Mchungaji David Benjamin Keldani, Kasisi wa Kikatoliki, Iran

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Kasisi wa Kirumi Mkatoliki wa madhehebu ya Uniate-Caldean abadili dini na kuwa Muislamu.

  • Na IPCI
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 1,188 (wastani wa kila siku: 1)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Alipoulizwa ni vipi aliingia katika Uislamu aliandika:

“Kusilimu kwangu hakuwezi kuhusishwa na sababu nyingine isipokuwa muongozo wa neema ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Bila mwongozo huu wa Kimungu kujifunza, kutafuta, na juhudi nyinginezo za kupata Ukweli zinaweza hata kumpoteza mtu. Wakati nilipoamini katika Umoja Kamili wa Mungu Mtume Wake Mtukufu Muhammad akawa kielelezo cha mwenendo na tabia yangu.”

Abdu ‘l-Ahad Dáwúd alikuwa Mchungaji David Benjamin Keldani, B.D., kasisi wa Kiroma wa Kikatoliki wa madhehebu ya Uniate-Chaldian. Alizaliwa mwaka 1867 huko Urmia Uajemi; alielimishwa tangu utoto wake katika mji huo. Kuanzia 1886-89 (miaka mitatu) alikuwa kwenye uhudumu wa kufundisha wa Askofu Mkuu wa Misheni ya Canterbury kwa Wakristo wa Ashuru (Nestorian) huko Urmia. Mwaka 1892 alitumwa na Kardinali Vaughan kwenda Roma, ambako alipitia masomo ya falsafa na theolojia katika Chuo cha Propaganda Fide, na mwaka 1895 akapewa daraja la Upadre. Wakati huo alichangia mfululizo wa makala kwenye Runulishi ya “Assyria, Rome, and Canterbury”; na pia Rekodi ya Ireland juu ya “Uhalisi wa Pentateki.” Alikuwa na tafsiri kadhaa za Ave Maria katika lugha tofauti, zilizochapishwa katika Misheni za Kikatoliki . Akiwa Konstantinopoli akielekea Uajemi mwaka wa 1895, alichangia mfululizo mrefu wa makala katika Kiingereza na Kifaransa kwenye gazeti la kila siku, lililochapishwa chini ya jina la The Levant Herald, kuhusu“Makanisa ya Mashariki.” Mnamo 1895 alijiunga na Misheni ya Walazari wa Ufaransa huko Urmia, na akachapisha kwa mara ya kwanza katika historia ya Misheni hiyo jarida katika lugha ya kienyeji la Kisiria liitwalo Qala-La Shárá, yaani, "Sauti ya Ukweli." Mwaka 1897 aliteuliwa na Maaskofu wakuu wawili wa Uniate-Chaldian wa Urmia na Salmas kuwakilisha Wakatoliki wa Mashariki katika Kongamano la Ekaristi lililofanyika Paray-le-Monial nchini Ufaransa chini ya raisi wa Kardinali Perraud. Hii ilikuwa, bila shaka, kwa mwaliko rasmi. Karatasi iliyosomwa kwenye Kongamano na "Baba Benjamin" ilichapishwa katika Annals ya Kongamano la Ekaristi, liitwalo "Le Pelirin" la mwaka huo. Katika jarida hili, Kasisi Mkuu wa Wakaldayo (hicho kilikuwa ni cheo chake rasmi) alichukia mfumo wa elimu wa Kikatoliki kati ya Wanestoria na kutabiri kutokea kwa makuhani wa Kirusi huko Urmia.

Mwaka 1898 Padre Benjamini alirudi tena Uajemi. Katika kijiji alichozaliwa, Digala, kama maili moja kutoka mjini, alifungua shule ya bila malipo. Mwaka uliofuata alitumwa na mamlaka ya Kikanisa kuchukua jukumu la dayosisi ya Salmas, ambapo mzozo mkali na wa kashfa kati ya Askofu Mkuu wa Muungano, Khudabásh, na Mababa wa Lazarist kwa muda mrefu ulikuwa unatishia mgawanyiko. Katika siku ya Mwaka Mpya 1900, Baba Benjamin alihubiri mahubiri yake ya mwisho na ya kukumbukwa kwa kutaniko kubwa, ikiwemo Waarmenia wengi wasio Wakatoliki na wengine katika Kanisa Kuu la Mtakatifu George Khorovábád, Salmas. Mada ya mahubiri ilikuwa “Karne Mpya na Wanadamu Wapya.” Alikumbuka kuwa Wamisionari wa Nestorian, kabla ya kutokea kwa Uislamu, walikuwa wamehubiri Injili katika Asia yote; walikuwa na vituo vingi nchini India (hasa katika Pwani ya Malbar), huko Tartary, Uchina na Mongolia; na kwamba walitafsiri Injili kwa Waighuri wa Kituruki na katika lugha nyinginezo; Misheni za Kikatoliki, Kimarekani na Kianglikana, licha ya mema kidogo waliokuwa wameufanya kwa taifa la Ashuru-Kaldayo katika njia ya elimu ya awali, ilikuwa imeigawanya taifa hilo - ambalo tayari lilikuwa gumu - katika Uajemi, Kurdistan, na Mesopotamia na kuwa na maadui wengi wa madhehebu; na juhudi zao zilikusudiwa kuleta anguko la mwisho. Kwa hiyo, aliwashauri wenyeji wafanye kafara ili waweze kusimama kwa miguu yao kama wanaume, na wasitegemee misheni ya kigeni, nk.

Misheni tano kubwa na za kustaajabisha - Wamarekani, Waanglikana, Wafaransa, Wajerumani, na Warusi - pamoja na vyuo vyao, Vyombo vya habari vilivyoungwa mkono na jumuiya tajiri za kidini, kanseli na Mabalozi walikuwa wakijaribu kubadilisha Waashuri-Kaldayo wapatao laki moja kutoka kwenye uzushi wa Nestorian moja au nyingine kati ya mitano. Lakini Misheni ya Urusi baadae iliwashinda wengine, na ilikuwa misheni hii ambayo mnamo 1915 ilisukuma au kuwalazimisha Waashuri wa Uajemi, na vile vile makabila ya wapanda milima ya Kurdistan, ambao wakati huo walikuwa wamehamia nchi tambarare za Salmas na Urmia, kuchukua silaha dhidi ya Serikali zao. Matokeo yalikuwa nusu ya watu wake waliangamia katika vita na waliosalia wakafukuzwa kutoka katika nchi zao za asili.

Swali kuu ambalo kwa muda mrefu lilikuwa likifanya kazi ya ufumbuzi wake akilini mwa kasisi huyu sasa lilikuwa linakaribia kilele chake. Je, Ukristo, pamoja na maumbo na rangi zake nyingi, na pamoja na Maandiko yake yasiyo ya kweli, ya uwongo, na yaliyopotoka, ndiyo Dini ya kweli ya Mungu? Katika kiangazi cha 1900, alistaafu katika jumba lake la kifahari lililo katikati ya mashamba ya mizabibu karibu na chemchemi ya Cháli-Boulaghi huko Digala, na huko kwa muda wa mwezi mmoja alitumia wakati wake katika sala na kutafakari, akisoma tena na tena Maandiko katika maandishi yao ya asili. Mgogoro huo uliisha kwa kujiuzulu rasmi na kutumwa kwa Askofu Mkuu wa Muungano wa Urmia, ambamo kwa uwazi alimweleza Mar (Mgr.) Touma Audu sababu za kuacha kazi zake za sacerdotal. Majaribio yote yaliyofanywa na wenye mamlaka ya kikanisa kuondoa uamuzi wake hayakufaulu. Hakukuwa na ugomvi au mabishano ya kibinafsi kati ya Padre Benjamini na wakuu wake; yote yalikuwa ni suala la dhamiri.

Kwa miezi kadhaa Bw. Dáwúd - kama alivyoitwa sasa - aliajiriwa huko Tabriz kama Inspekta katika Huduma ya Kiajemi ya Posta na Forodha chini ya wataalamu wa Ubelgiji. Kisha akachukuliwa katika utumishi wa Mwana Mfalme Muhummed Alí Mirsá kama mwalimu na mfasiri. Ilikuwa mwaka 1903 ambapo alitembelea tena Uingereza na hapo akajiunga na Jumuiya ya Waunitariani. Na mwaka 1904 alitumwa na Jumuiya ya Wayunitarian ya Uingereza ili kuendeleza kazi ya elimu na ufunuo miongoni mwa watu wa nchi yake. Akiwa njiani kuelekea Uajemi, alitembelea Konstantinopoli; na baada ya mahojiano kadhaa na Sheikhu ‘l-Islám Jemálu ‘d-Dín Effendi na Maulamaa wengine, alisilimu.

Mbaya Nzuri zaidi

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.