Maelezo ya moto wa Jahannamu (sehemu ya 1 kati ya 5): Utangulizi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Majina ya Jahannamu na uwepo wake wa milele, na walinzi wake.

  • Na Imam Mufti
  • Iliyochapishwa mnamo 13 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 5,723 (wastani wa kila siku: 7)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

A_Description_of_Hellfire_(part_1_of_5)_001.jpgUislamu unafundisha kwamba Jahannamu ni mahali pa kweli palipotayarishwa na Mwenyezi Mungu kwa wasiomuamini Yeye, na wanaasi dhidi ya sheria zake, na wanawakataa Mitume wake. Jahannamu ni mahali halisi, si hali tu ya mawazo au kipengele cha kiroho. Hofu, maumivu, uchungu, na adhabu zote ni za kweli, lakini ni tofauti kiasili kuliko za dunia. Jahannamu ni udhalilishaji mbaya zaidi na hasara usio na kifani. Na hakuna kitu kibaya zaidi kuliko Jahannamu:

"Mola wetu Mlezi! Hakika unayemtia Motoni umemhizi; na waliodhulumu hawana wasaidizi." (Kurani 3:192)

"Je, hawajui ya kwamba anaye shindana na Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi huyo atapata Moto wa Jahannamu adumu humo? Hiyo ndiyo hizaya kubwa." (Kurani 9:63)

Majina ya Jahannamu

Moto wa Jahannamu una majina tofauti katika maandiko ya Kiislamu Kila jina linatoa maelezo tofauti. Baadhi ya majina yake ni:

Jaheem – moto - kwa sababu ya moto wake mkali.

Jahannam - shimo la moto - kwa sababu ya kina cha shimo lake.

Ladthaa - moto mkali - kwa sababu ya miali yake wake.

Sa’eer - mwali mkali - kwa sababu umewaka na kuwashwa.

Saqar - kwa sababu ya kiwango cha joto lake.

Hatamah - vipande vilivyovunjika au vifusi - kwa sababu huvunja na kusaga kila kitu kinachotupwa ndani yake.

Haawiyah - pengo au shimo - kwa sababu anayetupwa ndani yake anatupwa kutoka juu hadi chini.

Pepo na Jahannamu Zipo na ni za Milele

Jahannamu ipo wakati huu na itaendelea kuwepo milele. Haitaisha kamwe, na wakazi wake watabaki ndani yake milele. Hakuna atakayetoka Jahannamu ila wale walioamini umoja wa Mwenyezi Mungu katika maisha haya, na wakawaamini manabii waliotumwa kwao (kabla ya kuja kwaMuhammad). Washirikina na makafiri watakaa humo milele. Imani hii imeshikiliwa tangu zamani na inatokana na aya zilizo wazi katika Kurani na taarifa zilizothibitishwa kutoka kwa Mtume wa Uislamu. Kurani inazungumzia Jahannamu katika mfumo wa wakati uliopita na inasema kwamba tayari ilishaumbwa:

"Na uogopeni Moto ambao umeandaliwa kwa ajili ya makafiri." (Kurani 3:131)

Nabii wa Uislamu alisema:

"Na atakapo kufa mmoja kati yenu anaonyeshwa pahala pake( kwenye ahera) asubuhi na jioni. Akiwa yeye ni miongoni mwa watu wa Peponi basi anaonyeshwa mahali pa watu wa Peponi. Na akiwa yeye ni katika watu wa Motoni basi ataonyeshwa pahala pa watu wa Motoni. Anaambiwa: Hii ndio kikao chako mpaka Mwenyezi Mungu akufufueni Siku ya Kiyama." (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)

Katika ripoti nyingine, Nabii alisema:

"Hakika nafsi ya Muumini ni ndege anaye kaa juu ya miti ya Peponi, mpaka Mwenyezi Mungu airudishe kwenye mwili wake Siku ya Kiyama." (Muwatta of Malik)

Maandiko haya yanabainisha kuwa Jahannamu na Pepo zipo, na nafsi zitaziingia kabla ya Siku ya Kiyama. Akizungumza kuhusu udaima wa Jahannamu, Mungu anasema:

"Watataka watoke Motoni, lakini hawatatoka humo, na watakuwa na adhabu inayo dumu." (Kurani 5:37)

"…wala hawatakuwa wenye kutoka Motoni." (Kurani 2:167)

"Hakika wale walio kufuru na wakadhulumu hawi Mwenyezi Mungu kuwasamehe wala kuwaongoa njia. Isipo kuwa njia ya Jahannamu. Humo watadumu milele" (Kurani 4:168-169)

"Hakika Mwenyezi Mungu amewalaani makafiri, na amewaandalia Moto unaowaka na watadumu humo milele." (Kurani 33:64-65)

"Na wenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi hakika hao watapata Moto wa Jahannamu wadumu humo milele." (Kurani 72:23)

Walinzi wa Jahannamu

Malaika wenye nguvu wamesimama juu ya Jahannamu wasiomuasi Mwenyezi Mungu. Wanafanya hasa kama walivyoagizwa. Mungu anasema:

"Enyi mlio amini! Jilindeni nafsi zenu na ahali zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe. Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu, hawamuasi Mwenyezi Mungu kwa anayo waamrisha, na wanatenda wanayo amrishwa." (Kurani 66:6)

Kuna walinzi kumi na tisa wa Jahannamu kama Mungu anavyosema:

"Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar. Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar? Haubakishi wala hausazi, na unababua ngozi iwe nyeusi! Juu yake wapo kumi na tisa (walinzi wa Jahannamu)." (Kurani 74:26-30)

Wala mtu asidhani kwamba watu wa Motoni watawashinda walinzi wa Jahannamu kwa sababu idadi yao ni kumi na tisa tu. Kila mmoja wao ana nguvu ya kuangamiza wanadamu wote peke yake. Mungu anawaita Malaika hawa kama Walinzi wa Jahannamu katika Kurani:

"Na walio Motoni watawaambia walinzi wa Jahannamu: Mwombeni Mola wenu Mlezi atupunguzie walau siku moja ya adhabu!’" (Kurani 40:49)

Jina la malaika mkuu anayelinda Jahannamu ni Malik, kama ilivyoelezwa katika Kurani:

"Hakika makafiri watakuwa katika adhabu ya Jahannamu wadumu humo milele. Wala hawatapunguziwa adhabu, nao wataangamizwa kwa majuto makubwa na huzuni na wenye kukata tamaa. Na hatukuwadhulumu, lakini wao walikuwa madhaalimu. Na watlilia: Ewe Malik! Na atukomesha Mola wako Mlezi. Atasema: Hakika nyinyi mtadumu milele. Hakika Sisi tumewaletea Haki, lakini wengi wenu mnachukia Haki" (Kurani 43:74-78)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.