Kenneth L. Jenkins, Mhudumu na Mzee wa Kanisa la Kipentekoste, Marekani (sehemu ya 3 kwa 3)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mvulana aliyewahi kupotoshwa anapata wokovu wake kupitia Kanisa la Kipentekoste na anajibu wito wake wa huduma akiwa na umri wa miaka 20, baadaye kuwa Muislamu. Sehemu ya 3: "Kuzaliwa kutoka gizani kuingia kwenye nuru."

  • Na Kenneth L. Jenkins
  • Iliyochapishwa mnamo 17 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,079 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Mwanzo Mpya

Haikupita muda mrefu baada ya kuwasili Saudi Arabia niliona tofauti ya mara moja katika mtindo wa maisha wa watu wa Kiislamu. Walikuwa tofauti na wafuasi wa Eliya Muhammad na Mhudumu Louis Farrakhan kwa kuwa walikuwa wa mataifa, rangi na lugha zote. Mara moja nilionyesha nia ya kujifunza zaidi kuhusu aina hii ya pekee ya dini. Nilishangazwa na maisha ya Mtume Muhammad na nilitaka kujua zaidi. Niliomba vitabu kutoka kwa mmoja wa ndugu ambaye alikuwa na bidii katika kuwalingania watu kwenye Uislamu. Nilipewa vitabu vyote ambavyo nilivitaka. Nilisoma kila kimoja. Kisha nikapewa Quran Tukufu na kuisoma mara kadhaa ndani ya miezi minne. Niliuliza swali baada ya swali na kupata majibu ya kuridhisha. Kilichonivutia ni kwamba ndugu hawakutaka kunivuta kwa ujuzi wao. Ikiwa ndugu hajui jibu la swali, aliniambia kwamba hajui na ingemlazimu kuuliza kwa mtu mwingine mwenye kujua. Siku iliyofuata alileta jibu. Niliona jinsi unyenyekevu ulivyochukua nafasi kubwa katika maisha ya watu hawa wa ajabu wa Mashariki ya Kati.

Nilishangaa kuona wanawake wakijifunika uso hadi miguu. Sikuona uongozi wowote wa kidini. Hakuna aliyekuwa akigombea nafasi yoyote ya kidini. Hayo yote yalikuwa ya ajabu, lakini ningewezaje kuwa na wazo la kuacha mafundisho ambayo yalikuwa yamenifuata tangu utotoni? Ni vipi kuhusu Biblia? Nilijua kwamba kuna ukweli ndani yake ingawa ilikuwa imebadilishwa na kusahihishwa mara kadhaa. Kisha nikapewa kaseti ya video ya mjadala kati ya Sheikh Ahmed Deedat na Mchungaji Jimmy Swaggart. Baada ya kuona mjadala huo mara moja nikawa Muislamu.

Nilipelekwa kwenye ofisi ya Sheikh Abdullah bin Abdulaziz bin Baz kutangaza rasmi kuukubali Uislamu. Hapo ndipo nilipopewa ushauri mzuri wa jinsi ya kujitayarisha kwa ajili ya safari ndefu iliyo mbele. Ilikuwa kuzaliwa kweli kutoka gizani kuingia kwenye nuru. Nilijiuliza wenzangu wa Kanisa watafikiria nini watakaposikia kwamba nimeukubali Uislamu. Haikupita muda nikagundua. Nilirudi Marekani kwa likizo na nilishutumiwa vikali kwa ajili ya “kutokuwa na imani”. Nilipigwa muhuri na lebo nyingi - kutoka mwasi hadi mtu aliyekataliwa. Watu waliambiwa na wanaojiita viongozi wa kanisa wasinikumbuke hata kwenye maombi. Ingawa inaweza kuonekana kuwa ya kushangaza, sikujisumbua hata kidogo. Nilifurahi sana kwamba Mungu Mweza-Yote, alikuwa amechagua kuniongoza ipasavyo bila kujali jambo lingine lolote.

Sasa nilitaka tu kuwa Muislamu anayejitolea kama nilivyokuwa Mkristo. Hii, bila shaka, ilimaanisha kujifunza. Niligundua kuwa mtu anaweza kukua vile anavyotaka katika Uislamu. Hakuna ukiritimba wa maarifa - ni bure kwa wote wanaotaka kupata fursa za kujifunza. Nilipewa seti ya Saheeh Muslim kama zawadi kutoka kwa mwalimu wangu wa Quran. Hapo ndipo nilipotambua haja ya kujifunza kuhusu maisha, maneno na mwenendo wa Mtume Muhammad, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake. Nilisoma na kujifunza mikusanyo mingi ya Hadiyth inayopatikana kwa Kiingereza. Nilitambua kwamba ujuzi wangu wa Biblia ulikuwa muhimu sana katika kushughulika na wale wenye malezi ya Kikristo. Maisha kwangu yamechukua maana mpya kabisa. Moja ya mabadiliko makubwa ya mtazamo ni matokeo ya kujua kwamba maisha haya lazima yatumike kwa ajili ya maandalizi ya maisha ya baadae. Ilikuwa pia uzoefu mpya kujua kwamba tunalipwa hata kwa nia yetu. Ukikusudia kufanya wema, basi utalipwa. Ilikuwa tofauti kabisa katika Kanisa. Mtazamo ulikuwa kwamba "njia ya Motoni imetengenezwa kwa nia njema." Hakukuwa na njia ya kushinda. Ikiwa ulitenda dhambi, basi ulipaswa kuungama kwa mchungaji, hasa ikiwa dhambi hiyo ilikuwa ni dhambi kubwa, kama vile uzinzi. Ulihukumiwa vikali kwa matendo yako.

Sasa na Baadae

Baada ya mahojiano na gazeti la Al-Madinah niliulizwa kuhusu shughuli zangu za sasa na mipango ya siku zijazo. Kwa sasa, lengo langu ni kujifunza Kiarabu na kuendelea kusoma ili kupata maarifa zaidi kuhusu Uislamu. Kwa sasa ninajishughulisha na fani ya dawah na naitwa kutoa mihadhara kwa wasio Waislamu ambao wanatoka katika malezi ya Kikristo. Ikiwa Mungu, Mwenyezi, atayalinda maisha yangu, natumaini kuandika zaidi juu ya somo la dini linganishi.

Ni wajibu wa Waislamu duniani kote kufanya kazi ya kueneza elimu ya Uislamu. Kama mtu ambaye nimetumia muda mwingi kama mwalimu wa Biblia, ninahisi hisia ya kipekee ya wajibu katika kuelimisha watu kuhusu makosa, migongano na hadithi za kubuni za kitabu kinachoaminiwa na mamilioni ya watu. Mojawapo ya furaha kuu ni kujua kwamba sihitaji kujihusisha katika mabishano makubwa na Wakristo, kwa sababu nilikuwa mwalimu ambaye alifundisha mbinu nyingi za mabishano wanazozitumia. Pia nilijifunza jinsi ya kubishana kwa kutumia Biblia kutetea Ukristo. Na wakati huo huo najua hoja za kupinga kila hoja ambazo sisi wahudumu tulikatazwa na viongozi wetu kuzijadili au kuzitoa.

Ni maombi yangu kwamba Mungu atusamehe ujinga wetu wote na atuongoze kwenye njia ya Peponi. Sifa njema zote ni za Mungu. Rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Mtume wa mwisho, Mtume Muhammad, familia yake, maswahaba zake, na wale wanaofuata uongofu wa kweli.

Kenneth_L._Jenkins__Minister_and_Elder_of_Pentecostal_Church__USA_(part_3_of_3)_001.gif

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.