Malaika (sehemu ya 1 kati ya 3): Wameumbwa kumuabudu na kumtii Mungu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+
  • Na Aisha Stacey (© 2009 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 11 Mar 2024
  • Ilichapishwa: 4
  • Imetazamwa: 6,223
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Angels_(part_1_of_3)_001.jpgWaislamu wanaamini uwepo wa malaika. Katika Uislamu kuna nguzo sita za imani; Kumuamini Mungu, Mmoja Pekee, Muumba na Mtunzaji wa yote yaliyopo, kuwaamini malaika Wake, vitabu vyake, wajumbe wake, Siku ya Mwisho na nguvu ya mungu.

Malaika ni sehemu ya ulimwengu wa ghaibu, lakini Waislamu wanaamini uwepo wao kwa uhakika kwa sababu Mungu na mjumbe Wake, Muhammad, wametupatia taarifa kuhusu wao. Malaika wameumbwana Mungu kwaajili ya kumuabudu na kumtii Yeye..

“Malaika wakali, wenye nguvu, hawamuasi Mwenyezi Mungu kwa anayo waamrisha, na wanatenda wanayo amrishwa. ” (Kurani 66:6)

Mungu aliumba malaika kutokana na nuru. Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alisema, “Malaika wameubwa kutokana na nuru,”[1]Hatuna maarifa ya kuwa lini malaika waliumbwa, Ila, tunajua kwamba ilikuwa kabla ya kuumbwa kwa wanadamu. Kurani inaelezea kuwa Mungu aliwaambia malaika nia yake ya kutaka kuumba msimamizi duniani. (2:30)

Waislamu wanajua kuwa malaika ni uumbaji mzuri. Ndani ya Kurani 53:6 Mungu anawaelezea malaika kama dhoo mirrah, neno hili la Kiarabu ambalo wasomi mashuhuru wa Kiislam[2] wanalielezea kuwa, refu na nzuri katika muonekano. Kurani (12:31) pia imemuelezea Mtume joseph kuwa mzuri,kama malaika mwenye kuheshimiwa

Malaika wana mabawa, na wanaweza kuwa kubwa sana. Hakuna chochote katika Kurani, au tamaduni za Mtume Muhammad ambazo zinaonyesha kuwa malaika ni watoto wenye mabawa au wana aina yoyote ya jinsia.[3] lakini tunajua, kuwa malaika wana mabawa na wengine ni wakubwa sana. Kutoka katika tamasuni za Mtume Muhammad tunajua kuwa ukubwa wa malaika Jibrili unajaza “nafasi ya katikakti ya mbingu na ardhi”[4] na ana mbawa mia sita[5].

“...aliye wafanya Malaika kuwa wajumbe wenye mbawa, mbili-mbili, na tatu- tatu, na nne-nne.....” (Kurani 35:1)

Kuna utofauti pia katika vyeo vya malaika. Malaika ambao walikuwa kwenye vita vya kwanza, Vita vya Badr, wanajulikana kuwa malaika "bora".

“Malaika Jibrili alikuja kwa Mtume na kuuliza, ‘unawakadiliaje baina ya watu waliokuwepo Badr?’ Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, akajibu, ‘Walikuwa Waislam bora,’ au kitu kilicho sawa. Kisha Jibrili akasema: ‘Pia kwa malaika waliokuwepo Badr.’”[6]

Waislamu wanaamini kuwa malaika hawana haja ya kula au kunywa. Uwepo wao ni kumtukuza Mungu na kurudia maneno, hakuna mungu ila Mungu. (Kurani 21:20).

“. . .walioko kwa Mola wako Mlezi wanamtakasa Yeye usiku na mchana, na wao hawachoki.” (Kurani 41:38)

Habari ya Mtume Abraham katika Kurani pia inaonyesha kuwa malaika hawana haja ya chakula. Malaika, kwa mfano wa wanaume, walipomtembelea Mtume Abraham kumpa habari njema ya kuzaliwa kwa mtoto wa kiume, aliwapa ndama kwa heshima yao. Walikataa kula na akaogopa, ndipo walipo jitambulisha kama malaika. (Kurani 51:26-28)

Kuna malaika wengi, lakini Mungu tu ndiye anayejua idadi kamili. Wakati wa kupaa mbinguni, Mtume Muhammad alitembelea Nyumba ya Ibada inayojulikana kama 'nyumba inayotembelewa sana', au, kwa Kiarabu al Bayt al-Mamoor, ya mbinguni inayofanana na Kaaba.[7]

Kisha nikapelekwa hadi kwenye "Nyumba inayotembelewa mara nyingi": kila siku malaika elfu sabini huitembelea na kuondoka, hawarudi tena,(kundi) lingine linakuja baada yao.”[8]

Mtume Muhammad pia ametufahamisha kuwa Siku ya Kiyama, Moto utaletwa na kuonyeshwa kwa watu.Amesema, “Moto utaletwa siku hiyo kwa njia ya kamba elfu sabini, ambayo kila moja itavutwa na malaika elfu sabini.”[9]

Malaika wana nguvu kubwa. Wana uwezo wa kuchukua aina tofauti ya umbo. Walionekana mbele ya Mtume Abraham na Nabii Loti kama wanaume. Malaika Jibrili alimtokea Mariamu mama wa Yesu akiwa mwanadamu, (Kurani 19:17) na alionekana mbele ya Mtume Muhammad kama mwanadamu, ambaye nguo zake zilikuwa nyeupe sana, na nywele zake zilikuwa nyeusi sana.[10]

Malaika ni wakakamavu. Malaika wanne hubeba kiti cha enzi cha Mungu, na Siku ya Kiyama, idadi yao itaongezeka hadi wanane. Miongoni mwa tamaduni ya Mtume Muhammad inaelezea mmoja wa malaika waliobeba kiti cha enzi cha Mungu. “Umbali kati ya masikio yake na mabega yake ni sawa na safari ya miaka mia saba.”[11]

Malaika hufanya wajibu na majukumu mbali mbali. Wengine wanahusika na mambo ya ulimwengu. Wengine wanahusika na bahari, au milima au upepo. Kipindi kimoja, baada ya kutembelea mji wa Ta’if, mji ulio karibu na Makka, Mtume Muhammad alipigwa mawe. Malaika Jibrili na malaika wa milima walimtembelea.

Malaika wa milima waliomba kuwaharibu watu wakaidi kwa kuwazika chini ya kifusi cha milima miwili iliyo karibu. Mtume Muhammad alikataa ombi hilo kwa sababu aliamini kwamba ikiwa wangepata nafasi ya kutulia na kuutazama Uislam, wangeukubali muunganiko huo na kumpenda Mungu.[12]

Malaika huchukua maagizo ya Mungu bila shaka au kusita. Kila malaika ana jukumu au kazi. Malaika wengine huwalinda na kuwaongoza wanadamu, wengine ni wajumbe. Katika sehemu ya pili tutaangalia majukumu haya na kujifunza majina ya malaika wengine ambao huyafanya.



Rejeleo la maelezo:

[1] Saheeh Muslim.

[2] Ibn Abbas & Qutadah.

[3] Matumizi ya neno Yeye ni kwa matumizi ya urahisi wa kisarufi na kwa njia yoyote haimaanishi kuwa malaika ni wanaume.

[4] Saheeh Muslim

[5] Musnad ya Imam Ahmad.

[6] Saheeh Al-Bukhari

[7] Jengo lenye mchemraba, katikati ya Masjid Takatifu, katika jiji la Makka, Saudi Arabia.

[8] Saheeh Al-Bukhari

[9] Saheeh Muslim

[10] Ibid

[11] Sunan Abu Dawood

[12] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim

Mbaya Nzuri zaidi

Malaika (sehemu ya 2 kati ya 3): Uwezo wa Mungu na nguvu juu ya malaika

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+
  • Na Aisha Stacey (© 2009 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 2
  • Imetazamwa: 4,548
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Angels_(part_2_of_3)_001.jpgMalaika ni viumbe walioumbwa na Mungu, kutokana na nuru. Hawana uwezo wa kutokumtii Mungu na hutekeleza majukumu waliyoamriwa bila shaka au kusita. Waislamu hupata uwelewa wa malaika kutoka kwenye Kurani na mila zilizothibitishwa za Mtume Muhammad. Katika sehemu ya kwanza tuligundua kuwa malaika ni viumbe wazuri wenye mabawa, ambao huwa kulingana na ukubwa mbali mbali na kwa idhini ya Mungu, wanaweza kubadilisha maumbo yao. Malaika wana majina na majukumu wanayotakiwa kutekelezwa.

Jina linalojulikana zaidi kwa Waislamu na wasio Waislamu ni Jibrili. Malaika Jibrili anatajwa katika jamii zote za Kiyahudi na Kikristo kama malaika mkuu na mjumbe wa Mungu, na yeye[1] anashikilia hadhi kubwa katika dini zote tatu zinazoamini mungu mmoja.

“ Kwamba hakika hii ni kauli (ya Kurani imeletwa na) Mjumbe Mtukufu,(Gabriel), kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa Mtume Muhammad. Mwenye nguvu na cheo kwa (Mungu) Mwenye Enzi,. Anayetiiwa (na malaika), na muaminifu. ” (Kurani 81:19-21)

Jibrili ameleta maneno ya Mungu – Kurani – kwa Mtume Muhammad.

“... Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Kurani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini. ”. (Kurani 2:97)

Michael (Mikaeel) ndiye malaika anayehusika na mvua na Israfeel ndiye malaika ambaye atapiga tarumbeta Siku ya hukumu. Malaika hawa watatu wapo katika safu ya malaika wakubwa kwa sababu ya umuhimu mkubwa wa majukumu yao. Kila moja ya majukumu yao hushughulika na hali ya maisha. Malaika Gabrieli alileta Kurani kutoka kwa Mungu kwenda kwa Nabii Muhammad, na Kurani inalisha moyo na roho. Malaika Michael anahusika na mvua, na inalisha dunia na pia kusafisha miili yetu, Malaika Israfeel anahusika na kupiga tarumbeta na inaashiria mwanzo wa maisha ya milele, iwe Peponi au Jehanamu.

Pindi Mtume Muhammad alipoamka usiku kuomba angeanza maombi yake kwa maneno, “Ee Mungu, Mola wa Jibreeli, Mikaeel na Israfeel, Muumba wa mbingu na ardhi, Mjuzi wa mambo ya yaliyojificha na yanayoonekana. Wewe ndiye Jaji wa mambo ambayo watumwa wako wanatofautiana. Niongoze kwa hoja za Ukweli kwa idhini Yako, kwa maana Wewe humwongoza yule Umtakaye kwenye Njia Iliyo Nyooka.”[2]

Tunajua pia majina ya malaika wengine kadhaa. "Malik, ndiye malaika anayejulikana kama mlinzi wa lango la motoni. "Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako!’. . .” (Kurani 43:77) Munkar na Nakeer ni malaika wanaohusika na kuhoji watu katika makaburi yao. Tunajua majina haya na tunaelewa kuwa tutaulizwa na malaika kaburini kama inavyotajwa katika mila ya Mtume Muhammad.

“Wakati marehemu anazikwa, wanakuja malaika wawili wenye rangi ya bluu-nyeusi, mmoja wao anaitwa Munkar na mwingine Nakeer. Wanamuuliza, "Ulikuwa unasema nini juu ya mtu huyu?" Na anasema kile alichokuwa akisema: "Yeye ni mtumwa na Mjumbe wa Mungu. Nashuhudia kwamba hakuna mungu ila Mungu na kwamba Muhammad ndiye mtumwa na Mjumbe wa Mungu. Wanasema, ‘Tulijua kabla ya hapo kuwa ulikuwa ukisema haya.’ Kisha kaburi lake litapanuliwa kwake kwa ukubwa wa dhiraa sabini na dhiraa sabini na atamulikwa. Halafu wanamwambia, ‘Lala.’ Anasema, ‘Rudi kwa familia yangu uwaambie.’ Wanamwambia, ‘Lala kama bwana harusi ambaye hakuna mtu atakayemuamsha isipokuwa mpendwa wake,’ mpaka Mungu atakapo mwinua....[3]

Katika Kurani tunapata hadithi ya malaika wawili walioitwa Haroot na Maroot, ambao walitumwa Babeli kuwafundisha watu uchawi. Matumizi ya uchawi hayaruhusiwi katika Uislamu lakini malaika hawa walitumwa kama mtihani kwa watu. Kabla ya kufunua au kufundisha uchawi Haroot na Maroot waliwaonya wazi wakazi wa Babeli kwamba walitumwa kama jaribio, na kwamba wanunuzi wa uchawi hawatakuwa na sehemu yoyote katika maisha ya baadaye, yaani wataenda kuzimu.(Kurani 2:102)

Ingawa wakati mwingine hufikiriwa kuwa Malaika wa Kifo anaitwa Azraeel, hakuna chochote katika Kurani au mila halisi ya Nabii Muhammad inayoonyesha hili. Hatujui jina la Malaika wa Kifo lakini tunajua wajibu wake na kwamba ana wasaidizi.

“Sema: Atakufisheni Malaika wa mauti aliye wakilishwa juu yenu; kisha mtarejeshwa kwa Mola wenu Mlezi.” (Kurani 32:11)

mpaka mmoja wenu yakimjia mauti wajumbe wetu humfisha, nao hawafanyi taksiri.Kisha watarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, Mola wao wa Haki. ” (Kurani 6:61-62)

Kuna kundi la Malaika wanaosafiri ulimwenguni kote, wakitafuta watu wanaomkumbuka Mungu. Kutoka kwenye mila ya Mtume Muhammad tunajua kuwa, Mungu ana malaika ambao hutembea katika barabara kuu kutafuta watu wa ukumbusho. Wanapopata watu wanaomkumbuka Mungu, wanaitatana , "Njoo kwa kile unachokuwa na njaa nacho na kuwafunika kwa mabawa yao, wakinyoosha hata mbingu ya chini kabisa. Basi Mola wao akauliza, na anajua zaidi yao, "Je! Watumwa wangu wanasema nini?" Wanasema: "Wanakutukuza, wanakutukuza, wanakuhimidi na kukusifu." Anauliza, "Je! Wameniona mimi?" Wanasema, "Hapana, na Mungu, hawajakuona." Anauliza, "Je! Ingekuwaje wakiniona?" Wanasema, "Wangekuwa wenye bidii zaidi na kujitolea katika sifa na ibada yao." Anauliza, "Wananiomba nini?" Wanasema, "Wanakuomba Pepo." Anauliza, "Na wameiona?" Wanasema, "Hapana, Mungu, Ee Mola, hawajaiona." Anauliza, "Na itakuwaje ikiwa wangeiona?" Wanasema: "Wangekuwa na hamu kubwa zaidi na wangekuomba kwa bidii zaidi." Anauliza, "Na wanaomba ulinzi Wangu kutokana na nini?" Wanasema, "Kutoka kwa Moto wa Jehanamu." Anauliza, "Je! Wameiona?" Wanasema, "Hapana, na Mungu, hawajaiona." Anauliza, "Na itakuwaje ikiwa wangeiona?" Wanasema: "Wangeogopa zaidi na wanahangaika kuukimbia." Mungu anasema: "Ninyi ni mashahidi Wangu kwamba nimewasamehe." Mmoja wa malaika anasema: "flani na flani siyo mmoja wao; alikuja (kwenye mkutano huo) kwa sababu zingine. ” Mwenyezi Mungu anasema, "Wote waliokuwa kwenye mkusanyiko huo, na mmoja wao hataondolewa (kwenye msamaha).”[4]

Waislamu wanaamini kuwa malaika wana majukumu maalum ya kufanya yanayowahusu wanadamu. Wanawalinda na kuwahifadhi, na malaika wawili wanaandika matendo mema na mabaya. Wanashuhudia sala na moja inawajibika hata kwa watoto waliomo ndani ya tumbo. Katika sehemu ya tatu tutaingia kwa undani zaidi na kuelezea ushirika kati ya malaika na wanadamu.



Rejeleo la maelezo:

[1] Matumizi ya neno yeye ni kwasababu ya urahisi wa kisarufi na haimaanishi kuwa malaika ni wanaume.

[2] Saheeh Muslim

[3] Sunan kwenye Tirmidhi. Abu Isa amesema:ni ghareeb hasan hadeeth. imehukumiwa na hasan ndani ya Saheeh al-Jaami’, nambari. 724.

[4] Saheeh Al-Bukhari

Mbaya Nzuri zaidi

Malaika (sehemu ya 3 kati ya 3): Ulinzi wa Malaika

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Muunganisho kati ya malaika na wanadamu.

  • Na Aisha Stacey (© 2009 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 5
  • Imetazamwa: 4,022
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Angels_(part_3_of_3)_001.jpgWaislamu wanaamini kuwa malaika hushiriki katika maisha ya wanadamu. Hii huanza mwanzo wa mimba na inaendelea hadi wakati wa kifo. Malaika na wanadamu wana maingiliano katika maisha ya baadaye. Malaika huingiza watu Peponi na hulinda malango ya Jehanamu. Kuamini malaika ni moja wapo ya misingi ya imani ya Uislamu.

Kutoka kwenye mila ya Nabii Muhammad, tunaelewa kuwa miezi michache baada ya kutunga mimba roho hupuliziwa ndani kwa idhini ya Mungu. Malaika kisha anaandika jibu la maswali manne katika kitabu cha matendo cha mwanadamu huyu. atakuwa wa kiume au wa kike? Je! Mtu huyu atakuwa na furaha au huzuni? Je! Maisha yake yatakuwa ya muda gani, na mtu huyu atafanya matendo mema au mabaya?[1]

Kuna malaika wanaohusika na kulinda watu katika maisha yao yote.

“Kila mtu analo kundi la malaika mbele yake na nyuma yake linamlinda kwa amri ya Mwenyezi Mungu.” (Kurani 13:11)

Kila mtu amepewa malaika wawili wanaotunza. Malaika hawa ni waandishi wa heshima na wajibu wao ni kuandika matendo mema na mabaya.

“. . . Na hukupelekeeni waangalizi, mpaka mmoja wenu yakimjia mauti . . .” (Kurani 6:61)

“Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong'ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika.” (Kurani 43:80)

“Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni. Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari. ” (Kurani 50:17-18)

“Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,Waandishi wenye hishima,” (Kurani 82:10-11)

Malaika wananakili kwa heshima lakini kwa umakini. Hakuna hata neno moja linaloachwa bila kunakiliwa. Ila, kama kawaida, rehema ya Mungu ni dhahiri. Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alielezea kwamba Mungu ameelezea na kutoa maelezo juu ya mbinu ya kunakili matendo mema na mabaya. “Ikiwa Yeyote atakusudia kufanya tendo jema, lakini hakulifanya, huandikwa kwake kama ametenda tendo hilo jema. Ikiwa kweli amelitenda tendo hilo jema basi huandikwa kama ametenda mema kumi, au hadi mara mia saba au zaidi. Ikiwa mtu alikusudia kufanya tendo baya, lakini hakulifanya, huandikwa kama ametenda tendo jema, ila ikiwa atakujakubadilisha mawazo na kulifanya, litaandikwa kama ametenda tendo baya moja.”[2]

Msomi mashuhuri wa Uislam Ibn Kathir alitoa maoni yake juu ya Kurani 13: 10-11 kwa kusema, "Kila mtu ana malaika ambao huchukua zamu kumlinda usiku na mchana, ambao humkinga na maovu na ajali, kama vile malaika wengine wanavyopokezana kunakili. matendo yake, mema na mabaya, usiku na mchana. ”

“Malaika wawili, kulia na kushoto, wanaandika matendo yake. Yule wa kulia anaandika matendo mema na yule wa kushoto anaandika matendo maovu. Malaika wengine wawili wanamuongoza na kumlinda, mmoja kutoka nyuma, na mmoja mbele. Kwa hivyo kuna malaika wanne mchana na wengine wanne usiku. ”

Mbali na malaika wanne kuwa kila siku na kila mwanadamu, wanaomlinda na kunakili, malaika wengine wanaendelea kuwatembelea wanadamu. Katika mila yake, Mtume Muhammad anawakumbusha wafuasi wake kuwa wanazuru kila wakati na malaika. Alisema, “Malaika wanakujia kwa mfululizo usiku na mchana na wote hukusanyika wakati wa sala ya Fajr (mapema asubuhi) na Asr (alasiri). Wale ambao wamepita usiku pamoja nawe (au walikaa nawe) hupanda (kwenda Mbinguni) na Mungu anawauliza, ingawa anajua kila kitu juu yako, "Je! Umewaacha watumwa wangu katika hali gani?" Malaika walijibu: "Tulipowaacha walikuwa wakisali na tulipowafikia, walikuwa wakisali.”[3]Wanakusanyika kushuhudia sala na kusikiliza mistari ya Kurani inavyosomwa.

Kwa hivyo inaweza kueleweka kuwa malaika wanahusika sana na maisha ya wanadamu na mwingiliano huu hauishii wakati malaika wa kifo anaondoa roho, na haimaliziki baada ya malaika kumuuliza mtu aliyekufa katika kaburi lake[4]. Malaika ni walinzi wa lango la Peponi.

“Na walio mcha Mola wao Mlezi wataongozwa kuendea Peponi kwa makundi, mpaka watakapo fikilia, nayo milango yake imekwisha funguliwa. Walinzi wake watawaambia: Salaam Alaikum, Amani iwe juu yenu! Mmet'ahirika. Basi ingieni humu mkae milele.” (Kurani 39:73)

“Na Malaika wanawaingilia katika kila mlango. (Wakiwaambia) Assalamu Alaikum! Amani iwe juu yenu, kwa sababu ya mlivyo subiri! Basi ni mema mno malipo ya Nyumba ya Akhera. ” (Kurani 13:23-24)

Malaika pia ni walinzi wa lango la Jehanamu.

“Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar? Haubakishi wala hausazi.Unababua ngozi iwe nyeusi. Unasimamiwa na (Malaika walinzi wa moto) kumi na tisa. Na hatukujaalia walinzi wa Moto ila Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwa ni mtihani kwa waliokufuru, ili wapate kuwa na yakini wale waliopewa Kitabu, na wazidi Imani wale walioamini, ” (Kurani 74:27-31)

Mungu aliwaumba malaika kutokana na nuru. Hawawezi kuacha kumtii Mungu na hufuata maagizo yake bila shaka au kusita. Malaika wanamwabudu Mungu. Ndiyo asili yao. Viumbe hawa wazuri wana jukumu muhimu katika maisha ya wanadamu. wanawaongoza na kuwalinda, kunakili na kuripoti, na kukusanyika kwa wanadamu wanaomkumbuka Mungu.



Rejeleo la maelezo:

[1] Saheeh Al-Bukhari

[2] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim

[3] Ibid.

[4] Angalia sehemu ya 2

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.