Kwa nini Mungu aliwaumba wanadamu? (sehemu ya 3 kati ya 4): Maisha kama Ibada

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kusudi la uumbaji wa wanadamu ni ibada. Sehemu ya 3: Katika mfumo wa Kiislamu, kila kitendo cha binadamu kinaweza kubadilishwa kuwa kitendo cha ibada.

  • Na Dr. Bilal Philips
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,921 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kila Tendo ni Ibada

Katika mfumo wa Kiislamu, kila kitendo cha binadamu kinaweza kubadilishwa kuwa kitendo cha ibada. Hakika Mwenyezi Mungu anawaamrisha Waumini wajitolee maisha yao yote kwake. Katika Qurani, Mungu anasema:

“Sema: Hakika Sala yangu, na dhabihu yangu, na uhai wangu, na kufa kwangu, ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote’” (Kurani 6:162)

Hata hivyo, kujitolea huku, ili kukubalika kwa Mungu, kila kitendo lazima kitimize masharti mawili ya kimsingi:

1. Kwanza, tendo hilo lazima lifanyike kwa dhati kwa ajili ya radhi ya Mungu na si kwa kutambuliwa na kusifiwa kwa wanadamu. Na muumini pia amjue Mwenyezi Mungu anapo fanya tendo ili kuhakikisha kwamba haijaharamishwa na Mwenyezi Mungu wala Mtume wa mwisho, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Ili kuwezesha mabadiliko hayo ya matendo ya kawaida kuwa ibada, Mungu alimuagiza Mtume wa mwisho, afundishe dua fupi za kusemwa kabla ya kufanya hata vitendo rahisi zaidi. Maombi mafupi ambayo inaweza kutumika kwa hali yoyote ni: Bismillaah (Kwa jina la Mungu). Hata hivyo kuna maombi mengine mengi yaliyowekwa kwa vipindi maalum. Kwa mfano, kila wakati ambao kipande kipya cha nguo huvaliwa, Mtume aliwafundisha masahaba wake kusema:

“Ewe Mwenyezi Mungu! Shukrani na sifa njema ni zako, kwani ni Wewe ndiye uliyenivisha. nakuomba manufaa yake na manufaa ya kila uliotengenezewa , na kujikinga kwako kutokana na uovu wake na uovu ulio uliotengenezewa.” (An-Nasa’i)

2. Sharti ya pili ni kwamba tendo lazima lifanyike kulingana na njia ya mtume, inayoitwa kwa Kiarabu Sunnah. Manabii wote waliwaagiza wafuasi wao wafuate njia yao kwa sababu waliongozwa na Mungu. Yale waliyofundisha yalikuwa ukweli kutoka kwa Mungu, na ni wale tu waliofuata njia yao na kukubali ukweli ndio wangerithi uzima wa milele katika paradiso. Ni katika muktadha huu ambapo Nabii Yesu, amani na baraka za Mungu ziwe juu yake, iliripotiwa kuwa alisema katika Injili kulingana na Yohana 14:6, akisema:

“Mimi ndiye njia na kweli na uzima, hakuna mtu ajaye kwa Baba ila kwa njia yangu.”

Vilevile, Abdullaah ibn Mas'ood alinukuli kwamba…

“Siku moja Mtume Muhammad alichora mstari kwenye mchanga na akasema: Hii ndiyo Njia ya Mwenyezi Mungu. Kisha akachora mistari kadhaa kuelekea kulia na kushoto, na akasema: Hizi ni njia ambazo Shet'ani anawaita watu kuzifuata. Kisha akasoma Aya: Na kwa hakika hii ndiyo Njia yangu Iliyo Nyooka. Basi ifuateni, wala msifuate njia nyingine, zikakutengeni na Njia yake. Haya amekuusieni ili mpate kuchamngu.’” (Ahmed)

Kwa hivyo, njia pekee inayokubalika ya kumwabudu Mungu ni kulingana na njia ya manabii. Kwa hivyo, uvumbuzi katika mambo ya dini utachukuliwa na Mungu kuwa kati ya madhambi mbaya zaidi. Mtume Muhammad, iliripotiwa kuwa alisema,

“Mambo mabaya zaidi ni uvumbuzi katika dini, kwa maana kila uvumbuzi katika dini ulilaaniwa, unaopotosha na unaongoza kwenye moto wa Jahannamu.” (An-Nasa’i)

Uvumbuzi katika dini ni haramu na haikubaliki kwa Mungu. Mke wa mtume, Aa'ishah, aliripoti kuwa Mtume alisema:

“Atakaye ongeza kitu katika dini yetu, ambacho si cha dini, basi kitakataliwa.” (Saheeh Al-Bukhari)

Kimsingi, ni kutokana na ubunifu ndipo ujumbe wa manabii wa awali ulipotoshwa na dini nyingi za uongo zilizoko leo zimeibuka. Kanuni ya jumla ya kufuata ili kuepukana na uvumbuzi katika dini ni kwamba aina zote za ibada ni marufuku, isipokuwa zile ambazo zimeagizwa hasa na Mungu na kuletewa kwa binadamu na mitume wa kweli wa Mungu.

Viumbe Bora Zaidi

Wale wanao mwamini Mungu Mmoja wa pekee, bila washiriki wala watoto, na wakatenda mema [kulingana na masharti yaliyotajwa hapo juu] huwa taji ya viumbe. Yaani, ingawa binadamu si kiumbe mkubwa zaidi kati ya viumbe wa Mungu, ana uwezo wa kuwa bora wa uumbaji Wake. Katika ufunuo wa mwisho, Mungu anasema ukweli huu kama ifuatavyo:

“Hakika walio amini na wakatenda mema ni bora wa uumbaji.” (Kurani 98:7)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.