Maryamu, Mamake Yesu (sehemu ya 1 kati ya 2): Maryamu ni nani?

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Wakristo wanamjua Maryamu, mamake Yesu. Vile vile Waislamu pia wanamtambua kama mamake Isa, au kwa Kiarabu, Umm Issa. Katika Uislamu Maria mara nyingi anaitwa Maryam bint Imran; Maryamu binti wa Imran. Makala haya yanatoa historia fulani kuhusu kulelewa kwake na Zakaria kwa hivyo aliweza kutumika hekaluni.

  • Na Aisha Stacey (© 2008 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 09 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 19 Sep 2022
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,431
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Inaweza kuwashangaza watu wengi kujua ya kwamba Maryamu ni mmoja wa wanawake waliotukuzwa na kuheshimiwa sana katika Uislamu na kwamba Kurani vile vile imempatia yeye umuhimu mkubwa sana. Maryam ni jina la sura ya 19 ya Kurani, na Sura ya 3 ni Al Imran, iliyopewa jina la familia yake. Uislamu umeipatia hadhi kubwa sana familia yote ya Imran. Kurani inatuambia kuwa:

“Hakika Mwenyezi Mungu alimteuwa Adam na Nuhu na ukoo wa Ibrahim na ukoo wa Imran juu ya walimwengu wote.” (Kurani 3:33)

Mungu alimchagua Adamu na Nuhu kibinafsi, lakini alizichagua familia za Ibrahim na Imrani.

“Ni wazao wao kwa wao; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kujua.” (Kurani 3:34)

Familia ya Imran inatokana na ukoo wa Ibrahim, familia ya Ibrahim wanatokana na ukoo wa Nuhu na Nuhu anatokana na ukoo wa Adam. Familia ya Imran pia inajumuisha watu wengi wanaojulikana na kuheshimiwa katika mila za Kikristo - Mitume Zakaria na Yohana (anayejulikana kama Mbatizaji), Mtume na Mjumbe Yesu na mamake, Maryamu.

Mwenyezi Mungu alimchagua Maryamu kuliko wanawake wote ulimwenguni. Alisema:

“Na angalia pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Kwa hakika Mwenyezi Mungu amekuteuwa, na akakutakasa, na akakutukuza kuliko wanawake wote.’” (Kurani 3:42)

Amesema Ali bin Abu Talib:

“Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema yakuwa Maryamu, binti ya Imran alikuwa bora kati ya wanawake.” (Saheeh Al-Bukhari)

Kwa Kiarabu jina la Maryamu linamaanisha mjakazi wa Mwenyezi Mungu, na kama tutakavyoona, Maryamu, mamake Yesu, alitolewa kumtumikia Mwenyezi Mungu hata kabla hajazaliwa.

Kuzaliwa kwa Maryamu

Biblia haina maelezo yoyote kuhusu kuzaliwa kwa Maryamu; hata hivyo, Kurani inatujulisha kwamba mke wa Imran alitoa wakfu mtoto wake ambaye hajazaliwa ili kumtumikia Mwenyezi Mungu. Mamake Maryamu, ambaye ni mke wa Imran, alijulikana kama Hana[1]. Aliyekuwa dada ya mke wa Mtume Zakaria. Hana na mumewe Imran walikuwa wameamini kuwa kamwe hawakujaaliwa kupata watoto, lakini siku moja Hana aliomba dua ya dhati kwa kuyenyekea kwa Mwenyezi Mungu abarikiwe mtoto, na kuweka nadhiri kwamba mtoto wake angetumika katika Nyumba ya Mwenyezi Mungu huko Yerusalemu. Mwenyezi Mungu alisikia maombi ya Hana na kumjaaliya kushika ujauzito. Hana alipotambua habari hizo tukufu alinyenyekea kwa Mwenyezi Mungu na kusema:

“Alipo sema mke wa Imran: Mola wangu Mlezi! Nimekuwekea nadhiri kilichomo tumboni mwangu kuwa wakfu; basi nikubalie. Hakika Wewe ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua..” (Kurani 3:35)

Kuna mafunzo ya kujifunza kutokana na nadhiri ya Hana kwa Mwenyezi Mungu, mojawapo ikiwa ni utunzaji wa elimu ya kidini ya watoto wetu. Hana hakuwa na fikira ya ulimwengu huu, bali, alikuwa akijaribu kuhakikisha kuwa mtoto wake alikuwa karibu na Mwenyezi Mungu na vile vile katika ibada zake. Watu wema hawa wateule wa Mwenyezi Mungu, kama vile familia ya Imran, ni wazazi ambao tunapaswa kuwaiga. Mwenyezi Mungu anasema mara nyingi katika Kurani kwamba Yeye ndiye anayetupatia riziki, na anatuonya tujiepushe sisi pamoja na familia zetu kutokana na moto wa Jehanamu.

Katika dua yake, Hana aliomba mtoto wake awe huru kutokana na shughuli zote za kikazi duniani. Kwa kuahidi kwamba mtoto wake atakuwa mtumwa wa Mwenyezi Mungu, Hana alikuwa akimhakikishia mtoto wake uhuru . Uhuru ni aina ya maisha ambayo kila mwanadamu anajitahidi kupata, lakini Hana alifahamu ya kwamba uhuru wa kweli unatokana na utiifu kamili kwa Mwenyezi Mungu. Chanzo chake cha kutamani kupata mtoto wake ambaye hakuwa amezaliwa kilisababishwa na hili. Hana alitaka mtoto wake awe mtu huru, ambaye hatokuwa mtumwa wa mtu yeyote ama mwenye matamanio, ila atakuwa mtumwa wa Mwenyezi Mungu tu. Baada ya muda, Hana alijifungua mtoto wa kike, na vile vile tena akanyenyekea kwa Mwenyezi Mungu katika sala na akasema;

“‘Basi alipo mzaa alisema: Mola wangu Mlezi! Nimemzaa mwanamke - na Mwenyezi Mungu anajua sana aliye mzaa- Na mwanamume si sawa na mwanamke. Na mimi nimemwita Maryamu. Nami namkinga kwako, yeye na uzao wake, uwalinde na Shet'ani aliye laaniwa.” (Kurani 3:36)

Hana alimwita mtoto wake Maryamu. Kwa kuzingatia nadhiri yake kwa Mwenyezi Mungu, Hana alijipata akikabiliwa na hali ngumu. Haikuwa desturi ya wanawake kuhudumu katika Nyumba ya Maombi. Imran, babake Maryamu, alikuwa amefariki kabla ya kuzaliwa, kwa hivyo Hana alimwendea shemeji yake, Zakaria. ambaye alimfariji Hana kwa kumsaidia kuelewa hilo MwenyeziMungu alijua kuwa amejifungua msichana. Mtoto huyu wa kike, Maryamu, alitokana na uumbaji bora zaidi. Mtume Mohammad alitaja[2] kwamba kila mtoto anapozaliwa Shetani humchoma na hivyo husababisha mtoto kulia kwa sauti kubwa. Hii ni ishara ya uhasama mkubwa baina ya wanadamu na Shetani; hata hivyo kulikuwa na tofauti mbili ya sheria hii. Shetani hakumpiga Maryamu vile vile na mwanawe Yesu[3], kutokana na dua ya mamake Maryamu.

Wakati rasmi ulipofika wa Maryamu kwenda kwenye Nyumba ya Maombi, kila mtu alitaka fursa ya kumtunza binti huyu wa Imran aliyekuwa mcha Mungu. Kama ilivyokuwa desturi ya wakati huo, wanaume hao walijaaliwa fadhila nyingi, na Mungu alihakikisha kuwa mlezi wake alikuwa Mtume Zakaria.

“Tena Mola wake Mlezi akampokea kwa mapokeo mema na akamkuza makuzo mema, na akamfanya Zakariya awe mlezi wake.” (Kurani 3:37)

Mtume Zakaria alihudumu katika Nyumba ya Mwenyezi Mungu na alikuwa mtu mwenye hekima na maarifa na aliyejitolea kufundisha. Alikuwa na chumba kilichojengwa maalum kwa ajili ya Maryamu, ili aweze kumwabudu Mwenyezi Mungu na kufanya kazi zake za kila siku faraghani. Kama mlezi wake,Mtume Zakaria alimtembelea Maryamu kila siku, na siku moja alishangaa kuona matunda mabichi kwenye chumba chake. Inasemekana kwamba wakati wa majira ya baridi kali angekuwa na matunda mapya ya kiangazi na wakati wa kiangazi angekuwa na matunda mapya ya majira ya baridi kali.[4] Mtume Zakaria alitaka kujua jinsi tunda lilivyofika pale, na Maryamu akamjibu, hakika ni Mwenyezi Mungu ndiye aliyempa riziki. Alisema:

“Hivi vinatoka kwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu.” (Kurani 3:37)

Fadhila za Maryamu kwa Mwenyezi Mungu wakati huo haukuwa na kifani, lakini imani yake ilikuwa karibu kujaribiwa



Rejeleo la maelezo:

[1] Kutoka kwenye Tafsiri ya Ibn Katheer.

[2] Saheeh Al-Bukhari.

[3] Saheeh Muslim.

[4] Kulingana na kazi ya Al Imam ibn Katheer. Hadithi za Mitume.

Mbaya Nzuri zaidi

Maryamu, Mamake Yesu (sehemu ya 2 kati ya 2): Kuzaliwa kwa Yesu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Makala hii inaeleza yale yaliyompata Maryamu baada ya kuwa chini ya ulezi wa Mtume Zakaria. Inasimulia jinsi malaika Gabrieli alivyotangaza kuzaliwa kwa mtoto wa kipekee, jinsi alivyokabiliana na kujifungua mtoto wake, na kusimulia baadhi ya miujiza iliyotukia wakati Yesu alipozaliwa.

  • Na Aisha Stacey (© 2008 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 10 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,946
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Aliyeheshimiwa na kupendwa na Waislamu wote na anayejulikana kama mwanamke mchamungu na msalihina, Maryamu, mamake Yesu alichaguliwa juu ya wanawake wote. Uislamu unakataa wazo la Kikristo kwamba Yesu ni sehemu ya utatu kuwa yeye ni Mungu, na unakataa kwa dhati kwamba Yesu ama mamake, Maryamu, wanastahili kuabudiwa. Kurani inatamka bayana kwamba hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu.

“Huyo ndiye Allah, Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu, hapana mungu ila Yeye, Muumba wa kila kitu. Basi muabuduni Yeye tu. Naye ni Mtegemewa wa kila kitu...” (Kurani 6:102)

Waislamu wanatakiwa, hata hivyo, kuwaamini na kuwapenda Mitume wote, akiwa ni pamoja na Mtume Yesu, ambaye ana nafasi maalum kwenye kanuni za imani za Kiislamu. Mamake, Maryamu, ana mahali pa heshima. Akiwa msichana, Maryamu alikwenda katika Nyumba ya Maombi huko Yerusalemu, maisha yake yote akiwa alijitolea kwa sala na ibada ya Mungu.

Maryamu Anapashwa Habari za Yesu

Wakati amejitenga na kila mtu, mtu mmoja alijitokeza mbele ya Maryamu. Mwenyezi Mungu alisema:

“Na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea Roho wetu, akajifananisha kwake sawa na mtu..” (Kurani 19:17)

Maryamu aliingiwa na hofu na kujaribu kukimbia. Alimwomba Mwenyezi Mungu akisema:

“(Maryamu) akasema: Hakika mimi najikinga kwa Mwingi wa Rehema aniepushe nawe, ukiwa ni mchamungu..” (Malaika) akasema: Hakika mimi ni mwenye kutumwa na Mola wako Mlezi ili nikubashirie tunu ya mwana aliye takasika..” (Kurani 19:18-19)

Maryamu alistaajabishwa na kutatanishwa na maneno hayo. Hakuwa ameolewa, bali alikuwa bikira aliyejisitiri na kujilinda. Aliuliza kwa mshangao:

“‘Maryamu akasema: Mola wangu Mlezi! Vipi nitampata mwana na hali hajanigusa mwanaadamu? Mwenyezi Mungu akasema: Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu huumba apendacho. Anapo hukumu jambo, huliambia: Kuwa! Likawa.” (Kurani 3:47)

Mwenyezi Mungu alimuumba Adam kwa vumbi la ardhi, bila mama wala baba. Alimuumba Hawa kutokana na ubavu wa Adam; na Yesu aliuumbwa bila ya baba, bali alikuwa na mama, Bikira Maryamu mchamungu. Mwenyezi Mungu, ambaye ni kauli ya lazima pindi anaposema ‘kitu Kiwe’ ili kukipatia uhai, alipuliza roho ya Yesu ndani ya tumbo la Maryamu kupitia Malaika Gabrieli.

“na tukampulizia humo[1] aliye linda ubikira wake, kutoka roho yetu, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi...” (Kurani 66:12)

Ingawa katika Kurani na Biblia hadithi za Maryamu zina vipengele vingi vinavyofanana, maoni ambayo Maryamu alikuwa ameposwa au kuolewa yanakataliwa kabisa na Uislamu. Muda ulipita, na Maryamu aliogopa kusemwa na watu waliokuwa karibu naye. Aliwaza jinsi ya kwamba watamuamini kuwa hakuna mwanaume aliyemgusa. Wanazuoni wengi katika Uislamu wanakubali kwamba muda wa ujauzito wa Maryamu ulikuwa wa kawaida.[2] Kisha, wakati ulipowadia wa yeye kujifungua, Maryamu aliamua kuondoka Yerusalemu, na kusafiri kuelekea mjini Bethlehemu. Ingawa Maryamu aliyakumbuka maneno ya Mwenyezi Mungu, na kwa kuwa imani yake ilikuwa yenye nguvu na thabiti, msichana huyo alikuwa na hofu na wasiwasi. Lakini malaika JibriliKadhalikaz alimpatia hakikisho:

“Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu).” (Kurani 3:45)

Kuzaliwa kwa Yesu

Uchungu wa kujifungua ulimfikisha kwenye mti wa mtende na akalikumbatia shina la mtende na kuendelea kulia kwa uchungu:

“Laiti ningeli kufa kabla ya haya, na nikawa niliye sahaulika kabisa!” (Kurani 19:23)

Maryamu alijifungua mtoto wake papo hapo, chini ya mti wa tende. Alikuwa amechoka baada ya kujifungua, na kujawa na dhiki na hofu, lakini hata hivyo alisikia sauti ikimuita. .

“ Usihuzunike! Hakika Mola wako Mlezi amejaalia chini yako kijito kidogo cha maji; Na litikise kwako hilo shina la mtende, utakuangushia tende nzuri zilizo mbivu.Basi kula, na kunywa, na litue jicho lako...” (Kurani 19:24)

Mungu alimpa Maryamu maji, kijito kilitokea ghafla chini ya mahali alipokuwa ameketi. Kadhalika, alimpa chakula; kile alichotakiwa kufanya ni kutikisa shina la mti wa tende. Maryamu aliogopa na alijawa na hofu; alijihisi dhaifu sana baada ya kujifungua, kwa hiyo hakuna na nguvu ya kutikisa shina kubwa la mtende? Lakini Mwenyezi Mungu aliendelea kumpa Maryamu riziki.

Tukio lililofuata kwa hakika lilikuwa la muujiza mwingine, na kama wanadamu tunajifunza somo kubwa kutokana na hili. Maryamu hakuhitaji kutikisa mti wa tende, jambo ambalo lisingewezekana; ilibidi atie juhudi tu. Alipojaribu kufuata amri ya Mwenyezi Mungu, tende mbivu zilianguka kutoka kwenye mti na Mwenyezi Mungu akamwambia Maryamu: “…basi kula, na kunywa, na litue jicho lako.” (Kurani 19:26)

Sasa ilimbidi Maryamu amchukue mtoto wake mchanga na kuikabili familia yake. Bila shaka aliogopa, na Mwenyezi Mungu alijua hili vizuri. Hivyo alimwagiza anyamaze kimya. Haingewezekana kwa Maryamu kueleza jinsi ambavyo ghafla amekuwa mama wa mtoto mchanga. Kwa kuwa alikuwa hajaolewa, watu wake hawakuamini maelezo yake. Mungu alisema:

“Basi kula, na kunywa, na litue jicho lako. Na pindi ukimwona mtu yeyote basi sema: Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga; kwa hivyo leo sitasema na mtu.’” (Kurani 19:26)

Maryamu alifika kwa watu wake akiwa amembeba mtoto, na hapo hapo wakaanza kumshutumu; wakasema, “Umefanya aibu gani? Umetoka katika familia nzuri, na wazazi wako walikuwa wachamungu.”

Kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza, Maryamu hakuzungumza, alinyoosha kidole tu kwa mtoto aliyekuwa mikononi mwake. Kisha Yesu, mwana wa Maryamu akasema. Kama mtoto mchanga, Yesu, Mtume wa Mungu alifanya muujiza wake wa kwanza. Kwa idhini ya Mwenyezi Mungu alisema:

“Akasema: Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu, amenipa Kitabu na amenifanya Nabii; Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo, Na ameniusia Swala na Zaka maadamu ni hai, na nimtendee wema mama yangu, wala hakunifanya niwe jeuri, mwovu. Na amani iko juu yangu siku niliyo zaliwa, na siku nitakayo kufa, na siku nitakayo fufuliwa kuwa hai!” (Kurani 19:30-34)

Maryamu ametajwa katika Kurani (5:75) kama siddqa (mkweli) lakini neno la Kiarabu siddiqa linamaanisha maana zaidi ya kusema ukweli . Lina maana ya kwamba mtu amefikia kiwango cha juu sana cha uadilifu. Pia lina maana kwamba mtu ni mkweli, si tu na yeye mwenyewe na wale walio karibu nao, bali pia kwa Mungu. Maryamu alikuwa ni mwanamke aliyetimiza agano lake na Mwenyezi Mungu, ambaye alimuabudu kwa utiifu. Alikuwa mchamungu, aliyejisitiri, na msalihina; mwanamke aliyechaguliwa juu ya wanawake wengine wote kuwa mamake Yesu alikuwa ni Maryamu binti Imran.



Rejeleo la maelezo:

[1] Hili limefafanuliwa vyema katika maelezo wazi kuhusu vazi lake, ingawa aya yenyewe inazungumzia kuhusu "ubikira wake" (yaani kujilinda kutokana na kuingiliana na wanaume wanaoweza kumuoa). Hivyo Mungu akapuliza roho ndani yake hata kama alikuwa amejihifadhi kwa njia ya malaika Jibrili.

[2] Sheikh al Shanqeeti in (Adwaa’ al-Bayaan, 4/264)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa