Uislam ni nini? (sehemu ya 1 kati ya 4): Msingi wa Uislamu

Ukadiriaji:
Ukubwa wa herufi:
A- A A+

Maelezo: Ujumbe wa Uislamu ni sawa sawa na msingi wa ujumbe uliofunuliwa na dini zote, kwakuwa zote zimetoka katika asili moja, na sababu zinazopatikana katika dini.

  • Na M. Abdulsalam (© 2006 IslamReligion.com)
  • Iliyochapishwa mnamo 06 Dec 2021
  • Ilirekebishwa mara ya mwisho mnamo 23 Oct 2023
  • Ilichapishwa: 13
  • Imetazamwa: 9,270 (wastani wa kila siku: 11)
  • Ukadiriaji: bado hakuna
  • Imekadiriwa na: 0
  • Imetumwa kwa barua pepe: 0
  • Ilitoa maoni kuhusu: 0
Mbaya Nzuri zaidi

What_is_Islam_(part_1_of_4)_001.jpgMiongoni mwa baraka na upendeleo ambao amewapa wanadamu ni kuwa Amewajaalia uwezo wa asili wa kutambua na kujua uwepo Wake. Aliweka ufahamu huu chini kabisa ya mioyo yao kama tabia ya asili ambayo haijabadilika tangu mwanzo wa mwanadamu alipoumbwa. Aidha, Ameiweka tabia hii ya asili na ishara ambazo ameziweka kwenye uumbaji ambazo zinathibitisha uwepo Wake. Lakini, kwakuwa haiwezekani kwa mwanadamu kuwa na maarifa ya kina juu ya Mungu isipokuwa kupitia ufunuo kutoka Kwake Yeye Mwenyewe, Mungu ametuma Wajumbe wake ili kuwafundisha watu kuhusu Muumbaji wao wanaotakiwa kumuabudu. Wajumbe hawa pia wameleta maelezo ya jinsi ya kumuabudu Mungu, sababu maelezo hayo hayawezi kujulikana isipokuwa kwa njia ya ufunuo. Misingi hii miwili ilikuwa vitu muhimu ambavyo Wajumbe wa funuo zote za Mungu walizileta kutoka kwa Mungu. Kwa msingi huu, funuo zote za Mungu zimekuwa na malengo yale yale, ambayo ni:

1. Kuthibitisha Umoja wa Mungu - Muumba wa kusifiwa na kutukuzwa – Katika asili Yake na sifa Zake.

2. Kuthibitisha Mungu peke yake ndiye anapaswa kuabudiwa na hakuna kuabudu kiumbe chochote sambamba na Yeye au badala Yake.

3. Kulinda maslahi ya mwanadamu na kupinga ufisadi na uovu. Hivyo, kila kitu kinacholinda imani, maisha, hoja, utajiri na kizazi ni sehemu ya maslahi ya mwanadamu huyu ambaye dini hulinda. Katika mkono mwingine, kitu chochote ambacho kinahatarisha mahitaji haya muhimu ni njia ya ufisadi ambayo dini inapinga na kukataza.

4. Kuwaalika watu kwa fadhila ya hali ya juu, maadili, na desturi safi.

Lengo la msingi la Ujumbe wa Mungu limekuwa lile lile: kuwaongoza watu kwa Mungu, kuwafanya wamjue Yeye, na kuwafanya wamuabudu Yeye. Kila Ujumbe wa Mungu umekuja kuiwekea nguvu maana hii, na maneno haya yafuatayo yalirudiwa katika ndimi za Wajumbe wote: “Muabuduni Mungu, hakuna mungu zaidi Yake.” Ujumbe huu ulifikishwa kwake mwanadamu kwa kupitia Manabii na Mitume ambayo Mungu aliwatuma Kila nchi. Wajumbe hawa wote walikuja na ujumbe ule ule, Ujumbe wa Uislamu.

Jumbe zote za Mungu zimekuja kufanya maisha ya watu katika kukubali kurudi kwa Mungu. Kwa sababu hii, zote zinachangia katika jina la “Uislamu”, au “Kumrudia” lililoletwa kutoka neno moja kama “Salam”, au “amani”, kwa Kiarabu. Uislamu, kwa maana hii, ilikuwa dini ya mitume yote, ila kwanini mmoja anaona aina tofauti tofauti za dini ya Mungu ikiwa zote zinatoka katika asili moja? Majibu yako mawili.

Sababu ya kwanza ni matokeo ya muda kupita, na kwa ukweli kwamba dini zilizopita hazikuwa katika ulinzi wa Mungu, zimepitia mabadiliko mengi na aina. Matokeo yake, tunaona msingi wa ukweli ambao uliletwa na wajumbe wote sasa unatofautiana kutoka kwa mmoja hadi mwingine, mbainisho wa wazi kabisa ni ukali wa imani ya kumuabudia Mungu na Mungu peke yake.

Sababu ya pili kwa aina hizi ni kwamba Mungu, katika Hekima yake ya milele na Mapenzi ya milele, alituma kazi zote za Kimungu kabala ya ujumbe wa mwisho wa Uislam ulioletwa na Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, kuwa katika wakati maalumu. Matokeo yake, sheria na mbinu zao ziliendana na hali mahususi za watu ambao walitumwa kuwaambia.

Mwanadamu amepitia vipindi vingi vya kuongozwa, kutokuongozwa, uadilifu, na kupotoka, kuanzia kipindi cha jamii isiyojitambua hadi jamii inayojitambua. Muongozo wa Mungu uliambatana na mwanadamu katika haya yote, mara zote kupata suluhisho sahihi na kuponya.

Hii ilikuwa kiini cha kuwepo utofauti baina ya dini mbali mbali. Kutokukubaliana huku kamwe hakuendi zaidi ya Sheria za Mungu. Kila ufunuo wa Sheria unaeleza matatizo fulani ya watu walio kusudiwa. Ila, sehemu zinazokubaliana ni kubwa na nyingi, kama vile msingi wa imani; kanuni na malengo ya Sheria za Mungu, kama vile kulinda imani, maisha, hoja, utajiri, na kizazi na kusimamia haki katika nchi. ; na baadhi ya makatazo ya kimsingi, baadhi ya haya yenye umuhimu ni ibada ya masanamu, uasherati, mauaji, wizi, na kutoa ushahidi wa uongo. Ila, pia hukubaliana katika maadili mema kama ukweli, haki, sadaka, ukarimu, usafi wa roho, wema, na rehema. Kanuni hizi na zingine ni za kudumu na zinaishi; ndio kiini cha Jumbe zote za Mungu na zinaunganisha zote pamoja.

Mbaya Nzuri zaidi

Sehemu za Makala hiki

Tazama sehemu zote pamoja

Ongeza maoni

  • (Haitaonyeshwa kwa umma)

  • Maoni yako yatakaguliwa na yanapaswa kuchapishwa ndani ya saa 24.

    Sehemu zilizo na alama ya nyota (*) zinahitajika.

Makala Nyingine katika Aina moja

Iliyotazamwa Zaidi

Kila siku
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
jumla
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Chaguo la Mhariri

(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Orodha Yaliyomo

Tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho
Orodha hii ipo tupu kwa sasa.
Zote kwa tarehe
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)

Maarufu sana

Iliyokadiriwa juu zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotumwa  kwa barua pepe zaidi
Iliyochapishwa zaidi
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
(Soma zaidi...)
Iliyotolewa maoni zaidi

Unazozipenda

Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.

Historia yako

Orodha yako ya historia ipo tupu.