Misingi ya Uislam

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Maelezo ya kina kuhusu sehemu ya kwanza ya ushuhuda wa imani “Hakuna apaswaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mungu (La ilaaha ‘ill-Allah).”

  • Na M. Abdulsalam (© 2006 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 07 May 2023
  • Ilichapishwa: 3
  • Imetazamwa: 3,465 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Basis_of_Islam_001.jpgMsingi wa dini ya Uislamu ni uthibitisho wa matamshi mawili:

(i) Hakuna apaswaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mungu (La ilaaha ‘ill-Allah), na

(ii) Muhammad ni Mtume wa Mungu (Muhammad-ur-Rasool-ullah).

Msemo huu unajulikana kama shahaadah, au ushuhuda wa imani. Kupitia imani na ushuhuda wa misemo hii miwili mtu huingia kwenye kundi la Uislam. Ni kauli mbiu ya waumini ambayo huihifadhi kwenye maisha yao yote, na msingi wa imani zao zote, ibada na kuishi. Nakala hii itajadili sehemu ya kwanza ya ushuhuda huu.

Umuhimu wa tamko la ‘Laa Ilaaha ill-Allah

Kama ilivyoelezwa hapo mwanzoni, ushuhuda huu ni sehemu muhimu zaidi ya dini ya Uislam, kwani inathibitisha imani ya Tawheed, au Umoja na upekee wa Mungu, ambapo dini yote imejengwa juu yake. Kwa sababu hii, inaitwa, "Tamko la Tawheed". Upekee na umoja huu unahitaji haki ya pekee ya Mungu ya kuabudiwa na kutiiwa. Dini ya Uislam kimsingi ni njia ya maisha ambayo mtu huabudu na kutii maagizo ya Mungu na sio mtu au kitu kingine. Ni dini pekee ya kweli ya kuamini Mungu mmoja, ikisisitiza kuwa hakuna ibada inayopaswa kuelekezwa kwa mtu au kitu kingine isipokuwa kwa Mungu. Kwa sababu hii, tunaona kuwa katika masimulizi mengi, Mtume, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alisema kuwa yeyote atakayesema msemo huu na kuutumia ataingia Peponi milele, na yeyote atakayeupinga atahukumiwa Moto wa Jehanamu milele. .

Tamko hili pia linasisitiza kusudi la maisha ya mtu, ambalo ni ibada ya Mungu peke yake, na kama kawaida, kusudi la kuishi na uwepo wake ni jambo muhimu zaidi katika maisha ya mmoja wenu. Mungu anasema katika Kurani:

“Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi. ” (Kurani 51:56)

Ujumbe wa Tawheed unaopatikana katika tamko hili halipo kwenye Uislam. Kwa sababu ya umuhimu, uwazi na ukweli wa ujumbe huu, ulikuwa ujumbe ulioletwa na mitume wote. Tangu mwanzo wa mwanadamu, Mungu alituma wajumbe kwa kila watu na taifa, akiwaamuru wamwabudu Yeye Peke yake, na kukataa miungu yote ya uwongo. Mungu anasema:

“Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani....” (Kurani 16:36)

Muda tu ambao fikra hii ya Tawheed itakapojikita ndani ya moyo na akili za mtu ndipo watakapofuata amri za Mungu kwa hiari na kumwabudu Yeye peke Yake. Kwa sababu hii, Mtume aliwaita watu wake kwa miaka kumi na tatu huko Makka kwa Tawheed peke yake, na ni ibada ndogo tu iliyoamriwa wakati huo.Muda tu ambao wazo hili lilipokuwa thabiti katika mioyo ya waumini na ndipo walipokuwa tayari kujitolea hata maisha yao wenyewe ndipo amri nyingi za Uislamu zilipofunuliwa. Kama msingi huu utakosekana, hakuna kitu baada yake kitakachokuwa na faida.

Maana ya Laa Ilaaha ill-Allah

La ilaaha ill-Allah, kwa kawaida inamaana "Hakuna mungu (Mwenyezi) isipokuwa Allah". Hapa, mungu aliye na herufi ndogo 'm' ni kitu chochote kinachoabudiwa. Maana ya tamko hili ni kwamba ingawa kunaweza kuwa na miungu mingine na miungu inayoabudiwa na wanadamu waliopo, hakuna hata mmoja wao anayeabudiwa kwa haki, ikimaanisha kuwa hakuna kitu kinachozingatiwa kama mungu kina haki yoyote ya ibada hiyo, na haistahili, isipokuwa Mungu Mmoja wa Kweli. Kwa hivyo, laa ilaaha ill-Allah inamaanisha, "Hakuna mungu anayepaswa kubudiwa kwa haki isipokuwa Allah."

La ilaaha… (Hakuna mungu anayepaswa kubudiwa…)

Maneno haya mawili yanakataa haki ya kiumbe yeyote aliyeumbwa kuabudiwa. Waislamu wanakataa ibada ya kila kitu isipokuwa Mungu. Kukataliwa huku hunahusisha ushirikina, itikadi, njia za maisha, au watu wowote wenye mamlaka ambao wanadai kujitolea kwa Mungu, upendo, au utii kamili. Mungu katika Kurani anatajwa katika maeneo mengi kwamba vitu vyote ambavyo watu huvichukulia kama vitu vya kuabudiwa badala yake Yeye havistahili kuabudiwa, wala hawana haki yoyote, kwani wao ni viumbe na hawana uwezo wa kuleta faida yoyote.

“Na wamechukua badala yake miungu ambayo haiumbi chochote, bali hiyo inaumbwa, haijimilikii nafsi zao madhara wala manufaa, wala haimiliki mauti, wala uhai, wala kufufuka. ” (Kurani 25:3)

Wengine huabudu kitu kingine au kiumbe kwa sababu wanaamini kuwa kina nguvu maalum, kama vile udhibiti fulani juu ya ulimwengu, nguvu fulani ya kufaidika au kudhuru, au kuwa kinastahili kuabudiwa ndani na chenyewe kwa sababu ya ukuu wake. Mungu anapuuza wazo kuwa vitu hivi ambavyo watu huchukulia kama vitu vya kuabudiwa, ikiwa ni vitu vya asili, kama vile upepo, miti, mawe, upepo; au viumbe vyenye ufahamu, kama wanadamu, manabii, watakatifu, malaika, wafalme, wana nguvu yoyote ndani yao. Wameubwa tu kama waabudu wenyewe na hawana uwezo wa kujisaidia wao wenyewe, na kwa hivyo hawapaswi kuabudiwa. Wao wameubwa tu na upungufu, chini ya Mapenzi ya Mungu, na kwa hivyo hawastahili aina yoyote ya ibada.

Kiuhalisia, wengi wanaamini katika udhibiti wa mwisho na nguvu ya Mungu, lakini wanafikiria Ufalme wa Utawala wa Mungu kuwa kama tawala za kidunia. Kama vile mfalme ana mawaziri wengi na washirika waaminifu, wanafikiria 'watakatifu' na miungu ndogo kuwa waombezi wetu kwa Mungu. Wanawachukulia kama mawakala ambao kwa kupitia kwao Mungu anafikiwa, kwa kuelekeza vitendo kadhaa vya ibada na huduma kwao. Mungu anasema:

“Na ukiwauliza: Ni nani aliye ziumba mbingu na ardhi.’

Bila shaka watasema: 'Mwenyezi Mungu'

Sema: Je! Mnawaonaje wale mnao waomba badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa Mwenyezi Mungu akitaka kunidhuru, wao wanaweza kuniondolea dhara yake? Au akitaka kunirehemu, je, wao wanaweza kuzuia rehema yake? '

Sema: Mwenyezi Mungu ananitosheleza. Kwake Yeye wategemee wanao tegemea.’” (Kurani 39:38)

Kiukweli, hakuna waombezi katika Uislamu. Hakuna mtu sahihi anayepaswa kuabudiwa, wala kiumbe mwingine yeyote anayepaswa kuabudiwa. Mwislamu anaelekeza kuabudu kote moja kwa moja na kikamilifu kwa Mungu peke yake.

…Ill-Allah (…Isipokuwa Allah)

Baada ya kukataa haki ya kiumbe aliyeumbwa kuabudiwa, shahaadah inathibitisha uungu kwa Mungu peke yake, na '… isipokuwa Mungu'. Katika maeneo mengi katika Kurani, baada ya Mungu kukanusha kuwa kitu chochote kilichoubwa hakina uwezo wa kuleta faida na madhara, kwa hivyo hakistahili kuabudiwa, Anasema kwamba Yeye mwenyewe ndiye anayepaswa kuabudiwa, kwa kuwa ana mamlaka juu ya umiliki wa ulimwengu wote. Ni Mungu Peke yake ambaye huwapa katika aliowaumba; Yeye ndiye mwenye udhibiti kamili. Yeye ndiye pekee anayeweza kuleta faida na madhara, na hakuna kitu kinachoweza kuzuia Mapenzi yake kuwa ukweli. Kwa hivyo ni Yeye mwenyewe, kupitia ukamilifu wake, kupitia nguvu Zake za mwisho, kwa sababu ya umiliki wake kamili, na kwa sababu ya ukuu Wake, ambaye anastahili kuabudiwa, kuhudumiwa na kuabudiwa peke yake.

“Sema: Ni nani Mola wa mbingu na ardhi?’

Sema: 'Ni Mwenyezi Mungu.’

Sema: 'Basi je, mmejifanyia badala yake walinzi (wengine) wasiomiliki juu ya nafsi zao manufaa wala madhara?'

Sema: 'Je, ni sawa kipofu na mwenye kuona, au je, ni sawa kiza na nuru? Au wamemjaaliya Mwenyezi Mungu kuwa na washirika wanaumba kama anavyoumba wakashabihiana viumbe (vyao) kwao?'

Sema: 'Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wa kila kitu, naye ni Mmoja Mwenye kushinda.'

Mungu pia anasema:

“Hakika nyinyi mnaabudu masanamu badala ya Mwenyezi Mungu, na mnazua uzushi. Hakika hao mnao waabudu badala ya Mwenyezi Mungu hawakumilikiini riziki yoyote. Takeni riziki kwa Mwenyezi Mungu, na mumuabudu Yeye, na mumshukuru Yeye. Kwake Yeye ndio mtarudishwa. ” (Kurani 29:17)

Mungu anasema:

“au nani yule aliye ziumba mbingu na ardhi, na akakuteremshieni maji kutoka mbinguni, na kwa hayo tukaziotesha bustani zenye kupendeza? Nyinyi hamna uwezo wa kuiotesha miti yake. Je! Yupo mungu pamoja na Mwenyezi Mungu? Bali hao ni watu walio potoka. ” (Kurani 27:60)

Kwa kuwa Mungu pekee ndiye anayestahili kuabudiwa, kitu chochote kinachoabudiwa sambamba au pamoja naye ni makosa. Matendo yote ya kujitolea yanapaswa kuelekezwa kwa Mungu peke yake. Mahitaji yote yanapaswa kutafutwa kupitia Yeye. Hofu yote isiyojulikana inapaswa kuogopwa kutoka Kwake, na tumaini lote liwekwe Kwake. Upendo wote wa kimungu unapaswa kuhisiwa kwa ajili yake, na yote ambayo mtu huchukia anapaswa kuchukiwa kwa ajili Yake. Matendo yote ya kheri yanapaswa kufanywa ili kutafuta upendeleo na raha Yake, na mabaya yote yanapaswa kuepukwa kwa ajili yake. Kwa njia hizi Waislamu humwabudu Mungu peke yake, na kutokana na hili, tunaelewa jinsi dini zima ya Uislam linavyotegemea tamko hili la Tawheed.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.