Kenneth L. Jenkins, Mhudumu na Mzee wa Kanisa la Kipentekoste, Marekani (sehemu ya 2 kwa 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mvulana aliyewahi kupotoshwa anapata wokovu wake kupitia Kanisa la Kipentekoste na anajibu wito wake wa huduma akiwa na umri wa miaka 20, baadaye kuwa Mwislamu. Sehemu ya 2: "Kila kitu kinachong'aa si dhahabu."

  • Na Kenneth L. Jenkins
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,192 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Nilikuwa nikitafakari nikiwa peke yangu na kumwomba Mungu aniongoze kwenye dini sahihi na anisamehe ikiwa nilichokuwa nikifanya ni makosa. Sikuwahi kuwa na mawasiliano yoyote na Waislamu. Watu pekee niliowajua waliodai Uislamu kuwa dini yao walikuwa wafuasi wa Eliya Muhammad, ambao waliitwa na wengi kuwa “Waislamu Weusi” au “Taifa Lililopotea.” Ilikuwa ni katika kipindi hiki mwishoni mwa miaka ya sabini ambapo Mhudumu Louis Farrakhan alikuwa tayari kujenga upya kile kilichoitwa "Taifa la Uislamu." Nilikwenda kumsikiliza Mhudumu Farrakhan akizungumza kwa mwaliko wa mfanyakazi mwenzangu na nikaona kuwa ni uzoefu ambao ungebadilisha maisha yangu kwa kiasi kikubwa. Sikuwahi kamwe kumsikia mtu mweusi mwingine maishani mwangu akiongea vile. Mara moja nilitaka kupanga kukutana naye ili kujaribu kumgeuza kuwa dini yangu. Nilifurahia kueneza injili, nikitumaini kupata roho zilizopotea ili kuziokoa kutoka kwenye Moto wa Jahanamu - bila kujali walikuwa akina nani.

Baada ya kuhitimu kutoka chuo kikuu nilianza kufanya kazi ya kutwa nzima. Nilipokuwa nikifikia kilele cha huduma yangu, wafuasi wa Eliya Muhammad walionekana zaidi, na nilithamini jitihada zao katika kujaribu kuiondoa jumuiya ya watu weusi kutoka katika maovu yaliyokuwa yakiiangamiza kutoka ndani. Nilianza kuwaunga mkono, kwa njia fulani, kwa kununua mafundisho yao na hata kukutana nao kwa mazungumzo. Nilihudhuria masomo yao ili kujua ni nini hasa walichokuwa wanaamini. Kwa jinsi nilivyojua wengi wao walikuwa waaminifu, sikuweza kulikubali wazo la Mungu kuwa mtu mweusi. Sikukubaliana na matumizi yao ya Biblia ili kuunga mkono msimamo wao kuhusu masuala fulani. Hiki kilikuwa kitabu ambacho nilikijua vizuri sana, na nilisikitishwa sana na kile nilichoona ni tafsiri yao isiyo sahihi. Nilikuwa nimehudhuria shule za Biblia zinazotegemewa katika eneo letu na nilikuwa na ujuzi mwingi katika nyanja mbalimbali za mafunzo ya Biblia.

Baada ya miaka sita hivi, nilihamia Texas na nikajiunga na makanisa mawili. Kanisa la kwanza liliongozwa na mchungaji kijana ambaye hakuwa na uzoefu na hakuwa na elimu sana. Ujuzi wangu wa maandiko ya Kikristo kwa wakati huu ulikuwa umekua na kuwa kitu kisicho cha kawaida. Nilivutiwa sana na mafundisho ya Biblia. Nilianza kutazama kwa undani maandiko na kugundua kuwa nilijua zaidi ya kiongozi wa sasa. Ili kuonyesha heshima, niliondoka na kujiunga na kanisa lingine katika jiji tofauti ambako nilihisi kwamba ningeweza kujifunza zaidi. Mchungaji wa kanisa hili alikuwa msomi sana. Alikuwa mwalimu bora lakini alikuwa na mawazo ambayo hayakuwa ya kawaida katika shirika letu la kanisa. Alikuwa na maoni ya uhuru kwa kiasi fulani, lakini bado nilifurahia mafundisho yake. Muda si muda nilijifunza somo muhimu zaidi katika maisha yangu ya Kikristo, ambalo lilikuwa “kila kitu kinachong'aa si dhahabu.” Licha ya mwonekano wake wa nje, kulikuwa na maovu yakifanyika ambayo sikuwahi kufikiria kuwa yanawezekana katika Kanisa. Maovu haya yalinifanya kutafakari kwa kina, na nikaanza kutilia shaka mafundisho ambayo nilijitolea sana.

Karibu katika Ulimwengu Halisi wa Kanisa

Muda mchache niligundua kwamba kulikuwa na wivu mwingi ulioenea katika ngazi ya wahudumu. Mambo yalikuwa yamebadilika kutoka yale niliyoyazoea. Wanawake walivaa mavazi ambayo nilifikiri yalikuwa ya aibu. Watu wanavaa ili waangaliwe, kwa kawaida kutoka kwa jinsia tofauti. Niligundua pesa na tamaa kama sehemu kubwa katika uendeshaji wa shughuli za kanisa. Kulikuwa na makanisa mengi madogo yaliyokuwa yakihangaika, na walituita tufanye mikutano ili kusaidia kukusanya pesa kwa ajili yao. Niliambiwa kwamba ikiwa kanisa halina idadi fulani ya washiriki, basi sikupaswa kupoteza muda wangu kuhubiri huko kwa sababu nisingeweza pata pesa ya kutosha. Kisha nilieleza kwamba sikuwa na nia ya pesa na kwamba ningehubiri hata kama kulikuwa na mshiriki mmoja tu ... na ningefanya bila malipo! Hili lilisababisha usumbufu. Nilianza kuwahoji wale ambao nilifikiri walikuwa na hekima, nikagundua kuwa walikuwa wakifanya maonyesho. Nilijifunza kwamba pesa, mamlaka na cheo ni muhimu zaidi kuliko mafundisho ya kweli kuhusu Biblia. Nikiwa mwanafunzi wa Biblia, nilijua kabisa kwamba kulikuwa na makosa, mizozo na uzushi. Nilifikiri kwamba watu walipaswa kufunuliwa ukweli kuhusu Biblia. Wazo la kuwafunulia watu mambo hayo ya Biblia lilikuwa wazo linalodaiwa kuwa lilitokana na Shetani. Lakini nilianza kuwauliza walimu wangu maswali hadharani wakati wa madarasa ya Biblia, ambayo hakuna hata mmoja wao aliyeweza kuyajibu. Hakuna hata mmoja ambaye angeweza kueleza jinsi Yesu alidhaniwa kuwa Mungu, na jinsi, wakati huohuo, alidhaniwa kuwa Baba, Mwana na Roho Mtakatifu aliyefungwa katika umoja na bado hakuwa sehemu ya utatu. Wahubiri kadhaa hatimaye walilazimika kukiri kwamba hawakuielewa lakini tulitakiwa tu kuiamini.

Kesi za uzinzi na uasherati zilikwenda bila kuadhibiwa. Baadhi ya wahubiri walikuwa wameingizwa kwenye dawa za kulevya na walikuwa wameharibu maisha yao na ya familia zao. Viongozi wa baadhi ya makanisa walipatikana kuwa ni mashoga. Kulikuwa na wachungaji hata wenye hatia ya kufanya uzinzi na mabinti wadogo wa washiriki wengine wa kanisa. Haya yote pamoja na kushindwa kupata majibu ya yale niliyofikiri ni maswali halali yalitosha kunifanya nitafute mabadiliko. Mabadiliko hayo yalikuja nilipokubali kazi katika Ufalme wa Saudi Arabia.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.