Ukweli ni Mmoja (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Sehemu ya kwanza ya hoja yenye mantiki inayothibitisha kwamba ukweli ni kamili na sio tegemezi, kupitia uchunguzi wa mafunzo na maadili katika nyakati na sehemu mbalimbali.

  • Na M. Abdulsalam (© 2006 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 29 Nov 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 27 Nov 2022
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 2,869 (wastani wa kila siku: 3)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

The_Truth_is_One_(part_1_of_2)_001.jpgMara nyingi wakati wa kujadili dini, mtu husikia taarifa kwamba hakuna aliye na haki ya kuhukumu imani ya mtu mwingine, au kwamba dini ni jambo la binafsi la mtu na hatuwezi kusema kuwa ni makosa au ni sawa. Katika historia yote, jamii zimejikita katika sheria na maadili yao juu ya "ukweli kamili" ambao wanaona ni "sawa", na hii inaweza kuwa ni matokeo ya maandishi ya nje yanayoonekana kama makuu, au ya tabia inayopatikana katika asili ya wanadamu ambayo huwafanya waone mambo fulani kuwa mazuri na mengine kuwa mabaya. Kwa kiwango kidogo, wanadamu wanaweza kuona vitu fulani kuwa vizuri na vibaya. Kwa mfano, wanadamu wote, wakiachwa kwa hali yao ya asili bila kupotoshwa kwa akili, wataona kinyesi na mkojo kuwa uchafu. Pia, vitendo vingine, kama kuiba, kuua na kusema uwongo pia hujulikana kuwa vibaya, wakati ukweli, uwazi, na heshima huonekana kuwa ni ya kujivunia. Hii ni matokeo ya tabia ambayo iliundwa kwa wanadamu wote, lakini kama ilivyoelezwa hapo juu, hisia hii ni ndogo.

Ikiwa mtu anasema kwamba hawana haki ya kuhukumu imani au matendo ya wengine, kwa kweli, wanajipinga wenyewe. Ikiwa ungeuliza wengi wa watu hawa ikiwa kuua watoto wachanga au kujiua ni sawa na inakubalika, kwa kawaida watajibu kwamba sio. Lakini tunapoangalia jamii zingine, kama dini zingine zinazopatikana Amerika ya Kati, mauaji ya watoto wachanga yalionekana kuwa njia ya kukaribia miungu yao. Pia leo, katika dini la Kihindu, ni sifa kwa mke kujiua baada ya kifo cha mumewe. Ikiwa wanaamini kweli kuwa dini ni kitu kilichoachwa kwa mtu binafsi na kwamba hakuna aliye na haki ya kuingilia kati au kuwahukumu, basi hii italazimisha kuruhusu kuua watoto wachanga kua ni jambo ambalo ni sawa kwa wale ambao wanaamini ni ya kusifiwa, na kwamba watu hawana haki ya kuwahukumu.

Ikiwa tungeleta suala hili kwa kiwango cha mtu binafsi, tungeona kwamba kila mtu ana maoni yake binafsi ya mema na mabaya, ikiwa mtazamo huu unategemea dini, sheria, utamaduni, au tafakari ya mtu binafsi. Mtu anaweza kuamini kwamba inakubalika kabisa kuzini wakati mwingine anaweza kudhani kuwa ni makosa. Mtu anaweza kuamini kuwa inaruhusiwa kwao kujiingiza katika mihadarati kwani ni miili yao, na wengine wanaweza kuamini kuwa ni jinai. Hakuna atakayeweza kusema kuwa kitu chochote ni sawa au kibaya, na watu wote wangeachwa kuamini kwa njia zao na kutekeleza kile wanachokiona kuwa "sahihi."

Ikiwa tungetekeleza imani hii katika jamii, tungekuwa na jamii inayotokana na machafuko, ambapo sheria hazingeweza kutungwa au kutekelezwa, kwani sheria inategemea kanuni kwamba mambo fulani yanapaswa kuwa ni mema na mengine ni mabaya. Ikiwa mtu angesema kwamba kuna ukweli fulani uliokubaliwa na wanadamu wote ambao unaweza kutumika kutunga sheria, taarifa hii ni ya kweli kwa kikomo fulani, kama tulivyosema kwamba wanadamu wote wana asili ya kujua mema kutoka kwa mabaya kwa hali finyu. Lakini kama inavyoonekana, tabia hii mara nyingi hupotoshwa kupitia mazingira, saikolojia, au sababu za kidini, kwa kuwa vitendo fulani ambavyo wakati mmoja vilionekana kuwa viovu na visivyo na maadili baadaye huonekana kuwa vyema na vinavyokubalika, na mambo mengine ambayo hayapatani na asili ya wanadamu yanaonekana kuwa ndo ufunguo za wokovu. Hii inaweza kuangaliwa katika jamii za kidemokrasia ambazo zinaweka sheria zao kuzingatia wingi. Tunaona kwamba mambo mengi ambayo yalichukuliwa kuwa ya kipuuzi kabisa au yasiyo na maadili sasa yanakubalika kijamii, kwa kiwango ambacho ikiwa mtu ana maoni tofauti kuhusu suala hilo, huonekana kama watengwa.

Kwa sababu hii, wanadamu hawawezi kuachwa kwa matakwa yao ya kutunga sheria kipi ni sahihi na sio sahihi. Hata katika jamii za dini moja ambazo zimeanzisha utengano wa dini na serikali, ingawa wanakubaliana na vitu ambavyo walishikilia kutoka kwa dini yao, wanatofautiana sana kwa kile kinachoonekana kuwa sahihi na sio sahihi katika jamii zao. Kinachochukuliwa kama umri halali wa idhini ya kufanya mapenzi nchini Ufaransa inachukuliwa kuwa ubakaji huko Amerika. Wakati utoaji mimba ni halali katika nchi moja, ni uhalifu katika nchi nyingine, na wakati ushoga unaonekana kama njia halali ya maisha katika jamii moja, inaonekana kama dhambi kubwa katika jamii nyingine.

Kwa hivyo ikiwa sasa tunasema ukweli ni kamili na mmoja na hauhusiani na kila mtu na jamii, basi swali linalofuata ni maadili gani ambayo yanaonyesha ukweli na ni nani wa kuamua? Je! Ni sheria gani ambazo zinapaswa kutekelezwa katika jamii? Je! Zinapaswa kuamuliwa na mawakili na majaji ambao wamefikia kiwango cha "ufahamu wa kisheria", wanasiasa ambao kawaida hufanya maamuzi kwa faida yao au faida ya nchi zao, au wanafalsafa ambao wamejua ukweli wa ulimwengu kupitia tafakari yao wenyewe? Kama ilivyoonekana hapo awali, wanadamu hawawezi kuachwa waamue maswala haya, isije ikawa na matokeo mabaya, kama inavyoonekana leo katika jamii nyingi zilizo na shida nyingi. Yule pekee aliye na haki ya kutunga sheria ya mema na mabaya ni yule ambaye alituumba na anajua ni nini kinachofaa kwetu, na huyo ni Mwenyezi Mungu aliyetukuka. Ni Mungu aliyeumba ulimwengu na ni Mungu aliyeweka mizani ya haki. Ni Mungu ambaye ni mkamilifu na ni Mungu ambaye hana makosa yoyote.

Mijadala yetu mingi imeshughulikia maswala ya imani ambayo yanahusu maadili na matendo, lakini la muhimu zaidi ni imani ambazo zinashughulika na Mungu, na hii itajadiliwa katika nakala ifuatayo.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.