요청한 문서 / 비디오는 아직 존재하지 않습니다.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
המאמר / הסרטון שביקשת אינו קיים עדיין.
The article/video you have requested doesn't exist yet.
Miongoni mwa baraka na upendeleo ambao amewapa wanadamu ni kuwa Amewajaalia uwezo wa asili wa kutambua na kujua uwepo Wake. Aliweka ufahamu huu chini kabisa ya mioyo yao kama tabia ya asili ambayo haijabadilika tangu mwanzo wa mwanadamu alipoumbwa. Aidha, Ameiweka tabia hii ya asili na ishara ambazo ameziweka kwenye uumbaji ambazo zinathibitisha uwepo Wake. Lakini, kwakuwa haiwezekani kwa mwanadamu kuwa na maarifa ya kina juu ya Mungu isipokuwa kupitia ufunuo kutoka Kwake Yeye Mwenyewe, Mungu ametuma Wajumbe wake ili kuwafundisha watu kuhusu Muumbaji wao wanaotakiwa kumuabudu. Wajumbe hawa pia wameleta maelezo ya jinsi ya kumuabudu Mungu, sababu maelezo hayo hayawezi kujulikana isipokuwa kwa njia ya ufunuo. Misingi hii miwili ilikuwa vitu muhimu ambavyo Wajumbe wa funuo zote za Mungu walizileta kutoka kwa Mungu. Kwa msingi huu, funuo zote za Mungu zimekuwa na malengo yale yale, ambayo ni:
1. Kuthibitisha Umoja wa Mungu - Muumba wa kusifiwa na kutukuzwa – Katika asili Yake na sifa Zake.
2. Kuthibitisha Mungu peke yake ndiye anapaswa kuabudiwa na hakuna kuabudu kiumbe chochote sambamba na Yeye au badala Yake.
3. Kulinda maslahi ya mwanadamu na kupinga ufisadi na uovu. Hivyo, kila kitu kinacholinda imani, maisha, hoja, utajiri na kizazi ni sehemu ya maslahi ya mwanadamu huyu ambaye dini hulinda. Katika mkono mwingine, kitu chochote ambacho kinahatarisha mahitaji haya muhimu ni njia ya ufisadi ambayo dini inapinga na kukataza.
4. Kuwaalika watu kwa fadhila ya hali ya juu, maadili, na desturi safi.
Lengo la msingi la Ujumbe wa Mungu limekuwa lile lile: kuwaongoza watu kwa Mungu, kuwafanya wamjue Yeye, na kuwafanya wamuabudu Yeye. Kila Ujumbe wa Mungu umekuja kuiwekea nguvu maana hii, na maneno haya yafuatayo yalirudiwa katika ndimi za Wajumbe wote: “Muabuduni Mungu, hakuna mungu zaidi Yake.” Ujumbe huu ulifikishwa kwake mwanadamu kwa kupitia Manabii na Mitume ambayo Mungu aliwatuma Kila nchi. Wajumbe hawa wote walikuja na ujumbe ule ule, Ujumbe wa Uislamu.
Jumbe zote za Mungu zimekuja kufanya maisha ya watu katika kukubali kurudi kwa Mungu. Kwa sababu hii, zote zinachangia katika jina la “Uislamu”, au “Kumrudia” lililoletwa kutoka neno moja kama “Salam”, au “amani”, kwa Kiarabu. Uislamu, kwa maana hii, ilikuwa dini ya mitume yote, ila kwanini mmoja anaona aina tofauti tofauti za dini ya Mungu ikiwa zote zinatoka katika asili moja? Majibu yako mawili.
Sababu ya kwanza ni matokeo ya muda kupita, na kwa ukweli kwamba dini zilizopita hazikuwa katika ulinzi wa Mungu, zimepitia mabadiliko mengi na aina. Matokeo yake, tunaona msingi wa ukweli ambao uliletwa na wajumbe wote sasa unatofautiana kutoka kwa mmoja hadi mwingine, mbainisho wa wazi kabisa ni ukali wa imani ya kumuabudia Mungu na Mungu peke yake.
Sababu ya pili kwa aina hizi ni kwamba Mungu, katika Hekima yake ya milele na Mapenzi ya milele, alituma kazi zote za Kimungu kabala ya ujumbe wa mwisho wa Uislam ulioletwa na Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake, kuwa katika wakati maalumu. Matokeo yake, sheria na mbinu zao ziliendana na hali mahususi za watu ambao walitumwa kuwaambia.
Mwanadamu amepitia vipindi vingi vya kuongozwa, kutokuongozwa, uadilifu, na kupotoka, kuanzia kipindi cha jamii isiyojitambua hadi jamii inayojitambua. Muongozo wa Mungu uliambatana na mwanadamu katika haya yote, mara zote kupata suluhisho sahihi na kuponya.
Hii ilikuwa kiini cha kuwepo utofauti baina ya dini mbali mbali. Kutokukubaliana huku kamwe hakuendi zaidi ya Sheria za Mungu. Kila ufunuo wa Sheria unaeleza matatizo fulani ya watu walio kusudiwa. Ila, sehemu zinazokubaliana ni kubwa na nyingi, kama vile msingi wa imani; kanuni na malengo ya Sheria za Mungu, kama vile kulinda imani, maisha, hoja, utajiri, na kizazi na kusimamia haki katika nchi. ; na baadhi ya makatazo ya kimsingi, baadhi ya haya yenye umuhimu ni ibada ya masanamu, uasherati, mauaji, wizi, na kutoa ushahidi wa uongo. Ila, pia hukubaliana katika maadili mema kama ukweli, haki, sadaka, ukarimu, usafi wa roho, wema, na rehema. Kanuni hizi na zingine ni za kudumu na zinaishi; ndio kiini cha Jumbe zote za Mungu na zinaunganisha zote pamoja.
Orodha ya unazozipenda ipo tupu. Unaweza kuongeza makala kwenye orodha hii kwa kutumia zana za makala.
Orodha yako ya historia ipo tupu.
Kwa nini kujiandikisha? Tovuti hii ina miundo kadhaa uliyoundwa mahsusi kwa ajili yako, kama vile: vipendwa vyako, historia yako, kutia alama makala ambazo umezitazama awali, kuorodhesha makala zilizochapishwa tangu ulivyo tembelea mara ya mwisho, kubadilisha ukubwa wa herufi, na zaidi. Vipengele hivi vinatokana na vidakuzi na vitafanya kazi ipasavyo tu unapotumia kompyuta ile ile. Ili kuwezesha vipengele hivi kutoka kwa kompyuta yoyote, unapaswa kuingia wakati katika tovuti hii.
Tafadhali ingiza Jina lako la mtumiaji na anwani ya barua pepe kisha ubofye kitufe cha Tuma neno la siri. Utapokea neno la siri jipya hivi karibuni. Tumia neno la siri hili jipya kufikia tovuti.
Ongeza maoni