Kenneth L. Jenkins, Mhudumu na Mzee wa Kanisa la Pentekoste, Marekani (sehemu ya 1 kwa 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mvulana aliyewahi kupotoshwa anapata wokovu wake kupitia Kanisa la Kipentekoste na anajibu wito wake wa huduma akiwa na umri wa miaka 20, baadaye kuwa Muislamu. Sehemu ya 1.

  • Na Kenneth L. Jenkins
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,062 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Utangulizi

Kama mhudumu wa zamani na mzee wa kanisa la Kikristo, imekuwa wajibu kwangu kuwaangazia wale wanaoendelea kutembea gizani. Baada ya kuukubali Uislamu, nilihisi haja kubwa ya kuwasaidia wale ambao bado hawajabarikiwa kupata nuru ya Uislamu.

Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunirehemu na kunifanya niujue uzuri wa Uislamu kama alivyofundisha Mtume Muhammad na wafuasi wake walioongoka. Ni kwa rehema za Mwenyezi Mungu tu kwamba tunapata mwongozo wa kweli na uwezo wa kufuata njia iliyonyooka, ambayo inaongoza kwenye mafanikio katika maisha ya dunia na Akhera.

Asifiwe Mwenyezi Mungu kwa wema alionitendea Sheikh Abdullah bin Abdulaziz bin Baz baada ya kuukubali Uislamu. Ninathamini na nitapitisha maarifa niliyopata kutoka kwenye kila kikao pamoja naye. Kuna wengine wengi ambao wamenisaidia kwa njia ya kunitia moyo na ujuzi, lakini kwa kuogopa kumsahau mtu yeyote, nitaepuka kujaribu kuwaorodhesha. Inatosha kusema kwamba ninamshukuru Mwenyezi Mungu, kwa kila kaka na dada ambaye amemruhusu kuchukua nafasi katika ukuaji na maendeleo yangu kama Muislamu.

Ninaomba kuwa kazi hii fupi iwe ya manufaa kwa wote. Natumaini kuwa Wakristo wataona kuwa bado kuna tumaini kwa ajili ya hali zenye kupotoka zinazoenea kwa wingi kwenye Jumuiya ya Wakristo. Majibu ya matatizo ya Kikristo hayapatikani kwa Wakristo wenyewe, kwa maana wao, mara nyingi, ndio chanzo cha matatizo yao wenyewe. Bali Uislamu ndio suluhu la matatizo yanayoukumba ulimwengu wa Kikristo, pamoja na matatizo yanayoukabili ulimwengu unaoitwa wa dini kwa ujumla. Mungu atuongoze sote na atulipe thawabu kulingana na matendo na nia zetu.

Abdullah Muhammad al-Faruque at-Ta’if, Ufalme wa Saudi Arabia.

Mwanzo

Nikiwa mvulana mdogo nililelewa na hofu kuu ya Mungu. Nikiwa nimelelewa kidogo na bibi ambaye alikuwa Mpentekoste, kanisa likawa sehemu muhimu ya maisha yangu nikiwa na umri mdogo sana. Nilipofika umri wa miaka sita, nilijua vyema faida zinazoningoja Mbinguni kwa kuwa mvulana mdogo mzuri na adhabu inayosubiri motoni kwa wavulana wadogo ambao ni watukutu. Nilifundishwa na bibi yangu kuwa waongo wote walihukumiwa kwenda Motoni, ambako wangeungua milele na milele.

Mama yangu alifanya kazi mbili na aliendelea kunikumbusha mafundisho niliyopewa na mama yake. Ndugu yangu mdogo na dada yangu mkubwa hawakuonekana kuchukua maonyo ya bibi yetu ya baada ya duniani kwa uzito kama nilivyofanya. Nakumbuka nilipouona mwezi mwandamo ukiwa na rangi nyekundu-nyekundu, na ningeanza kulia kwa sababu nilifundishwa kwamba moja ya ishara za mwisho wa dunia ni kwamba mwezi ungekuwa mwekundu kama damu. Nikiwa mtoto wa miaka minane, nilianza kuingiwa na woga kwa kile nilichofikiri ni ishara mbinguni na duniani za Siku ya Kiyama kwamba niliota ndoto za jinsi Siku ya Hukumu itakavyokuwa. Nyumba yetu ilikuwa karibu na seti ya reli, na treni zilipita mara kwa mara. Nakumbuka niliamshwa kutoka usingizini na sauti ya kutisha ya honi ya treni na kufikiria kwamba nilikuwa nimekufa na nilikuwa nikifufuliwa baada ya kusikia sauti ya tarumbeta. Mafundisho haya yaliota mizizi katika akili yangu changa kupitia mchanganyiko wa mafundisho ya mdomo na usomaji wa seti ya vitabu vya watoto vinavyojulikana kama Hadithi ya Biblia.

Kila Jumapili tulikuwa tukienda kanisani tukiwa tumevalia mavazi yetu ya kifahari. Babu yangu alikuwa chombo chetu cha usafiri. Kanisa lingedumu kwa kile kilichoonekana kwangu kama masaa. Tulifika karibu saa kumi na moja asubuhi na tulikuwa hatuondoki hadi muda mwingine saa tisa alasiri. Nakumbuka kulala kwenye mapaja ya bibi yangu mara nyingi. Katika muda fulani mimi na kaka yangu tuliruhusiwa kuondoka kanisani kati ya mwisho wa shule ya Jumapili na ibada ya asubuhi ili kuketi pamoja na babu yetu kwenye uwanja wa reli na kutazama treni zikipita. Hakuwa mshiriki wa kanisa, lakini alihakikisha kwamba familia yangu inafika huko kila Jumapili. Muda fulani baadaye, alipatwa na kiharusi ambacho kilimfanya apooze baadhi ya sehemu, na kwa sababu hiyo, hatukuweza kuhudhuria kanisa kama kawaida. Kipindi hiki kitakuwa mojawapo ya hatua muhimu zaidi za maendeleo yangu.

Kujitolea Upya

Nilifarijika, kwa namna fulani, kwa kutoweza tena kuhudhuria kanisa, lakini nilihisi hamu ya kwenda peke yangu kila mara. Nikiwa na umri wa miaka kumi na sita, nilianza kuhudhuria kanisa la rafiki ambaye baba yake alikuwa kasisi. Lilikuwa jengo dogo lenye duka mbele ikiwa familia ya rafiki yangu, mimi, na mwanafunzi mwenzangu mwingine kama washiriki. Hii iliendelea kwa miezi kadhaa tu kabla ya kanisa kufungwa. Baada ya kuhitimu kutoka shule ya upili na kuingia chuo kikuu, niligundua tena ahadi yangu ya kidini na nikazama kabisa katika mafundisho ya Kipentekoste. Nilibatizwa na “kujazwa na Roho Mtakatifu,” kama tukio lilivyoitwa wakati huo. Nikiwa mwanafunzi wa chuo kikuu, haraka nikawa fahari ya kanisa. Kila mtu alikuwa na matumaini makubwa kwangu, na nilifurahi kuwa tena "kwenye njia ya wokovu".

Nilihudhuria kanisani kila mara milango yake ilipofunguliwa. Nilijifunza Biblia kwa siku na majuma. Nilihudhuria mihadhara iliyotolewa na wasomi wa Kikristo wa siku zangu, na nilikubali wito wangu wa huduma nikiwa na umri wa miaka 20. Nilianza kuhubiri na nikajulikana haraka sana. Nilikuwa na msimamo mkali sana na niliamini kwamba hakuna mtu angeweza kupokea wokovu isipokuwa awe katika kundi la kanisa langu. Nilimlaani vikali kila mtu ambaye hakuwa anamjua Mungu kama nilivyomjua mimi. Nilifundishwa kwamba Yesu Kristo (rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake) na Mwenyezi Mungu walikuwa kitu kimoja. Nilifundishwa kwamba kanisa letu haliamini utatu, lakini Yesu (rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake) kwa hakika alikuwa Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Nilijaribu kuelewa japo ilinibidi nikiri kuwa sikuelewa kabisa. Kwa kadiri nilivyojali, lilikuwa ni fundisho pekee lililokuwa na maana kwangu. Nilifurahishwa na mavazi matakatifu ya wanawake na tabia ya uchamungu za wanaume. Nilifurahia kufuata fundisho ambayo wanawake walitakiwa kuvaa mavazi ya kujifunika kabisa, si kujipaka vipodozi vya nyuso zao, na kujiwakilisha kama mabalozi wa kweli wa Kristo. Nilisadikishwa pasipo shaka yoyote kwamba hatimaye nilikuwa nimepata njia ya kweli ya raha ya milele. Nilijadiliana na mtu yeyote kutoka kwenye kanisa tofauti mwenye imani tofauti na kuwanyamazisha kabisa kwa ujuzi wangu wa Biblia. Nilikariri mamia ya vifungu vya Biblia, na hilo likawa alama kuu ya mahubiri yangu. Hata hivyo, ingawa nilihisi kuhakikishiwa kuwa kwenye njia sahihi, sehemu yangu fulani ilikuwa bado ikitafuta. Nilihisi kwamba kulikuwa na ukweli wa hali ya juu zaidi ambao unapaswa kupatikana.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.