Ni nani aliyeanzisha Utatu? (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi wazo la Utatu lilivyoingizwa katika mafundisho ya Kikristo.

  • Na Aisha Brown (iiie.net)
  • Iliyochapishwa mnamo 19 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 2
  • Imetazamwa: 4,200
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Je! nini chanzo cha dhana ya Kikristo ya Utatu?

Who_Invented_the_Trinity_-_(part_1_of_2)_001.jpgDini tatu za monotheizimu- Uyahudi, Ukristo, na Uisilamu - zote zinakwenda sambamba katika wazo moja la kimsingi: imani katika Mungu kama Kiumbe Mkuu, Muumba na Mtegemezi wa Ulimwengu. Inayojulikana kama "tawhid" katika Uislamu, dhana hii ya Umoja wa Mungu ilisisitizwa na Musa katika kifungu cha Biblia kinachojulikana kama "Shema", au nguzo ya imani ya Kiyahudi:

“Sikieni, Waisraeli: Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja . ” (Kumbukumbu ya Torati 6: 4)

Ilirudiwa neno kwa neno karibu miaka 1500 baadaye na Yesu aliposema:

“... Amri ya kwanza ni hii, Sikieni, Waisraeli; Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja. ” (Marko 12:29)

Muhammad alikuja karibu miaka 600 baadaye, akileta ujumbe ule ule tena:

“Na Mungu wako ni Mungu Mmoja: hakuna Mungu ila Yeye ...” (Kurani 2:163)

Ukristo umejitenga kutoka kwenye dhana ya Umoja wa Mungu,ila , kuwa katika fundisho lisilo la uwazi na la kushangaza ambalo liliundwa wakati wa karne ya nne. Mafundisho haya, ambayo yanaendelea kuwa chanzo cha mabishano ndani na nje ya dini ya Kikristo, inajulikana kama Mafundisho ya Utatu. Kwa ufupi, mafundisho ya Kikristo ya Utatu yanasema kwamba Mungu ni umoja wa watu watatu wa kimungu - Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu - katika kiumbe mmoja wa kimungu.

Ikiwa dhana hiyo, inawekwa katika maneno ya kawaida, ina kutatanisha, lugha yenyewe ya maandiko halisi ya mafundisho haya inatatanisha zaidi katika jambo hili:

“... tunaabudu Mungu mmoja katika Utatu, na Utatu katika Umoja ... kwa maana kuna Mtu mmoja wa Baba, mwingine wa Mwana, mwingine wa Roho Mtakatifu wote ni mmoja ... sio miungu watatu, bali ni Mungu mmoja ... watu wote watatu hakika ni wa milele ... yeye, kwa hivyo, ambaye ataokolewa lazima afikirie juu ya Utatu ... ”(vifungu kutoka kwenye Imani ya Athanasius)

Ngoja tuliweke hii katika sura tofauti: mtu mmoja, Mungu Baba, pamoja na mtu mmoja, Mungu Mwana, pamoja na mtu mmoja, Mungu Roho Mtakatifu, ni sawa na mtu mmoja, Mungu ni nini? Je! Hiki nni Kingereza au hii ni upuuzi?

Inasemekana kuwa Athanasius, askofu aliyeunda mafundisho haya, alikiri kwamba kadri anavyoandika zaidi juu ya jambo hilo, ndivyo alivyokuwa na uwezo mdogo wa kutoa maoni yake juu yake.

Je! Fundisho hilo la kutatanisha lilianzaje?

Utatu ndani ya biblia

Marejeleo katika Bibilia juu ya Utatu wa viumbe vya kiungu hayaeleweki, kabisa.

Katika Mathayo 28:19, tunamwona Yesu akiwaambia wanafunzi wake kwenda nje na kuwahubiria mataifa yote. Wakati "Agano kuu" hili linataja watu watatu ambao baadaye wanakuwa sehemu ya Utatu, maneno "... kuwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu" ni wazi kabisa kuwa kuna nyongeza ya maandishi ya Biblia - ambayo sio maneno halisi ya Yesu - kama inavyoonekana katika mambo mawili:

1) ubatizo katika Kanisa la kwanza, kama ilivyojadiliwa na Paulo katika barua zake, ulifanywa tu kwa jina la Yesu; na

2) "Agizo Kuu" lilipatikana katika injili ya kwanza iliyoandikwa, ile ya Marko, haimtaji Baba, Mwana, na/au Roho Mtakatifu - angalia Marko 16:15.

Rejeo lingine pekee katika Biblia juu ya Utatu linaweza kupatikana katika Waraka wa 1 Yohana 5:7. Wasomi wa kibiblia wa leo, hata hivyo, wamekubali kifungu hicho kuwa:

“...kuna watatu wanaoshuhudia mbinguni, Baba, Neno, na Roho Mtakatifu: na hawa watatu ni mmoja”

…hakika ni "nyongeza ya baadaye" kwenye maandishi ya Kibiblia, na haipatikani katika matoleo yoyote ya leo ya Biblia.

Kwa hivyo, inaweza kuonekana kuwa wazo la Utatu wa viumbe wa kimungu halikuwa wazo lililowekwa na Yesu au nabii mwingine yeyote wa Mungu. Fundisho hili, ambalo sasa limesajiliwa na Wakristo kote ulimwenguni, limeundwa kabisa na wanadamu.

Mafundisho yanachukua Sura

Ilhali Paulo wa Tarso, mtu ambaye angehesabiwa kuwa mwanzilishi wa kweli wa Ukristo, aliunda mafundisho yake mengi, ile ya Utatu haikuwa kati yao. Hata hivyo, aliweka msingi alipoweka wazo la Yesu kuwa "Mwana wa kimungu". Baada ya yote, Mwana anahitaji Baba, na vipi kuhusu usafiri kwa Mungu kuwa ufunuo kwa mwanadamu? Kwa asili, Paulo aliwataja wafanyaji wakuu, lakini ni watu wa Kanisa la baadaye ambao waliliweka jambo hilo kwa pamoja.

Tertullian, mwanasheria na mkuu wa kanisa la karne ya tatu huko Carthage, alikuwa wa kwanza kutumia neno "Utatu" wakati akiweka nadharia ya kuwa Mwana na Roho wanashiriki kuwa Mungu, lakini wote wakiwa kitu kimoja na Baba.

Mbaya Nzuri zaidi

Ni nani aliyeanzisha Utatu? (sehemu ya 2 kwa 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi mafundisho yaliyoingizwa ya utatu yalibaki kuwa sehemu ya imani ya Wakristo na jinsi Uislamu unavyomfafanua Mungu.

  • Na Aisha Brown (iiie.net)
  • Iliyochapishwa mnamo 19 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 0
  • Imetazamwa: 3,545
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Mafundisho Kamili Yamewekwa

Wakati wa mabishano juu ya suala la Utatu yalipoibuka mnamo 318 kati ya wanaume wawili wa kanisa kutoka Alexandria - Arius, shemasi, na Alexander, askofu wake - Mfalme Constantine aliingia kwenye mzozo.

Ingawa fundisho la Kikristo lilikuwa halieleweki kikamilifu kwake, alitambua kuwa kanisa lenye umoja lilikuwa la muhimu katika ufalme wenye nguvu. Pindi mazungumzo yaliposhindwa kumaliza mzozo huo, Konstantino alitaka baraza la kwanza la kiekumene katika historia ya Kanisa ili kumaliza suala hilo mara moja.

Wiki sita baada ya maaskofu 300 kukusanyika kwa mara ya kwanza huko Nicea mnamo 325, fundisho la Utatu lilipigiliwa nyundo. Mungu wa Wakristo sasa alionekana kuwa na asili tatu, au maumbile, katika hali ya Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu.

Kanisa Kuweka Miguu Chini

Jambo hilo lilikuwa halijamalizika, hata hivyo, licha ya matumaini makubwa kwa Konstantino. Arius na askofu mpya wa Alexandria, mwanamume anayeitwa Athanasius, walianza kubisha juu ya jambo hilo hata wakati ule Imani ya Nicene ilipokuwa ikisainiwa; "Arianism" likawa neno la kuvutia kuanzia wakati huo na kuendelea kwa mtu yeyote ambaye hakushikilia mafundisho ya Utatu.

Ilikuwa hadi 451, katika Baraza la Chalcedon, kwa idhini ya Papa, Imani ya Nicene/ Konstantinopoli iliwekwa kama kimamlaka. Mjadala juu ya suala hilo haukuvumiliwa tena; kusema kwa kupingana na Utatu sasa lilionekana kama kufuru, na jambo kama hilo lilipata hukumu kali ambazo zilitokana na kuchinjwa hadi kifo. Wakristo sasa waliwageukia Wakristo, kuwafanya vilema na kuua maelfu kwa sababu ya tofauti ya maoni.

Mjadala Unaendelea

Adhabu za kikatili na hata kifo hazikuzuia mabishano juu ya mafundisho ya Utatu, hata hivyo, na utata huo unaendelea hata leo.

Wakristo wengi, wanapoulizwa kuelezea fundisho hili la kimsingi la imani yao, hawawezi kutoa chochote zaidi ya "Ninaiamini kwa sababu niliambiwa nifanye hivyo." Inaelezewa kama "siri" - lakini Biblia inasema katika 1 Wakorintho 14:33 kuwa:

“... Mungu sio mwandishi wa kutatiza...”

Dhehebu la Waunitaria la Ukristo limeyaweka hai mafundisho ya Arius kwa kusema kuwa Mungu ni mmoja; hawaamini Utatu. Kwa sababu hiyo, Wakristo wa kawaida huwachukia, na Baraza la Makanisa la Kitaifa limekataa kuwaingiza. Katika Uunitariani, tumaini linahifadhiwa kuwa Wakristo siku moja watarudi kwenye mahubiri ya Yesu:

“... Msujudie Bwana Mungu wako, na umwabudu yeye peke yake.” (Luka 4:8)

Uislamu na suala la Utatu

Wakati Ukristo wanakuwa na tatizo la kufafanua asili ya Mungu, haipo hivyo kwenye Uislamu:

“Kwa hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni wa tatu wa Utatu. Hali hakuna mungu ila Mungu Mmoja.” (Kurani 5:73)

Ni vizuri Ikumbukwe kuwa Biblia ya lugha ya Kiarabu hutumia jina "Allah" kama jina la Mungu.

Suzanne Haneef, katika kitabu chake "Nini Kila Mtu Anapaswa Kujua Kuhusu Uislamu na Waislamu" (Maktaba ya Uislam, 1985), anaweka jambo hilo kwa ufasaha kabisa anaposema:

“Lakini Mungu si kama pai au tufaha ambalo linaweza kugawanywa katika theluthi tatu ambazo hutengeneza moja kamili; ikiwa Mungu ni nafsi tatu au ana sehemu tatu, hakika yeye sio wa mmoja, wa kipekee, kiumbe asiyegawanyika ambavyo Mungu yupo na ambaye Ukristo unadai kuamini.”[1]

Ukiiangalia katika upande mwingine, Utatu unamtaja Mungu kama vitu vitatu tofauti - Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Ikiwa Mungu ni Baba na pia ni Mwana, basi atakuwa Baba yake mwenyewe kwa sababu Yeye ni Mwanawe mwenyewe. Hii haina mantiki kabisa.

Ukristo unadai kuwa dini ya monotheazimu. Monotheazimu, hata hivyo, ina imani yake ya kimsingi kwamba Mungu ni Mmoja; fundisho la Kikristo la Utatu-Mungu akiwa Tatu-kwa-Mmoja - linaonekana na Uislam kama aina ya ushirikina. Wakristo hawaheshimu Mungu Mmoja tu, wanawaheshimu watatu.

Hili ni shtaka ambalo halichukuliwi kirahisi na Wakristo, hata hivyo. Wao, kwa upande wao, wanawashutumu Waislamu kwa kutojua hata Utatu ni nini, wakisema kwamba Quran inaiweka kama Mwenyezi Mungu Baba, Yesu Mwana, na Mariamu mama yake. Wakati kumwabudu Mariamu imekuwa sifa ya Kanisa Katoliki tangu 431 Pindi alipopewa jina la "Mama wa Mungu" na Baraza la Efeso, uchunguzi wa karibu wa mistari katika Kurani mara nyingi inatajwa na Wakristo kuunga mkono mashtaka yao, inaonyesha kwamba kumtaja Mariamu katika Kurani kama "mshirika" wa Utatu, sio kweli .

Wakati ambapo Kurani inalaani Utatu ( Kurani 4:171; 5:73)[2] na ibada ya Yesu na mama mariamu (Kurani 5:116)[3], hakuna sehemu inayotambua Utatu wa Kikristo. Msimamo wa Kurani ni kwamba NANI au NINI yanayo husissha mafundisho haya sio swala la umuhimu; la muhimu ni kwamba dhana ya Utatu ni dharau dhidi ya dhana ya Mungu Mmoja.

Kwa kumalizia, tunaona kuwa mafundisho ya Utatu ni dhana iliyobuniwa na mwanadamu; hamna ruhusa yoyote iliyotoka kwa Mungu kuhusu jambo hilo kwa sababu tu wazo zima la Utatu wa viumbe wa kiungu halina nafasi katika imani ya Mungu mmoja. Katika Kurani, Ufunuo wa Mwisho wa Mungu kwa wanadamu, tunaona msimamo wake umeelezewa wazi wazi katika vifungu kadhaa kwa ufasaha:

“... Mungu wenu ni Mungu Mmoja. Mwenye kutaraji kukutana na Mola wake Mlezi basi naatende vitendo vyema, wala asimshirikishe yeyote katika ibada ya Mola wake Mlezi. ” (Kurani 18:110)

“... Wala usimweke pamoja na Mwenyezi Mungu mungu mwengine, usije ukatupwa katika Jahannamu ukilaumiwa na kufurushwa.” (Kurani 17:39)

– kwa sababu, Mungu anatuambia tena na tena katika Ujumbe ambao umeungwa mkono katika Maandiko Yake Yote Yaliyofunuliwa:

“...Mimi ni Mola wenu Mlezi. Kwa hivyo niabuduni Mimi ...” (Kurani 21:92)



Rejeleo la maelezo:

[1] What Everyone Should Know About Islam and Muslims (Maktaba ya Kiislamu, 1985) (uk. 183-184)

[2]Enyi Watu wa Kitabu! Msipite kiasi katika dini yenu, wala msimseme Mwenyezi Mungu ila kwa lilio kweli. Hakika Masihi Isa mwana wa Maryamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na neno lake tu alilo mpelekea Maryamu, na ni roho iliyo toka kwake. Basi Muaminini Mwenyezi Mungu na Mitume wake. Wala msiseme: Utatu. Komeni! Itakuwa kheri kwenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mungu mmoja tu. Ametukuka Yeye na kuwa na mwana. Ni vyake Yeye vyote viliomo katika mbingu na katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu ni Mtegemewa wa kutosha.” (Kurani 4:171)

[3] “Na pale Mwenyezi Mungu atakapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Ati wewe uliwaambia watu: Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu? (Na Isa) atasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hainifalii mimi kusema ambayo si haki yangu. Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwisha yajua. Wewe unayajua yaliyo ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo katika nafsi yako. Hakika Wewe ndiye Mjuzi mkubwa wa yaliyo fichikana.’ (Kurani 5:116)

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.