Kuamini Maandiko

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kwa nini Mungu alifunua ujumbe wake kwa njia ya maandiko, na maelezo mafupi ya maandiko mawili ya Mungu: Biblia, na Kurani.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 06 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 1
  • Imetazamwa: 2,176 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Belief_in_Scriptures_001.jpgKuamini maandiko yaliyofunuliwa na Mungu ni kifungu cha tatu cha imani ya Kiislamu.

Tunaweza kubainisha sababu kuu nne za kufunuliwa kwa maandiko:

(1) Andiko lililofunuliwa kwa nabii ni hatua ya kumbukumbu ya kujifunza dini na wajibu kwa Mungu na wanadamu wenzetu. Mungu hujionyesha na kuelezea kusudi la uumbaji wa wanadamu kupitia maandiko yaliyofunuliwa.

(2) Kwa kurejea kwake, "mizozo na tofauti kati ya wafuasi wake katika suala la imani ya kidini na matendo au katika maswala ya kijamii yanaweza kusuluhishwa.

(3) Maandiko yanakusudiwa kuiweka dini salama kutokana na ufisadi na kuzorota, angalau kwa muda baada ya kifo cha nabii. Kwa wakati huu wa sasa, Kurani iliyofunuliwa kwa Nabii wetu Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, ndio andiko pekee lililobaki salama kutokana na ufisadi.

(4) Ni uthibitisho wa Mungu dhidi ya wanadamu. Hawaruhusiwi kuipinga au kuivuka.

Muislamu anaamini kabisa kuwa vitabu vilivyofunuliwa na Mungu vilifunuliwa kweli na Mungu mwenye Huruma kwa manabii wake ili kuwaongoza wanadamu. Kurani sio tu Neno la Mungu lililonenwa, lakini Mungu pia alizungumza na manabii kabla ya Nabii Muhammad.

"…Na Mwenyezi Mungu alinena na Musa kwa maneno." (Kurani 4:164)

Mungu amewaelezea waumini wa kweli ni wale:

"…wanayaamini yaliyo teremshwa kwako, na yaliyo teremshwa kabla yako…" (Kurani 2:4)

Ujumbe muhimu na wa kimsingi zaidi wa maandiko yote ulikuwa kumwabudu Mungu na Mungu peke yake.

"Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hapana mungu isipo kuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi tu. ’" (Kurani 21:25)

Uislamu umejumuishwa zaidi katika ufunuo mtakatifu unaothibitisha kuliko dini nyingine yoyote katika hali yake ya sasa.

Waislamu wanashikilia na kuheshimu maandiko yafuatayo:

(i) Kurani yenyewe, ilifunuliwa kwa Mtume Muhammad.

(ii) Torati (Tawrah kwa Kiarabu) ilifunuliwa kwa Mtume Musa (tofauti na Agano la Kale linalosomwa leo).

(iii) Injili (Injeel kwa Kiarabu) ilifunuliwa kwa Mtume Yesu (tofauti na Agano Jipya linalosomwa makanisani leo).

(iv) Zaburi (Zaboor kwa Kiarabu) ya Daudi.

(v) Hatikunjo (Suhuf kwa Kiarabu) ya Musa na Ibrahimu.

Tatu, Waislamu wanaamini kila kitu cha kweli ndani yao kisichobadilishwa au kutafsiriwa vibaya kwa kusudi fulani.

Nne, Uislamu unathibitisha kuwa Mungu aliifunua Kurani kama shahidi juu ya maandiko yaliyotangulia na uthibitisho wake, kwa sababu Anasema ndani yake:

"Na tumekuteremshia wewe, kwa haki, Kitabu hichi kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Vitabu na kuyalinda. Basi hukumu baina yao kwa aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu.…" (Kurani 5:48)

Inamaana Kurani inathibitisha chochote kilicho cha kweli katika maandiko yaliyopita na inakataa mabadiliko yoyote na mabadiliko ambayo mikono ya wanadamu imeyafanya kwenye hayo maandiko.

Maandiko ya Asili na biblia

Lazima tutofautishe kati ya mambo mawili: Torati halisi, Injili, na Zaburi na Biblia ya leo. Halisi ulikuwa ufunuo wa Mungu, lakini Biblia ya leo haina maandiko yale halisi.

Hakuna maandiko matakatifu yaliyopo leo katika lugha ya asili ambayo yalifunuliwa nayo, isipokuwa Kurani. Biblia haikufunuliwa kwa Kiingereza. Vitabu tofauti vya Biblia ya leo viko katika tafsiri ya matoleo tofauti. Tafsiri hizi nyingi zilifanywa na watu ambao ujuzi, ustadi, au uaminifu wao haujulikani. Kwa sababu hii, biblia zingine ni kubwa kuliko zingine na zina utata na kutofautiana kwa ndani! Hakuna uhalisia uliopo. Kwa upande mwingine, Kurani ndiyo andiko pekee ambalo lipo leo katika lugha yake ya asili na maneno. Hakuna herufi hata moja ya Kurani iliyobadilishwa tangu kufunuliwa kwake. Ipo sawa kwa ndani na haina ubishi. Iliyopo leo ni sawa kama ilifunuliwa miaka 1400 iliyopita, ilisambazwa kwa mila thabiti ya kukariri na kuandika. Tofauti na maandiko mengine matakatifu, Kurani nzima imekaririwa na karibu kila msomi wa Kiislamu na mamia ya maelfu ya Waislamu wa kawaida, kizazi baada ya kizazi!

Maandiko yaliyotangulia kimsingi yana:

(i) Hadithi za uumbaji wa mwanadamu na mataifa ya mwanzo, hutabiri juu ya kile kitakachokuja kama ishara kabla ya Siku ya Hukumu, kutokea kwa manabii wapya, na habari zingine.

Hadithi, utabiri, na habari zilizo katika Biblia inayosomwa katika makanisa na masinagogi leo baadhi yana kweli na baadhi ni uwongo. Vitabu hivi vinajumuisha vipande vilivyotafsiriwa vya maandishi ya asili yaliyofunuliwa na Mungu, maneno ya manabii wengine, yaliyochanganywa na maelezo ya wasomi, makosa ya waandishi, na kuingizwa na kufutwa kwa nia mbaya. Kurani, ndilo andiko la mwisho na la kuaminika, linalotusaidia kutambua ukweli kutoka kwenye bunilizi, katika hadithi hizi. Kwa Muislamu, ni kigezo cha kuhukumu ukweli kutoka kwenye uwongo katika hadithi hizi. Kwa mfano, Biblia bado ina vifungu vinavyoonyesha umoja wa Mungu.[1] Kadhalika, baadhi ya utabiri kuhusu Nabii Muhammad unapatikana katika Biblia pia.[2] Ila, kuna vifungu, hata vitabu vizima, karibu vinatambulika kughushiwa na kuwa mkono wa mwanadamu.[3]

(ii) Sheria na kanuni, yaliyoruhusiwa na yaliyokatazwa, kama Sheria ya Musa.

Ikiwa tutadhania sheria, yaani yaliyohalalishwa na yaliyokatazwa, yaliyomo katika vitabu vya mwanzo hayakupata ufisadi, Kurani bado inafuta maamuzi hayo, inafuta sheria ya zamani ambayo ilikuwa inafaa kwa wakati wake na haitumiki tena leo. Kwa mfano, sheria za zamani zinazohusu lishe, ibada, kufunga, urithi, ndoa na talaka zimefutwa (au, mara nyingi, zimethibitishwa) na Sheria ya Kiislamu.

Kurani Tukufu

Kurani ipo tofauti na maandiko mengine katika vipengele vifuatavyo:

(1) Kurani ni mujiza na usio na kifani. Hakuna kama hiki kinachoweza kuzalishwa na wanadamu.

(2) Baada ya Kurani, hakuna maandiko mengine yatakayofunuliwa na Mungu. Kama vile Mtume Muhammad ndiye mtume wa mwisho, Kurani ndio andiko la mwisho.

(3) Mwenyezi Mungu amechukua jukumu mwenyewe kuilinda Kurani kutokana na mabadiliko, kuilinda na uharibifu, na kuihifadhi kutokana na upotovu. Kwa upande mwingine, maandiko yaliyotangulia yalibadilishwa na kupotoshwa na hayakubaki katika hali yake iliyofunuliwa hapo mwanzo.

(4) Kurani, kwa pamoja, inathibitisha maandiko ya mwanzo na, kwa lingine, ni shahidi wa kuaminika juu ya hiyo.

(5) Kurani inatengua, ikimaanisha inafuta hukumu za maandiko yaliyotangulia na kuzifanya kuwa zisizofaa. Sheria za maandiko ya zamani hazitumiki tena; Maamuzi ya hapo awali umetenguliwa na Sheria mpya ya Uislamu.



Rejeleo la maelezo:

[1] Kwa mfano tamko la Musa: "Sikilizeni, Ee Waisraeli, Mola Mungu wetu ni Mola mmoja" (Kumbukumbu ya Torati 6: 4) na elezo la Yesu: "... Amri ya kwanza ni hii, Sikia, Waisraeli; Mola Mungu wetu ni Mola mmoja." (Marko 12:29).

[2] Rejea (Kumbukumbu ya Torati 18:18), (Kumbukumbu ya Torati 33: 1-2), (Isaya 28:11), (Isaya 42: 1-13), (Habakuki 3: 3), (Yohana 16:13), (Yohana 1: 19-21), (Mathayo 21: 42-43), na zaidi.

[3] Kwa mfano, rejea kwenye vitabu vya Apokrifa.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako