana kwa kukamata kila boti nzuri kwa nguvu, lakini watu ambao walikuwa na mashua hiyo walikuwa watu masikini na ndiyo njia yao pekee ya kufaidika kwa hivyo Khidr alitaka mashua ionekane kuwa na makosa ili mfalme hakuikamata ili watu masikini waendelee kufaidika nayo.

[2] Aya hii iliongezwa kwenye nakala na manukuu.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.