Sunnah ni nini? (sehemu ya 2 kati ya 2): Sunnah katika Sheria ya Kiislamu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Makala fupi inayoelezea nini kinajumuisha Sunnah, na nafasi yake katika Sheria ya Kiislamu. Sehemu ya Pili: Jinsi Sunna inavyotofautiana na Kurani, na nafasi ya Sunnah katika Sheria ya Kiislamu.

  • Na The Editorial Team of Dr. Abdurrahman al-Muala (translated by islamtoday.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 29 Nov 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,126 (wastani wa kila siku: 4)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Tofauti kati ya Sunnah na Kurani

Kurani ndio msingi wa Sheria ya Kiislamu. Ni hotuba ya Mwenyezi Mungu ya kimiujiza iliyofunuliwa kwa Mtume, rehema na baraka za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kwa njia ya Malaika Gabrieli. Imepitishwa kwetu kwa minyororo mingi ya mamlaka hivyo ukweli wake wa kihistoria hauna shaka. Imeandikwa katika juzuu yake yenyewe, na usomaji wake ni aina ya ibada.

Sunnah, ni kila kitu isipokuwa Kurani kilichotoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu. Inafafanua na kutoa maelezo kwa sheria zinazopatikana katika Kurani. Pia inatoa mifano ya matumizi ya vitendo vya sheria hizi. Vile vile ni ufunuo wa moja kwa moja kutoka kwa Mwenyezi Mungu, au maamuzi ya Mtume ambayo yalithibitishwa kwa ufunuo. Kwa hiyo, chanzo cha Sunnah zote ni ufunuo.

Kurani ni ufunuo ambao unasomwa rasmi kama ibada, na Sunnah ni ufunuo ambao hausomwi rasmi. Sunnah, hata hivyo, ni kama Kurani kwa kuwa ni ufunuo unaopaswa kufuatwa na kuzingatiwa.

Kurani inapendekeza Sunnah kwa njia mbili. Kwa jambo moja, Kurani ina maneno kamili ya Mwenyezi Mungu, asili ya kimiujiza, hadi aya ya mwisho. Sunnah, hata hivyo, si lazima iwe na maneno halisi ya Mwenyezi Mungu, bali maana yake kama ilivyoelezwa na Mtume.

Nafasi ya Sunnah katika Sheria ya Kiislamu

Wakati wa uhai wa Mtume Kurani na Sunnah vilikuwa vyanzo pekee vya Sheria ya Kiislamu.

Kurani inatoa maamrisho ya jumla ambayo yaliunda msingi wa Sheria, bila kuingia katika maelezo yote na sheria ya pili, isipokuwa maagizo machache ambayo yamewekwa pamoja na kanuni za jumla. Maagizo haya hayawezi kubadilika kulingana na muda au kwa mabadiliko ya hali ya watu. Kurani vile vile, imekuja na kanuni za imani, imeweka matendo ya ibada, inataja hadithi za mataifa ya kale, na inatoa miongozo ya maadili.

Sunnah imekuja kwa kuafikiana na Kurani. Inafafanua maana ya kile kisichoeleweka katika maandiko, hutoa maelezo ya kile kinachoonyeshwa kwa maneno ya jumla, inabainisha kwa jumla, na inaelezea maagizo na malengo yake. Sunnah pia inakuja na maamrisho ambayo hayakutolewa na Kurani, lakini haya daima yanawiana na kanuni zake, na daima yanaendeleza malengo ambayo yameainishwa ndani ya Kurani.

Sunnah ni kielelezo cha kivitendo cha yale yaliyomo ndani ya Kurani. Usemi huu una sura nyingi. Wakati mwingine, huja kama kitendo kilichofanywa na Mtume. Wakati nyingine, ni kauli aliyoitoa akijibu jambo fulani. Wakati fulani, inachukua sura ya kauli au kitendo cha mmoja wa Maswahabah ambacho hakukizuiwa wala hakikukipingwa. Kinyume chake, alikaa kimya juu yake au alionyesha idhini yake kwa hilo.

Sunnah inaielezea na kuibainisha Kurani kwa njia nyingi. Inaeleza jinsi ya kufanya ibada na kutekeleza sheria ambazo zimetajwa katika Kurani. Mungu anawaamrisha waumini kusali bila kutaja nyakati ambazo maombi hayo yalipaswa kufanywa au namna ya kuyatekeleza. Mtume Mtukufu alilifafanua hili kupitia maombi yake mwenyewe na kwa kuwafundisha Waislamu jinsi ya kuswali. Akasema: “Swalini kama mlivyoniona nikiswali.”

Mwenyezi Mungu huifanya Hijja kuwa ni wajibu bila ya kueleza taratibu zake. Mtume wa Mwenyezi Mungu anafafanua hili kwa kusema:

“Fanyeni hajj kutoka kwangu”

Mwenyezi Mungu anaufanya ushuru wa Zakah kuwa ni wajibu bila ya kutaja ni aina gani ya mali na mazao yanayotozwa. Mungu pia hataji kiwango cha chini kabisa cha mali kinachofanya ushuru kuwa wa lazima. Sunnah, hata hivyo, inayaweka wazi haya yote.

Sunnah inabainisha kauli za jumla zinazopatikana ndani ya Kurani. Mungu anasema:

“Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Fungu la mwanamume ni kama fungu la wanawake wawili…” (Kurani 4:11)

Maneno haya ni ya jumla, yanatumika kwenye kila familia na kumfanya kila mtoto kuwa mrithi wa wazazi wake. Sunnah inaifanya hukumu hii kuwa maalum zaidi kwa kuwatenga watoto wa Mitume.Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema:

“Sisi Manabii hatuwachi urithi. Tunachoacha nyuma huwa ni sadaka.”

Sunnah zinaelezea kauli zisizo na sifa ndani ya Kurani. Mungu anasema:

“… na hamkupata maji, basi tayamamuni vumbi lilio safi, na mpake nyuso zenu na mikono yenu… (Kurani 5:6)

Aya haijataja sehemu ya mkono, kutoa fursa ya mtu kuuliza iwapo inafaa kupangusa mikono hadi kwenye kifundo au sehemu ya mbele ya mkono. Sunnah inabainisha hili kwa kuonyesha kuwa ni kwenye kifundo cha mkono kwa sababu hivi ndivyo alivyofanya Mtume wa Mwenyezi Mungu alipotawadha mkavu.

Sunnah pia inakuja ikisisitiza yale yaliyomo ndani ya Kurani au inatoa sheria ya pili kwa sheria iliyotajwa humo. Hii ni pamoja na Hadeeth zote zinazoashiria kuwa Swala, ushuru wa Zaka, saumu na kuhiji ni wajibu.

Mfano wa pale Sunnah inapotoa sheria saidizi kwa amri inayopatikana ndani ya Kurani ni hukumu inayopatikana katika Sunnah kwamba ni haramu kuuza tunda kabla halijaanza kuiva. Msingi wa sheria hii ni kauli ya Kurani:

Msile mali yenu baina yenu kwa dhulma, isipokuwa iwe biashara baina yenu kwa kuridhiana.

Sunnah ina hukumu ambazo hazikutajwa ndani ya Kurani na ambazo haziji kama ufafanuzi wa jambo lililotajwa ndani ya Kurani. Mfano wa hayo ni uharamu wa kula nyama ya punda na nyama ya wanyama wakali. Mfano mwingine wa hili ni uharamu wa kuoa mwanamke na shangazi yake kwa wakati mmoja. Hukumu hizi na nyinginezo zilizotolewa na Sunnah ni lazima zifuatwe.

Wajibu wa Kushikamana na Sunnah

Sharti la kuamini utume ni kukubali kuwa ni kweli kila alichosema Mtume wa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu aliwachagua Mitume wake miongoni mwa waja Wake ili kufikisha Sheria yake kwa wanadamu. Mungu anasema:

“…Mwenyezi Mungu ndiye Mjuzi kuliko wote kujua wapi anaweka ujumbe wake.…” (Kurani 6:124)

Mwenyezi Mungu pia anasema:

“…Basi lipo lolote juu ya Mitume isipo kuwa kubalighisha kwa uwazi?” (Kurani 16:35)

Mtume amehifadhiwa kutokana na upotovu katika matendo yake yote. Mungu ameulinda ulimi wake usiseme chochote isipokuwa ukweli. Mungu amevilinda viungo vyake visifanye lolote isipokuwa lililo sawa.

Mungu amemlinda dhidi ya kuonyesha kibali cha jambo lolote lililo kinyume na Sheria ya Kiislamu. Yeye ndiye aliyekamilika kwa uzuri zaidi kati ya Uumbaji wa Mungu. Hili liko wazi kutokana na jinsi Mwenyezi Mungu anavyomuelezea katika Kurani:

“Naapa kwa nyota inapo tua! Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea. Wala hatamki kwa matamanio. Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa.” (Kurani 53:1-4)

Tunaona katika Hadiyth kwamba hakuna hali yoyote, hata ijaribiwe vipi, ingeweza kumzuia Mtume kusema ukweli. Kuwa na hasira hakujawahi kuathiri hotuba yake. Hakusema uwongo hata alipokuwa akitania. Masilahi yake mwenyewe hayakumshawishi kamwe ktokusema ukweli. Lengo pekee ambalo alitafuta lilikuwa ni radhi ya Mwenyezi Mungu.

Abdullah b. Amr b. al-Aas alisimulia kwamba alikuwa akiandika kila alichosema Mtume wa Mwenyezi Mungu. Kisha watu wa kabila la Quraish wakamkataza kufanya hivyo, wakasema: "unaandika kila anachokisema Mtume wa Mwenyezi Mungu, naye ni mtu anayesema kwa matamnio na kwa hasira?”

Abdullah b. Amr aliacha kuandika na akamwambia hili Mtume wa Mwenyezi Mungu ambaye alimwambia:

“Andika, kwani kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mkononi Mwake, hakika ukweli utokao katika huu ndiyo haki." ... na kunyooshea kinywa chake.

Kurani, Sunnah, na makubaliano ya mafaqihi yote yanaelekeza kwenye ukweli wa kumtii Mtume wa Mwenyezi Mungu ni wajibu. Mwenyezi Mungu anasema katika Kurani:

“Enyi mlio amini! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. …” (Kurani 4:59)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.