Kisa cha Isa na Maryamu katika Kurani Tukufu (sehemu ya 1 kati ya 3): Maryamu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Mfululizo huu wa sehemu tatu una aya nyingi kutoka kwa Kurani Tukufu kuhusu Maryamu (Mama wa Isa) pamoja na kuzaliwa kwake, utoto wake, sifa zake za kibinafsi, na kuzaliwa kimiujiza kwa Isa.

  • Na IslamReligion.com
  • Iliyochapishwa mnamo 09 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 01 Jan 2024
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 4,061
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Kuzaliwa kwa Maryamu

The_Story_of_Jesus_and_Mary_in_the_Holy_Quran_(part_1_of_3)_001.jpg“Hakika Mwenyezi Mungu alimteua Adam na Nuhu na ukoo wa Ibrahim na ukoo wa Imran juu ya walimwengu wote. Ni wazao wao kwa wao; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye kujua. Aliposema mke wa Imran: ‘Mola wangu Mlezi! Nimekuwekea nadhiri kilichomo tumboni mwangu kuwa wakfu; basi nikubalie. Hakika Wewe ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua.’ Basi alipomzaa alisema: ‘Mola wangu Mlezi! Nimemzaa mwanamke - na Mwenyezi Mungu anajua sana aliyemzaa - Na mwanamume si sawa na mwanamke. Na mimi nimemwita Maryamu. Nami namkinga kwako, yeye na uzao wake, uwalinde na Shetani aliyelaaniwa.'" (Kurani 3: 33-36)

Wakati wa Utotoni wa Maryamu

“Tena Mola wake Mlezi akampokea kwa mapokeo mema na akamkuza makuzo mema, na akamfanya Zakariya awe mlezi wake. Kila mara Zakariya alipoingia chumbani kwake alimkuta na vyakula. Basi alimwambia: ‘Ewe Maryamu! Unavipata wapi hivi?’ Naye akasema: ‘Hivi vinatoka kwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hesabu.’” (Kurani 3:37)

Maryamu, Mnyenyekevu

“Na kumbuka pale malaika waliposema: ‘Ewe Maryamu! Kwa hakika Mwenyezi Mungu amekuteua, na akakutakasa, na akakutukuza kuliko wanawake wote.’ ‘Ewe Maryamu! Mnyenyekee Mola Mlezi wako na usujudu na uiname pamoja na wainamao.’ Hizi ni khabari za ghaibu tunazokufunulia; nawe hukuwa nao walipokuwa wakitupa kalamu zao nani wao atamlea Maryamu, na hukuwa nao walipokuwa wakishindana.” (Kurani 3:42-44)

Habari njema ya kuzaliwa mtoto mchanga

“Na pale malaika waliposema: ‘Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana kwa) neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye heshima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa waliokaribishwa (kwa Mwenyezi Mungu).’ ‘Naye atazungumza na watu katika utoto wake na katika utuuzima wake, na atakuwa katika watu wema.’ Maryamu akasema: ‘Mola wangu Mlezi! Vipi nitampata mwana na hali hajanigusa mwanadamu?’ Mwenyezi Mungu akasema: ‘Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu huumba apendacho. Anapohukumu jambo, huliambia: Kuwa!’ Likawa. Na atamfunza kuandika na Hekima na Taurati na Injili. Na ni mtume kwa Wana wa Israili kuwaambia: ‘Mimi nimekujieni na ishara kutoka kwa Mola wenu Mlezi, ya kwamba nakuundieni kwa udongo kama sura ya ndege. Kisha nampuliza anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na ninawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa na wakoma, na ninawafufua maiti kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na ninakwambieni mnachokila na mnachoweka akiba katika nyumba zenu. Hakika katika haya ipo ishara kwenu ikiwa nyinyi ni wenye kuamini. Na ninasadikisha yaliyokuwa kabla yangu katika Taurati, na ili nikuhalalishieni baadhi ya yale mlioharimishiwa, na nimekujieni na ishara kutokana na Mola wenu Mlezi. Kwa hivyo mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini mimi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi na ni Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo njia Iliyonyooka.’” (Kurani 3:45-51)

“Na mtaje Maryamu katika Kitabu, pale alipojitenga na jamaa zake mahali upande wa mashariki. Na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea Roho wetu, akajifananisha kwake sawa na mtu. (Maryamu) akasema: ‘Hakika mimi najikinga kwa Mwingi wa Rehema aniepushe nawe, ukiwa ni mcha Mungu.’[1] (Malaika) akasema: ‘Hakika mimi ni mwenye kutumwa na Mola wako Mlezi ili nikubashirie tunu ya mwana aliyetakasika.’ (Maryamu) akasema: ‘Nitampataje mwana hali mwanadamu yeyote hajanigusa, wala mimi si kahaba?’ (Malaika) akasema: Ndio hivyo hivyo! Mola wako Mlezi amesema: ‘Haya ni mepesi kwangu! Na ili tumfanye kuwa ni ishara kwa watu, na rehema itokayo kwetu, na hilo ni jambo liliokwisha hukumiwa.’”[2] (Kurani 19:16-21)

Utungaji mimba wa Bikira

“Na mwanamke aliyelinda uke wake, na tukampulizia katika roho yetu, na tukamfanya yeye na mwanawe kuwa ni ishara kwa walimwengu.”[3] (Kurani 21:91)

Kuzaliwa kwa Isa

“Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali. Kisha uchungu ukampeleka kwenye shina la mtende; akasema: ‘Laiti ningelikufa kabla ya haya, na nikawa niliyesahaulika kabisa!’ Pakatangazwa kutoka chini yake: ‘Usihuzunike! Hakika Mola wako Mlezi amejaalia chini yako kijito kidogo cha maji! Na litikise kwako hilo shina la mtende, utakuangushia tende nzuri zilizo mbivu. Basi kula, na kunywa, na litue jicho lako. Na pindi ukimwona mtu yeyote basi sema: Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga; kwa hivyo leo sitasema na mtu.’ Akaenda naye (mwanawe) kwa jamaa zake amembeba. Wakasema: ‘Ewe Maryamu! Hakika umeleta kitu cha ajabu!’ ‘Ewe dada yake Harun! Baba yako hakuwa mtu muovu, wala mama yako hakuwa kahaba.’ Akawaashiria (mtoto). Wakasema: ‘Vipi tumsemeze aliye bado mdogo yumo katika mlezi.’ Akasema (Isa): ‘Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu, amenipa Kitabu na amenifanya Nabii.[4] Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo. Na ameniusia sala na zaka maadamu ni hai. Na nimtendee wema mama yangu. Wala hakunifanya niwe jeuri, mwovu. Na amani iko juu yangu siku niliyozaliwa, na siku nitakayokufa, na siku nitakayofufuliwa kuwa hai.’” (Kurani 19:22-33)

“Hakika mfano wa Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam; alimuumba kwa udongo kisha akamwambia: ‘Kuwa!’ Basi akawa.”[5] (Kurani 3:59)

“Na tukamfanya mwana wa Maryamu na mama yake kuwa ni ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipoinuka penye utulivu na chemchemu za maji.”[6] (Kurani 23:50)

Ubora wa Maryamu

“Na Mwenyezi Mungu amewapigia mfano wa walioamini - mkewe Firauni, aliposema: ‘Mola wangu Mlezi! Nijengee kwako nyumba Peponi, na uniokoe na Firauni na vitendo vyake, na uniokoe na watu madhalimu. Na Maryamu binti wa Imran, aliyelinda ubikira wake, na tukampulizia humo kutoka roho yetu, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi na Vitabu vyake, na alikuwa miongoni mwa watiifu.” (KuranI 66:11-12)



Rejeleo la maelezo:

[1] Mwingi wa Rehema ni moja ya majina ya Mungu katika Kurani.

[2] Yesu ni ishara ya nguvu ya Mungu, ambapo Mungu aliwaonyesha watu kuwa angeweza kumuumba Isa bila baba, kama alivyomuumba Adam bila wazazi wowote. Yesu pia ni ishara kwamba Mungu ana uwezo wa kufufua watu wote baada ya wao kufa, kwani yule ambaye anaumba kutoka kutokuwepo kitu anaweza bila shida yoyote kurudisha uhai. Yeye pia ni ishara ya Siku ya Hukumu, wakati atakaporudi duniani na kumuua Masihi Dajali katika Nyakati za Mwisho wa dunia.

[3] Vivyo hivyo, kama vile Mungu alivyomuumba Adam bila baba wala mama, kuzaliwa kwa Isa kulitokana na mama bila baba. Ili jambo litokee, ilitosha Mungu kusema "Kuwa" na likawa; kwa sababu Mungu ana uwezo juu ya vitu vyote.

[4] Utume ni nafasi ya juu zaidi na yenye kuheshimika ambayo mwanadamu anaweza kuifikia. Mtume ni mtu anayepokea wahyi au ufunuo kutoka kwa Mungu kupitia Malaika Jibril.

[5] Adam aliumbwa wakati Mungu alisema, "Kuwa," na yeye kuwa bila baba wala mama. Vivyo hivyo Yesu aliumbwa kutokana na Neno la Mungu. Ikiwa mazazi ya ajabu ya Yesu yanamfanya kuwa Mungu, basi Adam anastahiki zaidi uungu huo kwa sababu Isa angalau alikuwa na mzazi mmoja, wakati Adam hakuwa na yeyote. Kwa kuwa Adam sio Mungu, vivyo hivyo Yesu sio Mungu, walakini wote ni watumishi wanyenyekevu wa Mungu.

[6] Hapa ndipo Maryamu alipojifungua Yesu.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

(Soma zaidi...) Ondoa