Biblia Inakana Umungu wa Yesu (sehemu ya 5 kati ya 7): Paulo Aliamini Kwamba Yesu sio Mungu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Watu wengi hutumia maandishi ya Paulo kama uthibitisho kwamba Yesu ni Mungu. Lakini hii sio haki kwa Paulo, kwa sababu Paulo aliamini wazi kwamba Yesu sio Mungu.

  • Na Shabir Ally
  • Iliyochapishwa mnamo 19 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 5
  • Imetazamwa: 4,121 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Katika barua yake ya kwanza kwa Timotheo, Paulo aliandika hivi: “Nakuagiza, mbele za Mungu, na mbele za Yesu Kristo, na mbele za malaika wateule, uyashike maagizo haya...” (1 Timotheo 5:21).

Ni wazi kutokana na hili kwamba cheo cha Mungu kinatumika sio kwa Kristo Yesu, bali kwa mtu mwingine. Katika sura inayofuata, anatofautisha tena kati ya Mungu na Yesu anaposema: “Mbele za Mungu, ambaye huvipa vitu vyote uzima, na mbele ya Yesu Kristo, ambaye alitoa ushuhuda wake mbele ya Pontio Pilato...” (1 Timotheo 6:13).

Kisha Paulo akaendelea kusema juu ya kutokea kwa Yesu mara ya pili: “kufunuliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo, ambako Mungu atafanya kwa wakati wake.” (1 Timotheo 6:14-15).

Tena, cheo cha Mungu kimeondolewa kwa makusudi kutoka kwa Yesu. Kwa bahati mbaya, watu wengi hufikiri kwamba Yesu anapoitwa “Bwana” katika Biblia, hilo linamaanisha “Mungu.” Lakini katika Biblia cheo hiki kinamaanisha bwana au mwalimu, na kinaweza kutumika kumuita wanadamu (angalia 1 Petro 3:6).

Hata hivyo, lililo la maana zaidi ni kuona yale ambayo Paulo alisema kumhusu Mungu katika kifungu kifuatacho, ambacho kinaonyesha waziwazi kwamba Yesu sio Mungu: “Mungu, Mtawala aliyebarikiwa na wa pekee, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana, ambaye peke yake asiyekufa na anayeishi katika nuru isiyoweza kukaribiwa, ambaye hakuna mtu aliyemwona au anayeweza kumuona. Heshima na uwezo upo kwake milele.” ( 1 Timotheo 6:15-16 ).

Paulo alisema kwamba Mungu pekee ndiye asiyeweza kufa. Kutokufa maana yake hafi. Angalia kamusi yoyote. Sasa, yeyote anayeamini kwamba Yesu alikufa hawezi kuamini kwamba Yesu ni Mungu. Imani kama hiyo ingepingana na kile Paulo alisema hapa. Zaidi ya hayo, kusema kwamba Mungu alikufa ni kumkufuru Mungu. Ni nani angeiongoza dunia ikiwa Mungu angekufa? Paulo aliamini kwamba Mungu hafi.

Paulo pia alisema katika kifungu hicho kwamba Mungu anakaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa — kwamba hakuna mtu ambaye amemwona Mungu au anayeweza kumwona. Paulo alijua kwamba maelfu ya watu walikuwa wamemwona Yesu. Lakini Paulo alisema kwamba hakuna mtu aliyemwona Mungu, kwa sababu Paulo alikuwa na hakika kwamba Yesu sio Mungu. Hii ndiyo sababu Paulo aliendelea kufundisha kwamba Yesu hakuwa Mungu, bali kwamba alikuwa Kristo (angalia Matendo 9:22 na 18:5).

Alipokuwa mji wa Athens, Paulo alisema juu ya Mungu kuwa “Mungu aliyeufanya ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na nchi, wala hakai katika mahekalu yaliyojengwa kwa mikono.” (Matendo 17:24). Kisha akamtambulisha Yesu kuwa “mtu ambaye (mf. Mungu) amemchagua.” ( Matendo 17:31 ).

Ni wazi kwamba kwa Paulo, Yesu hakuwa Mungu, na angeshangaa kuona maandishi yake yakitumiwa kuthibitisha kinyume cha yale aliyoamini. Paulo hata alitoa ushahidi mahakamani akisema: “Nakiri kwamba nina mwabudu Mungu wa baba zetu...” (Matendo 24:14).

Pia alisema kwamba Yesu ni mtumishi wa Mungu huyo, kwa maana tunasoma hivi katika Matendo: “Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu.” (Matendo 3:13).

Kwa Paulo, Baba pekee ndiye Mungu. Paulo alisema kwamba kuna “Mungu mmoja na Baba wa wote...” (Waefeso 4:6). Paulo alisema tena: “...kwetu sisi Mungu ni mmoja tu, aliye Baba . . . na Bwana ni mmoja tu, Yesu Kristo...” (1 Wakorintho 8:6).

Barua ya Paulo kwa Wafilipi (Wafilipi 2:6-11) mara nyingi inanukuliwa kama uthibitisho kwamba Yesu ni Mungu. Lakini kifungu hicho hicho kinaonyesha kwamba Yesu sio Mungu. Kifungu hiki kinapaswa kukubaliana na Isaya 45:22-24 ambapo Mungu alisema kila goti lipigwe kwa Mungu, na kila ulimi ukiri kwamba haki na nguvu ziko kwa Mungu pekee yake. Paulo alifahamu fungu hili, kwani alilinukuu katika Warumi 14:11. Akijua hilo, Paulo alisema hivi: “Napiga magoti mbele ya Baba.” (Waefeso 3:14).

Barua kwa Waebrania (Waebrania 1:6) inasema kwamba malaika wa Mungu wanapaswa kumwabudu Mwana. Lakini kifungu hiki kinategemea Kumbukumbu ya Torati 32:43, katika toleo la Septuajinti la Agano la Kale. Kifungu hiki cha maneno hakiwezi kupatikana katika Agano la Kale kinachotumiwa na Wakristo hivi sasa, na toleo la Septuajinti halifikiriwi kuwa halali tena na Wakristo. Hata hivyo, hata toleo la Septuajinti, halisemi tumwabudu Mwana. Inasema waache Malaika wa Mungu wamwabudu Mungu. Biblia inasisitiza kwamba Mungu pekee ndiye anayepaswa kuabudiwa: “BWANA alipofanya agano na Waisraeli, aliwaamuru hivi: ‘Msiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuwatolea sadaka. Lakini BWANA, aliyewapandisha kutoka Misri kwa nguvu kuu na mkono ulionyoshwa, ndiye mtakaye msujudia. Utamsujudia na kumtolea sadaka. Mnapaswa kuwa waangalifu siku zote kuzishika amri na hukumu, sheria na amri alizowaandikia. Usiabudu miungu mingine. Msilisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine. Bali mwabuduni BWANA, Mungu wenu; ndiye atakayekuokoa na mkono wa adui zako wote.’” (2 Wafalme 17:35-39).

Yesu, ambaye amani iwe juu yake, aliamini katika hili, kwa maana pia alisisitiza katika Luka 4:8. Na Yesu naye akaanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu (angalia Mathayo 26:39). Paulo alijua kwamba Yesu alimwabudu Mungu (angalia Waebrania 5:7). Paulo alifundisha kwamba Yesu atabaki kuwa mtiifu kwa Mungu milele (angalia 1 Wakorintho 15:28).

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.