Ni nani aliyeanzisha Utatu? (sehemu ya 1 kati ya 2)

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Jinsi wazo la Utatu lilivyoingizwa katika mafundisho ya Kikristo.

  • Na Aisha Brown (iiie.net)
  • Iliyochapishwa mnamo 19 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 18 Nov 2021
  • Ilichapishwa: 2
  • Imetazamwa: 4,187 (wastani wa kila siku: 5)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

Je! nini chanzo cha dhana ya Kikristo ya Utatu?

Who_Invented_the_Trinity_-_(part_1_of_2)_001.jpgDini tatu za monotheizimu- Uyahudi, Ukristo, na Uisilamu - zote zinakwenda sambamba katika wazo moja la kimsingi: imani katika Mungu kama Kiumbe Mkuu, Muumba na Mtegemezi wa Ulimwengu. Inayojulikana kama "tawhid" katika Uislamu, dhana hii ya Umoja wa Mungu ilisisitizwa na Musa katika kifungu cha Biblia kinachojulikana kama "Shema", au nguzo ya imani ya Kiyahudi:

“Sikieni, Waisraeli: Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja . ” (Kumbukumbu ya Torati 6: 4)

Ilirudiwa neno kwa neno karibu miaka 1500 baadaye na Yesu aliposema:

“... Amri ya kwanza ni hii, Sikieni, Waisraeli; Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja. ” (Marko 12:29)

Muhammad alikuja karibu miaka 600 baadaye, akileta ujumbe ule ule tena:

“Na Mungu wako ni Mungu Mmoja: hakuna Mungu ila Yeye ...” (Kurani 2:163)

Ukristo umejitenga kutoka kwenye dhana ya Umoja wa Mungu,ila , kuwa katika fundisho lisilo la uwazi na la kushangaza ambalo liliundwa wakati wa karne ya nne. Mafundisho haya, ambayo yanaendelea kuwa chanzo cha mabishano ndani na nje ya dini ya Kikristo, inajulikana kama Mafundisho ya Utatu. Kwa ufupi, mafundisho ya Kikristo ya Utatu yanasema kwamba Mungu ni umoja wa watu watatu wa kimungu - Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu - katika kiumbe mmoja wa kimungu.

Ikiwa dhana hiyo, inawekwa katika maneno ya kawaida, ina kutatanisha, lugha yenyewe ya maandiko halisi ya mafundisho haya inatatanisha zaidi katika jambo hili:

“... tunaabudu Mungu mmoja katika Utatu, na Utatu katika Umoja ... kwa maana kuna Mtu mmoja wa Baba, mwingine wa Mwana, mwingine wa Roho Mtakatifu wote ni mmoja ... sio miungu watatu, bali ni Mungu mmoja ... watu wote watatu hakika ni wa milele ... yeye, kwa hivyo, ambaye ataokolewa lazima afikirie juu ya Utatu ... ”(vifungu kutoka kwenye Imani ya Athanasius)

Ngoja tuliweke hii katika sura tofauti: mtu mmoja, Mungu Baba, pamoja na mtu mmoja, Mungu Mwana, pamoja na mtu mmoja, Mungu Roho Mtakatifu, ni sawa na mtu mmoja, Mungu ni nini? Je! Hiki nni Kingereza au hii ni upuuzi?

Inasemekana kuwa Athanasius, askofu aliyeunda mafundisho haya, alikiri kwamba kadri anavyoandika zaidi juu ya jambo hilo, ndivyo alivyokuwa na uwezo mdogo wa kutoa maoni yake juu yake.

Je! Fundisho hilo la kutatanisha lilianzaje?

Utatu ndani ya biblia

Marejeleo katika Bibilia juu ya Utatu wa viumbe vya kiungu hayaeleweki, kabisa.

Katika Mathayo 28:19, tunamwona Yesu akiwaambia wanafunzi wake kwenda nje na kuwahubiria mataifa yote. Wakati "Agano kuu" hili linataja watu watatu ambao baadaye wanakuwa sehemu ya Utatu, maneno "... kuwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu" ni wazi kabisa kuwa kuna nyongeza ya maandishi ya Biblia - ambayo sio maneno halisi ya Yesu - kama inavyoonekana katika mambo mawili:

1) ubatizo katika Kanisa la kwanza, kama ilivyojadiliwa na Paulo katika barua zake, ulifanywa tu kwa jina la Yesu; na

2) "Agizo Kuu" lilipatikana katika injili ya kwanza iliyoandikwa, ile ya Marko, haimtaji Baba, Mwana, na/au Roho Mtakatifu - angalia Marko 16:15.

Rejeo lingine pekee katika Biblia juu ya Utatu linaweza kupatikana katika Waraka wa 1 Yohana 5:7. Wasomi wa kibiblia wa leo, hata hivyo, wamekubali kifungu hicho kuwa:

“...kuna watatu wanaoshuhudia mbinguni, Baba, Neno, na Roho Mtakatifu: na hawa watatu ni mmoja”

…hakika ni "nyongeza ya baadaye" kwenye maandishi ya Kibiblia, na haipatikani katika matoleo yoyote ya leo ya Biblia.

Kwa hivyo, inaweza kuonekana kuwa wazo la Utatu wa viumbe wa kimungu halikuwa wazo lililowekwa na Yesu au nabii mwingine yeyote wa Mungu. Fundisho hili, ambalo sasa limesajiliwa na Wakristo kote ulimwenguni, limeundwa kabisa na wanadamu.

Mafundisho yanachukua Sura

Ilhali Paulo wa Tarso, mtu ambaye angehesabiwa kuwa mwanzilishi wa kweli wa Ukristo, aliunda mafundisho yake mengi, ile ya Utatu haikuwa kati yao. Hata hivyo, aliweka msingi alipoweka wazo la Yesu kuwa "Mwana wa kimungu". Baada ya yote, Mwana anahitaji Baba, na vipi kuhusu usafiri kwa Mungu kuwa ufunuo kwa mwanadamu? Kwa asili, Paulo aliwataja wafanyaji wakuu, lakini ni watu wa Kanisa la baadaye ambao waliliweka jambo hilo kwa pamoja.

Tertullian, mwanasheria na mkuu wa kanisa la karne ya tatu huko Carthage, alikuwa wa kwanza kutumia neno "Utatu" wakati akiweka nadharia ya kuwa Mwana na Roho wanashiriki kuwa Mungu, lakini wote wakiwa kitu kimoja na Baba.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.