Biblia Inakana Umungu wa Yesu (sehemu ya 2 kati ya 7): Matendo ya Mitume

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Uthibitisho kutoka kwa Matendo ya Mitume kwamba Yesu hakuwa Mungu.

  • Na Shabir Ally
  • Iliyochapishwa mnamo 18 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 1
  • Imetazamwa: 4,238 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Yesu alifanya miujiza mingi, na bila shaka alisema mambo mengi ya ajabu juu yake mwenyewe. Watu fulani hutumia yale aliyosema na kufanya kuwa uthibitisho wa kwamba yeye ni Mungu. Lakini wanafunzi wake wa awali walioishi na kutembea pamoja naye, na walioshuhudia kwa macho yale aliyosema na kufanya, hawakufikia hitimisho hili.

Matendo ya Mitume katika Biblia yanaeleza kwa undani kazi ya wanafunzi katika kipindi cha miaka thelathini baada ya Yesu kuinuliwa mbinguni. Katika kipindi hiki chote hawamrejelei Yesu kuwa Mungu. Daima na kwa uthabiti wanatumia jina la cheo cha Mungu kurejelea mtu mwingine zaidi ya Yesu.

Petro akasimama pamoja na wale wanafunzi kumi na moja, akawaambia umati:

“Enyi watu wa Israeli, sikilizeni neno hili: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kati yenu kwa yeye, kama ninyi wenyewe mjuavyo.” (Matendo 2:22).

Kwa hiyo, Mungu ndiye aliyefanya miujiza hiyo kupitia Yesu ili kuwasadikisha watu kwamba Yesu aliungwa mkono na Mungu. Petro hakuona miujiza hiyo kuwa uthibitisho wa kwamba Yesu ni Mungu.

Kwa kweli, jinsi Petro anavyomtaja Mungu na Yesu huonyesha wazi kwamba Yesu sio Mungu. Kwa maana daima anageuza jina la Mungu kutoka kwa Yesu. Chukua marejeleo yafuatayo kwa mfano:

“Mungu amemfufua huyu Yesu…” (Matendo 2:32).

"Mungu amemfanya huyu Yesu mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo." (Matendo 2:36)

Katika vifungu vyote viwili, jina la Mungu limegeuzwa kutoka kwa Yesu. Basi kwa nini alifanya hivi, ikiwa Yesu alikuwa Mungu?

Kwa Petro, Yesu alikuwa mtumishi wa Mungu. Petro alisema:

“Mungu alimfufua mtumishi wake…” (Matendo 3:26).

Cheo cha mtumishi kinarejelea Yesu. Hili liko wazi kutokana na kifungu kilichotangulia ambapo Petro alisema:

"Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu." (Matendo 3:13).

Lazima Petro alijua kwamba Ibrahimu, Isaka, na Yakobo hawakuzungumza kamwe juu ya Mungu wa Utatu. Siku zote walizungumza juu ya Mungu kama Mungu pekee. Hapa, kama katika Mathayo 12:18, Yesu ni mtumishi wa Mungu. Mathayo anatuambia kwamba Yesu alikuwa mtumishi yule yule wa Mungu aliyetajwa katika Isaya 42:1. Kwa hiyo, kulingana na Mathayo na Petro, Yesu sio Mungu, bali mtumishi wa Mungu. Agano la Kale linasema tena na tena kwamba Mungu yuko peke yake (kama vile Isaya 45:5).

Wanafunzi wote wa Yesu walikuwa na maoni haya. Katika Matendo 4:24 tunaambiwa kwamba waumini walimwomba Mungu wakisema:

“...wakapaza sauti zao pamoja katika kumwomba Mungu. Wakasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu, wewe ndiye uliyeziumba mbingu na dunia na bahari na vyote vilivyomo.’”

Ni wazi kwamba yule waliyekuwa wakimuomba hakuwa Yesu, kwa sababu, mistari miwili baadaye, walimtaja Yesu kuwa

"...mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta." (Matendo 4:27).

Ikiwa Yesu alikuwa Mungu, wanafunzi wake walipaswa kusema hivyo waziwazi. Badala yake, waliendelea kuhubiri kwamba Yesu alikuwa Kristo wa Mungu. Tunaambiwa katika Matendo::

“Siku baada ya siku, katika hekalu kutoka nyumba kwa nyumba, hawakuacha kamwe kufundisha na kutangaza habari njema kwamba Yesu ndiye Kristo.” (Matendo 5:42).

Neno la Kigiriki “Kristo” ni cheo cha kibinadamu. Inamaanisha “Mtiwa-Mafuta.” Ikiwa Yesu alikuwa Mungu, kwa nini daima wanafunzi wangemrejelea kwa vyeo vya kibinadamu kama vile mtumishi na Kristo wa Mungu, na mara kwa mara watumie jina la cheo Mungu kwa yule aliyemfufua Yesu? Je, waliogopa wanadamu? Hapana! Walihubiri kweli kwa ujasiri bila kuogopa kufungwa au kuuawa. Walipokabiliwa na upinzani kutoka kwa wenye mamlaka, Petro alisema:

“Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu! Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu...” (Matendo 5:29-30).

Je, walikuwa wamepungukiwa na Roho Mtakatifu? Hapana! Waliungwa mkono na Roho Mtakatifu (angalia Matendo 2:3, 4:8, na 5:32). Walikuwa wakifundisha tu yale waliyokuwa wamejifunza kutoka kwa Yesu—kwamba Yesu hakuwa Mungu bali, mtumishi wa Mungu na Kristo.

Quran inathibitisha kwamba Yesu alikuwa Masihi (Kristo), na kwamba alikuwa mtumishi wa Mungu (angalia Quran Tukufu 3:45 na 19:30).

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.