Jinsi ya Kuishi Ukipata Ugonjwa (sehemu ya 2 kati ya 2): Huruma ya Mungu haina mipaka

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Hatua za kuchukua unapopata ugonjwa au jeraha.

  • Na Aisha Stacey (© 2009 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 03 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,971 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

How_to_Behave_When_Struck_by_Illness_(part_2_of_2)_001.jpgKatika Sehemu ya kwanza tulijadili kustahamili majaribio na mitihani kwa uvumilivu na kuelewa kwamba hakuna kinachotokea bila idhini ya Mungu.

“Na ziko pamoja Naye funguo za Ghaib (yote yaliyofichika), hakuna anayewajua ila Yeye. Naye anajua viliomo ndani (au juu ya) ardhi na baharini. jani halianguki ila kwa elimu yake. ” (Kurani 6:59)

Wakati ugonjwa au jeraha linapotokea sababu zinaweza kuwa hazionekani, au hata kuwa zaidi ya ufahamu wetu. Walakini Mungu anataka mema tu kwa wanadamu. Kwa hivyo tunafaa kuwa na hakika kwamba kuna hekima kubwa nyuma ya shida na kwamba inatupatia fursa ya kukuza uhusiano wa karibu na Mungu. Kama wanadamu kwa kweli tuna uhuru wa kuchagua na tuko huru kuchagua njia yetu ya kutenda katika hali yoyote ile, lakini tendo bora ni uvumilivu na kuwa na subra.

Nabii Muhammad rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, alituarifu kwamba tutajaribiwa kulingana na kiwango chetu cha imani na matokeo mazuri ya majaribiyo haya itakuwa utakaso wa dhambi. Alisema, mtu atajaribiwa kulingana na kiwango cha kujitolea kwake kwa dini, na majaribio yataendelea kumuathiri mtumwa wa Mungu mpaka atakapobaki kutembea duniani bila mzigo wowote wa dhambi.[1]

Wakati ugonjwa au jeraha itatupata ni kawaida ya mja kuogopa. Wakati mwingine tunaweza hata kuhisi chuki, tukishangaa kwa nini Mungu amejali hii itendeke. Tunahoji na kulalamika lakini kwa kweli hii haitumiki isipokuwa kuzidisha huzuni au mateso yetu. Mungu kwa hekima na huruma yake isiyo na mwisho ametupa miongozo wazi kuhusu jinsi ya kuishi tunapopigwa na ugonjwa au jeraha. Ikiwa tunafuata miongozo hii inawezekana kuvumilia shida kwa urahisi na hata kushukuru. Ugonjwa ukikupata au kuumia muumini huweka tumaini lake kwa Mungu, anaonyesha shukrani kwa hali yoyote ambayo Mungu amemjalia na kutafuta msaada wa matibabu.

Matibabu inaruhusiwa katika Uislamu na kutafuta matibabu haukatazi wazo la kuweka imani kwa Mungu. Nabii Muhammad alitubainisha hii aliposema, "Hakuna ugonjwa unaoasibu ila kwamba una tiba."[2] Muumini anaweza kwenda kwa daktari kwa matibabu ya magonjwa na majeraha. Anaweza kwenda kutafuta uchunguzi na tiba ya magonjwa ya akili au hali ya kihemko. Isitoshe kuna kanuni kadhaa kwamba tiba haiwezi kutafutwa katika kitu ambacho ni kimeharimishwa kama vile pombe. Mwishowe Mungu hawekei uponyaji katika kitu ambacho amekiharamisha.

Hairuhusiwi kutafuta tiba kutoka kwa waganga, wachawi na watapeli wa aina yoyote. Watu hawa wanadai kuwa wana ujuzi wa mambo yasiyoonekana ambayo hayawezekani ilhali wanajaribu tu kuwanyang'anya watu na kuwapotosha kutoka kwa Mungu wa Pekee na wa Kweli. Mungu pia amekataza matumizi ya hirizi kwa minajili ya ugonjwa na jeraha. Nguvu zote na uwezo zinatoka kwa Mungu peke yake. Kumwita mtu au kitu kingine isipokuwa Mungu kutuponya au kutuweka salama ni dhambi kubwa sana.

Unapotafuta matibabu katika ulimwengu huu ni muhimu pia kutafuta tiba kupitia tiba za kiroho. Jambo la kwanza kufanya ni kufikiria vyema juu ya Mungu, kuthibitisha imani yako kwake, na kutafakari majina na sifa zake. Yeye ni Mwingi wa Rehema, mwenye mapenzi ya dhati kwa waja wake na Mwenye hikima. Tunashauriwa kumwita kwa majina ambayo yanafaa zaidi kwa mahitaji yetu.

"Na (yote) Majina Mazuri zaidi ni ya Mungu kwa hivyo mwiteni kwake." (Kurani 7: 180)

Mungu hajatuacha kwenye majaribio na shida za ulimwengu huu ametupatia mwongozo na silaha zenye nguvu zaidi dhidi ya mateso na dhiki na hiyo ni Kurani, maneno ya ukumbusho na dua, na sala.[3] Katika karne ya 21 tumeanza kutegemea msaada wa matibabu badala ya tiba halisi za kiroho, hata hivyo kutumia hizo mbili pamoja mara nyingi unaweza kuwa mzuri. Wakati mwingine magonjwa yanaendelea wakati mwingine majeraha huwa sugu, lakini wakati mwingine afya mbaya inaweza kuleta ufahamu mzuri wa kiroho.

Ni mara ngapi tumesikia watu wenye magonjwa mabaya au walemavu wa kutisha wakimshukuru Mungu kwa hali zao, au kuongelelea jinsi maumivu na mateso yalivyoleta baraka na wema maishani mwao? Tukihisi upweke na huzuni Mungu ndiye mkono wetu pekee wa kutushikilia. Wakati maumivu na mateso yanapokuwa hayavumiliki, wakati hakuna chochote kilichobaki isipokuwa hofu na taabu hapo ndipo tunapofikiria jambo moja ambalo linaweza kuleta ukombozi na si lingine bali – Mungu. Uaminifu kamili utegemevu kwa mapenzi ya Mungu huleta furaha na uhuru ambao unajulikana kama utamu wa imani. Ni amani na utulivu na inamuwezesha mtu kukubali hali zote zinazoletwa na ulimwengu, nzuri, mbaya, chungu, dhiki na furaha.

Hatimaye ni muhimu kuelewa kwamba magonjwa na majeraha inaweza kuwa njia ya Mungu ya kututsafisha. Wanadamu kamwe si wakamilifu tunafanya makosa, tunafanya matendo mabaya, na hata kwa makusudi tunakaidi amri za Mungu.

"Na misiba inayo kusibuni ni kwa sababu ya vitendo vya mikono yenu. Naye anasamehe mengi." (Kurani 42:30)

Rehema ya Mungu haipaswi kamwe kudharauliwa. Anatuhimiza tutafute msamaha kwake. Nabii Mohammad alitukumbusha kwamba Mungu anatungojea tumgeukie Yeye. Katika sehemu ya mwisho ya usiku, wakati giza limetanda sana nchi nzima Mungu hushuka mpaka mbingu ya chini kabisa na kuwauliza watumwa Wake. "Ni nani atakayeomba niijibu? Ni nani anayeuliza kitu kwangu ili nimpe? Ni nani anayeomba msamaha kwangu ili nimsamehe?”[4]

Mara nyingi bahati mbaya, maumivu, na mateso huja kwa sababu ya matendo yetu wenyewe. Tunachagua kutenda dhambi lakini Mungu hutusafisha kupitia kupoteza mali, afya au vitu tunavyopenda. Wakati mwingine mateso katika ulimwengu huu inamaanisha kuwa hatutateseka kwa umilele, wakati mwingine maumivu na dhiki yote inamaanisha kwamba tutapata kituo cha juu peponi.

Mungu ndiye anajua kuna hekima gani kwanini mambo mazuri hufanyika kwa watu wabaya au kwanini mambo mabaya huwatokea watu wema. Kwa ujumla chochote kinachotufanya tumgeukie Mungu ni nzuri. Wakati wa shida watu hukimbilia kwa Mungu, wakati wa faraja mara nyingi tunasahau kutoka kwa faraja hiyo. Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kutoa na ni Mkarimu zaidi. Mungu anataka kutupatia uzima wa milele na ikiwa maumivu na mateso yanaweza kuhakikisha peponi basi afya mbaya na majeraha ni baraka. Nabii Muhammad alisema, "Ikiwa Mungu anataka kumtendea mema mtu, Yeye humsumbua na majaribu.”[5]

Ugonjwa unapotokea njia bora ni kumshukuru Mungu, jaribu kuwa karibu naye na kutafuta msaada wa matibabu na ukumbuke baraka ambazo ametupatia.



Rejeleo la maelezo:

[1] Ibn Majah.

[2] Bukhari

[3] Kwa ufafanuzi kamili wa nguvu ya uponyaji ya Kurani tafadhali angalia nakala ya Afya katika Uislam Sehemu ya 2.

[4] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim, Malik, At Tirmidhi, Abu Dawud

[5] Saheeh Al-Bukhari.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.