Miujiza ya Muhammad (sehemu ya 1 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Asili ya miujiza iliyofanywa mikononi mwa manabii.

  • Na IslamReligion.com
  • Iliyochapishwa mnamo 27 Nov 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 8
  • Imetazamwa: 6,680
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Mbali na muujiza mkubwa zaidi aliopewa, Kurani Mtume Muhammad alifanya miujiza mingi ya halisi iliyoshuhudiwa na watu wa zama zake waliofikia mamia, na katika visa fulani maelfu.[1] Ripoti za miujiza zimetufikia kwa njia ya kuaminika na dhabiti ya uenezaji wa kifanisi katika historia ya ulimwengu. Ni kana kwamba miujiza ilifanywa mbele ya macho yetu. Njia ya upokezaji ndiyo inayotusadikisha kuwa Muhammad kwa hakika alifanya miujiza hii mikubwa kwa usaidizi wa kimungu na, hivyo, tunaweza kumwamini aliposema, ‘Mimi ni Mtume wa Mungu.’

Miujiza mikubwa ya Muhammad ilishuhudiwa na maelfu ya waumini na wenye kutilia shaka, kufuatia aya za Kurani zilifunuliwa zikitaja matukio ya ajabu. Kurani ilifanya baadhi ya miujiza kuwa ya milele kwa kuitia katika fahamu za waumini. Wapinzani wa zamani wangekaa kimya tu wakati aya hizi zilikaririwa. Lau miujiza hii isingetokea, wangechukua muda wa kuichafua na kumsingizia Muhammad. Lakini badala yake, kinyume cha matarajio kilifanyika. Waumini walikua na uhakika zaidi wa ukweli wa Muhammad na Kurani. Ukweli kwamba waumini walikua na nguvu zaidi katika imani yao na kunyamaza kwa wasioamini na kutokataa kutokea kwao ni kukiri kutoka kwa wote wawili kwamba miujiza ilifanyika sawa na Kurani inavyoelezea.

Katika sehemu hii tutazungumzia baadhi ya miujiza halisi aliyoifanya Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Miujiza inatokana na Nguvu ya Mungu

Muujiza ni mojawapo ya mambo ambayo yanaimarisha zaidi madai ya nabii wa Mungu. (nukta inahitajika) Miujiza haipaswi kuwa kiini pekee cha imani, kwani matukio ya kiungu yanaweza pia kutokea kwa kutumia uchawi na ushetani. Ukweli wa utume uko wazi na dhahiri katika ujumbe halisi unaoletwa, kwani Mungu ameweka uwezo, ingawa ni mdogo, kwa wanadamu kutambua ukweli kwa jinsi ulivyo, hasa katika suala la monotheazimu (imani kwamba kuna Mungu mmoja tu) Lakini ili kuimarisha zaidi hoja ya Utume, Mwenyezi Mungu alifanya miujiza mikononi mwa Mitume wake kuanzia Musa, Yesu hadi Muhammad. Kwa sababu hii, Mungu hakuleta miujiza kwa matakwa ya watu wa Makkah, lakini Mungu Mwenye Busara alimpa Muhammad miujiza Aliyotaka wakati aliouchagua:

“Na walisema: Hatutakuamini mpaka ututimbulie chemchem katika ardhi hii. Au uwe na kitalu cha mitende na mizabibu, na utupitishie mito kati yake ikimiminika. Au utuangushie mbingu vipande vipande kama ulivyo dai; au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika uso kwa uso Au uwe na nyumba ya dhahabu, au upae mbinguni. Wala hatutaamini kupaa kwako mpaka ututeremshie kitabu tukisome. Sema: Subhana Rabbi, Ametakasika Mola wangu Mlezi! Kwani mimi ni nani isipo kuwa ni mwanaadamu na Mtume?’’’ (Kurani 17:90-93)

Jibu lilikuwa:

“Na hapana kinacho tuzuia kupeleka miujiza ila ni kuwa watu wa zamani waliikanusha. Na tuliwapa Wathamudi ngamia jike kuwa ni Ishara iliyo dhaahiri, lakini walidhulumu kwaye. Nasi hatupeleki Ishara ila kwa ajili ya kuhadharisha.” (Kurani 17:59)

Walipotaka kwa nguvu, Mungu kwa hekima yake alijua kwamba hawataamini, kwa hiyo alikataa kuwaonyesha miujiza:

“Na waliapa kwa Mwenyezi Mungu kwa ukomo wa viapo vyao, kuwa ikiwafikia Ishara wataiamini. Sema: Ishara ziko kwa Mwenyezi Mungu. Na nyinyi hamjui kuwa zitapo kuja hawato amini. Nasi twazigeuza nyoyo zao na macho yao. Kama walivyo kuwa hawakuamini mara ya kwanza, tunawaacha katika maasi yao wakitangatanga.’” (Kurani 6:109-110)

Tunakusanya hapa baadhi ya miujiza halisi mikubwa iliyofanywa na Mtume Muhammad.



Rejeleo la maelezo:

[1] Miujiza hiyo imeongezeka zaidi hadi elfu . Tazama ‘Muqaddima SharhSaheeh Muslim’ cha al-Nawawi na ‘al-Madkhal’ cha al-Baihaqi.

Mbaya Nzuri zaidi

Miujiza ya Muhammad (sehemu ya 2 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kugawanywa kwa mwezi, na safari ya Mtume kwenda Yerusalemu na kupaa Mbinguni.

  • Na IslamReligion.com
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 1
  • Imetazamwa: 4,752
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kugawanywa kwa Mwezi

Moja ya nyakati ambapo Mungu alifanya miujiza kwa mkono wa Mtume ilikuwa wakati watu wa Makkah walitaka kuona muujiza kutoka kwa Muhammad ili kuthibitisha ukweli wake. Mungu aliugawanya mwezi katika vipande viwili tofauti na kisha ukaunganisha tena. Kurani iliandika tukio hilo:

“Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!” (Kurani 54:1)

Mtume Muhammad alikuwa akisoma aya hizi za Kurani katika makundi makubwa ya sala ya Ijumaa ya kila juma na sala za Idi mara mbili kwa mwaka.[1] Kama tukio hilo lisingetokea, Waislamu wenyewe wangeitilia shaka dini yao na wengi wangeiacha! Watu wa Makkah wangesema, ‘Haya, Nabii wenu ni mwongo, mwezi haukugawanyika, na hatujawahi kuuona ukigawanyika!’ Badala yake, Waumini walikua na nguvu zaidi katika imani yao na maelezo pekee ambayo watu wa Makkah wangeweza kujanayo ni, 'ulikuwa ni uchawi '

“Saa imekaribia, na mwezi umepasuka! Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.” (Kurani 54:1-3)

Kugawanywa kwa mwezi kunathibitishwa kupitia ushuhuda wa mashahidi uliyopitishwa kwa wasomiwengi wanaoaminika kiasi kwamba inakuwa haiwezekani kuwa ya uwongo (hadith mutawatir).[2]

Mtu mwenye shaka anaweza kuuliza, je, tuna ushahidi wowote huru wa kihistoria kupendekeza mwezi uliwahi kupasuliwa? Baada ya yote, watu ulimwenguni pote walipaswa kuona tukio hili la ajabu na kulirekodi.

Majibu ya swali hili ni mawili

Moja, watu ulimwenguni kote wasingeweza kuiona kama ingekuwa mchana, usiku wa manane, au asubuhi na mapema katika sehemu nyingi za ulimwengu. Jedwali lifuatalo litampa msomaji wazo la nyakati za dunia zinazolingana na saa 9:00 alasiri saa za Makka:

Nchi

Muda

Makka

9:00 pm

India

11:30 pm

Perth

2:00 am

Reykjavik

6:00 pm

Washington D.C.

2:00 pm

Rio de Janeiro

3:00 pm

Tokyo

3:00 am

Beijing

2:00 am

Pia, sio kawaida kwamba idadi kubwa ya watu katika nchi zilizo karibu wangekuwa wakitazama mwezi kwa wakati uleule. Hawakuwa na sababu. Hata kama mtu fulani aliuona, haimaanishi kwamba watu walimwamini na kuweka rekodi yake, wakati watu wengi wa wakati huo hawakuhifadhi historia yao wenyewe kwa maandishi.

Mbili, hakika tuna uthibitisho huru na wa kushangaza kabisa, wa kihistoria wa tukio kutoka kwa mfalme wa Kihindi wa wakati huo.

Kerala ni jimbo la India. Jimbo hilo lina urefu wa maili 360 (kilomita 580) kando ya Pwani ya Malabar upande wa kusini magharibi mwa rasi ya India.[3] Mfalme Chakrawati Farmas wa Malabar alikuwa mfalme wa Chera, Cheraman perumal wa Kodungallure. Imerekodiwa kuwa aliona mwezi ukigawanyika. Tukio hilo limeandikwa katika andiko lililohifadhiwa katika Maktaba ya Ofisi ya India, London, nambari ya kumbukumbu: Arabic, 2807, 152-173.[4] Kundi la wafanyabiashara Waislamu waliokuwa wakipita Malabar wakielekea Uchina walizungumza na mfalme kuhusu jinsi Mungu alivyomuunga mkono nabii wa Kiarabu kwa muujiza wa kugawanyika kwa mwezi. Yule mfalme alishtuka akasema kuwa ameiona kwa macho yake pia, akampa mwanawe msaidizi, na akaondoka kwenda Uarabuni kukutana na Mtume ana kwa ana. Mfalme wa Malabari alikutana na Mtume, akatoa shuhuda hizo mbili za imani, akajifunza misingi ya imani, lakini alifariki dunia akiwa njiani kurudi na akazikwa katika mji wa bandari wa Zafar, Yemen.[5]

Inasemekana kuwa kikosi hicho kiliongozwa na Mwislamu, Malik ibn Dinar, na kuendelea hadi Kodungallure, mji mkuu wa Chera, na kujenga msikiti wa kwanza, na wa zamani zaidi wa India, katika eneo hilo mnamo 629 BK ambao upo hadi leo.

The_Miracles_of_Muhammad_(part_2_of_3)_001.jpg

Picha ya kabla ya ukarabati wa Msikiti wa Cheraman Juma Masjid, msikiti mkongwe zaidi nchini India ulioanzia 629 BK. Picha kwa hisani ya www.islamicvoice.com.

Habari za kusilimu kwake zilifika Kerala ambapo watu waliukubali Uislamu. Watu wa Lakshadweep na Moplas (Mapillais) kutoka jimbo la Calicut la Kerala waliukubali uislam tangu siku hizo.

The_Miracles_of_Muhammad_(part_2_of_3)_002.jpg

Cheraman Juma Masjid, iliyopewa jina la Muislamu wa kwanza wa India aliyesilimu, Cheraman perumal Chakrawati Farmas, baada ya ukarabati. Picha kwa hisani ya www.indianholiday.com.

Kuonekana India na kukutana kwa mfalme wa India na Mtume Muhammad pia kunaripotiwa na vyanzo vya Kiislamu. Mwanahistoria mashuhuri wa Kiislamu, Ibn Kathir, anataja kugawanyika kwa mwezi kuliripotiwa katika sehemu za India.[6] Pia, vitabu vya Hadith vimeandika kuwasili kwa mfalme wa Kihindi na kukutana kwake na Mtume. Abu Sa’id al-Khudri, sahaba wa Mtume Muhammad, anasema:

“Mfalme wa Kihindi alimpa Mtume zawadi ya mtungi wa tangawizi. Maswahaba wakala kipande kwa kipande. nilitafuna pia.”[7]

Kwa hiyo mfalme alichukuliwa kama ‘sahaba’ – neno linalotumiwa kwa mtu ambaye alikutana na Mtume na akafa kama Muislam– jina lake limeandikwa katika vitabu vingi vya kumbukumbu za masahaba wa Mtume.[8]

Safari ya Usiku na Kupaa Mbinguni

Miezi michache kabla ya kuhama kutoka Makka kwenda Madina, Mungu alimchukua Muhammad kwa usiku mmoja kutoka Msikiti Mkuu wa Makka hadi Msikiti wa al-Aqsa huko Jerusalem, safari ya mwezi ya km 1230 kwa msafara. Kutoka Yerusalemu, alipaa hadi mbinguni, akipita mipaka ya ulimwengu katika uwepo wa Mwenyezi Mungu, kukutana na Mungu, na kushuhudia Ishara Kuu (al-Ayat ul-Kubra). Ukweli wake ulionekana wazi kwa njia mbili. Moja, ‘Mtume alieleza misafara aliyoipita njiani kuelekea nyumbani na akasema mahali ilipo na kuhusu lini wangetarajiwa kufika Makka; na kila mmoja akafika kama ilivyotabiriwa, na maelezo yalikuwa kama alivyoeleza.’[9] Pili, hakuwahi kujulikana kuwa aliwahi kufika Yerusalemu, lakini aliuelezea Msikiti wa al-Aqsa kwa wenye shaka kama shahidi wa kuona.

The_Miracles_of_Muhammad_(part_2_of_3)_003.jpg

Safari ya ajabu imetajwa katika Kurani:

“SUBHANA, Ametakasika aliye mchukua mja wake usiku mmoja kutoka Msikiti Mtukufu mpaka Msikiti wa Mbali, ambao tumevibariki vilivyo uzunguka, ili tumuonyeshe baadhi ya Ishara zetu. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia na Mwenye kuona.” (Kurani 17:1)

“Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona? Na akamwona mara nyingine, Penye Mkunazi wa mwisho. Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa. Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.” (Kurani 53:12-18)

Tukio hilo pia linathibitishwa kupitia ushuhuda wa mashahidi wa kuona uliopitishwa katika zama kupitia mlolongo wa uhakika wa wanazuoni(hadith mutawatir).[10]

The_Miracles_of_Muhammad_(part_2_of_3)_004.jpg

Mlango wa Msikiti wa Al-Aqsa ambapo Muhammad alipaa mbinguni. Picha kwa hisani ya Thekra A. Sabri.



Vielezi-chini:

[1] Saheeh Muslim.

[2] AngaliaNadhm al-Mutanathira min al-Hadith al-Mutawatir,’ na al-Kattani p. 215.

[3] “Kerala.” Encyclopædia Britannica kutoka Encyclopædia Britannica Premium Service. (http://www.britannica.com/eb/article-9111226)

[4]Imenukuliwa katika kitabu "Muhammad Rasulullah," na Muhammad Hamidullah: "Kuna hadithi ya zamani sana huko Malabar, Pwani ya Kusini-Magharibi ya India, kwamba Chakrawati Farmas, mmoja wa wafalme wao, aliona kugawanyika kwa mwezi. alisherehekea muujiza wa Mtukufu Mtume pale Makka, na alipopata kujua kwamba kulikuwa na utabiri wa kuja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kutoka Uarabuni, alimteua mwanawe kama mtawala na akatoka kwenda kukutana naye. aliukubali uislam kwa mkono wa Mtume, na aliporudi nyumbani, kwa maelekezo ya Mtume, alifariki kwenye bandari ya Zafar, Yemen, ambapo kaburi la “mfalme wa Kihindi” lilitembelewa kwa uchamungu kwa karne nyingi.

[5]Zafar: Sephar ya kibiblia, Safa ya zamani, au sehemu ya Uarabuni ya kale ya Saphar iliyoko kusini-magharibi mwa Yarim kusini mwa Yemeni. Ulikuwa mji mkuu wa Wahiyariti, kabila lililotawala sehemu kubwa ya Uarabuni ya kusini kuanzia mwaka wa 115 KK hadi karibu BK 525. Hadi kufikia utekaji wa Waajemi (c. AD 575), Zafar ilikuwa mojawapo ya miji muhimu na iliyosherehekewa sana kusini mwa Uarabuni. -jambo ambalo limethibitishwa si tu na wanajiografia na wanahistoria Waarabu bali pia na waandishi wa Kigiriki na Waroma. Baada ya kutoweka kwa ufalme wa Himyar na kuinuka kwa Uislamu, Zafar taratibu ilianguka kwenye kugawanyika.’ “Zafar.” Encyclopædia Britannica kutoka Encyclopædia Britannica Premium Service. (http://www.britannica.com/eb/article-9078191)

[6]Al-Bidaya wal-Nihaya,’ na Ibn Kathir, vol 3, uk. 130.

[7]Imeripotiwa na Hakim ndani ya‘Mustadrik’ vol 4, uk. 150. Hakim anasema, ‘sijakariri ripoti nyingine yoyote inayosema mtume alikula tangawizi’

[8]Al-Isaba’ na Ibn Hajr, vol 3. p. 279 na‘Lisan ul-Mizan’ na Imam al-Dhahabi, juzuu ya 3 uk. 10 chini ya jina la ‘Sarbanak,’ jina ambalo waarabu walimjua.

[9]‘Muhammad: Maisha yake kulingana na vyanzo vya mwanzo Martin Lings, uk. 103.

[10] Masahaba arobaini na watano wa Mtume waliwasilisha taarifa za Safari yake ya Usiku na Kupaa Mbinguni. Tazama kazi za masomi wa hadithi: ‘Azhar al-Mutanathira fi al-Ahadith al-Mutawatira’ cha al-Suyuti uk. 263 na ‘Nadhm al-Mutanathira min al-Hadith al-Mutawatir,’ cha al-Kattani uk. 207.

Mbaya Nzuri zaidi

Miujiza ya Muhammad (sehemu ya 3 kati ya 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kutajwa kwa miujiza mingine mbali mbali ya Mtume, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

  • Na IslamReligion.com
  • Iliyochapishwa mnamo 29 Nov 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,339
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Ipo miujiza mingine mingi aliyoifanya Mtume inayohusiana na Sunnah, au muunganiko wa maneno, matendo, idhini na maelezo ya Mtume.

Shina la Mti

Huko Madina Muhammad alikuwa akitoa mahubiri akiwa ameegemea shina la mti. Pindi idadi ya wanaoabudu ilipongezeka, mtu mmoja alipendekeza mimbari ijengwe ili aweze kuitumia kutoa mahubiri. Mimbari ilipojengwa, aliliacha shina la mti. Abdullah ibn Umar, mmoja wa masahaba, alitoa ushuhuda wa shahidi wa kile kilichotokea. Shina likasikika likilia, Mtume wa rehema akaliendea na kulifariji kwa mkono wake.[1]

Tukio hilo pia linathibitishwa kupitia ushuhuda wa mashahidi uliopitishwa kwa mda mrefu kwa wasomi wanaoaminika (hadith mutawatir).[2]

Mtiririko wa Maji

Zaidi ya wakati mmoja katika tukio ambalo watu walikuwa na uhitaji mkubwa wa maji, baraka ya Muhammad iliwaokoa. Katika mwaka wa sita baada ya kuhama kutoka Makka kwenda Madina, Muhammad alikwenda Makka kwa ajili ya kuhiji. Katika safari ndefu ya jangwani, watu waliishiwa maji yote, ni Mtume tu ndiye aliyebakiwa na chombo ambacho alichukulia udhu kwa ajili ya kuswali. Akaingiza mkono kwenye chombo, maji yakaanza kutoka katikati ya vidole vyake. Jabir ibn Abdullah, ambaye alishuhudia muujiza huo, anasema watu elfu moja na mia tano, ‘Tulikunywa na tukatawadha.'[3] Muujiza huu umepitishwa kwa wasomi wakuaminika (hadith mutawatir).[4]

Kutoka kwa maji kutoka kwa vidole vya binadamu ni sawa na muujiza wa Musa wa kutokeza maji kutoka kwenye mwamba.

Baraka ya Chakula

Zaidi ya tukio moja, Mtume alibariki chakula kwa kuswali au kukigusa ili wote waliokuwepo wapate kushiba. Hili lilitokea nyakati ambapo uhaba wa chakula na maji uliathiri Waislamu.[5] Miujiza hii ilifanyika mbele ya idadi kubwa ya watu, hivyo, haiwezekani kukataa.

Kuwaponya Wagonjwa

Abdullah ibn Ateek alivunjika mguu wake na Muhammad akauponya kwa kuufuta mkono wake juu yake. Abdullah akasema ni kana kwamba hakuna kilichotokea kwake! Mtu aliyeshuhudia muujiza huo alikuwa ni sahaba mwingine, Bara’ ibn Azib (Saheeh Al-Bukhari)

Wakati wa msafara wa Khaybar, Muhammad aliponya macho yenye kuuma ya Ali ibn Abi Talib mbele ya jeshi zima. Ali, miaka mingi baadaye, akawa khalifa wa nne wa Waislamu.[6]

Kutoa Mashetani

Muhammad alimtoa shetani kutoka kwa mvulana aliyeletwa na mama yake kwa ajili ya uponyaji kwa kusema, ‘Toka! Mimi ni Muhammad, Mtume wa Mwenyezi Mungu!’ Yule mwanamke akasema, ‘Naapa kwa Yule aliyekutuma kwa haki, hatujaona tatizo lake lolote kutoka kipindi hicho.'[7]

Maombi Kujibiwa

(1) Mama yake Abu Huraira, sahaba wa karibu wa Muhammad, alikuwa akiusema vibaya Uislamu na Mtume wake. Siku moja, Abu Huraira alikuja kwa Muhammad akilia na akamwomba amwombee mama yake apone. Muhammad aliomba na Abu Huraira aliporudi nyumbani alimkuta mama yake yupo tayari kuukubali Uislam. Alitoa ushuhuda wa imani mbele ya mwanawe na akaingia katika Uislamu.[8]

(2) Jarir ibn Abdullah alipewa maagizo na Mtume kuliondoa katika ardhi sanamu lililoabudiwa badala ya Mwenyezi Mungu, lakini alilalamika kuwa hawezi kumpanda farasi vizuri! Mtume akamuombea, ‘Ewe Mola, mjaalie kuwa mpanda farasi mwenye nguvu na mjaalie kuwa ni muongozaji na mwenye kuongozwa.’ Jarir anashuhudia kuwa hakuwahi kumdondosha farasi wake baada ya Mtume kumswalia.[9]

(3) Watu walipatwa na njaa wakati wa Muhammad. Mtu mmoja alisimama wakati Muhammad alipokuwa akitoa hutuba yake ya kila Ijumaa, akasema, ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, mali zetu zimeharibiwa na watoto wetu wanakufa njaa. Tuombee kwa Mungu.’ Muhammad aliinua mikono yake katika sala.

Wale waliohudhuria wanashuhudia kwamba mara tu aliposhusha mikono yake baada ya kusali, mawingu yalianza kutanda kama milima!

Wakati anashuka kutoka kwenye mimbari yake, mvua ilikuwa inadondoka kutoka kwenye ndevu zake!

Mvua ilinyesha wiki nzima hadi Ijumaa iliyofuatia!

Mtu huyo huyo akasimama tena, akilalamika mara hii, ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, majengo yetu yameharibiwa, na mali zetu zimezama, tuombee kwa Mungu!’

Muhammad aliinua mikono yake na kuomba, ‘Ewe Mungu, (inyeshe mvua) karibu nasi, lakini isiwe juu yetu.

Waliohudhuria wanashuhudia kwamba mawingu yaliondoka kuelekea upande aliouelekeza, mji wa Madina ulizungukwa na mawingu, lakini hapakuwa na mawingu juu yake![10]

(4) Hii hapa hadithi nzuri ya Jabir. Anashuhudia kwamba wakati mmoja, ngamia aliokuwa amepanda alikuwa amechoka kwa sababu ilitumika kubebea maji. Ngamia hakuweza kutembea. Muhammad akamuuliza, ‘Kuna nini juu ya ngamia wako?’ Alipogundua jinsi ngamia alivyochoka, Muhammad alimswalia mnyama na kuanzia wakati huo, Jabir anatuambia, ngamia alikuwa daima mbele ya wengine! Muhammad akamuuliza Jabir, ‘unamuonaje ngamia wako?’ Jabir akajibu, ‘Yuko vizuri, baraka yako imemfikia’ Muhammad alimnunua ngamia kutoka kwa Jabir pale pale kwa kipande cha dhahabu, kwa sharti kwamba Jabir ampande. kurudi mjini! Alipofika Madina, Jabir anasema alimleta ngamia kwa Muhammad asubuhi iliyofuata. Muhammad akampa kipande cha dhahabu na akamwambia amchunge ngamia wake![11]

Si ajabu kwa nini wale waliokuwa karibu naye walioshuhudia miujiza hiyo mikuu ikifanywa mbele ya umati walikuwa na hakika juu ya ukweli wake.



Rejeleo la maelezo:

[1] Saheeh Al-Bukhari.

[2]Zaidi ya masahaba kumi wa Mtume walisambaza taarifa hizo baada ya kusikia kilio cha shina la mti. Tazama kazi za mabwana wa hadithi: ‘Azhar al-Mutanathira fi al-Ahadith al-Mutawatira’ cha al-Suyuti uk. 267, ‘Nadhm al-Mutanathira min al-Hadith al-Mutawatir,’ cha al-Kattani uk. 209 na ‘Shamail’ cha Ibn Kathir uk. 239.

[3] Saheeh Al-Bukhari.

[4]Zaidi ya masahaba kumi wa Mtume (s.a.w.w.) walisambaza taarifa hizo baada ya kusikia kilio cha shina la mti. Tazama ‘Nadhm al-Mutanathira min al-Hadith al-Mutawatir,’ cha al-Kattani uk. 212, ‘al-Shifa’ cha Qadhi Iyyad, juzuu ya 1, uk. 405, na ‘al-’Ilaam’ cha al-Qurtubi, uk. 352.

[5] Saheeh Al-Bukhari. Angalia ‘Nadhm al-Mutanathira min al-Hadith al-Mutawatir,’ by al-Kattani p. 213 and ‘al-Shifa’ by Qadhi Iyyad, juzuu ya 1, uk. 419.

[6] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim

[7] Musnad wa Imam Ahmad, and Sharh’ al-Sunnah

[8] Saheeh Muslim

[9] Saheeh Muslim

[10]Saheeh Al-Bukhar, Saheeh Muslim

[11] Saheeh Al-Bukhar, Saheeh Muslim

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.