Wokovu katika Uislamu (sehemu ya 3 kati ya 3): Toba

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Toba inaashiria njia ya wokovu.

  • Na Aisha Stacey (© 2010 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 02 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,187 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Salvation_in_Islam_(part_3_of_3)_001.jpg

Njia ya wokovu ni kupitia imani hakika ya kuwa kuna Mungu Mmoja tu na kuwa Yeye ni Msamehevu na Mwenye kurehemu. Uislamu unasema bila kujibakiza kuwa hakuna dhana ya dhambi ya asili na kwamba Mungu haitaji kafara ya damu ili kuwasamehe wanadamu kwa dhambi zao na makosa yao.

“ Sema: Enyi waja wangu ambao wamedhulumu nafsi zao (kwa kufanya maasiya)! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Msamehevu, Mwenye kurehemu. ” (kurani 39:53)

Kufanya makosa, kupungukiwa katika utii wetu kwa Mungu, kusahau, na kutenda dhambi zote ni sehemu za asili zisizo kamilika za wanadamu. Hakuna mwanadamu aliye huru na dhambi, bila kujali jinsi tunavyoonekana kuwa wazuri na kila mwanadamu anahitaji msamaha wa Mungu. Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alikuwa akijua jambo hili wakati akipozungumza na mashahaba zake.

“Kwa Yeye ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, ikiwa haukufanya dhambi Mungu angekuondoa na kuleta watu ambao wangefanya dhambi kisha wakaomba msamaha.”[1]

“Kila mwana wa Adamu anatenda dhambi na bora ya wale wanaotenda dhambi ni wale wanaotubu.”[2]

Sisi sote ni dhaifu, sote tunafanya dhambi, na sote tunahitaji kusamehewa. Tuna uhitaji wa kiasili wa kujisikia karibu na Mungu na Mungu katika hekima yake isiyo na kipimo ametufanyia njia ya msamaha iwe rahisi. Mtume Muhammad mwenyewe alipata furaha kuu iliyotokana na kujisikia "sawa" na Mola wake. Alisema, “Kwa Mungu, natafuta msamaha wa Mungu na ninamgeukia kwa toba zaidi ya mara sabini kila siku.”[3]

Mungu, Muumbaji anawajua wanadamu kikamilifu, Anajua kutokamilika kwetu na mapungufu yetu, na kwa hivyo ameamuru toba kwetu na akaacha mlango wa toba umefunguliwa mpaka jua litakapotokea magharibi (karibu na Siku ya Hukumu).

“Na rejeeni kwa Mola wenu Mlezi, na silimuni kwake, kabla ya kukujieni adhabu. Kisha hapo hamtanusuriwa.” (Kurani 39:54)

“ Enyi mlio amini! Tubuni kwa Mwenyezi Mungu toba iliyo ya kweli! Asaa Mola wenu Mlezi akakufutieni maovu yenu na akakuingizeni katika Pepo zipitazo mito kati yake(Peponi)…”(Kurani 66:8)

“Na tubuni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa.” (Kurani 24:31)

Toba ni rahisi ni kumgeukia Mungu na kutafuta rehema na msamaha Wake. Katika saa ya giza au usiku mrefu zaidi, Mungu husubiri wote wamwombe, na watubu kwake.

“Mungu hunyosha mkono wake usiku ili kukubali toba ya yule aliyetenda dhambi wakati wa mchana, na ananyoosha mkono wake mchana ili kukubali toba ya yule aliyetenda usiku, (na hiyo itaendelea) mpaka jua litakapotoka magharibi. ”[4]

Hakuna makosa madogo sana au dhambi kubwa ambayo Mungu hatakuwa na huruma kwa yule anayemwita. Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alisimulia hadithi ya mtu ambaye dhambi zake zilionekana kuwa kubwa mno kwake hata kutokuwa na tumaini la rehema, lakini Mungu ni mwenye busara na mwenye kusamehe sana. Hata wale ambao maisha yao yanaonekana kuharibika kupita kiasi na kuwa meusi na dhambi, wanapata faraja.

“Kulikuwa na miongoni mwa watu waliokuja kabla yako mtu aliyewaua watu tisini na tisa. Kisha akamuulizia mtu aliye na ufahamu zaidi duniani, na akaelekezwa kwenye ngome, kwa hivyo akaenda kwake, akamwambia kuwa ameua watu tisini na tisa, na akauliza ikiwa anaweza kusamehewa. Mkubwa huyo alisema, 'Hapana,' kwa hivyo akamwua, na hivyo kukamilisha idadi ya watu mia moja. Kisha akamuulizia mtu mwingine mwenye ujuzi zaidi duniani na akaelekezwa kwa msomi. Alimwambia kuwa ameua watu mia moja, na akauliza ikiwa anaweza kusamehewa. Msomi alisema, ‘Ndio, ni nini kinachoweza kukukinga kati yako na toba? Nenda katika mji fulani na fulani, kwa maana ndani yake kuna watu wanaomwabudu Mungu. Nenda ukaabudu pamoja nao, wala usirudi katika mji wako, kwa maana mahali hapa ni pabaya. ” Kwa hivyo yule mtu akaondoka, lakini wakati akiwa katikati, malaika wa kifo alimjia, na malaika wa rehema na malaika wa adhabu walianza kujadili juu yake. Malaika wa rehema walisema: ‘Alikuwa ametubu na alikuwa akimtafuta Mungu.’ Malaika wa adhabu wakasema: ‘Hakufanya jambo lolote jema.’ Malaika aliye na umbo la kibinadamu alikuja kwao, na wakamwuliza aamue jambo hilo. Alisema, "Pima umbali kati ya ardhi hizo mbili (mji wake na mji aliokuwa akielekea), na ambayo ipo karibu zaidi kati ya hizo mbili ndiyo ambayo anamiliki." Kwa hivyo walipima umbali, na wakapata alikuwa karibu na mji ambao alikuwa ameelekea, kwa hivyo malaika wa rehema walimchukua.” [5]

Katika toleo jingine kutoka katika mila ya Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, inasema, mtu huyo alikuwa karibu na mji wa haki kwa urefu wa mkono, kwa hivyo alihesabiwa kati ya watu wa mji huo.[6]

Toba ni muhimu kwa mtu ili aweze kuishi maisha ya amani. Zawadi ya toba ni maisha mazuri ya ukaribu na Mungu na kufunikwa na kuridhika na amani ya akili. Hata hivyo, kuna hali tatu za kutubu. Ambazo ni, kuachana na dhambi hiyo, kujuta milele kuwa umefanya dhambi hiyo na kuazimia kutorudia tena kwenye dhambi. Ikiwa hali hizi tatu zinatimizwa kwa uaminifu basi Mungu atasamehe. Ikiwa dhambi hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya haki za mtu mwingine basi kuna hali ya nne. Hiyo ni kurudisha, ikiwezekana kibinadamu, haki zilizochukuliwa.

Rehema na msamaha wa Mungu vyote vinajumuisha kuwa ataendelea kusamehe. Ikiwa mtu ni mkweli, Mungu atamsamehe hadi wakati ambapo sauti ya kifo itafikia kwenye koo.

Msomi mashuhuri wa Kiisilamu Ibn Kathir alisema, “Hakika, wakati tumaini la kuendelea kuishi linapopungua, Malaika wa Kifo hujitokeza kukusanya roho. Nafsi inapofika kooni, na kutolewa hatua kwa hatua, wakati huo hakuna toba inayokubaliwa.”[7]

Toba ya kweli inaashiria njia ya wokovu. Wokovu unapatikana kupitia kwa kumwabudu Mungu kwa dhati. Hakuna Mungu ila Yeye, mwenye nguvu zaidi, mwenye kurehemu, na mwenye kusamehe.[8]



Rejeleo la maelezo:

[1] Saheeh Muslim

[2] At Tirmidhi

[3] Saheeh Al-Bukhari

[4] Saheeh Muslim

[5] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim

[6] Saheeh Muslim

[7] Tafsir Ibn Kathir, Sura ya 4, aya ya 18.

[8] Kwa taarifa zaidi juu ya msamaha wa Mungu tafadhali angalia nakala zenye kichwa Kuukubali Uislamu sehemu ya 1 & 2. (http://www.islamreligion.com/articles/3727/viewall/)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.