요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Katika moyo wa Uislam kuna kumwamini Mungu.
Katika moyo wa Uislamu kuna kumwamini Mungu. Msingi wa imani ya Uislam unashuhudia kifungu hicho, La illaha illa Allah, "Hakuna mungu wa kweli anayepaswa kuabudiwa isipokuwa Mungu." Ushuhuda wa imani hii, inayoitwa tawhid, ndio mhimili ambao Uislamu unauzunguka. Cha kuongezea, ni moja ya shuhuda kati ya mbili ambazo zinamfanya mtu kuwa Muislamu. Kujitahidi baada ya utambuzi wa umoja, au tawhid, ndio msingi wa maisha ya Uislamu.
Kwa watu wengi wasio Waislamu, neno Allah, jina la Kiarabu la Mungu, linahusu mungu fulani wa mbali na wa ajabu anayeabudiwa na Waarabu. Wengine hata huwa wanafikiria ni "mungu mwezi" wa kipagani. Ila, kwa Kiarabu, neno Allah linamaanisha Mungu Mmoja wa Kweli. Hata, Wayahudi na Wakristo wanaozungumza Kiarabu wanamtaja Kiumbe Mtakatifu kuwa Allah.
Wanafalsafa wa Magharibi, Maistiki wa mashariki na vile vile wanasayansi wa leo wanajaribu kumfikia Mungu kwa njia zao wenyewe. Maistiki hufundisha juu ya Mungu ambaye hupatikana kupitia uzoefu wa kiroho, Mungu ambaye ni sehemu ya ulimwengu na anakaa ndani ya uumbaji wake. Wanafalsafa wanamtafuta Mungu kwa mawazo ya kimantiki na mara nyingi huongea juu ya Mungu kama Mtengenezaji aliyejitenga asiye na hamu ya uumbaji Wake. Kikundi cha wanafalsafa hufundisha ujamaa, itikadi ambayo inashikilia kuwa mtu hawezi kuthibitisha wala kupinga uwepo wa Mungu. Hakika, mtu agnostiki anadai lazima awe na uwezo wa kumtambua Mungu moja kwa moja ili awe na imani. Mungu amesema:
" Na walisema wale wasio jua kitu: Mbona Mwenyezi Mungu hasemi nasi au zikatufikia Ishara. Kama hivyo walisema wale walio kuwa kabla yao mfano wa kauli yao hii. Nyoyo zao zimefanana..." (Kurani 2:118)
Hoja sio mpya; watu wa zamani na wa sasa wameibua pingamizi hilo hilo.
Kulingana na Uislamu, njia sahihi ya kumpata Mungu ni kupitia mafundisho yaliyohifadhiwa ya manabii. Uislamu unashikilia kuwa manabii walitumwa na Mungu mwenyewe katika zama zote ili kuwaongoza wanadamu. Mungu anasema katika Kurani Tukufu kwamba njia sahihi ya imani ni kutafakari juu ya ishara Zake, zinazoelekeza kwake:
"…Hakika Sisi tumeziweka wazi Ishara kwa watu wenye yakini. " (Kurani 2:118)
Kutajwa kwa kazi ya mikono ya Mungu hufanyika mara nyingi katika Kurani kama eneo la ufunuo wa kimungu. Mtu yeyote anayeuona ulimwengu wa asili katika maajabu yake yote kwa macho yote na moyo wote ataona ishara zisizo na shaka za Muumba.
"Sema: Tembeeni katika ardhi na tazameni jinsi alivyo anzisha uumbaji; kisha Mwenyezi Mungu ndiye anaye umba umbo la baadaye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza juu ya kila kitu. " (Kurani 29:20)
Kazi ya mikono ya Mungu pia ipo ndani ya mtu binafsi:
"Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini. Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni? " (Kurani 51:20-21)
Uzuri na ugumu wa ulimwengu wetu. Cone Nebula iliyoonyeshwa na Darubini ya Anga ya Hubble ya NASA. (AP Photo/NASA)
Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.
Orodha yako ya historia ipo tupu.
Kwa nini kujiandikisha? Tovuti hii ina miundo kadhaa uliyoundwa mahsusi kwa ajili yako, kama vile: vipendwa vyako, historia yako, kutia alama makala ambazo umezitazama awali, kuorodhesha makala zilizochapishwa tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho, kubadilisha ukubwa wa herufi, na zaidi. Vipengele hivi vinatokana na vidakuzi na vitafanya kazi ipasavyo tu unapotumia kompyuta ile ile. Ili kuwezesha vipengele hivi kutoka kwa kompyuta yoyote, unapaswa kuingia wakati katika tovuti hii.
Tafadhali ingiza Jina lako la mtumiaji na anwani ya barua pepe kisha ubofye kitufe cha Tuma neno la siri. Utapokea neno la siri jipya hivi karibuni. Tumia neno la siri hili jipya kufikia tovuti.
Ongeza maoni