Kutafuta kwa utulivu na amani ya ndani (sehemu ya 1 kati ya 4): Vikwazo vya Kufikia Amani ya Ndani

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mtazamo wa jinsi watu wanavyofafanua amani ya ndani na jinsi wanavyojitahidi kuipata; angalia pia vizuizi vinavyotuzuia kupata amani ya ndani.

  • Na Dr. Bilal Philips (transcribed from an audio lecture by Aboo Uthmaan)
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 08 Jan 2024
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,497
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Search_for_Inner_Peace_(part_1_of_4)_001.jpg Mada ya utulivu au amani ya ndani hushugulikia hitaji la kilimwengu. Hakuna mtu katika ulimwengu ambaye hatamani amani ya ndani ama ukipenda utulivu wa ndani wa nafsi. Sio tamaa ambayo ni mpya kwa wakati wetu bali ni jambo ambalo kila mtu amekuwa akitafuta kwa miaka bila kujali rangi, imani, dini, rangi, utaifa, umri, jinsia, utajiri, uwezo au maendeleo ya kiteknolojia.

Watu wamefuata njia tofauti tofauti katika jitihada za kupata utulivu au amani ya ndani, wengnine kupitia kukusanya mali na utajiri, wengine kupitia dawa za kulevya; wengine kupitia muziki, wengine kupitia tafakuri za kimawazo; wengine kupitia waume na wake zao, wengine kupitia kazi zao na wengine kupitia mafanikio ya watoto wao. Na mengineyo mengi.

Bado utafiti unaendelea. Katika wakati wetu tumeongozwa kuamini kwamba ubunifu na maendeleo ya kiteknolojia na kisasa vitatuletea raha, na kupitia hizi tutapata amani ya ndani.

Isitoshe, ikiwa tungechukuwa taifa lenye maendeleo zaidi ya kiteknolojia na viwanda vya kisasa ulimwenguni kama Marekani basi tungegundua kwamba kile ambacho tumeongozwa kuamini sio ukweli. Takwimu zinaonyesha kuwa huko Amerika idadi ya watu milioni 20 wanakabiliwa na unyogovu; na unyogovu ni nini isipokuwa ukosefu wa utulivu na amani ya ndani? Isitoshe, katika mwaka 2000 idadi ya vifo vilivyotokana na mauaji ya kibinafsi viliongezeka maradufu ya kiwango cha wale waliokufa kutokana na Ukimwi. Walakini, vyombo vya habari kwa kawaida yao, tunasikia habari zaidi kuhusu waliokufa kwa Ukimwi kuliko wale wanaokufa kwa kujiua. Watu wengi hufa kutokana na kujiua huko Amerika kuliko kwa mauaji, na viwango vya mauaji wenyewe ni kubwa.

Kwa hivyo ukweli ni kwamba maendeleo ya kiteknolojia na kisasa haijatuletea amani ya ndani na utulivu. Bali, licha ya faraja ambayo kisasa imetuletea, tuko mbali zaidi na amani ya ndani na utulivu wa nafsi kuliko vile babu zetu walikuwa.

Amani ya ndani ni sehemu kubwa ya maisha yetu ambayo hatuwezi ona wala kuihisi na mikono yetu.

Wengi wetu hukosea kulinganisha raha za kibinafsi kwa amani ya ndani kwa ndani; tunapata vitu vya raha kutoka kwa vitu kadhaa iwe ni utajiri, mahusiano ya kimapenzi au mengineyo mengi. Lakini hizi hazidumu, zinakuja na kwenda. Ndio tuna raha za kibinafsi mara kwa mara na tunafurahishwa na vitu mingi mara kwa mara, lakini hii sio amani ya ndani. Amani ya ndani ya kweli ni hali ya utulivu na kuridhika ambayo hutupitisha katika majaribiyo na shida zote za maisha.

Tunapaswa kuelewa kuwa amani sio kitu ambacho kitakuwepo katika ulimwengu huu kwa sababu tunapofafanua amani kulingana na kamusi inasema kwamba amani ni uhuru kutoka kwa vita au mapigano ya wenyewe kwa wenyewe. Je! Hii ina wapi? Daima kuna vita au aina fulani ya machafuko ya wenyewe kwa wenyewe yanayotokea mahali fulani ulimwenguni. Tunapoangalia amani kulingana na kiwango cha serikali basi amani ni uhuru kutoka kwa machafuko ya umma na usalama, lakini wapi ulimwenguni tunayo hii kamili? Tukiangalia amani katika kiwango cha kijamii, familia na kazi basi amani ni uhuru kutoka kwa kutoafikiana na malumbano, lakini je! Kuna mazingira ya kijamii ambayo kamwe hayana kutoafikiana au malumbano? Kulingana na eneo basi ndio, tunaweza kuwa na mahali penye utulivu na amani, kwa mfano amani na utulivu katika baadhi ya visiwa , lakini amani hii ipo kwa muda kidogo tu, baadaye dhoruba au kimbunga kitakuja.

Mungu anasema:

"Hakika, nimemuumba mja katika taabu (mapambano)." (Kurani 90: 4)

Hii ndio hali ya maisha yetu tuko katika taabu na mapambano, nyakati za shida na nyakati za raha.

Ni maisha yaliyojaa majaribio kama vile Mungu anasema:

"Na hakika, tutakujaribu kwa mtihani ya hofu, njaa, upungufu wa mali, maisha na matunda, lakini tumpelekee habari njema As-Saabirin (wanaosubiri)" (Kurani 2: 155)

Ili kukabiliana na hali zetu, hali ya shida na mapambano ambayo tunayopitia, uvumilivu na subira ndio ufunguo.

Lakini ikiwa tutarudi kwa amani ya ndani ambayo tunatafuta, basi uvumilivu hauwezi kujidhihirisha ikiwa hatuna amani ya ndani.

Tunaishi katika ulimwengu wa shida na mapambano lakini bado ndani yetu tunaweza kupata amani ya ndani, amani na mazingira na ulimwengu tunamoishi.

Ni wazi kwamba kuna vizuizi vingine ambavyo vinatuzuia kupata amani. Kwa hivyo kwanza tunapaswa kutambua vizuizi katika maisha yetu ambavyo vinatuzuia kufikia amani ya ndani na kutafuta namna kuziondoa. Vizuizi havitaondolewa kwa kufikiria tu kwamba tunahitaji kuviondoa tunapaswa kuchukuwa hatua kadhaa kufikia hili. Kwa hivyo tunawezaje kuondoa vizuizi hivi ili tuweze kufikia kile kinachotuwezesha tupate amani ya ndani?

Hatua ya kwanza ni kujua tatizo lenyewe na tuwe maakini nayo kwani tusipoijua hatutaweza kuyaondoa.

Hatua ya pili ni kukubali vizuizi ndani yetu. Kwa mfano hasira ni moja ya kizuizi kikubwa kwa amani ya ndani ikiwa mtu ana hasira, anawezaje kuwa na amani ya ndani katika hali hiyo? Haiwezekani. Kwa hivyo mtu huyo anahitaji kutambua kuwa hasira ni kikwazo kwa ukosefu amani ya ndani.

Ikiwa mtu anasema kwamba "Ndio, ni kizuizi lakini sikasiriki", basi mtu kama huyo ana shida. Hajakubali kikwazo hicho kama shida na yuko katika hali ya kujikana mwenyewe. Kwa hivyo hawezi kuiondoa.

Tukiangalia vizuizi maishani tunaweza kuvipanga katika mada au maudhui anuwai: shida za kibinafsi, maswala ya kifamilia, shida za kifedha, shinikizo la kazi na mchanganyiko wa kiroho. Na kuna maswala mengi chini ya mada hizi.


Mbaya Nzuri zaidi

Utafutaji wa Amani ya ndani (sehemu ya 2 kati ya 4): Kukubali Hatima au takdiri

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Nakala hii ya pili inatoa mifano halisi na hadithi zinazoonyesha umuhimu wa kutambua kwamba kila mtu maishani anakabiliwa na vizuizi ndani ya uwezo wake na vizuizi vilivyo nje ya uwezo wake na kwamba vizuizi vilivyo nje ya uwezo wa mtu vinapaswa kuzingatiwa kama hatima kutoka kwa Mungu Mwenyezi.

  • Na Dr. Bilal Philips (transcribed from an audio lecture by Aboo Uthmaan)
  • Iliyochapishwa mnamo 04 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,417
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Tuna shida nyingi, vikwazo vingi sana kwamba ni kama magonjwa. Tukijaribu kushughulikia moja baada ya nyingine hatutavimaliza vyote. Tunahitaji kuvitambua, kuviweka katika jumla na kukabiliana navyo kama kikundi badala ya kujaribu kushughulikia kikwazo na shida ya kila mtu.

Ili kufanya hivyo lazima kwanza tuondoe vizuizi ambavyo viko zaidi ya uwezo wetu. Tunapaswa kuwa na uwezo wa kutofautisha ni vizuizi vipi ambavyo viko ndani ya udhibiti wetu na ni vipi ambavyo viko nje ya uwezo wetu. Wakati tunatambua zile ambazo ziko nje ya uwezo wetu kama vizuizi ukweli ni kwamba sio. Ndio vitu ambavyo Mungu amekusudia kwa ajili yetu katika maisha yetu, sio vizuizi kweli, lakini tumevitafsiri vibaya kuwa ni vizuizi.

Kwa mfano, katika wakati huu mtu anaweza kujikuta amezaliwa mweusi katika ulimwengu ambao unapendelea watu weupe kuliko watu weusi au kuzaliwa maskini katika ulimwengu unaowapendelea matajiri kuliko masikini, au aliyezaliwa mfupi, vilema au hali nyingine yoyote ya mwili ambayo inachukuliwa kuwa ni ulemavu.

Hivi ni vitu vyote ambavyo vilikuwa na viko nje ya uwezo wetu. Hatukuchagua familia ipi ingetuzaa;ni mwili gani ili roho zetu zipulizwe, hii sio chaguo letu. Kwa hivyo chochote tunachopata ya aina hizi za vizuizi basi lazima tuwe na subira nazo na tujue kwamba sio vizuizi kweli. Mungu alituambia:

“… Lakini huenda mkachukia kitu nacho ni kheri kwenu. Na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu. Na Mwenyezi Mungu anajua na nyinyi hamjui.” (Kurani 2: 216)

Kwa hivyo vizuizi ambavyo viko nje ya uwezo wetu tunaweza kuvichukia na kutaka kuvibadilisha, na watu wengine hutumia pesa nyingi kujaribu kuvibadilisha. Michael Jackson ni mfano bora. Alizaliwa mweusi katika ulimwengu unaopendelea watu weupe, kwa hivyo alitumia pesa nyingi kujaribu kujibadilisha lakini aliishia kuharibu mambo.

Amani ya ndani inaweza kupatikana tu ikiwa vizuizi ambavyo viko nje ya udhibiti wetu vinakubaliwa na sisi kwa uvumilivu kama sehemu ya hatima ya Mungu.

Jua kuwa chochote kinachotokea au hatuna uwezo juu yake, basi Mungu ameweka ndani yake kitu kizuri, ikiwa tunao au hatuna uwezo wa kufahamu yaliyo mema ndani yake basi mema bado yapo. Kwa hivyo tunaikubali!

Kulikuwa na nakala kwenye gazeti ambayo ilikuwa na picha ya mtu wa Misri anayetabasamu. Alikuwa na tabasamu usoni mwake kutoka sikio hadi sikio huku mikono yake ikiwa imenyooshwa na vidole gumba vyote vikiwa vimeinama juu baba yake alikuwa akimbusu kwenye shavu moja na dada yake kwenye shavu lingine.

Chini ya picha hiyo kulikuwa na maelezo mafupi. Alipaswa kuwa kwenye ndege ya Gulf Air ya Uarabuni siku iliyopita kutoka Kairo kwenda Bahrain. Alikuwa amekimbilia uwanja wa ndege kuwahi ndege na alipofika huko alikosa mhuri mmoja kwenye Pasipoti yake (huko Cairo lazima uwe na mihuri mingi kwenye stakbathi zako. Unapata mtu wa kupiga muhuri hii na kusaini hiyo na mtu huyo mwingine kufanya vile) lakini hapo alipo kwenye uwanja wa ndege bila muhuri mmoja. Kwa kuwa alikuwa mwalimu huko Bahrain na ndege hii ilikuwa ya mwisho kurudi Bahrain ambayo ingemwezesha kufika kwa wakati, kukosa ilimaanisha kuwa angepoteza kazi. Kwa hivyo aliwasumbua wamruhusu kwenye ndege. Alijawa na wasiwasi, akaanza kulia na kupiga kelele na kuchanganyikiwa akili, lakini hakuweza kupanda kwenye ndege. Ilienda bila yeye. Alikwenda (nyumbani kwake Kairo) akiwa na wasiwasi akifikiri kwamba alikuwa amefika mwisho na kwamba kazi yake ilikuwa imekwisha. Familia yake ilimfariji na kumwambia asijali. Siku iliyofuata, alisikia habari kwamba ndege aliyokusudiwa kupanda ilianguka na kila mtu ndani ya ndege alikufa. Na hapo alikuwa anafurahi kwamba hakufanya safari, lakini siku moja kabla yake ilikuwa kana kwamba ulikuwa mwisho wa maisha yake, msiba ambao hakuupata wakati wa kuwahi ndege.

Hizi ni ishara na ishara kama hizo zinaweza kupatikana katika hadithi ya Mosa na Khidr (ambayo boratusome kila Jumu’ah, yaani Sura ya al-Kahf ya Kurani Tukufu). Wakati Khidr alipofanya shimo kwenye mashua ya watu ambao walikuwa wema kumchukua yeye na Mosa kuvuka mto, Mosa aliuliza ni kwanini yeye (Khidr) alifanya hivyo.

Wamiliki wa mashua walipoona shimo kwenye mashua walishangaa ni nani aliyeifanya na walidhani kuwa ni jambo baya kufanya. Muda mfupi baadaye mfalme alishuka mtoni na kujinyakulia mashua zote isipokuwa ile iliyo na shimo. Kwa hivyo wamiliki wa mashua walimsifu Mungu kwa sababu ya ukweli kwamba kulikuwa na shimo katika mashua yao.[1]

Kuna vikwazo vingine au tuseme mambo ambayo yanaonekana kama vizuizi katika maisha yetu. Haya ni mambo ambayo hatuwezi kujua ni nini kilicho mbele yao. Jambo hufanyika na hatujui ni kwanini, hatuna ufafanuzi wake. Kwa watu wengine hii inawafanya wakufuru. Ikiwa utamskiliza mkanamungu, hana amani ya ndani na amemkataa Mungu. Kwa nini mtu huyo haamini uwepo wa Mungu? Si kawaida kutomwamini Mungu, wakati ni kawaida kwetu kumwamini Mungu kwa sababu Mungu alituumba tukiwa na mwelekeo wa asili wa kumwamini.

Mungu anasema:

"Basi (ewe Muhammad) uwelekeze uso wako sawa sawa kwenye Dini (msimwabudu mwingine isipokuwa Mungu Peke Yake) Ndilo umbile la Mwenyezi Mungu (yaani Mungu wa Kiislamu wa Mungu Mmoja), alilo waumbia watu. Hapana mabadilko katika uumbaji wa Mwenyezi Mungu (yaani umoja wa Mungu ya Kiislamu). Hiyo ndio Dini ilionyoka sawa, lakini watu wengi hawajui." (Kurani 30:30) [2]

Nabii Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alisema:

"Kila mtoto huzaliwa na asili safi (kama Mwislamu na mwelekeo wa asili wa kumwamini Mungu)…" (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)

Hii ndio hali ya wanadamu, lakini mtu ambaye anakanusha kuwepo kwa Mungu bila kufundishwa tangu utoto kawaida hufanya hivyo kwa sababu ya msiba. Ikiwa msiba unatokea katika maisha yao hawana maelezo kwa nini ilitokea.

Kwa mfano, mtu ambaye alikua haamini Mungu anaweza kusema kwamba alikuwa na shangazi mzuri; alikuwa mtu mzuri sana na kila mtu alimpenda, lakini siku moja wakati alikuwa nje akivuka barabara gari ilitoka ghafla na kumpiga na akafa. Kwa nini hii ilitokea kwake miongoni mwa watu wote? Kwa nini? Hakuna maelezo! Au mtu (ambaye alikua haamini Mungu) anaweza kuwa na mtoto aliyekufa na kusema kwanini hii ilitokea kwa mtoto wangu? Kwa nini? Hakuna maelezo! Kama matokeo ya mikosi kwa hiyo basi wanafikiria kwamba haiwezekani kuwepo kwa Mungu.



Rejeleo la maelezo:

[1] Mfalme alikuwa mkandamizaji na alijulikana kwa kukamata kila boti nzuri kwa nguvu, lakini watu ambao walikuwa na mashua hiyo walikuwa watu masikini na ndiyo njia yao pekee ya kufaidika kwa hivyo Khidr alitaka mashua ionekane kuwa na makosa ili mfalme hakuikamata ili watu masikini waendelee kufaidika nayo.

[2] Aya hii iliongezwa kwenye nakala na manukuu.

Mbaya Nzuri zaidi

Utafutaji wa Amani ya ndani (sehemu ya 3 kati ya 4): Uvumilivu na Malengo maishani

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Katika ulimwengu huu wenye misukosuko, uvumilivu na kutofanya maisha haya kuwa lengo kuu, ni suluhisho muhimu kwa kutatua vizuizi ambavyo viko katika udhibiti wetu.

  • Na Dr. Bilal Philips (transcribed from an audio lecture by Aboo Uthmaan)
  • Iliyochapishwa mnamo 04 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,101
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Search_for_Inner_Peace_(part_3_of_4)_001.jpgTunaporejelea hadithi ya Musa na Khidr, baada ya kuvuka mto walipata mtoto na Khidr alimuua mtoto huyo kwa kukusudia. Musa alimuuliza Khidr angewezaje kufanya jambo kama hilo? Mtoto hakuwa na hatia na Khidr alimuua tu! Khidr alimwambia Musa kuwa mtoto huyo alikuwa na wazazi wachamungu na ikiwa mtoto angekua (Mungu alijua hivyo) angekuwa hofu kwa wazazi wake hata angewafanya wasiamini, kwa hivyo Mungu aliamuru kifo cha mtoto huyo.

Kwa kweli wazazi walihuzunika walipompata mtoto wao amekufa. Lakini, Mungu alibadilisha mtoto wao na kumweka yule aliye mwadilifu na bora kwao. Mtoto huyu aliwaheshimu na alikuwa mzuri kwao, lakini wazazi kila wakati watakuwa na shimo moyoni mwao kwa sababu ya kupoteza mtoto wao wa kwanza, hadi Siku ya Kiyama watakaposimama mbele za Mungu na atawaambia sababu kwanini alichukua roho ya mtoto wao wa kwanza na ndipo wataelewa na kumsifu Mungu.

Kwa hivyo, hii ndio hali ya maisha yetu. Kuna mambo, mambo ambayo yanaonekana hasi, mambo ambayo hufanyika katika maisha yetu ambayo yanaonekana kuwa kikwazo kwa amani ya ndani kwa sababu hatuelewi au kwanini yalitupata, lakini lazima tuyaweke kando.

Zinatoka kwa Mungu na tunapaswa kuamini kwamba mwishowe kuna mema nyuma yao, ikiwa tunaweza kuiona au la. Kisha tunaendelea na mambo ambayo tunaweza kubadilisha. Kwanza tunawatambua, kisha tunaenda kwenye hatua kuu ya pili na hiyo ni kuondoa vizuizi kwa kutengeneza suluhisho. Ili kuondoa vizuizi tunapaswa kuzingatia zaidi mabadiliko ya kibinafsi na hii ni kwa sababu Mungu anasema:

“Hakika Mwenyezi Mungu habadili yaliyoko kwa watu mpaka wabadili wao yaliyomo nafsini mwao…”(Kurani 13:11)

Hili ni eneo tunalolidhibiti. Tunaweza hata kukuza uvumilivu, ingawa wazo la kawaida ni kwamba watu wengine wanazaliwa tu wakiwa wavumilivu.

Mtu mmoja alikuja kwa Mtume, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake na akauliza ni nini anahitaji kufanya ili afike Peponi, kwa hivyo Nabii akamwambia: "Usikasirike." (Saheeh Al-Bukhari)

Mtu huyo alikuwa mtu kukasirika haraka, kwa hivyo Mtume alimwambia mtu huyo kwamba anahitaji kubadilisha hali yake ya hasira. Kwa hivyo kujibadilisha tabia ya mtu ni jambo linaloweza kufikiwa.

Mtume pia alisema: "Yeyote anayejifanya kuwa mvumilivu (kwa hamu ya kuwa mvumilivu) Mungu atampa subira."

Hili limeandikwa katika Saheeh Al-Bukhari. Hii inamaanisha kuwa ingawa watu wengine huzaliwa wakiwa wavumilivu sisi wengine tunaweza kujifunza kuwa wavumilivu.

Katika kisaikolojia ya Magharibi walikuwa wakituambia tuiondoe kifuani mwetu, usiishike kwa sababu ikiwa tungefanya hivyo tungeangamia, kwa hivyo bora kuiruhusu yote itoke.

Baadaye waligundua kuwa wakati watu wangeiacha yote mishipa ndogo ya damu itapasuka katika ubongo wao kwa sababu walikuwa na hasira sana. Waligundua kuwa ilikuwa hatari sana kuiruhusu yote itoke. Kwa hivyo sasa wanasema ni bora sio kuachilia yote.

Mtume alituambia tujaribu kuwa wavumilivu, kwa hivyo kwa nje tunapaswa kuonyesha sura hiyo ya kuwa mvumilivu hata wakati tunachemka ndani. Na tusijaribu kuwa wavumilivu kwa nje ili kudanganya watu bali tunafanya hivyo ili kukuza uvumilivu. Tukizingatia hivyo basi sura ya nje ya uvumilivu pia inakuwa ya ndani na uvumilivu kamili unafanikiwa kama ilivyotajwa katika Hadeeth iliyonukuliwa hapo juu.

Miongoni mwa njia hizi ni kuangalia ni vipi vitu vya nyenzo katika maisha yetu vinavyocheza sehemu kubwa kwa uvumilivu na sisi kuifanikisha.

Mtume alitupa ushauri wa jinsi ya kushughulikia mambo haya kwa kusema:

"Usiangalie wale walio juu yako ambao wamebahatika zaidi, badala yake angalia wale walio chini yako au ambao hawajafanikiwa..."

Hii ni kwa sababu kwa hali yeyote ile, kuna wale ambao ni mbaya kuliko sisi. Huu unapaswa kuwa mkakati wetu wa jumla kuhusu maisha ya raslimali. Siku hizi maisha ya kupenda mali ni sehemu kubwa ya maisha yetu, tunaonekana kuwa tunaitamani sana, kupata kila tuwezalo katika ulimwengu huu inaonekana kuwa jambo kuu ambalo wengi wetu huweka nguvu zetu. Kwa hivyo ikiwa mtu lazima afanye hivi basi hawapaswi kuiruhusu iathiri amani yake ya ndani.

Tunashughulika na ulimwengu wa raslimali hatupaswi kuendelea kuzingatia wale walio bora zaidi kuliko sisi vinginevyo hatutaridhika na kile tulicho nacho. Mtume akasema:

"Ukimpatia mwana wa Adamu bonde la dhahabu atataka bonde jingine." (Saheeh Muslim)

Msemo ni kwamba nyasi siku zote huwa kijani kibichi upande mwingine na kadiri mtu anavyo zaidi ndivyo mtu anataka zaidi. Hatuwezi kufikia kuridhika katika ulimwengu ikiwa tunaifuata kwa njia hiyo bali tunapaswa kutazama kwa wale walio na hali duni, kwa njia hii tutakumbuka zawadi, faida na rehema ambazo Mungu ametupatia sisi kwa utajiri wetu, bila kujali ni ndogo kiasi gani.

Kuna msemo mwingine wa Nabii Muhammad ambao hutusaidia kuweka mambo yetu katika mtazamo wao sahihi, na ni mfano wa kinabii wa kanuni ya Steven Covey[1] ya "vitu vya kwanza mwanzo". Mtume alisema kanuni hii zaidi ya miaka 1400 iliyopita na akaiweka kanuni hii kwa waumini kwa kusema:

"Yeyote anayeufanya ulimwengu huu kuwa lengo lake Mungu atachanganya mambo yake na kuweka umasikini mbele ya macho yake na hataweza kupata chochote kutoka kwa ulimwengu huu isipokuwa yale ambayo Mungu amekwisha andikia yeye…" (Ibn Maajah, Ibn Hibbaan)

Kwa hivyo, mambo ya mtu hayatakusanyika pamoja kwake, atakuwa kila mahali kama kuku aliyekatwa kichwa akikimbia bila mpangilio; ikiwa atafanya ulimwengu huu kuwa lengo lake. Mungu ataweka umasikini mbele ya macho yake na bila kujali ana pesa ngapi atajisikia maskini. Kila wakati mtu ni mzuri kwake au anamtabasamu anahisi kwamba wanafanya hivyo tu kwa sababu wanataka pesa yake, hawezi kumwamini mtu yeyote na hafurahi.

Wakati soko la hisa linaanguka unasoma juu ya baadhi ya wale ambao waliwekeza ndani yake kujiua. Mtu anaweza kuwa na milioni 8 na kupoteza milioni 5 na milioni 3 zilizobaki baada ya soko kuanguka, lakini kupoteza hiyo milioni 5 inaonekana kwake kuwa mwisho. Haoni maana ya kuishi baada ya hapo, kwani Mungu ameweka umaskini kati ya macho yake.



Rejeleo la maelezo:

[1] Stephen Covey ni mamlaka ya uongozi inayoheshimiwa kimataifa na mwanzilishi wa Kituo cha Uongozi cha Covey. Alipokea M.B yake

Mbaya Nzuri zaidi

Utafutaji wa Amani ya Ndani (sehemu ya 4 kati ya 4): Amani ya ndani hufikiwa kwa kujitiisha kwa Mungu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Amani ya kweli ya ndani hupatikana kwa kujitiisha kwa Mungu Mwenyezi, kuishi maisha haya kwa ajili Yake, kumkumbuka na kwa kuifanya Akhera kuwa kipaumbele kuliko maisha haya.

  • Na Dr. Bilal Philips (transcribed from an audio lecture by Aboo Uthmaan)
  • Iliyochapishwa mnamo 04 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,158
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Tunapaswa kuzingatia kwamba watu hawatapata kutoka kwa ulimwengu huu isipokuwa yale ambayo Mungu amewaandikia tayari, haya ndiyo malengo kamili. Baada ya kuzungukazunguka, kukaa macho usiku, kuwa mchapa kazi mwenye atapata tu kile ambacho tayari Mungu amemkusudia. Nabii, Mungu ainue jina lake, alisema:

"Yeyote anayeweka Akhera kuwa lengo lake, Mungu humkusanyia mambo yake, humpa utajiri wa (imani katika) moyo na ulimwengu utamjia kwa kulalamika na kwa unyenyekevu." (Ibn Maajah, Ibn Hibbaan)

Mtu kama huyo anafikia utajiri wa moyo. Utajiri sio kuwa na mali nyingi, lakini utajiri ni kuwa na utajiri wa moyo, na utajiri wa moyo ni nini? Ni kuridhika, na hapa ndipo amani hutoka wakati mtu anaporudi kwa Mungu, na huu ndiyo Uislam.

Amani ya ndani ni kukubali Uislamu mioyoni mwetu na kuishi kwa kanuni za Uislamu. Kwa hivyo Mungu ataweka utajiri ndani ya moyo wa mtu na ulimwengu huu utamjia kwa unyenyekevu, kwa magoti yake na kunyenyekezwa. Mtu kama huyo hatalazimika kuifukuza.

Hii ni Ahadi ya Mtume ikiwa mtu ataweka "mambo ya kwanza mbele", na hiyo ni Akhera. Ikiwa ni Peponi ambayo tunataka basi hiyo inapaswa kudhihirika katika maisha yetu, inapaswa kuwa hatua ya mwelekeo wetu kile tunachoendelea kuweka mbele.

Kwa hivyo tunajuaje wakati Akhera ni mwelekeo wetu? Ikiwa tunakaa chini na mtu na tunayozungumza tu ni magari ya hivi karibuni, nyumba za gharama kubwa, kusafiri na likizo na pesa, ikiwa mazungumzo yetu mengi ni juu ya mali au uvumi, tukiongea juu ya mtu huyu na yule basi ni inamaanisha kwamba Akhera sio mwelekeo wetu. Ikiwa Akhera ingekuwa lengo letu basi ingeonekana katika mazungumzo yetu. Hii ni kiwango cha msingi ambacho tunaweza kujihukumu wenyewe, kwa hivyo tunapaswa kusimama na kujiuliza, "Je! Tunatumia wakati wetu mwingi kuzungumza juu ya nini"?

Ikiwa tunaona kuwa kipaumbele chetu ni ulimwengu huu basi tunahitaji kuzingatia tena, tunahitaji kuweka "vitu vya kwanza mbele", ikimaanisha Akhera kabla ya maisha ya ulimwengu huu na tukifanya hivyo tunaweza kufikia amani ya ndani, na Mungu alitujulisha hii katika Kurani, hatua sahihi ya kuchukua ili kupata amani ya ndani, na Mungu anasema:

"Hakika kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu ndio nyoyo hutua." (Kurani 13:28)

Kwa hivyo ni kwa kumkumbuka Mungu tu kwamba mioyo hupata raha. Hii ndio amani ya ndani. Kumkumbuka Mungu katika kila kitu tunachofanya kama Waislamu. Uislamu unaishi maisha ya kumkumbuka Mungu, na Mungu anasema:

“Na ushike Swala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi…” (Kurani 20:14)

Kila kitu tunachofanya (katika Uislamu) kinajumuisha kumkumbuka Mungu. Mungu anasema:

"Sema: Hakika Sala yangu, na ibada zangu, na uhai wangu, na kufa kwangu, ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote.’”(Kurani 6: 162)

Kwa hivyo hii ndio njia ya kufikia amani ya ndani, kumkumbuka Mungu katika nyanja zote za maisha yetu.

Ukumbusho huu (dhikr) sio kama watu wengine wanavyofikiria, yaani, kukaa kwenye kona ya chumba giza nikirudia kila mara “Allah, Allah, Allah…” Hivi sivyo tunavyomkumbuka Mungu. Ndio, mtu kama huyo anasema jina la Mungu, lakini tufikirie kwamba ikiwa mtu alikuja kwako (na kwa mfano jina lako ni Muhammad) na akaendelea kusema "Muhammad, Muhammad, Muhammad…" ungejiuliza ni nini kilichokoseka naye. Je! Anataka kitu? Je! Kuna kitu ambacho anahitaji? Ni nini kusudi la kurudia jina langu bila mazungumzo zaidi?

Hii sio njia ya kumkumbuka Mungu kwa sababu hii sio jinsi Nabii alimkumbuka Mungu na hakuna rekodi ya yeye kufanya hivyo. Watu wengine wanasema kwamba tunapaswa kumkumbuka Mungu kwa kucheza karibu au kutetereka kutoka upande hadi upande. Hii sio njia ya kumkumbuka Mungu, kwani hii pia sio jinsi Nabii alimkumbuka Mungu na hakuna rekodi ya yeye kufanya hivyo.

Nabii alimkumbuka Mungu maishani mwake. Maisha yake yalikuwa maisha ya kumkumbuka Mungu, aliishi maisha ya kumkumbuka Mungu na hii ndio ukumbusho wa kweli, katika maombi yetu na katika kuishi kwetu na kufa kwetu.

Kwa muhtasari, utaftaji wa amani ya ndani unajumuisha kutambua shida ambazo tunazo katika maisha yetu, kutambua vizuizi vyetu, kutambua kwamba amani ya ndani itakuja tu tunapotambua vizuizi hivyo na kuelewa ni yapi kati yetu tunaweza kubadilisha na kwamba tunazingatia vizuizi ambavyo tunaweza vibadilisha, vile ambavyo vinahusiana na nafsi yetu.

Ikiwa tutabadilisha nafsi zetu basi Mungu atabadilisha ulimwengu na kutupa njia za kushughulika na ulimwengu unaotuzunguka. Ijapokuwa ulimwengu uko kwenye machafuko Mungu hutupa amani ya ndani nayo.

Chochote kinachotokea tunajua kuwa ni matakio ya Mungu na kwamba ni majaribio ya Mungu na tunajua kwamba mwishowe ni kwa faida yetu na ina mema ndani yake. Mungu alituumba katika ulimwengu huu na ulimwengu kama njia ya kufikia Peponi na majaribio ya ulimwengu huu ni ukuaji wetu wa kiroho. Ikiwa tunaweza kukubali haya yote, tukimkubali Mungu katika nyoyo zetu basi tunaweza kupata amani ya ndani kwa ndani.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa