Aisha Canlas,Mkatoliki wa Zamani, Ufilipino

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Safari yake kutoka Ufilipino hadi Saudi Arabia.

  • Na Aisha Canlas
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,510 (wastani wa kila siku: 2)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Jina langu ni Aisha Canlas. Kabla sijafika hapa Riyadh, Ufalme wa Saudi Arabia, nilikuwa Mkatoliki kwa sababu wazazi wangu pia ni Wakatoliki.

Tulikwenda makanisa mbalimbali ili kumwomba Mungu lakini kwa njia ya picha zilizotengenezwa na wanadamu. Wakati huo nilikuwa nikijiuliza kama huo ndio uso halisi wa Mungu? Inakuaje mtu yeyote angeweza kujua anavyokaa? Je! Wamemwona Yeye tayari?

Kuna sehemu moja huko Manila ambako kuna msikiti. Kila wakati ulipokuwa muda wa kusali na nikasikia Adhana, ningefunga macho yangu na kusikia amani na utulivu ingawa sikujua maana yake. Ilikuwa kama muziki kwa moyo wangu.

Hakuna mtu, hata mimi, aliyejua kwamba ningekuwa Muislamu hatimaye. Niliomba kazi nchini Saudi Arabia ili niwape familia yangu maisha bora zaidi.

Ili nijiandae na nisipate mshtuko wa kitamaduni, nilitafiti mambo ambayo yangeweza kunisaidia kuelewana vizuri na watu nikienda kuishi katika nchi za Mashariki ya Kati.

Nilitafiti kuhusu utamaduni, nchi hiyo kwa ujumla, lugha na bila shaka dini. Nilipata hamu kubwa ya kujua kuhusu Uislamu, hadi kwamba hata kabla sijachukua ndege kwenda huko nilisoma mambo kadhaa kuhusu dini hiyo.

Uongofu wangu haukufanyika kwa ghafla. Mara nyingi ninawauliza madaktari wangu kuhusu Uislamu. Kwa sababu katika mawazo yangu wataweza kunisaidia kuelewa zaidi kuhusu Uislamu kwa kuwa wameishi maisha yao yote Saudia.

Ilikuwa mnamo Januari 15, 2008 ndipo nilijifunza kuwa kuna Madrasa au 'Mafundisho ya Kiislamu' katika mahali pangu pa kazi. Hapo ndipo nilipoamua kuhudhuria masomo hayo. Nilihudhuria mara ya kwanza na rafiki yangu na mwenzangu, ambaye ni Muislamu tangu kuzaliwa kwake, mnamo tarehe 17 Januari 2008.

Macho yote yalikuwa juu yangu mwanzoni, kwa kuwa nilikuwa mpya darasani na nilikuwa Mkristo pekee aliyeketi kati yao. Nilisikiliza yale mwalimu wetu alikuwa anatuambia kuhusu Uislamu, Qur'ani na kuhusu Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, na kuhusu Mungu.

Kuanzia wakati huo, nilianza kuelewa vizuri Uislamu. Baada ya hapo niliomba ruhusa kutoka kwa Mama yangu ambaye yuko nchini Ufilipino aniruhusu nitoke kutoka Ukatoliki kwenda Uislamu.

Alhumdullillah (Mwenyezi Mungu ndiye wa kusifiwa), mama yangu hakupinga. (Baba yangu alikufa Novemba mwaka jana). Alisema kuwa alikuwa na hofu tu kwamba nitakapobadilisha dini nitawasahau. Nikasema kuwa Waislamu wana heshima kubwa kwa wazazi, hasa kwa Mama.

Ilikuwa Januari 24, 2008 nilipochukua Shahadah yangu mbele ya mwalimu wangu na wanafunzi wengine. Nilipokuwa nikisoma Shahada kulikuwa na joto lililotoka kwangu. Siwezi kueleza hisia hiyo.

Kitu pekee nilichojua baada ya kusoma Shahadah yangu ni kwamba moyo wangu ulihisi kana kwamba uliondolewa mzigo. Hatimaye nilipata amani ya ndani niliyokuwa nikitafuta katika maisha yangu yote. Kuwa katika Uislamu ni tofauti kabisa.

Niliulizwa na wenzangu wengine kwa nini niliamua kuingia katika Uislamu. Nilisema kuwa naamini kwamba hakuna mwingine wa kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu, na mmoja katika wajumbe wake ni Mtume Muhammad.

Baadhi ya wakristo walidhani kwamba nilisaliti dini na imani yangu. Hata hivyo, ndani ya moyoni mwangu najua kwamba si kweli. Alhumdulillah (Mwenyezi Mungu ndiye wa kusifiwa), pia nilienda Umrah. Nilienda Umrah Machi iliyopita, tarehe 5, 2008 na lilikuwa jambo la kukumbukwa daima na hisia ya kipekee.

Ni kana kwamba nimetengwa na matatizo yangu, wasiwasi wangu na mambo mabaya yote duniani. Nilifurahi sana na nilihisi kuwa ninaweza kukaa huko maisha yote nikimwomba Mungu na kumsifu kwa mambo yote ya ajabu aliyoyatendea wanadamu.

Sijawahi kujua kwamba nitaweza kuona Kabah katika maisha halisi. Nimeiona katika picha nilipokuwa mdogo lakini kuiona kikweli kulinijaza furaha; na shukrani zilijaza moyo wangu.

Ninahudhuria Madrasa (Mafundisho ya Kiislamu) mwisho wa wiki katika sehemu yangu ya kazi. Wakati unapopita, nimekuwa nikijifunza kuhusu Uislamu. Nahisi kila kitu kitatokea vizuri iwapo imani yangu kwa Mungu ni imara na inaendelea kuzidi.

Natumai na ninamwomba Mungu kwamba nitaweza kuwashawishi familia yangu waingie katika Uislamu pia. Nataka waokolewe na ghadhabu Siku ya Kiama.

Kwa maoni yangu, jambo bora zaidi ambalo Muislamu anaweza kufanya ni kuongoza maisha ya wema na kuwa mfano mzuri. Hilo linawafanya wasio Waislamu wawe na hamu ya kuijua dini hii na pia huwasaidia kutambua kwamba taswira mbaya waliyo nayo kuhusu Uislamu siyo sahihi.

Nilikuwa Mkristo mwenye imani imara sana ya kikristo ambaye aliolewa na Muislamu. Nilifunga ndoa naye kwa sababu ya tabia yake, kwa sababu sikumjua mtu yeyote Mkristo aliyeonyesha mafundisho ya Yesu kama huyu Muislamu alivyofanya.

Hata hivyo, niliamua kumthibitishia mume wangu kwamba alikuwa kwa njia mbaya na kwamba anapaswa kuwa Mkristo. Yote aliyoyafanya ni kuniuliza maswali makuu na ya kimsingi kuhusu imani yangu, kama vile “Yesu alifundisha wapi katika Biblia kwamba yeye ni Mungu?”

Nilipogundua kuwa hakuna mahali kama hiyo, nilianza kutafiti zaidi na zaidi. Baada ya utafiti mwingi, nilikasirika na kupoteza matumaini. Nilisoma tafsiri ya Kiingereza ya Qurani Tukufu (La kushangaza ni kuwa mchungaji wangu ndiye aliyenipa) ili niwe na mjadala bora na mume wangu.

Badala yake, nilipata maandishi ya Quran yanaambatana na mafundisho ya Biblia. Nilipata faraja katika dhana ya kuwepo kwa Mungu Mmoja. Shukrani ziwe kwa Mungu, sisi sasa ni familia ya Kiislamu.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.