Статьи / видео вы запросили еще не существует.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
O artigo / vídeo que você requisitou não existe ainda.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Статьи / видео вы запросили еще не существует.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
O artigo / vídeo que você requisitou não existe ainda.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
L'articolo / video che hai richiesto non esiste ancora.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
“Hakika Mwenyezi Mungu alimteua Adam na Nuhu na ukoo wa Ibrahim na ukoo wa Imran juu ya walimwengu wote. Ni wazao wao kwa wao; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kujua. Aliposema mke wa Imran: ‘Mola wangu Mlezi! Nimekuwekea nadhiri kilichomo tumboni mwangu kuwa wakfu; basi nikubalie. Hakika Wewe ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua.’ Basi alipomzaa alisema: ‘Mola wangu Mlezi! Nimemzaa mwanamke - na Mwenyezi Mungu anajua sana aliyemzaa - Na mwanamume si sawa na mwanamke. Na mimi nimemwita Maryamu. Nami namkinga kwako, yeye na uzao wake, uwalinde na Shetani aliyelaaniwa.'" (Kurani 3: 33-36)
“Tena Mola wake Mlezi akampokea kwa mapokeo mema na akamkuza makuzo mema, na akamfanya Zakariya awe mlezi wake. Kila mara Zakariya alipoingia chumbani kwake alimkuta na vyakula. Basi alimwambia: ‘Ewe Maryamu! Unavipata wapi hivi?’ Naye akasema: ‘Hivi vinatoka kwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hesabu.’” (Kurani 3:37)
“Na kumbuka pale malaika waliposema: ‘Ewe Maryamu! Kwa hakika Mwenyezi Mungu amekuteua, na akakutakasa, na akakutukuza kuliko wanawake wote.’ ‘Ewe Maryamu! Mnyenyekee Mola Mlezi wako na usujudu na uiname pamoja na wainamao.’ Hizi ni khabari za ghaibu tunazokufunulia; nawe hukuwa nao walipokuwa wakitupa kalamu zao nani wao atamlea Maryamu, na hukuwa nao walipokuwa wakishindana.” (Kurani 3:42-44)
“Na pale malaika waliposema: ‘Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana kwa) neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye heshima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa waliokaribishwa (kwa Mwenyezi Mungu).’ ‘Naye atazungumza na watu katika utoto wake na katika utuuzima wake, na atakuwa katika watu wema.’ Maryamu akasema: ‘Mola wangu Mlezi! Vipi nitampata mwana na hali hajanigusa mwanadamu?’ Mwenyezi Mungu akasema: ‘Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu huumba apendacho. Anapohukumu jambo, huliambia: Kuwa!’ Likawa. Na atamfunza kuandika na Hekima na Taurati na Injili. Na ni mtume kwa Wana wa Israili kuwaambia: ‘Mimi nimekujieni na ishara kutoka kwa Mola wenu Mlezi, ya kwamba nakuundieni kwa udongo kama sura ya ndege. Kisha nampuliza anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na ninawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa na wakoma, na ninawafufua maiti kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na ninakwambieni mnachokila na mnachoweka akiba katika nyumba zenu. Hakika katika haya ipo ishara kwenu ikiwa nyinyi ni wenye kuamini. Na ninasadikisha yaliyokuwa kabla yangu katika Taurati, na ili nikuhalalishieni baadhi ya yale mlioharimishiwa, na nimekujieni na ishara kutokana na Mola wenu Mlezi. Kwa hivyo mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini mimi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi na ni Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo njia Iliyonyooka.’” (Kurani 3:45-51)
“Na mtaje Maryamu katika Kitabu, pale alipojitenga na jamaa zake mahali upande wa mashariki. Na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea Roho wetu, akajifananisha kwake sawa na mtu. (Maryamu) akasema: ‘Hakika mimi najikinga kwa Mwingi wa Rehema aniepushe nawe, ukiwa ni mcha Mungu.’[1] (Malaika) akasema: ‘Hakika mimi ni mwenye kutumwa na Mola wako Mlezi ili nikubashirie tunu ya mwana aliyetakasika.’ (Maryamu) akasema: ‘Nitampataje mwana hali mwanadamu yeyote hajanigusa, wala mimi si kahaba?’ (Malaika) akasema: Ndio hivyo hivyo! Mola wako Mlezi amesema: ‘Haya ni mepesi kwangu! Na ili tumfanye kuwa ni ishara kwa watu, na rehema itokayo kwetu, na hilo ni jambo liliokwisha hukumiwa.’”[2] (Kurani 19:16-21)
“Na mwanamke aliyelinda uke wake, na tukampulizia katika roho yetu, na tukamfanya yeye na mwanawe kuwa ni ishara kwa walimwengu.”[3] (Kurani 21:91)
“Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali. Kisha uchungu ukampeleka kwenye shina la mtende; akasema: ‘Laiti ningelikufa kabla ya haya, na nikawa niliyesahaulika kabisa!’ Pakatangazwa kutoka chini yake: ‘Usihuzunike! Hakika Mola wako Mlezi amejaalia chini yako kijito kidogo cha maji! Na litikise kwako hilo shina la mtende, utakuangushia tende nzuri zilizo mbivu. Basi kula, na kunywa, na litue jicho lako. Na pindi ukimwona mtu yeyote basi sema: Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga; kwa hivyo leo sitasema na mtu.’ Akaenda naye (mwanawe) kwa jamaa zake amembeba. Wakasema: ‘Ewe Maryamu! Hakika umeleta kitu cha ajabu!’ ‘Ewe dada yake Harun! Baba yako hakuwa mtu muovu, wala mama yako hakuwa kahaba.’ Akawaashiria (mtoto). Wakasema: ‘Vipi tumsemeze aliye bado mdogo yumo katika mlezi.’ Akasema (Isa): ‘Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu, amenipa Kitabu na amenifanya Nabii.[4] Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo. Na ameniusia sala na zaka maadamu ni hai. Na nimtendee wema mama yangu. Wala hakunifanya niwe jeuri, mwovu. Na amani iko juu yangu siku niliyozaliwa, na siku nitakayokufa, na siku nitakayofufuliwa kuwa hai.’” (Kurani 19:22-33)
“Hakika mfano wa Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam; alimuumba kwa udongo kisha akamwambia: ‘Kuwa!’ Basi akawa.”[5] (Kurani 3:59)
“Na tukamfanya mwana wa Maryamu na mama yake kuwa ni ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipoinuka penye utulivu na chemchemu za maji.”[6] (Kurani 23:50)
“Na Mwenyezi Mungu amewapigia mfano wa walioamini - mkewe Firauni, aliposema: ‘Mola wangu Mlezi! Nijengee kwako nyumba Peponi, na uniokoe na Firauni na vitendo vyake, na uniokoe na watu madhalimu. Na Maryamu binti wa Imran, aliyelinda ubikira wake, na tukampulizia humo kutoka roho yetu, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi na Vitabu vyake, na alikuwa miongoni mwa watiifu.” (KuranI 66:11-12)
[1] Mwingi wa Rehema ni moja ya majina ya Mungu katika Kurani.
[2] Yesu ni ishara ya nguvu ya Mungu, ambapo Mungu aliwaonyesha watu kuwa angeweza kumuumba Isa bila baba, kama alivyomuumba Adam bila wazazi wowote. Yesu pia ni ishara kwamba Mungu ana uwezo wa kufufua watu wote baada ya wao kufa, kwani yule ambaye anaumba kutoka kutokuwepo kitu anaweza bila shida yoyote kurudisha uhai. Yeye pia ni ishara ya Siku ya Hukumu, wakati atakaporudi duniani na kumuua Masihi Dajali katika Nyakati za Mwisho wa dunia.
[3] Vivyo hivyo, kama vile Mungu alivyomuumba Adam bila baba wala mama, kuzaliwa kwa Isa kulitokana na mama bila baba. Ili jambo litokee, ilitosha Mungu kusema "Kuwa" na likawa; kwa sababu Mungu ana uwezo juu ya vitu vyote.
[4] Utume ni nafasi ya juu zaidi na yenye kuheshimika ambayo mwanadamu anaweza kuifikia. Mtume ni mtu anayepokea wahyi au ufunuo kutoka kwa Mungu kupitia Malaika Jibril.
[5] Adam aliumbwa wakati Mungu alisema, "Kuwa," na yeye kuwa bila baba wala mama. Vivyo hivyo Yesu aliumbwa kutokana na Neno la Mungu. Ikiwa mazazi ya ajabu ya Yesu yanamfanya kuwa Mungu, basi Adam anastahiki zaidi uungu huo kwa sababu Isa angalau alikuwa na mzazi mmoja, wakati Adam hakuwa na yeyote. Kwa kuwa Adam sio Mungu, vivyo hivyo Yesu sio Mungu, walakini wote ni watumishi wanyenyekevu wa Mungu.
[6] Hapa ndipo Maryamu alipojifungua Yesu.
Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.
Orodha yako ya historia ipo tupu.
Kwa nini kujiandikisha? Tovuti hii ina miundo kadhaa uliyoundwa mahsusi kwa ajili yako, kama vile: vipendwa vyako, historia yako, kutia alama makala ambazo umezitazama awali, kuorodhesha makala zilizochapishwa tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho, kubadilisha ukubwa wa herufi, na zaidi. Vipengele hivi vinatokana na vidakuzi na vitafanya kazi ipasavyo tu unapotumia kompyuta ile ile. Ili kuwezesha vipengele hivi kutoka kwa kompyuta yoyote, unapaswa kuingia wakati katika tovuti hii.
Tafadhali ingiza Jina lako la mtumiaji na anwani ya barua pepe kisha ubofye kitufe cha Tuma neno la siri. Utapokea neno la siri jipya hivi karibuni. Tumia neno la siri hili jipya kufikia tovuti.