Wicca (sehemu ya 2 kati ya 2): Ubaya wa Asili

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Uislamu na Wicca - je zinaendana kwa namna yoyote?

  • Na Aisha Stacey (© 2012 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 18 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,668 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Wicca2.jpgPindi mtu anathibitisha kuwa Wicca na Ushetani ni tofauti ni rahisi kufikiri kwamba Wicca ni dini isiyo na madhara. Inaweza hata kuonekana kuwa Wicca katika karne ya 21 ni zaidi ya hisia zenye usawa za hippy na dini za asili za kale zilizogeuzwa kuwa aina ya uzingatiaji wa mazingira. Ila huu sio ukweli. Kufanya uchawi kwa umakini, au kwa kujifurahisha, ni mchezo hatari. Kuruhusu mistari ifiche kati ya nani au nini kinadhibiti hatima ya wanadamu ni hatari, tena ni hatari zaidi. Ingawa inaonekana wazi kwamba idadi kubwa ya Wawiccani hawaamini wala kufanya kazi na Shetani kwa kujua, maoni ya Kiislamu ni kwamba dini ya Wiccan imeathiriwa sana na Shetani, iwe watendaji wanakusudia iwe hivyo au la.

Kwanza, hebu tuchunguze mojawapo ya kanuni za kimsingi za Uislamu. Kama moja ya nguzo za imani, Mwislamu anaamini katika Qadr, au kudra ya Mwenyezi Mungu. Chochote kitakachotokea katika maisha yetu, mema, na kile tunachoona kuwa kibaya, ni sehemu ya yale ambayo Mungu aliamuru muda mrefu kabla hata hatujaumbwa. Hakuna kinachotokea bila idhini ya Mungu, hata jani linaloanguka kutoka kwenye mti au tone la mvua kuanguka kwenye dirisha lako. Hivyo, kufikiria kuwa mtu au maneno fulani ya uchawi yanaweza kubadilisha nzuri kuwa mbaya au kuleta matokeo yanayohitajika ni upuuzi kabisa. Kuweka imani yetu katika kitu kingine zaidi ya Mungu Mwenyewe ni bure, lakini si hivyo tu, kwa Muislamu ni hatari.

Kuamini kwamba Mungu ana washirika au kwamba kuna watu wanaoweza kumfikia Mungu zaidi kuliko wengine ni dhambi kubwa, na Shetani hataki chochote zaidi ya kuwaongoza watu mbali na Mungu na kuwaingiza kwenye njia ya uharibifu. Humo kuna hatari katika Wicca. Wale wanaoichukulia Wicca kama dini wanasema kwamba kuroga ni zaidi ya kuomba msaada wa kimungu. Hata hivyo Mungu kwa sababu ya upendo wake kwa viumbe wake ametupa Kurani na Sunna sahihi (mafundisho ya Mtume Muhammad) ambayo kwa hayo tunajifunza njia sahihi ya kuomba msaada wa kiungu. Usaidizi wa Kimungu haupatikani kwa msaada wa kengele, mishumaa, mifagio, sufuria, fimbo, au vifaa vingine vya Wiccan. Mtu anapaswa kuweka tumaini lake kwa Mungu na kuomba msaada kutoka kwake pekee. Mungu peke yake ndiye anayetoa baraka au kuondoa madhara na kuondoa dhiki.

“Sema: Hapana katika mbingu na ardhi ajuaye ya ghaibu isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Wala wao hawajui lini watafufuliwa.”(Kurani 27: 65)

Uchawi, kubashiri, na utabiri wa kiakili si kingine zaidi ya hila kutoka kwa Shetani iliyoundwa kuwaongoza wanadamu kwenye maangamizi yao. Baada ya kusema hivyo hata hivyo, kuwepo kwa uchawi kunathibitishwa na Kurani na Hadithi za Mtume Muhammad. Ni halisi na ukweli. Ujanja upo katika kuwafanya watu waamini kwamba kucheza na nguvu za uovu hakuna madhara. Hata kama jambo lililo karibu ni zuri, uchawi katika aina zake zote huugeuza uso wa mtu kutoka kwa Mungu. Uchawi ni sanaa inayohitaji ujuzi na ustadi, na ni aina ya maarifa ambayo ina msingi, mbinu, na kanuni. Kuisoma haijuzu katika Uislamu. Ufundi huo na jamaa zake wa karibu kama vile kadi za Tarot, kusoma majani ya chai na kusoma elimu ya nyota ni marufuku kwa Waislamu.

“Atakayekwenda kwa mtabiri na kumuuliza chochote, maombi yake hayatakubaliwa kwa muda wa siku arobaini.”[1]

Hii inaelezea kwa kiasi kikubwa juu ya uzito wa kitendo na katika baadhi ya nchi hata kucheza na uchawi na zana za uchawi uhukumiwa kisheria.

Hivi karibuni wanaume wawili walikamatwa katika uwanja wa ndege wa Umoja wa Falme za Kiarabu. Katika mizigo yao vilikutwa vitu 1200 vilivyoainishwa kuwa haramu katika makundi 28, hizi zilihusisha maandishi yenye miiko na matambiko ya uchawi, hirizi, ngozi na mifupa ya wanyama, vyombo vyenye damu na vimiminika vingine, nyuzi, na pete za ajabu. Mkurugenzi wa forodha hapo alisema kwamba uaminifu wa watu mara nyingi ulilipwa kwa ulaghai. Hii ni sababu nyingine kwa nini Wicca haikubaliwi na Uislamu, iwe inatekelezwa kama dini au la.

Watu wanaodai kuwa wanaweza kukuambia kile kitakachotokea kwa wakati ujao katika sehemu kubwa wanatabiri uwongo kulingana na ujuzi wao wa haiba, lugha ya mwili, n.k. Hata hivyo, kuna aina nyingine ya watu ambao kwa hakika hufanya kazi na Shetani na wafuasi wake katika majini na watu. Watu hawa wamegubikwa na maovu wakijua au wasijue na cha kusikitisha ni kwamba madhara makubwa yanaweza kufanywa na watu wanaofikiri kuwa wanafanya mema au kujiingiza katika mchezo usio na madhara.

Kuna aina ya uchawi ambayo inalenga kujenga chuki au upendo. Inafanywa kwa kuunganisha vifungo na kupuliziwa juu yao, na kutumia vitiririka. Uchawi huu una uwezo wa kumfanya mwanaume ampende au amchukie mkewe, au mwanamke ampende au amchukie mumewe. Inaweza pia kuathiri uhusiano wa mtu na watu wengine zaidi ya mwenzi wake wa ndoa. Kwa hiyo Mungu ametuamrisha tujikinge Kwake kutokana na shari ya wale wanaopuliza mafundo na kujikinga Kwake kutokana na kila uovu.

Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko, Na shari ya alivyo viumba, Na shari ya giza la usiku liingiapo,Na shari ya wanao pulizia mafundoni, Na shari ya hasidi anapo husudu.” (Kurani 113)

Kwa kumalizia, mifumo ya imani ya kipagani ya kale ni hiyo tu, mifumo ya imani ya kipagani ya kale. Hakuna haja ya kuunda tena imani kwa maelfu ya miaka. Mungu ametupa dini (yaani Uislamu) inayostahiki kwa wanadamu na kwa hakika ina majibu yote. Wicca inaweza kuonekana kama mahali penye amani kwa wengi lakini amani ya kweli iko katika kutii amri za Mungu na kuishi maisha yaliyoamuliwa kwako na Mungu.



Rejeleo la maelezo:

[1] Saheeh Muslim

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.