Kuwaamini Mitume

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kusudi na jukumu la Manabii, asili ya ujumbe ambao walileta kwa wanadamu, na msisitizo wa kuwa walikuwa wanadamu tu wasio na sifa za kimungu.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 06 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,458 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Belief_in_Prophets_001.jpgKuwaamini mitume ambao Mungu alichagua kupeleka ujumbe wake kwa wanadamu ni kifungu kinachohitajika katika imani ya Kiislamu

"Mtume ameamini yaliyo teremshwa kwake kutoka kwa Mola Mlezi wake, na Waumini vile vile. Wote wamemuamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake na Mitume wake. Hatutafautishi baina ya yeyote katika Mitume wake...’" (Kurani 2:285)

Mungu huwasilisha ujumbe wake na anaelezea mapenzi yake kupitia manabii wa kibinadamu. Wanaunda uhusiano kati ya viumbe wa duniani na mbinguni, kwa maana kwamba Mungu amewachagua kupeleka ujumbe wake kwa wanadamu. Hakuna njia zingine za kupokea mawasiliano ya kimungu. Ni mfumo wa mawasiliano kati ya Muumba na aliyeumbwa. Mungu hatumi malaika kwa kila mtu, wala hafungui mbingu ili watu waweze kupanda juu kupokea ujumbe. Njia yake ya mawasiliano ni kupitia manabii wa kibinadamu ambao hupokea ujumbe kupitia malaika.

Kuwa na imani na manabii (au wajumbe) ni kuamini kwamba Mungu alichagua watu wenye maadili mema ili kubeba ujumbe wake na kuupitisha kwa wanadamu. Wamebarikiwa wale waliowafuata, na wamelaaniwa wale waliokataa kutii. Waliwasilisha ujumbe huo kwa uaminifu, bila kuuficha, kuubadilisha, au kuuharibu. Kumkataa nabii ni kumkataa Yule aliyemtuma, na kutomtii nabii ni kutomtii Yule aliyeamuru kumtii.

Mungu alituma kwa kila taifa nabii, hususani kutokana na wao, kuwaita wamwabudu Mungu peke yake na waachane na miungu ya uwongo.

"Na waulize Mitume wetu tulio watuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Rah'mani? ’" (Kurani 43:45)

Waislamu wanaamini katika manabii hao waliotajwa kwa majina katika vyanzo vya Kiislamu, kama vile Adamu, Nuhu, Ibrahimu, Isaka, Ismaili, Daudi, Sulemani, Musa, Yesu, na Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, kwa kutaja wachache . Imani ya jumla inafanyika kwa wale ambao hawajatajwa kwa majina, kama Mungu alivyosema:

"Na bila ya shaka tuliwatuma Mitume kabla yako. Wengine katika hao tumekusimulia khabari zao, na wengine hatukukusimulia..." (Kurani 40:78)

Waislamu wanaamini kabisa kuwa nabii wa mwisho alikuwa Nabii wa Uislamu, Muhammad, na hakutakuwa na nabii au mjumbe baada yake.

Ili kufahamu ukweli huu, mtu lazima aelewe kwamba mafundisho ya nabii wa mwisho yamehifadhiwa kwa lugha asili katika chanzo chake cha mwanzo. Hakuna haja ya nabii mwingine. Kwa upande wa manabii wa awali, maandiko yao yalipotea au ujumbe wao uliharibiwa hadi ukweli haukuweza kutofautishwa na uwongo. Ujumbe wa Nabii Muhammad uko wazi na umehifadhiwa na utabaki hivyo mpaka mwisho wa muda.

Kusudi la kutuma Mitume

Tunaweza Kuona sababu kuu zifuatazo za kutuma manabii:

(1) Kuongoza wanadamu kutoka kwenye ibada ya viumbe vilivyoumbwa hadi ibada ya Muumba wao, kutoka kwenye katika hali ya utumwa hadi uumbaji hadi uhuru wa kumwabudu Mola wao.

(2) Kufafanua kwa wanadamu kusudi la uumbaji: kumwabudu Mungu na kutii amri Zake, na pia kufafanua kuwa maisha haya ni mtihani kwa kila mtu, jaribio ambalo matokeo yake yataamua aina ya maisha ambayo mtu ataelekea baada ya kifo; maisha ya taabu ya milele au raha ya milele. Hakuna njia nyingine dhahiri ya kupata kusudi la kweli la uumbaji.

(3) Kuonyesha wanadamu njia sahihi ambayo itawaongoza kwenda Peponi nakuokolewa kutokana na Moto wa Jehanamu.

(4) Kuweka uthibitisho dhidi ya wanadamu kwa kutuma manabii, kwa hivyo watu hawatakuwa na udhuru pindi watakapoulizwa Siku ya Hukumu. Hawataweza kudai kutojua kusudi la kuumbwa kwao na maisha baada ya kifo.

(5) Kufunua "ulimwengu" usioonekana ambao upo juu ya akili za kawaida na ulimwengu wa mwili, kama vile kumjua Mungu, uwepo wa malaika, na ukweli wa Siku ya Hukumu.

(6) Kuwapa wanadamu mifano kwa vitendo ili kuwaongoza katika maisha ya maadili, ya haki, yanayotokana na kusudi lisilo na mashaka na mkanganyiko. Kiuhalisia, wanadamu wanapenda wanadamu wenzao, kwa hivyo mifano bora ya haki kwa wanadamu ili iweze kuigwa ni ile ya manabii wa Mungu.

(7) Kuitakasa roho kutokana na mapenzi ya mali, dhambi, na kutokuzingatia.

(8) Kuwaonyesha wanadamu mafundisho ya Mungu, ambayo ni kwa faida yao wenyewe katika maisha haya na maisha ya Baadae.

Ujumbe Wao

Ujumbe mmoja wa muhimu zaidi wa manabii wote kwa watu wao ulikuwa kumwabudu Mungu peke yake na sio mwingine na kufuata mafundisho Yake. Wote hao, Nuhu, Ibrahim, Iskhaka, Ismail, Musa, Haruni, Daudi, Sulemani, Yesu, Muhammad na wengineo, pamoja na wale ambao hatuwajui - waliwaalika watu kumwabudu Mungu na kuachana na miungu ya uwongo.

Moses alieleza: "Sikieni, Enyi Waisraeli, Mola, Mungu wetu, ni Mola mmoja." (Kumbukumbu la Torati 6:4).

Hii ilirudiwa miaka 1500 baadaye na Yesu, aliposema: "Amri ya kwanza ni hii," Sikieni, Waisraeli; Mola Mungu wetu ni Mola mmoja. "(Marko 12:29).

Mwisho, wito wa Muhammad miaka 600 baadaye ulisikika tena kwenye milima ya Makka:

"Na Mungu wenu ni Mungu mmoja tu, hapana mungu ila Yeye..." (Kurani 2:163)

Quran Tukufu imeeleza wazi wazi:

"Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hapana mungu isipokuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi tu. " (Kurani 21:25)

Wabebaji wa Ujumbe

Mungu alichagua wabora kati ya wanadamu kufikisha ujumbe wake. Utume haupatikani au hupatikana kama elimu ya juu. Mungu humchagua amtakaye kwa kusudi hili.

Walikuwa wabora kimaadili na walikuwa sawa kiakili na kimwili, walilindwa na Mungu wasiangukie kwenye dhambi kuu. Hawakukosea au kufanya makosa katika kufikisha ujumbe. Walikuwa zaidi ya manabii laki moja waliotumwa kwa wanadamu wote, kwa mataifa yote na jamii, katika pembe zote za ulimwengu. Manabii wengine walikuwa wabora kuliko wengine. Waliokuwa wa bora miongoni mwao walikuwa ni Nuhu, Ibrahim, Musa, Yesu, na Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake.

Watu waliwakorofisha sana manabii. Walikataliwa na kushutumiwa kuwa wachawi, wendawazimu, na waongo. Wengine waliwageuza miungu kwa kuwapa nguvu za kimungu, au kuwatangaza kuwa watoto Wake, kama kilichotokea kwa Yesu.

Ukweni ni kwamba, walikuwa wanadamu kamili bila sifa za kimungu au nguvu. Walikuwa watumwa wa kumwabudu Mungu. Walikula, kunywa, kulala, na kuishi maisha ya kawaida ya wanadamu. Hawakuwa na uwezo wa kumfanya mtu yeyote akubali ujumbe wao au kusamehe dhambi. Ujuzi wao wa siku zijazo ulikuwa mdogo kwa kile Mungu aliwafunulia. Hawakuwa na sehemu katika kuendesha shughuli za ulimwengu.

Kutokana na Rehema na Upendo wa Mungu usio na mwisho, Aliwatuma manabii kwa wanadamu, akiwaongoza kwa yaliyo bora zaidi. Aliwatuma kama mfano kwa wanadamu ili waweze kuwafuata, na ikiwa mtu atafuata mfano wao, ataishi maisha kulingana na Mapenzi ya Mungu, akipata Upendo na Raha yake.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako