Mtu wa mwisho kuingia Peponi (sehemu 1 kati ya sehemu 2): Na Mti Utatokea.

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Atakapo tambaa mtu wa mwisho nje ya Jahannamu, na atakapoingizwa Peponi, milango ya Jahannamu itafungwa milele.

  • Na Aisha Stacey (© 2013 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 11 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 10 Sep 2023
  • Ilichapishwa: 1
  • Imetazamwa: 3,915
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

LastPersonEnterParadise1.jpg Pepo ni thawabu ya ajabu ambayo Mwenyezi Mungu amewaandalia Waumini, kwa wanao mt'ii Yeye. Ni mahali pa furaha kamili na utulivu na hakuna kitu ulimwenguni ambacho kinaweza kuvuruga utulivu huu. Itaendelea milele na tunatarajia kuwa itakuwa nyumba yetu ya milele. Kile ambacho Mungu na Mtume wake Muhammad wametuambia kuhusu Paradiso kinaweza vurumisha vichwa vyetu na akili zetu. Katika hadithi moja ya Mtume Muhammad, Mungu anasema: "Mimi nimewaandalia waja wangu wema ambao jicho halijapata kuuona, wala sikio halijapata kuusikia wala haujawahi kufikiriwa na akili za mwanadamu yeyote."[1] Hii ndio sisi, wanadamu, tumekuwa tukisubiri, na tukiwa na hekima na tuifanyie kazi, basi hii ndiyo malipo ya mapambano ya maisha haya ya muda mfupi. Tunatafakari na kujiuliza maswali kuhusu makao yetu ya milele, tunafikiri kuhusu Pepo kwa kuitamani na Jahannamu kwa kuihofia, lakini hata kama nyoyo zetu hutetemeka, mawazo ya Paradiso huleta furaha.

Maelezo ya peponi na Jahannamu katika hadeeth za Mtume Muhammad zina masimulizi kuhusu nani atakuwa mtu wa kwanza kuingia Peponi. Siku Kuu ya Kiyama Mtume Muhammad ndiye atakuwa mtu huyo. Aliwaambia wenzake kuwa atakuwa “wa kwanza kubisha kwenye milango ya Peponi”.[2]Na Mtume Muhammad alisema: "Nitakuja kwenye milango ya Pepo na nitaomba ifunguliwe. Mlinzi wa mlango atauliza, “Wewe ni nani?” Nitasema: 'Muhammad' Mlinzi wa mlango atasema “Niliamrishwa nisifungue mlango kwa mtu mwingine yeyote kabla yako”.[3]

Mtume Muhammad anaingia kwanza, na hiyo ni heshima anayoustahili. Itakuwa rahisi kwa Akili zetu kuelewa sababu za heshima hii kubwa, lakini baada ya muda fulani tunaanza kujiuliza ni nani atakayekuwa mtu wa mwisho kuingia Peponi. Kwa sababu kutakuwa na mtu wa mwisho na kisha milango itafungwa. Masahaba wa Mtume Muhammad pia walishangaa kuhusu Paradiso kwa namna ile ile tunayofanya sisi. Hata hivyo walikuwa na fursa ya kipekee ya kuweza kumuuliza Mtume wao mpendwa ni nani hasa atakayekuwa mtu wa mwisho kuingia Peponi?

Kama tunavyojua mapokeo ya Mtume Muhammad yanakuja kwetu kwa namna mbalimbali na mojawapo ya hayo ni hadith qudsi au hadith takatifu. Hadithi hizi ni muhimu hasa kwa sababu huku maneno yanasemwa na Mtume Muhammad, maana yake hutoka kwa Mwenyezi Mungu. Ni aina ya ufunuo. Hadithi hizi zinaunda mwelekeo mwingine wa ujumbe wa Mungu kwa wanadamu na kwa kawaida hushughulikia masuala ya kiroho au ya kimaadili. Jibu la swali lililoulizwa na masahaba linapatikana katika hadith qudsi na ni mojawapo ya hadeeth nzuri sana. Yafuatayo ni tafsiri ya hadeeth hii.

Mtu wa mwisho kuingia peponi atakuwa mtu ambaye atatembea kiasi, kisha akajikwaa mara na kuchomwa na moto mara nyingine. Mara atakapokwisha kuupita, atageuka na kukabiliana nao akisema: 'Ahimidiwe Yule Aliyeniokoa na wewe. Mwenyezi Mungu amenipa kitu ambacho hakumpa wa kwanza wala wa mwisho.'

Kisha mti utainuliwa mbele yake, naye atasema: 'Mola wangu Mlezi! Nipeleke karibu na mti huu, ili nipate kukaa chini ya kivuli chake na kunywa maji yake,' na Mwenyezi Mungu Mwenye Utukufu wote, atasema: 'Ewe mwana wa Adam nikikupa hili, utaniomba kitu kingine?' Atasema: 'Hapana Mola Mlezi!' Naye ataahidi kuwa hatamwomba chochote kingine, na Mola wake Mlezi atamsamehe kwa sababu ameona kitu ambacho hawezi kujizuia nacho. Basi ataletwa karibu nayo, naye atakaa katika kivuli chake na kunywa maji yake.

Kisha ataonyeshwa mti mzuri zaidi kuliko ule wa kwanza, na atasema: 'Mola wangu Mlezi! Nipeleke karibu na mti huo, ili nipate kunywa maji yake na nikae chini kivuli chake, wala sitakuomba kitu kingine chochote,' na atasema: 'Ewe mwana wa Adam hukuniahidi kuwa hutaniuliza kitu kingine chochote?” Atasema: 'Nikikuleta karibu nao huenda ukaniomba kitu kingine,' naye ataahidi kuwa hutamwomba chochote kingine, na Mola wake Mlezi atamsamehe kwa sababu ameona kitu ambacho hana kujizuia nacho. Basi ataletwa karibu nao, naye atakaa katika kivuli chake na kunywa maji yake.

Kisha atainuliwa mti mwingine kwenye mlango wa Pepo, ambao ni mzuri zaidi kuliko wa kwanza, na atasema: 'Mola wangu Mlezi! Nipeleke karibu na mti huo, ili nipate kukaa chini ya kivuli chake, na niyanywe maji yake, wala sitakuomba chochote kingine.' Atasema: 'Ewe mwana wa Adam! Kwani hukuniahidi kuwa hutaniomba chochote kingine?' Naye atasema: 'Naam, Ewe Mola, sitakuomba chochote kingine.' Mola wake Mlezi atamsamehe kwa sababu ameona kitu ambacho hana subra ya kujizuia nacho. Ataukaribia, na atakapo kuja karibu atasikia sauti za watu wa Peponi, na atasema: 'Mola Mlezi! Niingize humo.' Atasema: 'Ewe mwana wa Adam! Ni nini kitakacho kuacha kuuliza tena? Je, itakuridhisha nikikupa ulimwengu na mfano wake tena?” Atasema: 'Ewe Mola Mlezi! Unanidhihaki na hali Wewe ni Mola Mlezi wa walimwengu wote?'

Ibn Mas'ood (sahaba anayesimulia simulizi hii nzuri) alitabasamu na kusema: Kwa nini hamniulizi kwanini nina tabasamu? Wakasema: Kwa nini unatabasamu? Akasema: Hivi ndivyo Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake alitabasamu, na wao ( masahaba waliokuwa karibu naye) wakamuuliza: Kwa nini unatabasamu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Kwa sababu Mola Mlezi wa walimwengu wote atatabasamu anapo sema: Je! Unanidhihaki na hali Wewe ni Mola Mlezi wa walimwengu wote? Na (Mwenyezi Mungu) atasema: Mimi sikukudhihaki, lakini mimi ni Muweza wa kutenda nitakavyo.’”[4]

Katika sehemu ya pili tutajadili jinsi fadhili na rehema za Mungu zinavyoonyeshwa katika hadithi hii na kuangalia jinsi Mola wa walimwengu wote anavyojua vizuri na kuelewa uumbaji wake.



Vielezi-chini:

[1] Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim

[2] Saheeh Muslim

[3] Ibid

[4] Saheeh Muslim

Mbaya Nzuri zaidi

Mtu wa mwisho kuingia Peponi (sehemu ya 2 kati ya 2): Kidogo tu Zaidi

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mtu wa mwisho kuingia Peponi na walio kama yeye wanahisi athari kamili ya huruma ya Mungu.

  • Na Aisha Stacey (© 2013 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 11 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 1
  • Imetazamwa: 3,562
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

LastPersonEnterParadise2.jpgKatika makala iliyotangulia tuliangalia kwa kina hadeeth kutoka kwa Mtume Muhammad. Ni hadithi fupi kuhusu tabia za mwanadamu inayokuja kwa umbo la simulizi kuhusu mtu wa mwisho kuingia Peponi. Ni mtu aliyetoka Jahannamu, kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Mwanzoni mtu huyo alishukuru kwa kuwa katika nafasi kati ya Pepo na Jahannamu na kumhimidi Mungu kwa wema Wake na rehema Yake. Muda ulipita, hata hivyo, na akatambua kwamba kuna mti ulikuwa umetokea hapo. Aliangalia shina lake imara, matawi yake na majani na akatamani kuwa chini ya kivuli chake na kuzima kiu chake na maji yake. Hadithi inavyoendelea tunaona kwamba kila Mungu anapompa mtu huyo kile anachotamani, mtu huyo alitaka kitu kingine; kidogo tu zaidi.

Hadithi hii inaonyesha ukweli kwamba mwanadamu kamwe haridhiki, daima anataka zaidi. Ingawa hili linaweza kuwa jambo la kushangaza kwa mtu ambaye hajawahi kufikiria kuhusu mzunguko wa matakwa, mahitaji na tamaa ambazo wengi wetu tunajipata ndani yake, si jambo geni kwa Mungu. Yeye, Muumba na Mwanzilishi wa ulimwengu, anafahamu vizuri hali ya viumbe Vyake.

Mungu, Muumba, ana maarifa kamili. Anayajua yaliyo wazi na yasiyoonekana. Anajua yaliyo kuwa na yatakayokuwa. Na Yeye ndiye Mwenye kusikia yote, Mwenye kujua yote. Mungu amesema kwamba yeye yupo karibu na sisi kuliko mshipa wa shingoni, hakuna kitu kinachoepuka maarifa yake. Tunaweza kuficha hulka zetu mbaya na sifa zetu kutoka kwa wenzetu na familia zetu lakini Mungu anaona yote; sio tu hilo, lakini anaelewa pia vitu vipi vinatuhamasisha, vipi tunavyoviogopa, tunavyovipenda au tunavyovitamani. Na ndiyo sababu Yeye daima anatusamehe na anatupa rehema yake . Tunapohitaji rehema ya Mungu kwa jambo lolote, tunafaa kuiulizia tu.

“ Na hakika tumemuumba mtu, nasi tunayajua yanayo mpitikia katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake." (Kurani 50:16)

Kamusi inafafanua rehema kuwa tabia ya kuwa mwema na kusamehe, na hisia inayoleta huruma. Neno la Kiarabu la rehema ni Rahmah na majina mawili muhimu zaidi ya Mwenyezi Mungu yanatokana na neno hili, Ar-Rahman, Mwingi wa Rehema na Ar-Raheem, Mwingi wa Rehema. Rehema ya Mungu inajumuisha upole, utunzaji, kujali, upendo na msamaha. Sifa hizi zinapoonekana katika ulimwengu huu, ni mfano tu wa rehema ya Mungu kwa uumbaji wake. Katika hadithi hii tunaweza kuona wazi rehema ya Mungu kwa jinsi anavyomwitikia huyu mtu wa mwisho kutoka Jahannamu.

Katika hatua hii ni muhimu kutambua kwamba mtu huyu hakuingia Paradiso kwa sababu ya matendo yake mema, la hasha. Mwishowe aliingia Peponi kwa huruma ya Mungu. Inaweza kusemwa kuwa Mungu hupeana rehema yake ingawa haionekani, kwa mtazamo ya mwanadamu, kuwa ya kustahiliwa. Hakika Mwenyezi Mungu ameahidi kwamba mwenye kuamini kwa moyoni mwake hata kama amefanya dhambi nyingi, ataingia Peponi siku moja. Ili kuimarisha ufahamu huu Mtume Muhammad alituacha na maneno yafuatayo:

"Na atakaye kufa bila ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu basi ataingia Peponi.”[1]

Ukweli kwamba watu hawa pamoja na mtu anayezungumziwa watatolewa nje ya Jahannamu na kupelekwa Peponi haitawafanya watu hawa wenye heri wapate huzuni wowote au dhiki. Hayo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu anatuambia kwamba Pepo ndiyo nyumba ya neema. Hakuna chochote ndani ya Qurani au hadeeth za Mtume Muhammad kinachopendekeza kwamba watu hawa wataishi na majuto baada ya kuingia Peponi kutokana na adhabu waliyopata katika Jahannamu. Hii inaonekana wazi kwa furaha ya mtu huyo alipojikuta katika nafasi kati ya Peponi na Jahannamu. Anaonekana kuwa amepona mara moja na tayari anaangalia upande wa siku zijazo. Katika hadeeth zingine kutoka kwa Mtume Muhammad tunajua kwamba Pepo itawasahaulisha Waislamu shida zote walizozipata duniani, kwa hivyo tunaweza kusema kwamba hii pia inajumuisha shida zilizopitiwa katika Jahannamu kabla ya kuingia Peponi. Mtume wa Mwenyezi Mungu (rehema za Mwenyezi Mungu na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) alisema:

“Mtu aliyekuwa tajiri zaidi duniani, miongoni mwa watakao ingia Jahannamu, atahudhurishwa Siku ya Kiyama, na kutiwa Motoni mara moja. Kisha ataulizwa: Ewe mwana wa Adamu, Je! uliwahi ona kheri yoyote? Je! Umewahi kuwa na furaha yoyote? Atasema: Hapana, naapa kwa Mwenyezi Mungu, ewe Mola. Kisha aliyekuwa masikini zaidi duniani, miongoni mwa wanaoingia Peponi, ataletwa na atawekwa Peponi, na ataambiwa: Ewe mwana wa Adam! Je, umewahi kupata shida yoyote? Atasema: Hapana, naapa kwa Mwenyezi Mungu, ewe Mola. Sijawahi kuona chochote kibaya na sijawahi kupata shida yoyote."[2]

Dalili nyingine ya kuonyesha kwamba mtu kuzama katika neema ya Pepo itaondoa shida zote zilizotangulia, hata shida ya kuadhibiwa Jahannamu, ni kauli ya Mtume: “Anayeingia Peponi atafurahia neema na hatakuwa na huzuni, nguo zake hazitaisha na ujana wake hautapotea.”[3]

Baraka hii inaonyesha kwamba taabu itafutwa kwa yule anayeingia Peponi, na inajumuisha kila mtu anayeingia humo, awe ameipitia Jahannamu au la.

Na rehema ya Mwenyezi Mungu haina mipaka. Mtume Muhammad pia alisema:

"Mwenyezi Mungu ana sehemu mia za rehema, ambazo katika hizo ameteremsha moja baina ya majini, watu, wanyama na wadudu, na kwa hiyo sehemu wanahurumiana kati yao, na ni kwa hiyo sehemu wanyama wa pori wanahurumia watoto wao. Na Mwenyezi Mungu amewawekea waja wake sehemu tisini na tisa za rehema ambazo atawahurumia nazo Siku ya Kiyama."[4]



Vielezi-chini:

[1] Saheeh Muslim

[2] Ibid

[3] Ibid

[4] Ibid

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.